Anataka upako toka kwako
Wadau, nimfanyaje huyu binti, tunasali kanisa moja, ila anapenda sana kuja kukaa pale ninapo kaa mimi kila mara wakati wa misa, atategea kuona nakaa wapi atakuja kukaa hapo hapo, na mara nyingi hupenda kushare na mimi vitabu vyake vya nyimbo na neno.
Hivi ni viashiria gani..anataka nimtongoze ama anjisikia vizuri tu kukaa na mimi..jumapili iliyopita nilifikiri atachelewa lakini kaja muda uleule, na kanifuata moja kwa moja kukaa na mimi..ni mzuri tu..ila najiuliza mara mbili mbili kama ni sahihi kutupa ndoano nisije jutia bure..msaada tutani
hahahahaaa, hii kali arifu..!kama vip kakae mazabahuni ili ukae peke yako
wa mjini wanajichanganya tu! upande wa kiume utakuta kuna wanawake wache, hii inatokana na wingi wa KE kupenda kufanya ibadaMimi ninavyofahamu mara nyingi wanawake na wanaume wanatengannishwa katika viti kanisani. sasa wewe huwa unakaa upande wa wanawake kila misa?
usije ukatongoza watoto wa under 18,shauri yako.mwache binti wa watu kama alivyo.wewe si unaenda kanisani kusali?fata kilichokuleta kanisani.kama unae mpenzi huyo uliekuwa nae anakutosha.