chiko
JF-Expert Member
- Feb 24, 2010
- 580
- 245
Nina Rafiki yangu tumejuana kitambo, kwa sasa ni zaidi ya ndugu. Ni mtu mzima amenizidi ki-umri. Bwana huyu amekua mgonjwa wa Figo kwa muda zaidi ya miaka Minne sasa. Ka talaka mke wake wa kwanza, na ana watoto watu wazima. Kaoa tena kama miaka mitatu iliopita, mama mmoja ambae aliachwa pia.
Huyu bwana kila mwezi akija matibabu mjini mimi ndio humsimamia, na humsaidia. Juzi kaja kama kawaida kwa matibabu, akanitobolea siri, kuwa ana mambo mazito yanayomsumbua. Akanambia mke alienda kupima HIV, akapatikana Positive, kaja nyumbani na kuzusha war!, bwana akawa mpole kwa sababu huwa anapimwa kila mara akija matibabu, na anajua hali yake ni Negative. Wote wawili wakaenda kupimwa pamoja, Bibi Positive na bwana Negative. Wakaambiwa warudi tena baada ya miezi mitatu(Incubation Period), majibu yalikuwa vile vile. Bibi karudi chini, lakini bwana, hasira zikampanda...utapata talaka, kwanza nani kakupatia haya maradhi, na mimi mgonjwa, hata unyumba wenyewe wanishinda!.
Bwana kaja kwangu, anataka ushauri, lakini moyoni amejaa hasira ya kutendewa, akaniambia amewacha bibi akilia nyumbani, hajui afanyeje.
Mimi ushauri wangu ni kamwambia, akirudi nyumbani asiwe na hasira, akae chini na mkewe, wazungumze maisha ya baadae, kwa vile ameomba msamaha, amwachie mungu, atahukumu na waendelee kuishi pamoja na kusaidiana, kwani wote wagonjwa, haina haja kuachana, waendelee na matibabu, kila mtu amsaidie mwenziwe kwa ushauri!.
Sijui wanajamvi, kama nilitoa ushauri mzuri ama nilikosea..... Nyinyi mungemshauri vipi?????????
Huyu bwana kila mwezi akija matibabu mjini mimi ndio humsimamia, na humsaidia. Juzi kaja kama kawaida kwa matibabu, akanitobolea siri, kuwa ana mambo mazito yanayomsumbua. Akanambia mke alienda kupima HIV, akapatikana Positive, kaja nyumbani na kuzusha war!, bwana akawa mpole kwa sababu huwa anapimwa kila mara akija matibabu, na anajua hali yake ni Negative. Wote wawili wakaenda kupimwa pamoja, Bibi Positive na bwana Negative. Wakaambiwa warudi tena baada ya miezi mitatu(Incubation Period), majibu yalikuwa vile vile. Bibi karudi chini, lakini bwana, hasira zikampanda...utapata talaka, kwanza nani kakupatia haya maradhi, na mimi mgonjwa, hata unyumba wenyewe wanishinda!.
Bwana kaja kwangu, anataka ushauri, lakini moyoni amejaa hasira ya kutendewa, akaniambia amewacha bibi akilia nyumbani, hajui afanyeje.
Mimi ushauri wangu ni kamwambia, akirudi nyumbani asiwe na hasira, akae chini na mkewe, wazungumze maisha ya baadae, kwa vile ameomba msamaha, amwachie mungu, atahukumu na waendelee kuishi pamoja na kusaidiana, kwani wote wagonjwa, haina haja kuachana, waendelee na matibabu, kila mtu amsaidie mwenziwe kwa ushauri!.
Sijui wanajamvi, kama nilitoa ushauri mzuri ama nilikosea..... Nyinyi mungemshauri vipi?????????