Nimerudi zangu toka kazini na kufikia katika sofa hapa sebuleni kwangu. Nikaamua kuwasha ka-tv kangu ka nchi kumi na nne ili nijiburudishe na kupata taarifa. Baada ya muda nasikia sauti ya Pinda ikitaja majina ya wakuu wa wilaya wapya. Baada ya kutajwa majina kwa mshituko nikasikia na jina langu ni mojawapo ya majina yaliyopo. Nilipatwa na furaha na kuruka juu kwa furaha............kushtuka kumbe nilikuwa naota na TV ilikuwa ikionyesha tukio la kutangazwa wakuu wapya wa wilaya..........NDOTO HIZI...!!!!!