ndyoko
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 4,971
- 1,650
Jamani hiki ni kisa cha kweli kimetokea masaa 48 yalopita. Ishu yenyewe iko hivi:-
Nilikuwa naishi kwenye nyumba pamoja na mpangaji mwenzangu huko mkoani manyara wilaya ya kiteto. Kwa bahati nzuri nikahama kwenda kuishi kwa nyumba ya ofisi. wakati nahama, mke wa mpangaji mwenzangu alikuwa mjamzito na mwezi ulopita kajifungua mtoto.
Sasa nilipopata taarifa za huyo mke wa mpangaji mwenzangu kupata mtoto nikaona sio mbaya niende kumpongeza-nikiamini ni jambo jema kadiri ya mila zetu waafrika, si mnajua tena. Kwa bahati nzuri nilienda muda ambao na mume wa huyo mzazi alikuwepo. Nikapiga stori na baadae nikaamua kumpa mzazi nguo-niliona nimpe zawadi ya kitenge kwa ajili ya kukafunika kachanga-na nikaondoka zangu.
Kumbe baada ya mimi kuondoka, huko nyuma nikaacha kivumbi. Mume akahoji iweje niende pale na kutoa zawadi? Kwa nini nilifika kwake badala ya kwenda kwa mwenye nyumba? Mwanaume akaamua kuchukua hicho kitenge na kukichoma moto. Wakati zogo linaendelea mwenye nyumba aliwasikia na akaamua kupata full details. Na leo hii, tarehe 12/02/2012 saa 6 mchana huu, akaamua anitaarifu kuhusu issue hii yote akihofia kwa isije nikaenda pale kumbe jamaa ana 'machungu' na mimi.
Binafsi nimefadhaika sana na suala hili ukizingatia nilikaa nao kwa miaka miwili na nusu, hivyo kwangu walikuwa kama ndugu, maana kuna siku, kabla sijahama, mke aliwahi kupata complications za ujauzito, walikuwa wakiwasiliana nami kumuangalia mtoto wao kwanza aliyekuwa amelala usiku wakati wao walienda hospitali.
Jamani naomba mnieleweshe nilikosea wapi ktk mchakato wote niloulezea hapo juu. na nahisi huyu jamaa iko siku anaweza hata akaniwekea sumu kwa hisia chafu alizopata ktk stori hii yote.
Nilikuwa naishi kwenye nyumba pamoja na mpangaji mwenzangu huko mkoani manyara wilaya ya kiteto. Kwa bahati nzuri nikahama kwenda kuishi kwa nyumba ya ofisi. wakati nahama, mke wa mpangaji mwenzangu alikuwa mjamzito na mwezi ulopita kajifungua mtoto.
Sasa nilipopata taarifa za huyo mke wa mpangaji mwenzangu kupata mtoto nikaona sio mbaya niende kumpongeza-nikiamini ni jambo jema kadiri ya mila zetu waafrika, si mnajua tena. Kwa bahati nzuri nilienda muda ambao na mume wa huyo mzazi alikuwepo. Nikapiga stori na baadae nikaamua kumpa mzazi nguo-niliona nimpe zawadi ya kitenge kwa ajili ya kukafunika kachanga-na nikaondoka zangu.
Kumbe baada ya mimi kuondoka, huko nyuma nikaacha kivumbi. Mume akahoji iweje niende pale na kutoa zawadi? Kwa nini nilifika kwake badala ya kwenda kwa mwenye nyumba? Mwanaume akaamua kuchukua hicho kitenge na kukichoma moto. Wakati zogo linaendelea mwenye nyumba aliwasikia na akaamua kupata full details. Na leo hii, tarehe 12/02/2012 saa 6 mchana huu, akaamua anitaarifu kuhusu issue hii yote akihofia kwa isije nikaenda pale kumbe jamaa ana 'machungu' na mimi.
Binafsi nimefadhaika sana na suala hili ukizingatia nilikaa nao kwa miaka miwili na nusu, hivyo kwangu walikuwa kama ndugu, maana kuna siku, kabla sijahama, mke aliwahi kupata complications za ujauzito, walikuwa wakiwasiliana nami kumuangalia mtoto wao kwanza aliyekuwa amelala usiku wakati wao walienda hospitali.
Jamani naomba mnieleweshe nilikosea wapi ktk mchakato wote niloulezea hapo juu. na nahisi huyu jamaa iko siku anaweza hata akaniwekea sumu kwa hisia chafu alizopata ktk stori hii yote.