Nimemkumbuka Haruna Moshi Shaaban

sembo

JF-Expert Member
May 25, 2011
4,350
3,451
Tangu karne hii mpya ianze, mnamo mwaka 2000, mmoja kati ya wachezaji bora kabisa toka nchini kwetu Tanzania [kama si bora kuliko wote].. niliobahatika kumshuhudia ni "Mtalamu" Haruna Moshi Boban.
Boban alikua ni mchezaji mwenye akili nyingi sana za mpira pamoja na kipaji halisi alichojaaliwa na Mwenyezi Mungu.

Haruna alipata mafanikio makubwa katika uchezaji
wake wa soka alipokuwa katika timu ya Simba S.C kwani aliweza kuchukua makombe ya ligi kuu katika misimu ya 2003/2004.. 2006/2007.. pamoja na 2011/12 [Invincible Simba S.C ikimaliza msimu bila kufungwa mechi hata moja, kwa kumchapa mtani 5-0 katika mechi ya mwisho].

Boban ameitumikia Simba S.C kati ya miaka 2004 mpaka 2009 na 2011mpaka 2013.

Mambo yaliyofanya nimkumbuke.. Haruna Moshi Boban, ni haya hapa chini;

1. Uwezo mkubwa sana aliokua nao wa kutengeneza na kufunga magoli, pia alikua na jicho kali sana la pasi muhimu [kwake kutoa pasi mkaa ilikua ni mwiko].
Pia Boban alikua na uwezo wa kufanya vitu vya kustaajabisha [madoido] kila aingiapo uwanjani.. ambavyo viliwaacha mashabiki na maswali kibao.. kama vile.. "Amewezaje?!".. " Haiwezekani bhana!?".. "Boban ni wa ulaya!!".. " Duh.. Kama Gaucho vile?!" .. n.k.

2. Kipaji cha hali ya juu cha kuudhibiti, kukaa, na kuuamuru mpira ufanye anachotaka.. Hakua na papara wala kuogopa kupewa mpira na wenzie uwanjani.
Pamoja na uwezo huo hakupenda kukaa na mpira lakini pindi apatapo mpira [ndo utajua kwanini alipewa a.k.a ya Boban] kwani hujua nini cha kufanya juu ya huo mpira, kabla hata hujatua mguuni mwake.

3. Kama ilivyo ngumu kwa Ngamia kupenya katika tundu la sindano, ndivyo ilivyokua ngumu [tena sana tu] kwa Boban kupoteza mpira ulio mguuni kwake.
Boban alikua na uwezo mkubwa sana wa kuulinda mpira ukiwa miguuni mwake.. Na changamoto kubwa kwa wachezaji wa timu pinzani ilikua wanamdhibiti vipi Boban.. hivyo wakawa wanaishia kupokea kadi kama njugu.

4. Haruna alikua na mawazo ya ziada ya kujua wenzie wanawaza nini na hivyo kufanya kama wanavyotarajia. Kwa upande wa pili wa shilingi.
Haruna alikua akitofautiana mara chache na wenzake uwanjani.. na hii ilitokana na wenzake kushindwa kumuelewa anataka nini uwanjani [nadhani hii ni kutokana na kuwa dk. 3 mbele].

Japo nafahamu, Jua linaelekea kuzama kwa upande wa Haruna Moshi Boban.. Namtakia kila ya heri, yeye na timu yake ya Friends Rangers iweze kupanda daraja msimu ujao.. Ili tuweze kumshudia tena Living Legend huyu.

1444547904054.jpg
Long Live..
The Living Legend...
Haruna Moshi Boban.
 
Kuna ile picha anachanganya maji ya kunywa na kiroba mwenye nayo ailete hapa.
 
Nakubaliana nawe, huyu ni mmoja kati ya wachezaji bora kuwahi kutokea Tanzania na Afrika kwa ujumla.
Bado sijajua kwa nini Watanzania ambao baadhi yao wana uwezo kuliko wachezaji wa Afrika Magharibi wameshindwa kucheza hata timu za daraja la pili Uingereza, Ufaransa na Hispania.
 
Nakubaliana nawe, huyu ni mmoja kati ya wachezaji bora kuwahi kutokea Tanzania na Afrika kwa ujumla.
Bado sijajua kwa nini Watanzania ambao baadhi yao wana uwezo kuliko wachezaji wa Afrika Magharibi wameshindwa kucheza hata timu za daraja la pili Uingereza, Ufaransa na Hispania.

Mkuu kama ulipata bahati ya kuona vipaji kwa hawa wachache tuu huwezi kumtaja bobani kuwa ni kipaji zaidi ya hawa..Hamisi Gaga,Athuman China,Malota Soma,Stiven Mussa,Method Mogela,Michael paul nylon,Hussein Marsha,Said Mwamba,George Lukas,Nteze john,Mao mkami,wakina Njohole,Shabani Ramadhani,keneth Mkapa,Twaha hamidu,peter Tino,Edo Chumila mkuu nina kumbukumbu ya timu nyingi mpaka wa akiba maana that time ilikua ni mpira na shule hakuna fiesta wala nn..
 
Mkuu kama ulipata bahati ya kuona vipaji kwa hawa wachache tuu huwezi kumtaja bobani kuwa ni kipaji zaidi ya hawa..Hamisi Gaga,Athuman China,Malota Soma,Stiven Mussa,Method Mogela,Michael paul nylon,Hussein Marsha,Said Mwamba,George Lukas,Nteze john,Mao mkami,wakina Njohole,Shabani Ramadhani,keneth Mkapa,Twaha hamidu,peter Tino,Edo Chumila mkuu nina kumbukumbu ya timu nyingi mpaka wa akiba maana that time ilikua ni mpira na shule hakuna fiesta wala nn..

Acha ubishi Boban Ni Fundi sanaaaa
 
Tangu karne hii mpya ianze, mnamo mwaka 2000, mmoja kati ya wachezaji bora kabisa toka nchini kwetu Tanzania [kama si bora kuliko wote].. niliobahatika kumshuhudia ni "Mtalamu" Haruna Moshi Boban.
Boban alikua ni mchezaji mwenye akili nyingi sana za mpira pamoja na kipaji halisi alichojaaliwa na Mwenyezi Mungu.

Haruna alipata mafanikio makubwa katika uchezaji
wake wa soka alipokuwa katika timu ya Simba S.C kwani aliweza kuchukua makombe ya ligi kuu katika misimu ya 2003/2004.. 2006/2007.. pamoja na 2011/12 [Invincible Simba S.C ikimaliza msimu bila kufungwa mechi hata moja, kwa kumchapa mtani 5-0 katika mechi ya mwisho].

Boban ameitumikia Simba S.C kati ya miaka 2004 mpaka 2009 na 2011mpaka 2013.

Mambo yaliyofanya nimkumbuke.. Haruna Moshi Boban, ni haya hapa chini;

1. Uwezo mkubwa sana aliokua nao wa kutengeneza na kufunga magoli, pia alikua na jicho kali sana la pasi muhimu [kwake kutoa pasi mkaa ilikua ni mwiko].
Pia Boban alikua na uwezo wa kufanya vitu vya kustaajabisha [madoido] kila aingiapo uwanjani.. ambavyo viliwaacha mashabiki na maswali kibao.. kama vile.. "Amewezaje?!".. " Haiwezekani bhana!?".. "Boban ni wa ulaya!!".. " Duh.. Kama Gaucho vile?!" .. n.k.

2. Kipaji cha hali ya juu cha kuudhibiti, kukaa, na kuuamuru mpira ufanye anachotaka.. Hakua na papara wala kuogopa kupewa mpira na wenzie uwanjani.
Pamoja na uwezo huo hakupenda kukaa na mpira lakini pindi apatapo mpira [ndo utajua kwanini alipewa a.k.a ya Boban] kwani hujua nini cha kufanya juu ya huo mpira, kabla hata hujatua mguuni mwake.

3. Kama ilivyo ngumu kwa Ngamia kupenya katika tundu la sindano, ndivyo ilivyokua ngumu [tena sana tu] kwa Boban kupoteza mpira ulio mguuni kwake.
Boban alikua na uwezo mkubwa sana wa kuulinda mpira ukiwa miguuni mwake.. Na changamoto kubwa kwa wachezaji wa timu pinzani ilikua wanamdhibiti vipi Boban.. hivyo wakawa wanaishia kupokea kadi kama njugu.

4. Haruna alikua na mawazo ya ziada ya kujua wenzie wanawaza nini na hivyo kufanya kama wanavyotarajia. Kwa upande wa pili wa shilingi.
Haruna alikua akitofautiana mara chache na wenzake uwanjani.. na hii ilitokana na wenzake kushindwa kumuelewa anataka nini uwanjani [nadhani hii ni kutokana na kuwa dk. 3 mbele].

Japo nafahamu, Jua linaelekea kuzama kwa upande wa Haruna Moshi Boban.. Namtakia kila ya heri, yeye na timu yake ya Friends Rangers iweze kupanda daraja msimu ujao.. Ili tuweze kumshudia tena Living Legend huyu.

View attachment 297364
Long Live..
The Living Legend...
Haruna Moshi Boban.

5. Alikuwa mvuta bhangi na mnywaji ulanzi, mambo haya yalimfanya ashindwe kuendelea kucheza soka Ughaibuni (maana huko hayapo) na kurejea Bongo akidai kuwa Ulaya kuna lolote, maisha yako Bongo!
 
Dedication "Hujafa hujasifiwa" by mwl wa walimu marehemu banza stone(twanga pepeta).
 
Back
Top Bottom