Nimepata Msiba WanaJF

pole sana sipo mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake za kuishi si nyingi na zinahesabiwa
Mungu akutie nguvu katika kipindi hiki kigumu
Amen
 
Msiba uko Arusha. Ndio tuko kwenye maandalizi ya kufanya mipango ya kusafiri kesho kwa sisi tulioko DSM.

Arusha sehemu gani mkuu?
If you give me directions i promise to be together with you guys!
Embu sema fasta!
Otherwise pole sana mkuu wangu!
Babu alale Pema Peponi!
 
Ndugu wana JF leo mchana nimepata msiba wa Babu yangu Mzaa Mama. Huu msiba mzito sana kwangu kutokana na maisha niliyoishi. Kwa wale ambao hawakukulia kwa Baba na Mama wanajua role ya Babu na Bibi nami ndio inayonifanya niomboleze sana. Kwa kifupi alikuwa ni Baba mzazi. Bwana alitoa na Bwana ametwaa. Jina la Bwana lihimidiwe milele. Amen

Pole mpendwa "SIPO"

Bwana alitoa na Bwana ametwaa; Jina la Bwana libarikiwe. Amen.
 
Pole sana kwa msiba Mola akupe nguvu uweze kuvuka kipindi hiki kigumu. R.I.P. BABU.
 
Pole sana ndugu yangu! kumbuka ipo siku wote tutakutana hai! utiwe nguvu na Mungu
 
Pole sana Mkuu Sipo....wote tu wasafiri na mwisho wetu ndo huo. Mungu akutie Nguvu katika kipindi hiki kigumu.
 
Pole sana Sipo. Pole pia kwa familia na ndugu wote kwa ujumla. Mungu akupeni nguvu ya kustahimili machungu katika kipindi hiki kigumu.
R.I.P. Babu Sipo.
 
Back
Top Bottom