Kaa la Moto
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 7,903
- 1,053
Kwa sasa nina miaka 50+ na nimekuwa na mawazo sana hadi kumlilia Nyerere. Nimejaribu kumuangalia nyerere na nimelazimika kulia kabisa. Hakika watanzania tumepoteza lulu. Wale watanzania wa kizazi cha jana wanaweza wasijue hili lakini wale wa kizazi chetu tutamkumbuka daima. Nimegundua kwa nini wanasiasa umtumia Nyerere kwenye midomo yao. Nimegundua kwa nini tumepoteza tumaini kuu katika maendeleo ya nchi yetu.
Wakati namfikiria Nyerere nimeshangaa sana jinsi mtu huyu alivyokuwa na maono makubwa sana kuhusu nchi hii. Jamani Nyerere alikuwa na maono makubwa sana kuhusu nchi hii ya Tanzania na alikusudia kuijenga nchi hii.
Nimegundua Nyerere alijua kitu kile kile wanachojua wachumi wetu kuwa nchi inapata maendeleo kwa kuwa industrialized na kwa kujua hilo aliifanya nchi kujenga viwanda vingi sana ili kuongeza uchumi wetu. Sidhani kama alikosea. Hapana, alijua nini alikusudia kufanya na wapi alikusudia kuifikisha nchi hii. Leo kama laiti tungelipata viongozi wenye maono kama Nyerere tungekuwa na nchi iliyo na neema ya viwanda kuliko nchi nyingi za Africa ukiondoa Africa kusini. Leo kwa mfano Kenya inaonekana imekuwa kiviwanda lakini kwa sasa hivi kwa maono aliyokuwa nayo Nyerere hakika tungelikuwa mbali kuliko hata Kenya.
Ebu tujikumbushe kidogo. Nyerere akijua umuhimu wa kujenga taifa lenye viwanda kwanza aliunda taasisi iliyokuwa ikijulikana kwa jina la NDC (NATIONAL DEVELOPMENT CORPORATION) ambalo kwa kiswahili lilijulikana kama (SHIRIKA LA TAIFA LA MAENDELEO) ambalo lilipewa jukumu ya kuleta maendeleo ya kiviwanda na kwa kweli lilifanya kazi ya kutengeneza viwanda vya kila aina kiasi kwamba kila kitu kingeweza kuzalishwa hapa Tanzania. Kwa Nyerere viwanda na mining ilikuwa ni maendeleo. Wakati yeye alianzisha shirika hilo wenzetu waliomfuata wao walianzisha tume ya kuua yote aliyoanzisha Nyerere kwa kuunda tume ya ubinafsishaji wa mali ya umma (kwa maana nyingine tume ya kuharibu mipango yote ya Nyerere).
Nimekuwa nikifikiria ni viwanda vingapi viliasisiwa na Nyerere hata nimeshindwa kuhesabu kwa wingi wa idadi. Nakumbuka kulikuwa na viwanda vyote katika fani za ujenzi, Viwanda vya sementi Tanga,Twiga, Mbeya, viwanda vya nondo, viwanda vya misumali, Kiwanda cha mabati ambacho kiliitwa aluminium na kilitengeza pamoja na mabati pia vifaa vya nyumbani kama masinia glass za aluminium, mabakuli, masufuria na vitu vingine, aliasisi Kiwanda cha kutengeneza vioo kikiitwa kwa jina la Kioo ltd kikitengeneza sio vioo vya ujenzi tu bali hata vifaa vingine vya kioo kama glass, sahani nk, kulikuwa na viwanda vya kutengezeza mabomba ya aluminium na plastic, aliasisi ujenzi wa viwanda vya vifaa vya umeme kule Tanalec kiasi walizalisha hadi transformer na vitu vingine vya umeme, alianzisha viwanda ambavyo vilitengeza bidhaa za mbao kama ceiling boards na chip boards, kulikuwa na kiwanda cha kutengeneza almas kule Iringa hivyo hakukuwa na haja ya kusafirisha madini yetu kwenda kuyafanyia finishing nje. Ina maana yaliongezwa thamani hapa hapa kwetu, alianzisha viwanda vya kutengeneza packing materials kama kile kilikuwa kinatengeneza maboksi na kile cha kutengeza makopo ya packing! Alitengeneza viwanda vya kuprocess nyama na hakuishia hapo tu alitengeneza na viwanda vya kuprocess ngozi ili kuziongezea thamani, hatuwezi kusahau viwanda vya kutengeneza nguo kama mwatex, kiltex, urafiki na vyote vya aina yake. Akaanzisha viwanda vya kutengeneza mablanketi, nyuzi kule Tabora na hapo usisahau viwanda vya kutengeneza zana za kilimo, kwani sikuwa na haja ya kununua panga, jembe, slasher, wheelbarrow kutoka china, hakuishia huko tu akaanzisha viwanda vya kuunganisha magari kule Kibaha, akaanzisha viwanda vya kuunganisha matrekta, kujenga board za magari, viwanda vya kutengeneza betri za magari, Kiwanda cha kutengeneza betri za majumbani Cha National, hatungekuwa na haja ya kuagiza betri duni toka china. Sijasahau jinsi ambavyo alianzisha kiwanda cha kutengeneza pipi, biscuits, jiuice, kachumbali kule Iringa. Sijasahau kiwanda cha kusindika Kahawa alichokijenga kule Bukoba ambacho ni moja kati ya viwanda viwili tu Afrika vya aina yake. Nakumbuka kile kiwanda cha Amboni , kile cha kuzalisha mbolea kule Tanga. Sijasahau sabuni za rumi, mbuni na Ilula. Sijasahau Mashirika ya uvuvi aliyoasisi ili kuongeza pato kutokana na uvuvi maliasili ya baharini na ziwani, sijasahau shirika la Stamico alilounda kuratibu shughuli za madini yetu ambayo leo yanavunwa bila utaratibu na bila aibu tunaambiwa yametunufaisha na sasa watu wanapigwa risasi na kuuawa, Sijasahau kile kiwanda cha kutengeneza matundubali, kiwanda cha kutengeneza baiskeli za Swala na spea zote za baiskeli, kiwanda cha general tyre, kiwanda cha viberiti, viwanda vya maziwa, viwanda vya kusindika tumbaku, Pamba na Alianzisha benki kadhaa kuwasaidia wananchi mbali na zile alizotaifisha. Alitaifisha kiwanda cha sigara na kukiendeleza na sasa wamerudishiwa wakoloni wale wale mambo leo, usinikumbushe kiwanda cha bia, Tanzania distilleries kinachotengenza konyagi, kiwanda cha pombe ya walala hoi kibuku, Kiwanda cha mvinyo Dodoma, kiwanda cha vigae na unaweza kuendelea na orodha kama unakumbuka.
Kila nikikumbuka namlilia Nyerere. Nasema namlilia Nyerere si kwamba hakuwa na mapungufu!, la hasha namlilia kwa sababu tumepoteza kiongozi aliyekuwa na maono ambayo yamepotea! tumepoteza kiongozi ambaye aliona ambako waliomfuata hawakuoana.
Najua kuna hoja dhaifu kuwa utandawizi usingeepukika, Sawa lakini si utandawizi ungetukuta na mali zetu? mbona badala ya kuziboresha tumeziua huku tukiwadanganya watanzania kuwa watanufaika wakati si kweli? Nina kila sababu ya kumlilia Nyerere. Nalilia kifo cha maono yake, Naililia Tanzania isiyokuwa na tumaini maana kila aliyemfuata alikuwa na kusudi la kufaidi peke yake kwa kuyaua yale aliyoanzisha. Namlilia Nyerere!
Kweli bado tuna tumaini la maono yale yaliyoanzishwa na Nyerere? Nani tena anaweza kurudisha tumaini hili? Nani atawarudishia watoto wa Kitanzania tumaini la nchi yenye viwanda tena akiwa mkweli mpaka nafsini mwake? Nasema nani???????????
Je wewe unakumbuka aliyoanzisha Nyerere ambayo sikuyataja? ebu endeleza orodha hii ndefu alafu utagundua kwa nini namlilia Nyerere!
Wakati namfikiria Nyerere nimeshangaa sana jinsi mtu huyu alivyokuwa na maono makubwa sana kuhusu nchi hii. Jamani Nyerere alikuwa na maono makubwa sana kuhusu nchi hii ya Tanzania na alikusudia kuijenga nchi hii.
Nimegundua Nyerere alijua kitu kile kile wanachojua wachumi wetu kuwa nchi inapata maendeleo kwa kuwa industrialized na kwa kujua hilo aliifanya nchi kujenga viwanda vingi sana ili kuongeza uchumi wetu. Sidhani kama alikosea. Hapana, alijua nini alikusudia kufanya na wapi alikusudia kuifikisha nchi hii. Leo kama laiti tungelipata viongozi wenye maono kama Nyerere tungekuwa na nchi iliyo na neema ya viwanda kuliko nchi nyingi za Africa ukiondoa Africa kusini. Leo kwa mfano Kenya inaonekana imekuwa kiviwanda lakini kwa sasa hivi kwa maono aliyokuwa nayo Nyerere hakika tungelikuwa mbali kuliko hata Kenya.
Ebu tujikumbushe kidogo. Nyerere akijua umuhimu wa kujenga taifa lenye viwanda kwanza aliunda taasisi iliyokuwa ikijulikana kwa jina la NDC (NATIONAL DEVELOPMENT CORPORATION) ambalo kwa kiswahili lilijulikana kama (SHIRIKA LA TAIFA LA MAENDELEO) ambalo lilipewa jukumu ya kuleta maendeleo ya kiviwanda na kwa kweli lilifanya kazi ya kutengeneza viwanda vya kila aina kiasi kwamba kila kitu kingeweza kuzalishwa hapa Tanzania. Kwa Nyerere viwanda na mining ilikuwa ni maendeleo. Wakati yeye alianzisha shirika hilo wenzetu waliomfuata wao walianzisha tume ya kuua yote aliyoanzisha Nyerere kwa kuunda tume ya ubinafsishaji wa mali ya umma (kwa maana nyingine tume ya kuharibu mipango yote ya Nyerere).
Nimekuwa nikifikiria ni viwanda vingapi viliasisiwa na Nyerere hata nimeshindwa kuhesabu kwa wingi wa idadi. Nakumbuka kulikuwa na viwanda vyote katika fani za ujenzi, Viwanda vya sementi Tanga,Twiga, Mbeya, viwanda vya nondo, viwanda vya misumali, Kiwanda cha mabati ambacho kiliitwa aluminium na kilitengeza pamoja na mabati pia vifaa vya nyumbani kama masinia glass za aluminium, mabakuli, masufuria na vitu vingine, aliasisi Kiwanda cha kutengeneza vioo kikiitwa kwa jina la Kioo ltd kikitengeneza sio vioo vya ujenzi tu bali hata vifaa vingine vya kioo kama glass, sahani nk, kulikuwa na viwanda vya kutengezeza mabomba ya aluminium na plastic, aliasisi ujenzi wa viwanda vya vifaa vya umeme kule Tanalec kiasi walizalisha hadi transformer na vitu vingine vya umeme, alianzisha viwanda ambavyo vilitengeza bidhaa za mbao kama ceiling boards na chip boards, kulikuwa na kiwanda cha kutengeneza almas kule Iringa hivyo hakukuwa na haja ya kusafirisha madini yetu kwenda kuyafanyia finishing nje. Ina maana yaliongezwa thamani hapa hapa kwetu, alianzisha viwanda vya kutengeneza packing materials kama kile kilikuwa kinatengeneza maboksi na kile cha kutengeza makopo ya packing! Alitengeneza viwanda vya kuprocess nyama na hakuishia hapo tu alitengeneza na viwanda vya kuprocess ngozi ili kuziongezea thamani, hatuwezi kusahau viwanda vya kutengeneza nguo kama mwatex, kiltex, urafiki na vyote vya aina yake. Akaanzisha viwanda vya kutengeneza mablanketi, nyuzi kule Tabora na hapo usisahau viwanda vya kutengeneza zana za kilimo, kwani sikuwa na haja ya kununua panga, jembe, slasher, wheelbarrow kutoka china, hakuishia huko tu akaanzisha viwanda vya kuunganisha magari kule Kibaha, akaanzisha viwanda vya kuunganisha matrekta, kujenga board za magari, viwanda vya kutengeneza betri za magari, Kiwanda cha kutengeneza betri za majumbani Cha National, hatungekuwa na haja ya kuagiza betri duni toka china. Sijasahau jinsi ambavyo alianzisha kiwanda cha kutengeneza pipi, biscuits, jiuice, kachumbali kule Iringa. Sijasahau kiwanda cha kusindika Kahawa alichokijenga kule Bukoba ambacho ni moja kati ya viwanda viwili tu Afrika vya aina yake. Nakumbuka kile kiwanda cha Amboni , kile cha kuzalisha mbolea kule Tanga. Sijasahau sabuni za rumi, mbuni na Ilula. Sijasahau Mashirika ya uvuvi aliyoasisi ili kuongeza pato kutokana na uvuvi maliasili ya baharini na ziwani, sijasahau shirika la Stamico alilounda kuratibu shughuli za madini yetu ambayo leo yanavunwa bila utaratibu na bila aibu tunaambiwa yametunufaisha na sasa watu wanapigwa risasi na kuuawa, Sijasahau kile kiwanda cha kutengeneza matundubali, kiwanda cha kutengeneza baiskeli za Swala na spea zote za baiskeli, kiwanda cha general tyre, kiwanda cha viberiti, viwanda vya maziwa, viwanda vya kusindika tumbaku, Pamba na Alianzisha benki kadhaa kuwasaidia wananchi mbali na zile alizotaifisha. Alitaifisha kiwanda cha sigara na kukiendeleza na sasa wamerudishiwa wakoloni wale wale mambo leo, usinikumbushe kiwanda cha bia, Tanzania distilleries kinachotengenza konyagi, kiwanda cha pombe ya walala hoi kibuku, Kiwanda cha mvinyo Dodoma, kiwanda cha vigae na unaweza kuendelea na orodha kama unakumbuka.
Kila nikikumbuka namlilia Nyerere. Nasema namlilia Nyerere si kwamba hakuwa na mapungufu!, la hasha namlilia kwa sababu tumepoteza kiongozi aliyekuwa na maono ambayo yamepotea! tumepoteza kiongozi ambaye aliona ambako waliomfuata hawakuoana.
Najua kuna hoja dhaifu kuwa utandawizi usingeepukika, Sawa lakini si utandawizi ungetukuta na mali zetu? mbona badala ya kuziboresha tumeziua huku tukiwadanganya watanzania kuwa watanufaika wakati si kweli? Nina kila sababu ya kumlilia Nyerere. Nalilia kifo cha maono yake, Naililia Tanzania isiyokuwa na tumaini maana kila aliyemfuata alikuwa na kusudi la kufaidi peke yake kwa kuyaua yale aliyoanzisha. Namlilia Nyerere!
Kweli bado tuna tumaini la maono yale yaliyoanzishwa na Nyerere? Nani tena anaweza kurudisha tumaini hili? Nani atawarudishia watoto wa Kitanzania tumaini la nchi yenye viwanda tena akiwa mkweli mpaka nafsini mwake? Nasema nani???????????
Je wewe unakumbuka aliyoanzisha Nyerere ambayo sikuyataja? ebu endeleza orodha hii ndefu alafu utagundua kwa nini namlilia Nyerere!