Nimeoa na ninaishi na mke mwenye VVU kwa miaka 7

Na wale ambao hawana HIV ila bado huumwa na kufa unawaongeleaje?
We si umesema ARV huleta ukimwi,, hivyo wale wanaotest positive na hawatumii dawa ila huumwa magonjwa nyemelezi na kufa,, ama kuharibika baadhi ya organ za mwili unawaelezeaje? Let's also talk of the numbers,, wangapi ambao wako HIV negative na hupata magonjwa nyemelezi ? Na wale ambao wako positive je what are the chances kwao kupata magonjwa nyemelezi ama kufa kabisa?? Do you think it's a coincidence?
Ndo maana swali lako haina basis,, maana you don't speak science!!

Bottom line, kama umesoma comments humu ndani vizuri then naamini at this point it is clear to you kwamba people don't take you seriously!! You are just another deluded clown dancing in circles!! You will have to try harder bro,, lasivyo utabaki kukalamika tuuu kwamba unaumia sana kuona huyu na yule bado wanaamini kile na hiki!! Grow some common sense brah,, it may help you.
 
Tatizo watu wanashindwa kumuelewa deception . Yeye dhumuni lake la kupinga hiv ni kupata wateja yaani wagonjwa waliokata tamaa ili awapeleke kwenye dispensary yake kama zile za akina dokta mitishamba waliomkimbia waziri juzi juzi. Maana pia atakwambia ana uwezo wa kutibu kansa . Huyu mtu hatari sana. Na uzi nyingine humu huwa anazianzisha ili kupata watu.in short huyu ni marketing officer wa mitishamba wa kizazi kipya

Mkuu hebu mtake radhi, Wapi ametangaza kuwa ana dispensary. Hizi ndio belief system zinazotuua . Wewe una power ya kufanya research zako ,mbona library zimejaa makala na vitabu vya sayansi , tiba na afya ni kipi kigumu . Mtu hatari ni mtu kama wewe usiyetaka kutenga muda wa kutosha na kusoma, kujadiliana na madaktari, kuwauliza maswali , kujadiliana na wasio madaktari na mwisho wa yote kufanya upembuzi wa ulichosoma na kudiscuss.
Mtu hatari ni yule anayeng'ang'ania wazo moja bila ya kutoa nafasi ya kudadisi kuwa anachoamini kimeanzia wapi . Kuna mengi mazuri yameandikwa ila kwa kuwa tumezoea kuamini kama tunavyoaminishwa (kuanzia dini, afya, jamii, kazi) basi hatuna budi kubaki kama tulivyo na kutoa majibu kwa jinsi ile ile. You own the power to your personal self .
 
Kwenye reply namba 88 niliyomjibu mleta mada katika kipengele namba 3 nimedokeza kwa kifupi tu suala la vipimo.Wewe uko confused kwakuwa hujui sayansi inayotumika kwenye vipimo vya HIV.Vipimo vya HIV ni feki sana,havipimi HIV bali hupima mambo mengine tofauti sana.Somo hili kuhusu vipimo ni refu,ndio maana nimeona nitoe dokezo tu halafu watu wafuatilie wenyewe.

Ningefurahi sana pia ungeuliza kwamba;Kwanini kuna watu wengi wanapimwa HIV+ halafu baada ya muda fulani kupita wakipima tena kituo hichohicho au kingine wanakutwa HIV-.Au kwanini vipimo vinatoa majibu tata,au kwanini kuna vipimo vya aina nyingi vya HIV,au kwanini watumie kipimo zaidi ya kimoja kuthibitisha majibu ya mtu wanayempima.

Jibu lako utalipata kwenye sayansi ya vipimo vyenyewe.Kama utakuwa tayari nitakutumia link zitakazokuwezesha kujua kwanini mimi nasema kwamba vipimo vya HIV ni feki/vya uongo.Vipimo hivi vinaweza kumpima mtu yeyote HIV+ au HIV- bila kujali kama aliwahi kuwa kwenye hizo risk wanazozisema za kuambukizwa au la.Vinaweza kukupima HIV+ leo lakini HIV- kesho.Ukiwa na Mimba,lishe duni,unatumia dawa za kulevya,unakunywa pombe kali bila kula,Malaria kali,TB,Hepatitis,Pneumonia na magonjwa mengie zaidi ya 50 ni vikigezo tosha vinavyoweza kufanya vipimo hivi vikupime HIV+.

Hivyo basi,kupimwa HIV+ sio ishu ya kutilia maana au ya kuijali,ni trick tu ya vipimo ambayo imewekwa kwa makusudi maalum na wale waliotudanganya ili kuwaongezea idadi ya wateja watarajiwa wa ARVs.Kuogopa HIV na kukimbilia kula ARVs ni sawa na kuruka maji na kukanyaga moto.Tatizo hapa si HIV,bali tatizo ni ARVs.Inanisikitisha sana watu wengi hadi leo hii hawajui ujanja huu.
Mkuu inakuaje kuna kuwa na watoto waliozaliwa HIV+ kutoka kwa wamama ambao ni HIV+ au nayo ni kiini macho?
 
Hakika Mungu ni mwema, kwa mtu wa kawaida utaona kama ndoto lakini huu ndio ukweli.

Nilimchumbia mpenzi wangu bila kutambua status zetu za maambukizo ya VVU.

Kosa nililofanya ni kutokwenda nae ANGAZA siku hizo kwa kujiamini kuwa yeye pia anajali afya.

Nilicheki afya peke yangu na kukutwa sina maambukizo ya vvu. Nikamsisitiza na kumshauli pia nae acheki.

Lakini baada ya kucheki akanificha hali yake ya maambukizo ya VVU kwa kuogopa ningemwaacha.

Tuliendelea kukutana as husband & wife bila kinga. Very innocent and stupid, tukakubaliana tuzae mtoto na MUNGU akatubariki, baada mtoto kuzaliwa nikagundua ahaaa kumbe mwenzangu looh ana VVU na alitumia dawa akiwa mjamzito ili kumkinga kiumbe.

Baada ya hapo sasa, je, nikawaza nimwache au. Nikasikia sauti ininiambia nikimwacha tu, atakufa ghafla hivyo nijipe moyo tufunge ndoa nae na nimwaanzishie dawa na nikafanya hivyo na yupo salama nami pia kwa neema za MUNGU bado sina maambukizi ya VVU angalau hadi leo.

Tunaishi tu kwa amani na tunashiriki kwa kutumia kinga kama wataalam wanavyoshauri. Huu ndio msalaba wangu nimeamua kuubeba kwa gharama zote kwani bado nampenda sana mke wangu kipenzi na tunaheshimiana vizuri.

Niliwaza pia, je ningekuwa ndio mimi yeye angefanyaje, na kama ningemwacha ninayemjua tayari ni yupi tena, huwezi jua ningekutana na mabaya zaidi ya VVU.

Ujumbe wangu: vijana wote ninawaomba tumshirikishe MUNGU kwa kila hatua ili kumpata mke/ mume mwema na tusipende kwa matamanio ya kitandani au sura, umbile, na mali tusije tukajilaumu mpaka kufa.

Mungu ni mwema anitiae nguvu mpaka leo nimekuwa karibu nae zaidi na zaidi na anazidi kufanya miujiza mingi tu maishani mwangu.
Mkuu ntaku PM!
 
Hakika Mungu ni mwema, kwa mtu wa kawaida utaona kama ndoto lakini huu ndio ukweli.

Nilimchumbia mpenzi wangu bila kutambua status zetu za maambukizo ya VVU.

Kosa nililofanya ni kutokwenda nae ANGAZA siku hizo kwa kujiamini kuwa yeye pia anajali afya.

Nilicheki afya peke yangu na kukutwa sina maambukizo ya vvu. Nikamsisitiza na kumshauli pia nae acheki.

Lakini baada ya kucheki akanificha hali yake ya maambukizo ya VVU kwa kuogopa ningemwaacha.

Tuliendelea kukutana as husband & wife bila kinga. Very innocent and stupid, tukakubaliana tuzae mtoto na MUNGU akatubariki, baada mtoto kuzaliwa nikagundua ahaaa kumbe mwenzangu looh ana VVU na alitumia dawa akiwa mjamzito ili kumkinga kiumbe.

Baada ya hapo sasa, je, nikawaza nimwache au. Nikasikia sauti ininiambia nikimwacha tu, atakufa ghafla hivyo nijipe moyo tufunge ndoa nae na nimwaanzishie dawa na nikafanya hivyo na yupo salama nami pia kwa neema za MUNGU bado sina maambukizi ya VVU angalau hadi leo.

Tunaishi tu kwa amani na tunashiriki kwa kutumia kinga kama wataalam wanavyoshauri. Huu ndio msalaba wangu nimeamua kuubeba kwa gharama zote kwani bado nampenda sana mke wangu kipenzi na tunaheshimiana vizuri.

Niliwaza pia, je ningekuwa ndio mimi yeye angefanyaje, na kama ningemwacha ninayemjua tayari ni yupi tena, huwezi jua ningekutana na mabaya zaidi ya VVU.

Ujumbe wangu: vijana wote ninawaomba tumshirikishe MUNGU kwa kila hatua ili kumpata mke/ mume mwema na tusipende kwa matamanio ya kitandani au sura, umbile, na mali tusije tukajilaumu mpaka kufa.

Mungu ni mwema anitiae nguvu mpaka leo nimekuwa karibu nae zaidi na zaidi na anazidi kufanya miujiza mingi tu maishani mwangu.
Mkuu ayo ni maamuzi magum kushinda ya Magufuli ya kubomoa nyumba za watu umetisha ujasil wa ivyo ata siutaki mm kwakweli
 
Deception hayuko peke yake wako kama kikundi humu wanatafuta wateja. So ppl b careful na hao watu........hapa wameshamkosa huyu mleta uzi walishaanza kumhadaa wakakuta yuko strong. Mtu anakwambia mkewe ni hiv positive . Wewe unamjibu eti ni fake hakuna hiv. Nini lengo lako. Si anataka amfuate inbox ili amuelekeze wakutane kwenye vi dispensary vyao vya uchochoroni vya akina mwaka........mwingine naye atajifanya kuleta ushuhuda wa kansa kupona kwa apple juice........nachoshauri kama una uwezo wa kutibu hiv au kansa yanini upoteze muda hapa jf . Wewe tayari mtu muhimu duniani andika vitabu.......tembelea hospital zote tz zina wagonjwa wa hiv au nenda ocean road huko kaokoe wagonjwa. Nenda mikoa ya iringa na njombe kuna ngoma kibao nenda kawaokoeni. Hapa hamtampata mtu wa kumpeleka huko vichochoroni kwenu.
 
Kinga ni muhimu sana. Of coz mimi nimekaa nae kwa miaka miwili bila kinga lakini tokea hapo nilishauliwa tutumie kinga mara zote na ndivyo ilivyo isipokuwa wakati wa kutengeneza mtoto tu tena kwa maandalizi mazuri. Just for information.
Unajuaje kama kaupata wiki moja kabla ya kuzaa au kupima
 
Asante sana wote kwa michango yenu.., ni kweli kama nilivyosema awali wote mnatoa michango mizuri sana na tayari nimeokota mawazo mema mengi tu kutoka kwa wote bila kubagua kwa kunitia moyo na ujasili wa kuendelea kupambana kadhalika toka kwa brother Deception, na Kinyau kwa kunipa alternatives za kukabiliana na hali hii na nyingine zinazofanana na hizo. Mfano, kuanzia mwaka 2014 uanze hadi leo January 2016 nafanya water therapy ya kutosha kabisa. Na nishuhudie tu kwakweli nina muda mrefu (miaka mingi) sana sijaugua malaria, wala vihoma homa vyovyote vya kijingajinga.
 
Unajuaje kama kaupata wiki moja kabla ya kuzaa au kupima
Lavian, sio hivyo unavyofikiri, in fact alikuja confess yeye mwenyewe kuwa aliijua hali yake muda kabla hata ya kuwa karibu na mimi. Na kwa wenye roho nyepesi chap ningeweza kumpiga chini.
 
Jamani, Uambukizwaji wa HIV siyo ishu ya michumbuko zaidi, kwa maana michubuko haiwezi kukosa, kumbuka HIV ni mdogo kuliko Hiyo micro michubuko ambayo huwezi kuiona kwa macho.

Issue ya Virus wa HIV kuingia katika blood stream, ni kupitia zaidi katika Epithelium cells, Yaani hizi ni aina ya cells zinazopatikana katika kichwa cha uume usiotahiriwa, Au katika tip ya tundu la mkojo, Au kwa mfano ukibinua jicho ile ngozi nyekundu ndani yake, Au kwa mwanamke ile ngozi za kuta za ndani za Uke, Au ukibinua mdomo, ile ngozi nyekundu ya ndani.

Hizi Epithelium cells ndiyo huwa na Receptors ambazo HIV hujiattach.

Na katika Fluids zenye High concentration ya HIV ya kwanza ni damu, then Shahawa na Maji ya Uke

Kwa hiyo usijidanganye eti unaweza kupiga mdogomdogo ukanusurika kiurahisi, Nusura yako itatokana na HIV kama hajajiattach katika hizo epithelium Cells ili kuingia katika damu.

Faida ya Kutahiri kwa mwanaume inakuja kwa kuwa kichwa cha uume kinaota sugu, exposure ya zile cells inapungua, ila tu inabaki sehemu ndogo ya exposure ambayo ni pale katika lile tundu inapoishia Urethra.

Ukitaka kujua athari ya Epithelium cells kama entrance ya HIV basi unaweza kumpiga finger demu mwenye HIV na usipate, lakini ingiza Dudu uje uone shughuli yake!
 
Last edited:
We si umesema ARV huleta ukimwi,, hivyo wale wanaotest positive na hawatumii dawa ila huumwa magonjwa nyemelezi na kufa,, ama kuharibika baadhi ya organ za mwili unawaelezeaje? Let's also talk of the numbers,, wangapi ambao wako HIV negative na hupata magonjwa nyemelezi ? Na wale ambao wako positive je what are the chances kwao kupata magonjwa nyemelezi ama kufa kabisa?? Do you think it's a coincidence?
Ndo maana swali lako haina basis,, maana you don't speak science!!

Bottom line, kama umesoma comments humu ndani vizuri then naamini at this point it is clear to you kwamba people don't take you seriously!! You are just another deluded clown dancing in circles!! You will have to try harder bro,, lasivyo utabaki kukalamika tuuu kwamba unaumia sana kuona huyu na yule bado wanaamini kile na hiki!! Grow some common sense brah,, it may help you.

We are at different vibrational frequencies.You are at very low level vibration.Ndio maana unajichanganya bila hata kujijua,ndio maana una quote mambo yasiyokuwepo,ndio maana unakana kauli zako mwenyewe,ndio maana unatoa lugha chafu.

Nitaendelea tu kujadiliana na wewe kwasababu ya upendo wangu kwako,lakini kwa mtu yeyote mwenye moyo mwepesi hawezi kuendelea kujadiliana na wewe.Jaribu kujitahidi kufanya meditation itakayokuwezesha kujitambua wewe ni nani,kwanini unaishi,na kukuwezesha pia kujua historia halisi ya dunia ambayo kwayo ndio inatoa majibu yote ya kwanini hivi sasa dunia iko hivi ilivyo.
 
Mkuu inakuaje kuna kuwa na watoto waliozaliwa HIV+ kutoka kwa wamama ambao ni HIV+ au nayo ni kiini macho?

Je,umeshawahi kuona/kusikia watoto waliozaliwa HIV+ kutoka kwa mama ambaye ni HIV-?Najua hii itakushangaza sana,lakini ndio ukweli wenyewe.Cha msingi hapa ni wewe kuelewa point kuu za msingi 4 ambazo uongo kuhusu HIV/AIDS umelalia,bila kujua point hizi 4 utajikuta unauliza maswali mengi sana ambayo nimeshayajibu.

Najua wewe ni mfuatiliaji sana wa mada hizi humu JF,lakini hujazisoma na kuzifuatilia point hizi 4 kwa undani kama nilivyoshauri,kwenye reply yangu namba 88 nimeorodhesha point hizi,sasa ni jukumu lako kuzifuatilia na kama una swali utaniuliza.Swali lako litajibiwa na kipengele namba 3 cha reply hiyo.

Pia ninarudia,unatakiwa ufahamu kwamba kuna watoto wamezaliwa HIV+ kutoka kwa mama ambaye ni HIV-,watu wengi hawalijui jambo hili.Sina haja ya kuweka ushuhuda humu,nataka watu washuhudie wenyewe.Ukifanya uchunguzi wako binafsi utajua tu.Ushuhuda ulioutafuta wewe mwenyewe una nguvu kuliko nitakaoleta mimi,fanya hivyo basi.

Swali:Je,watoto hawa wamepata HIV kutoka kwa nani kama mama na baba zao ni HIV-?Najua wapo watu watakaokurupuka na kutoa majibu kwa hisia tu.Ipo siku watu watajua ukweli tu.Its just a matter of time.
 
Thank you Mr. Deception, and please just take it easy kwa wale wanaokwaza. In fact ndio maana mimi kama mhusika nimeyachukua yote na nayafanyia kazi. Sikutaka kuweka some sort of objections zisizo kuwa na tija. Humu jamvini tumo wengi sana inabidi kuwachukulia tu watu wote. See now, nilikuwa sijui ati mtoto HIV+ kutoka mama na baba HIV-, please funguka zaidi I'm interested to know more.
 
Thank you Mr. Deception, and please just take it easy kwa wale wanaokwaza. In fact ndio maana mimi kama mhusika nimeyachukua yote na nayafanyia kazi. Sikutaka kuweka some sort of objections zisizo kuwa na tija. Humu jamvini tumo wengi sana inabidi kuwachukulia tu watu wote. See now, nilikuwa sijui ati mtoto HIV+ kutoka mama na baba HIV-, please funguka zaidi I'm interested to know more.

Si hili tu,yapo mambo mengi sana hata madaktari wanakutana nayo kwenye clinics lakini wanayadharau na kuyaona ya kawaida kutokana na kujawa na kasumba kwenye ubongo wao.Madaktari na watu wengine wengi wanapoona au kusikia mambo haya huwa mara nyingi wanamsingizia mungu,watu wanadhani kwamba mambo haya ni nadra sana kutokea ilihali haya ndio mengi zaidi ya yale tulioaminishwa.Hata wewe ukiamua kufuatilia ndoa za watu ambao mmoja au wote wamepimwa HIV+ utagundua kwamba ndoa ambazo baba na mama ni HIV+ ni chache sana ukilinganisha na ndoa ambazo mmoja wao(yaani si wote wawili) ni HIV+,fanya uchunguzi wako mwenyewe.Sasa kama kweli HIV yupo na anaambukizwa kwa njia ya ngono kwanini yanatokea haya?Kama ni vgumu kiasi hiki kuambukizwa HIV,kwanini kampeni za HIV/AIDS duniani ni kubwa sana na hutumia pesa nyingi sana kuliko zile za magonjwa ambayo huua zaidi na kwa kasi?

Kufahamu kama tumedanganywa kuhusu HIV/AIDS ni rahisi sana kama watu watakuwa na fikra huru zitakazowawezesha kujihoji kwa mantiki,lakini ni vigumu sana kama watu wataruhusu akili za kupinga zaidi ya kuhoji/kudadisi.

Yafuatayo ni baadhi ya mambo yanayodhihirisha uongo kuhusu HIV/AIDS;
1.Tumeambiwa kwamba HIV huambukizwa kwa njia ya ngono.Lakini kuna ndoa nyingi mitaani ambazo mmoja ni HIV+ na mwingine ni HIV- na mara nyingi hata watoto wao nao ni HIV-,wewe ni mmoja wapo.Hapa waliotudanganya wametunga nadharia nyingi sana ili kurubuni akili za watu kufafanua kwanini hili linatokea,lakini ukweli ni kwamba hili linatokea tu kwasababu hakuna HIV hivyo haileti pia mantiki kusema kwamba HIV anaambukizwa kwa njia ya ngono.

2.Kuna watoto wengi wamepimwa HIV+ wakati wazazi wao wote wawili wamepimwa HIV-.Hapa pia ukiwauliza madaktari lazima watakuwa na jibu ambalo wanaliona ni sahihi.

3.Kuna watu wanapimwa HIV+ wakati fulani lakini baada ya muda fulani kupita wanapimwa HIV- hata kama hawatumii ARVs au dawa yoyote ya hospitali.Hapa pia ukiwauliza lazima watakuwa na jibu.Sasa umeshajiuliza ni wangapi wamekufa kwa kihoro au kujiua au kwa madhara ya kula ARVs kwa kupewa majibu ya namna hii?

4.Kuna hali fulani ukiwanazo mwilini unaweza kupimwa HIV+ lakini hali hizo zinapotoweka/kuondoka unapimwa HIV-.Hali hizo ni mimba,magonjwa mbalimbali kama TB,Malaria nk na nyinginezo nilizozitaja kwenye reply zangu za nyuma.Sasa kwanini vipimo vikupime HIV+ kama una TB,Malaria,mimba nk halafu vikupime HIV- kama huna hali hizo?Fanya uchunguzi wako.Ukielewa hili ndipo utakapojua kwamba kinachopimwa na vipimo hivi sio HIV bali ni kitu kingine tofauti kabisa.

5.Kuna watu wengi wamepimwa HIV+ miaka zaidi ya 20 na hawatumii ARVs lakini bado wana afya njema na nguvu.Hapa watakwambia kwamba watu hawa wanaitwa CARRIERS,hili sitalizungumzia sasa lakini ukweli ni kwamba nadharia hii kuhusu CARRIERS ni uongo wa wazi kabisa kwa kuwa HIV mwenyewe anayezungumziwa hayupo kiuhalisia.

6.Unaweza kujidunga damu ya mtu aliyepimwa HIV+ na baada ya miezi 3/4/5... ukienda kupima unaweza kupimwa HIV-.

7.Ukimpa ARVs mtu ambaye amepimwa HIV- na ana afya njema kwa muda mrefu,mtu huyo ataanza kudhoofu na kuwa na matatizo moja au zaidi ya yafuatayo;Moyo,ini,figo,upungufu wa damu,kisukari,cancer/saratani.Matatizo haya ndio yaleyale yanayowaua watu wanaotumia ARVs kwa muda mrefu.Nenda hospitalini kachunguze wewe mwenyewe,kumbuka kwamba matatizo haya hayasababishwi na vijidudu,hivyo hatutarajii HIV(hata kama yupo) asababishe matatizo haya.Nadhani pia umeshawahi kusikia kuna watu huwa wanaenda nje ya nchi kubadilisha damu,fahamu kwamba matatizo yao ya damu hayakuletwa na HIV bali ARVs kwa kuwa bone marrow zao zimeathiriwa na ARVs kiasi cha kushindwa kuzalisha damu.Hili liko wazi kabisa hata madaktari wanalifahamu.Halafu kuna watu wanakuja hapa wanasema eti kila dawa ukitumia muda mrefu ina madhara,suala hapa si madhara tu bali ni madhara gani.


Kama nilivyodokeza mwanzo kwamba,ili watu wabadilike kimtazamo inabidi wawe na uelewa wa mambo mengi sana,kwa mfano;Historia ya western medicine,Federal Reserve System ya Marekani,Kuanzishwa kwa UNO na mashirika yake,mfumo wa serikali ya Marekani nakadharika.Kama huna misingi ya uelewa kama hii ni vigumu kuelewa na badala yake watu watapinga kila kitu ambacho kwao ni kipya.Hata nikija kusema kwamba cancer zote zinatibika watu watapinga pia,sasa ni vigumu sana kuelewesha watu wa namna hii kwa kuwa hawana uelewa wa mambo mengi sana.Ndio maana wengine huja na kusema kwamba mimi nafanya biashara,ukiwaomba wathibitishe kama kweli mimi nafanya biashara hawawezi kuthibitisha,watu wanaongea hovyo tu, hawajielewi/hawajitambui wao ni kina nani.

Ukiwa na uelewa huu ndio utajua kwanini matangazo ya HIV/AIDS kwenye vyombo vya habari ni kwa hisani ya watu wa marekani,matangazo ya uzazi wa mpango ni hisani ya watu wa Marekani,matangazo ya Malaria ni hisani ya watu wa Marekani,Chanjo za mabusha ni hisani ya watu wa Marekani,matembezi ya cancer ya matiti ni hisani ya watu wa Marekani nakadharika.Watu wanaona kama wamarekani wanatupenda sana lakini hawajiulizi kwanini wamarekani haohao wanaotupenda wanaua watu wakiwemo watoto wasio na hatia kwenye vita Afghanistan,Iraq,Syria,Mashariki ya kati nk.

Wamarekani haohao wametunga sheria inayoruhusu uvutaji wa sigara/tumbaku ambayo ina maandishi "uvutaji wa sigara ni hatari kwa afya yako" lakini sheria hiyo inakataza bangi kwa ujumla wake,wanakataza dawa za kulevya wakati haohao ndio wazalishaji wakubwa na wakati huohuo wanaruhusu pombe kali zinazoharibu maini.Vitu vyote hivi vina maana kubwa sana lakini watu wanaviona ni vya kawaida kutokana na kuzongwa na viburudisho vingi vinavyotokana na kukua kwa sayansi na tekinolojia.Watu wanaporuhusu kutawaliwa na viburudisho wakumbuke pia uwezo wao wa kufikiri unapungua kwa kiwango kikubwa,sina maana kwamba hatutakiwi kujiburudisha,nadhani nimeeleweka.

Pole kwa post ndefu,lakini haya bado ni maneno machache sana ukilinganisha na ninachokusudia watu wakijue.Watu wengi sana wanafikiria katika level ya chini sana kutokana na kukosa uelewa kama huu.
 
Back
Top Bottom