Nimekula NYAMA YA MBWA

Leo Nikapiga kama vipande kumi, nikaagiza Serengeti nyingine ya baridi.
Nikiwa katikati ya zoezi la pombe nyama, mara wakaingia Polisi wakiwa na sare zao na kuelekea jikoni.
Huko wakawaweka chini ya ulinzi watumishi wote na kufanya msako mkali. Jikoni vimekamatwa vichwa viwili vya mbwa na ngozi mbili. Kuweni makini wenzangu, yasije kuwakuta yaliyonikuta.

Nakupa Pole kwa sababbu unahofu ya kula nyama ya Mbwa.

Lakini hiyo ni nyama kama ilivyo mbuzi, kwani watani zangu kutoka IRINGA MBONA WANAKULA, Na angalia Wahehe jinsi walivyo kuwa na afya.

NYAMA NYAMA NYAMA..... NYAMA ya MBWA...NYAMA.....



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
wakuu tena niwaongezee habari nyingine,kwa wanaosafiri kwenda mbeya,iringa pale mikumi ukila nyama kama umewahi kuagiza nyama ukaambiwa ya mbuzi andika umeshawahi kula nyani!mi mwenyewe nishawahi kula nyani pale,watamu,wamewekewa spice kama nyama spice ya dinah bar pale usa!

tulikula pale mpaka tukajilamba ulimi,kumuuliza mpishi hii mbuzi kweli akawa anajing'atang'ata haeleweki,nilipokubali kuwa ni nyani bahati nzuri kumbe gazeti nililonunua siku hiyo liliandika habari ya mkazi wa mikumi kakamatwa na nyama na vichwa kadhaa vya nyani!nilisoma gazeti nikiwa tayari mbeya na mbuzi-nyani yule alikuwa katulia tu tumboni!

wakazi wa mikumi njooni mthibitishe habari hii!

Mimi niwapo Safarini huwa sina tabia ya kula kitu chochote zaidi ya Soda, maji na pipi.

Naogopa mambo kama haya,



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Wapi Yesu kahalalisha nguruwe ? leta aya.


Kwa mpango kama huu wa kula mbuzi kumbe ni mbwa........ ndugu yangu heri kula nyama ya nguruwe kwani akiwekwa pale jikoni juu lazima utajua tu kuwa huyu ndiye mbuzi Katoliki.


Lakini ukiagiza mbuzi meeeee lazima ukutane na kula mbwa, nyani, fisi, nk.



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Kwani Biblia inapingana ?

mahmood,mara nyingi ukizungumzia kitu cha mwenzako kana kwamba wewe unakijua zaidi kuliko mhusika unajizuia wewe mwenyewe kupata maarifa!anyway ngoja nijaribu kukuweka sawa

kwa ufupi ni kwamba-ukristo umesimama ktk agano jipya!na agano jipya linazungumzia mambo ya zamani ktk misingi inayopaswa kuwa baada ya kristo kuja!na huo ndio ukristo!

ndio maana sisi RC ktk misa au ibada yetu kuna somo la kwanza na somo la pili,yote yanaendana lakini mwisho wa siku tunasimama ktk somo la pili ambalo hutoka agano jipya!na huo ndio ukristo

na Yesu alishasema kiingiacho si najisi bali kitokacho!labda nikuulize-kipi ni bora kwako-huwa unakunywa soda,lakini ukirudi nyumbani unapiga mkeo na watoto na kila aina ya fujo,au unakunywa pombe lakini ukirudi nyumbani umtulivu na kila aina ya upendo kwa wanao na mkeo?unadhani mkeo na watoto wakikuona ktk hali hizo mbili wakaulizwa baba anywe kinywaji gani watachagua soda?
 
Leo kwenye hangaika zangu za kutwa nzima nikaamua nirudi nyumbani.
Mama watoto hakutaka nitoke hivyo basi akaniambia mechi ya Brazil Vs Mexico niiangalizie nyumbani.
Nikakaa nyumbani nikiangalia mechi mwenyewe kama jini Njabagumu.
Katikati ya mpira nikaona siinjoi chochote, nikaaga kuwa naenda kununua vocha dukani.
Nikaingia taratibi baa ya jirani, nikaagiza Serengeti moja baridi sana, nikaipiga fasta kama mwanariadha aliyetoka kumaliza marathon akutanapo na jagi la maji. Haikunitosha niaagiza ya pili, kabla haijaja mara ghafla mama watoto akapiga simu "vp darling mbona unakawia?" ndio lililokua swali lake, nikamjibu niko na mwenyekiti wa mtaa tuna mazungumzo.
Nikaagiza mbuzi, daima huwa napenda jembe (wataalam wa mbuzi wanaelewa ninachokiongea). Baada ya nusu saa ikawa mezani.
Nikapiga kama vipande kumi, nikaagiza Serengeti nyingine ya baridi.
Nikiwa katikati ya zoezi la pombe nyama, mara wakaingia Polisi wakiwa na sare zao na kuelekea jikoni.
Huko wakawaweka chini ya ulinzi watumishi wote na kufanya msako mkali. Jikoni vimekamatwa vichwa viwili vya mbwa na ngozi mbili.
Na t ayari mie nsha kula huyu kiumbe mlinzi jamani.
KUlia nataka, kucheka nataka, najitapisha sitapiki.
Kuweni makini wenzangu, yasije kuwakuta yaliyonikuta.

Tunaomba ututajie jina la baa hiyo ili watu waijue wasilishwe mbwa tena.
 
Nyama ni nyama tu, hamna shida yeyote.Asia nyama ya mbwa mbona ni delicacy.Na kabla hujajua mbona uli-enjoy?

Si kweli.

Kama kweli Nyama ni nyama tu, hamna shida yeyote! Kula nyama ya mtu basi.
 

Nakupa Pole kwa sababbu unahofu ya kula nyama ya Mbwa.

Lakini hiyo ni nyama kama ilivyo mbuzi, kwani watani zangu kutoka IRINGA MBONA WANAKULA, Na angalia Wahehe jinsi walivyo kuwa na afya.

NYAMA NYAMA NYAMA..... NYAMA ya MBWA...NYAMA.....



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!

Mimi niwapo Safarini huwa sina tabia ya kula kitu chochote zaidi ya Soda, maji na pipi.

Naogopa mambo kama haya,



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!

Rafiki, Mbona maneno yako yanapingana ?
 
mahmood,mara nyingi ukizungumzia kitu cha mwenzako kana kwamba wewe unakijua zaidi kuliko mhusika unajizuia wewe mwenyewe kupata maarifa!anyway ngoja nijaribu kukuweka sawa

kwa ufupi ni kwamba-ukristo umesimama ktk agano jipya!na agano jipya linazungumzia mambo ya zamani ktk misingi inayopaswa kuwa baada ya kristo kuja!na huo ndio ukristo!

ndio maana sisi RC ktk misa au ibada yetu kuna somo la kwanza na somo la pili,yote yanaendana lakini mwisho wa siku tunasimama ktk somo la pili ambalo hutoka agano jipya!na huo ndio ukristo

Rafiki Mc Tilly Chizenga,

Soma hapo chini kisha tufafanulie.

Yesu Mwenyewe anasema katika mathayo 5:17-19.

17``Msidhani kwamba nimekuja kufuta sheria ya Musa na mafundisho ya manabii. kwamba mpaka mbingu na dunia zitaka potoweka, hakuna hata herufi moja ya sheria itakayopotea mpaka shabaha yake ikamilike.

19 Kwa hiyo ye yote atakayelegeza hata mojawapo ya amri ndogo kuliko amri zote na akawafundisha wengine kufanya hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika Ufalme wa mbinguni. Sikuja kuzifuta bali kuzitimiza.

18 Kwa maana ninawaambia hakika Lakini atakayetii amri hizi na kuwafundisha wengine kuzitii ataitwa mkuu katika Ufalme wa mbinguni.

Luka 24:44

44 Akawaambia, ``Haya ndiyo mambo niliyowaambia nilipokuwa pamoja nanyi; kwamba yote yaliyoandikwa kunihusu mimi katika sheria ya Musa, katika Maandiko ya manabii na Zaburi hayana budi kutimizwa.


na Yesu alishasema kiingiacho si najisi bali kitokacho!labda nikuulize-kipi ni bora kwako-huwa unakunywa soda,lakini ukirudi nyumbani unapiga mkeo na watoto na kila aina ya fujo,au unakunywa pombe lakini ukirudi nyumbani umtulivu na kila aina ya upendo kwa wanao na mkeo?unadhani mkeo na watoto wakikuona ktk hali hizo mbili wakaulizwa baba anywe kinywaji gani watachagua soda?


Hakuifahamu aya hiyo, maana ya aya hiyo ni hii kula chakula bila kunawa mikono hakumtii mtu najisi. (si kula nguruwe ni halali, kula nguruwe ni haramu kabisa, Biblia inasema hivyo kwa lugha safi kabisa Mambo ya Walawi 11:07-08)

Soma aya hizo za Biblia vizuri (Matayo 15:1-20)

1 Kisha Mafarisayo na walimu wa Sheria wakafika kutoka Yerusalemu, wakamwendea Yesu, wakamwuliza, 2 Kwa nini wanafunzi wako hawajali mapokeo tuliyopokea kutoka kwa wazee wetu? Hawanawi mikono yao kama ipasavyo kabla ya kula! 3 Yesu akawajibu, "Kwa nini nanyi mnapendelea mapokeo yenu wenyewe na hamuijali Sheria ya Mungu? 4 Mungu amesema: Waheshimu baba yako na mama yako, na Anayemkashifu baba yake au mama yake, lazima auawe. 5 Lakini ninyi mwafundisha ati mtu akiwa na kitu ambacho angeweza kuwasaidia nacho baba au mama yake, lakini akasema: Kitu hiki nimemtolea Mungu, 6 basi, hapaswi tena kumheshimu baba yake! Ndivyo mnavyodharau neno la Mungu kwa kufuata mafundisho yenu wenyewe. 7 Enyi wanafiki! Isaya alitabiri sawa kabisa juu yenu: 8 Watu hawa, asema Mungu, huniheshimu kwa maneno tu, lakini mioyoni mwao wako mbali nami.
9 Kuniabudu kwao hakufai, maana mambo wanayofundisha ni maagizo ya kibinadamu tu."
10 Yesu aliuita ule umati wa watu, akawaambia, "Sikilizeni na muelewe! 11 Kitu kinachomtia mtu najisi si kile kiingiacho kinywani, bali kile kitokacho kinywani. Hicho ndicho kimtiacho mtu najisi."
12 Kisha wanafunzi wakamwendea, wakamwambia, "Je, unajua kwamba Mafarisayo walichukizwa waliposikia maneno yako?" 13 Lakini yeye akawajibu, "Kila mmea ambao Baba yangu aliye mbinguni hakuupanda, utang'olewa. 14 Waacheni wenyewe! Wao ni vipofu, viongozi wa vipofu; na kipofu akimwongoza kipofu, wote wawili hutumbukia shimoni."
15 Petro akadakia, "Tufafanulie huo mfano." 16 Yesu akasema, "Hata nyinyi hamwelewi? 17 Je, hamwelewi kwamba kila kinachoingia kinywani huenda tumboni na baadaye hutupwa nje chooni? 18 Lakini yale yatokayo kinywani hutoka moyoni, na hayo ndiyo yanayomtia mtu najisi. 19 Maana moyoni hutoka mawazo maovu yanayosababisha uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushahidi wa uongo na kashfa. 20 Hayo ndiyo yanayomtia mtu najisi. Lakini kula chakula bila kunawa mikono hakumtii mtu najisi." (Matayo 15:1-20)

kula nguruwe ni haramu , Biblia inasema hivyo kwa lugha safi kabisa, Biblia inasema (katika Mambo ya Walawi 11:07-08)

Naye nguruwe ingawa anazo kwato zilizogawanyika sehemu mbili, lakini hacheui, ni najisi kwenu. Kamwe msile nyama yao wala kugusa mizoga yao, wao ni najisi kwenu.
 
mbuzi na mbwa kama wakichinjwa na wakachunwa, mikia na vichwa vikaondolewa huwezi kuona tofauti kati yao na ndio maana ma'bwana mifugo huwashauri wachinjaji wa mbuzi kuacha kuuchuna mkia au kuuondoa maana ndio uthibitisho pekee kuwa huyu anayeuzwa hapa ni mbuzi na sio mbwa, hukukuta mkia hiyo nyama achana nayo
 
Mkuu wahi ukapate tiba ya kichaa cha mbwa kabla hujaanza kubweka hapa JF. Ni hatari hiyo, wale mnaopenda kula kula baa wakati uwezo wa kununua buchani na kuandaa wenyewe mnao! Mtaisoma namba.
 
Na nguruwe je ? mbona Biblia inasema kuwa "Nguruwe ni najisi kwenu. Msiile nyama yao, wala msiiguse mizoga yao" ? Biblia inasema hivi, "Na nguruwe, kwa sababu yeye anazo kwato, ni mwenye miguu iliyopasuka kati, lakini hacheui, yeye ni najisi kwenu. Msiile nyama yao, wala msiiguse mizoga yao; hao ni najisi kwenu." (Mambo ya Walawi 11:07-08)
mahmood, Mungu amefanya kazi na watu wengi na kwa namna nyingi. kabla ya walawi, alikuwepo adamu, na baadaye NUHU. NUHU aliambia kila mmea wa kondeni itakuwa mboga kwenu, na kila kitambaacho kilcho hai kitakuwa nyama/chakula chenu. hapo hajabagua nini cha kula na nini cha kuacha. Ukija kwa walawi, walawi walikuwa ni watu walioteuliwa na MUNGU kwa kazi maalum ya kulihudumia hekalu. sasa ili kuwatenga na jamii nyingine, walipewa sheria ya kutokula baadhi ya wanyama. Lakini sheria hiyo, haikuwahusu watu wengine. kwa mfano, wakati walawi walikuwa hawali, wayuda, wabenyamini, waisrael(yakobo) hawakukatazwa kutumia kitu hiyo ispokuwa walawi tu. sasa wewe mahmood, unakataa kula nguruwe, wewe ni mlawi? wewe ni msukuma, mnyamwezi, mha, mnyantuzu n.k hivyo sheria hiyo haikuhusu mkuu.
 
.[/B] (si kula nguruwe ni halali, kula nguruwe ni haramu kabisa, Biblia inasema hivyo kwa lugha safi kabisa Mambo ya Walawi 11:07-08)

Soma aya hizo za Biblia vizuri (Matayo 15:1-20)
kula nguruwe ni haramu , Biblia inasema hivyo kwa lugha safi kabisa, Biblia inasema (katika Mambo ya Walawi 11:07-08)

Naye nguruwe ingawa anazo kwato zilizogawanyika sehemu mbili, lakini hacheui, ni najisi kwenu. Kamwe msile nyama yao wala kugusa mizoga yao, wao ni najisi kwenu.

mahmood, Mungu amefanya kazi na watu wengi na kwa namna nyingi. kabla ya walawi, alikuwepo adamu, na baadaye NUHU. NUHU aliambia kila mmea wa kondeni itakuwa mboga kwenu, na kila kitambaacho kilcho hai kitakuwa nyama/chakula chenu. hapo hajabagua nini cha kula na nini cha kuacha. Ukija kwa walawi, walawi walikuwa ni watu walioteuliwa na MUNGU kwa kazi maalum ya kulihudumia hekalu. sasa ili kuwatenga na jamii nyingine, walipewa sheria ya kutokula baadhi ya wanyama. Lakini sheria hiyo, haikuwahusu watu wengine. kwa mfano, wakati walawi walikuwa hawali, wayuda, wabenyamini, waisrael(yakobo) hawakukatazwa kutumia kitu hiyo ispokuwa walawi tu. sasa wewe mahmood, unakataa kula nguruwe, wewe ni mlawi? wewe ni msukuma, mnyamwezi, mha, mnyantuzu n.k hivyo sheria hiyo haikuhusu mkuu.

Ni Haswaaaaaaaaa!!!!!!!!!!!

na ndio maana siku hizi nyama ya mbuzi katoliki inatumika kama kitoweo kwa watu wa Dini zote, madhehebu yote. Si mkristo, si Muislamu wote tunakula Mbuzi Katoliki.

Tena nimeshuhudia Waislamu ni wateja wakubwa sana wa mbuzi katoliki, tunao mitaani.

Kwa wauzaji mbuzi Katoliki kipindi cha mfungo wa Mwezi Ramadhani huwa wanakosa wateja wa kutosha.


Je, unafikiri kwa nini hali hii inatokea???



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Kweli umeijua kweli, nayo kweli imekuweka huru, nawe umekuwa huru kwelikweli
mahmood, Mungu amefanya kazi na watu wengi na kwa namna nyingi. kabla ya walawi, alikuwepo adamu, na baadaye NUHU. NUHU aliambia kila mmea wa kondeni itakuwa mboga kwenu, na kila kitambaacho kilcho hai kitakuwa nyama/chakula chenu. hapo hajabagua nini cha kula na nini cha kuacha. Ukija kwa walawi, walawi walikuwa ni watu walioteuliwa na MUNGU kwa kazi maalum ya kulihudumia hekalu. sasa ili kuwatenga na jamii nyingine, walipewa sheria ya kutokula baadhi ya wanyama. Lakini sheria hiyo, haikuwahusu watu wengine. kwa mfano, wakati walawi walikuwa hawali, wayuda, wabenyamini, waisrael(yakobo) hawakukatazwa kutumia kitu hiyo ispokuwa walawi tu. sasa wewe mahmood, unakataa kula nguruwe, wewe ni mlawi? wewe ni msukuma, mnyamwezi, mha, mnyantuzu n.k hivyo sheria hiyo haikuhusu mkuu.
 
Sisi ngamia twala, twapiga dua hadi mwenyewe anaelekea kibla
inawezekana kwa vile @Madela Wa- Madilu kaandika lugha ya malkia hamjamuelewa: acha ninukuu kwa kiswahili halafu mjibu hili swali:

Walawi 11:4-5
msile ngamia, kwani hucheua lakini kwato zake hazikugawanyika sehemu mbili. kwenu huyo ni najisi.
 
Kama Toka umekula bado upo hai basi na mimi ntajaribu kuionja unawezakuta tunakosa vitu vitamu duniani.kitu cha Wuuuuuwuuuuu
 

Similar Discussions

12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom