Nimekwama window xp

Kaa la Moto

JF-Expert Member
Apr 24, 2008
7,903
1,053
Wakuu mimi hii computer yangu ya HP imekwama. Kwa siku kama tatu imekuwa ikikwama kufungua page au kutii komandi mapema.

HDD yangu imefanyiwa partition na ina drive ya C na D. Drive C ina OS ya window xp na drive D naitumia kama backup kwa kipindi cha miaka kama 4 hivi sasa na ina data zangu muhimu sana.
Niliamua ku repair window nikihisi kuna files haziko sawa. Lakini nilishangaa kukuta ile DOS command imeandikwa D:\windows> maana najua window iko C.

Baada ya kuhangaika bila mafanikio niliamua ku restore kwa tarehe ya nyuma kama wiki nne hivi na ilikubali kuanza kufanya kazi lakini KIS ilikuwa haionekani ingawa PC ilisema imo. Mara ghafla na mouse ikakwama kufanya kazi.

Nikapata maamuzi ni format na kuweka OS upya. Lakini cha ajabu ni kwamba bado niligundua kuwa iliyokuwa driive C kwenye computer imekuwa renamed drive D na iliyokuwa drive D imekuwa renamed drive C. Kwa hiyo nikiweka window mpya inakwenda kwenye drive D ingawa ni ile ile iliyokuwa C zamani ila imekuwa renamed D. Sasa C ndio inaonekana kuwa ni ile back up iliyokuwa D zamani.

Shida ni kwamba software zingine niki install zinajipeleka C ambayo kwa sasa ni back up badala ya kwenda kule kuliko na window ambayo sasa ni D.

Nimejaribu kuzi rename tena hizi drives kwenye Disk management lakini zimekataa kuwa renamed.
Je nifanyeje ili nizi rename kwa drive letters zile zile za zamani? mwenye kujua anisaidie tafadhali.
 
Maadamu unaweza ku-access mafile yako,basi bila kuchelewa fanya backup ya data zako zote to external/secondary drive and run a windows fresh install,hakikisha una-delete or format logical drives zote 2 then create new ones. Install ur KIS and u r done.
 
Maadamu unaweza ku-access mafile yako,basi bila kuchelewa fanya backup ya data zako zote to external/secondary drive and run a windows fresh install,hakikisha una-delete or format logical drives zote 2 then create new ones. Install ur KIS and u r done.
Asante mkuu wangu. Ubarikiwe.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom