Nimekipata Kigori,wenye wivu jinyongeni,

Magulumangu

JF-Expert Member
Jan 7, 2010
3,047
452
Hayawi yawi jamani,mwenzenu nimeopoa,
Ndoto ile singizini,kamwe sijapata doa,
Kipenzi wangu mwandani,ya maisha pingu ndoa,
Nimekipata Kigori,Wenye wivu jinyongeni,

Upepo wa baharini,mawimbi kutuimbia,
ufukweni kigamboni,ndiko tulikotulia,
Hii ni hanemooni,kithungu sikilizia,
Nimekipata kigori, wenye wivu jinyongeni,

Sitaki ushakudaku,mwenyewe natoa onyo,
Shuga mami marufuku,utulie wangu moyo,
Toa yangu dukuduku,asali wangu wa moyo,
Nimekipata kigori,wenye wivu jinyongeni,

Umbo lake namba nane,kipotabo nasifia,
Kama kizazi cha nne,watengenezaji nokia,
Kiamshe wa manane,uzuri sio fifia,
Nimekipata kigori,wenye wivu jinyongeni,

Brand nimefungua,bado kuchakachuliwa,
Fyuzi hazijaungua,kitu tight muruwa,
Msukuma si mzigua,pongezi kwako mtawa,
Nimekipata Kigori,wenye wivu jinyongeni,

Hata da yetu Saida,kisha toa hili onyo,
Usije jiita akida,kuja kuonja nyonyo,
Kwa panga bila shida,nitaja kutoa moyo,
Nimekipata kigori,wenye wivu jinyongeni,

Mwisho naishilia,mwanzo wangu kumpenda,
Ishara naashilia,mapenzi chati kupanda,
Roho kaishikilia,sitaki tena kimada,
NIPE MAMA NIPE,TUFAIDI PENZI LETU.
 
duuuuuuuhhh
kumbe hata kwenye hii idara umekamilika hahaha lol
:amen::amen:
 
duuuuuuuhhh
kumbe hata kwenye hii idara umekamilika hahaha lol
:amen::amen:

Wengi walinisuta,wakidhania mi sifai,
Wangu ameniita,penzi langu bado hai,
Jina sio Mwamvita,hajatokea kandahai,
Mungu kanionyeshea,lililo penzi la kweli,

Kwenye yake macho lipo,penzi la kweli jamani,
Sio yule ndege popo,Mwanakijiji porini,
Mawimbi hata upepo,nywele zake nyumani,
Mungu kanionyeshea,lilipo penzi la kweli,

mafataki walijaribu, mafisadi kuchakachua,
lulu wamemharibu,wangu kawaumbua,
hata wetu nyani ngabu,dhahiri anatambua,
Mungu kanionyeshea,lilipo penzi la kweli,

Afrodenzi nakualika, masanilo naye mokoyo,
Rose lete gharika,judi mama wa kimoyo,
msije kuferudhika,mumuonapo wa moyo,
Mungu kanionyeshea,lilipo penzi la kweli,

Sio ki hivi hivi, magoti niliyapiga,
wazee hata wa mvi,salani walizipiga,
kafundwa sio kwa muvi,kina mama wameaga,
mungu kanionyeshea,lilipo penzi la kweli,
 
Wengi walinisuta,wakidhania mi sifai,
Wangu ameniita,penzi langu bado hai,
Jina sio Mwamvita,hajatokea kandahai,
Mungu kanionyeshea,lililo penzi la kweli,

Kwenye yake macho lipo,penzi la kweli jamani,
Sio yule ndege popo,Mwanakijiji porini,
Mawimbi hata upepo,nywele zake nyumani,
Mungu kanionyeshea,lilipo penzi la kweli,

mafataki walijaribu, mafisadi kuchakachua,
lulu wamemharibu,wangu kawaumbua,
hata wetu nyani ngabu,dhahiri anatambua,
Mungu kanionyeshea,lilipo penzi la kweli,

Afrodenzi nakualika, masanilo naye mokoyo,
Rose lete gharika,judi mama wa kimoyo,
msije kuferudhika,mumuonapo wa moyo,
Mungu kanionyeshea,lilipo penzi la kweli,


Sio ki hivi hivi, magoti niliyapiga,
wazee hata wa mvi,salani walizipiga,
kafundwa sio kwa muvi,kina mama wameaga,
mungu kanionyeshea,lilipo penzi la kweli,


Kwa kweli umebarikiwa Magulumangu wangu...
mmhhh shahiri tamu hilo..

mie itanichukua wiki kuandika shairi moja wewe umeandika
2 ndani ya nusu saaa..
ama kweli umebarikiwa..

halafu una maneno maataamuu saana..
mmhh utaniingiza pabaya/pazuri hahahh lol
mwaliko nimesha upokea na kwao nimeshafika lol
 
MAlenoga wetu asante sana vina vimetulia


kigori mzee wa kweli,desidii nakwambia,
si mtoto wa Kimweli,chapa ya ng'ombe sikia,
huwezi hata tabili,ugali akikupikia,
Walisema haliwiki,jogoo la shamba mjini,

Jogoo la shamba mjini,lisema halitawika,
uzuri kisiginoni,ile mbaya kafunika,
kwa tabia shukrani,mfano wake ni nyika,
Walisema haliwiki,jogoo la shamba mjini,

kawambia watajiju,mashambenga mashangingi,
walidhani kama mwaju,hatishiki na shilingi,
ndimu hata maukwaju,chipisi mayai tungi,
Walisema haliwiki,jogoo la shamba mjini,
 
Kwa kweli umebarikiwa Magulumangu wangu...
mmhhh shahiri tamu hilo..

mie itanichukua wiki kuandika shairi moja wewe umeandika
2 ndani ya nusu saaa..
ama kweli umebarikiwa..

halafu una maneno maataamuu saana..
mmhh utaniingiza pabaya/pazuri hahahh lol
mwaliko nimesha upokea na kwao nimeshafika lol

Sifa nampa muumba,aliemuumba kigori,
kamwe kwake sitoyumba,kama wana wa misri,
hata akina liyumba,kigori kwake makafri,
Mwaliko ukiupata,waambie na wengine,

sikutaka kuwaleti,chini wazazi wangu,
chini nao niliketi,kuhusu kigori changu,
mamangu alinileti,nijue maisha yangu,
Mwaliko ukiupata,waambie na wengine,

tabiaye sio kama,yule wa profu jei,
togwa taka boga mama,faidisha pedejei,
twanga pepeta mama,mwanamasanja jjei,
Ukiupata mwaliko,waambie na wengine,
 
Wengi walinisuta,wakidhania mi sifai,
Wangu ameniita,penzi langu bado hai,
Jina sio Mwamvita,hajatokea kandahai,
Mungu kanionyeshea,lililo penzi la kweli,

Kwenye yake macho lipo,penzi la kweli jamani,
Sio yule ndege popo,Mwanakijiji porini,
Mawimbi hata upepo,nywele zake nyumani,
Mungu kanionyeshea,lilipo penzi la kweli,

mafataki walijaribu, mafisadi kuchakachua,
lulu wamemharibu,wangu kawaumbua,
hata wetu nyani ngabu,dhahiri anatambua,
Mungu kanionyeshea,lilipo penzi la kweli,

Afrodenzi nakualika, masanilo naye mokoyo,
Rose lete gharika,judi mama wa kimoyo,
msije kuferudhika,mumuonapo wa moyo,
Mungu kanionyeshea,lilipo penzi la kweli,

Sio ki hivi hivi, magoti niliyapiga,
wazee hata wa mvi,salani walizipiga,
kafundwa sio kwa muvi,kina mama wameaga,
mungu kanionyeshea,lilipo penzi la kweli,

Loh, Safi sana kwa hizi tenzi. Kipaji maalum hicho.
 
Hayawi yawi jamani,mwenzenu nimeopoa,
Ndoto ile singizini,kamwe sijapata doa,
Kipenzi wangu mwandani,ya maisha pingu ndoa,
Nimekipata Kigori,Wenye wivu jinyongeni,

Upepo wa baharini,mawimbi kutuimbia,
ufukweni kigamboni,ndiko tulikotulia,
Hii ni hanemooni,kithungu sikilizia,
Nimekipata kigori, wenye wivu jinyongeni,

Sitaki ushakudaku,mwenyewe natoa onyo,
Shuga mami marufuku,utulie wangu moyo,
Toa yangu dukuduku,asali wangu wa moyo,
Nimekipata kigori,wenye wivu jinyongeni,

Umbo lake namba nane,kipotabo nasifia,
Kama kizazi cha nne,watengenezaji nokia,
Kiamshe wa manane,uzuri sio fifia,
Nimekipata kigori,wenye wivu jinyongeni,

Brand nimefungua,bado kuchakachuliwa,
Fyuzi hazijaungua,kitu tight muruwa,
Msukuma si mzigua,pongezi kwako mtawa,
Nimekipata Kigori,wenye wivu jinyongeni,

Hata da yetu Saida,kisha toa hili onyo,
Usije jiita akida,kuja kuonja nyonyo,
Kwa panga bila shida,nitaja kutoa moyo,
Nimekipata kigori,wenye wivu jinyongeni,

Mwisho naishilia,mwanzo wangu kumpenda,
Ishara naashilia,mapenzi chati kupanda,
Roho kaishikilia,sitaki tena kimada,
NIPE MAMA NIPE,TUFAIDI PENZI LETU.
Si utani hii kitu imetulia. Hongera sana. Hivi utunzi wa mashairi ni kipaji mtu anazaliwa nacho au naweza kujifunza na nikaweza?
 
Wengi walinisuta,wakidhania mi sifai,
Wangu ameniita,penzi langu bado hai,
Jina sio Mwamvita,hajatokea kandahai,
Mungu kanionyeshea,lililo penzi la kweli,

Kwenye yake macho lipo,penzi la kweli jamani,
Sio yule ndege popo,Mwanakijiji porini,
Mawimbi hata upepo,nywele zake nyumani,
Mungu kanionyeshea,lilipo penzi la kweli,

mafataki walijaribu, mafisadi kuchakachua,
lulu wamemharibu,wangu kawaumbua,
hata wetu nyani ngabu,dhahiri anatambua,
Mungu kanionyeshea,lilipo penzi la kweli,

Afrodenzi nakualika, masanilo naye mokoyo,
Rose lete gharika,judi mama wa kimoyo,
msije kuferudhika,mumuonapo wa moyo,
Mungu kanionyeshea,lilipo penzi la kweli,


Sio ki hivi hivi, magoti niliyapiga,
wazee hata wa mvi,salani walizipiga,
kafundwa sio kwa muvi,kina mama wameaga,
mungu kanionyeshea,lilipo penzi la kweli,

Hongera Magulumangu, heko ewe mla halwa
kufika hata uvungu, japo weye si kulwa,
wakiri heri za Mungu, kupata binti wamalwa,
Sasa muweke nyumbani, upate heri za Mungu

nilipokagua vina, mizani sikudharau,
kuona langu jina, Judi hukusahau,
yamoyo kufanya kina, katika yako nahau,
Sasa muweke nyumbani, upate heri za Mungu

Heko kupata kigori, uwajibike kwa huba,
japo waona cha pori, yadumu hayo mahaba
bila ogopa mahari, kibebe hadi kwa baba
Sasa muweke nyumbani, upate heri za Mungu

nimekubali mwaliko, harusiyo kujongea,
bila kusahau mwiko, wifi yetu mchongea,
siku afikapo kwako, apate kuyawezea
Sasa muweke nyumbani, upate heri za Mungu
 
Hayawi yawi jamani,mwenzenu nimeopoa,
Ndoto ile singizini,kamwe sijapata doa,
Kipenzi wangu mwandani,ya maisha pingu ndoa,
Nimekipata Kigori,Wenye wivu jinyongeni,

Upepo wa baharini,mawimbi kutuimbia,
ufukweni kigamboni,ndiko tulikotulia,
Hii ni hanemooni,kithungu sikilizia,
Nimekipata kigori, wenye wivu jinyongeni,

Sitaki ushakudaku,mwenyewe natoa onyo,
Shuga mami marufuku,utulie wangu moyo,
Toa yangu dukuduku,asali wangu wa moyo,
Nimekipata kigori,wenye wivu jinyongeni,

Umbo lake namba nane,kipotabo nasifia,
Kama kizazi cha nne,watengenezaji nokia,
Kiamshe wa manane,uzuri sio fifia,
Nimekipata kigori,wenye wivu jinyongeni,

Brand nimefungua,bado kuchakachuliwa,
Fyuzi hazijaungua,kitu tight muruwa,
Msukuma si mzigua,pongezi kwako mtawa,
Nimekipata Kigori,wenye wivu jinyongeni,

Hata da yetu Saida,kisha toa hili onyo,
Usije jiita akida,kuja kuonja nyonyo,
Kwa panga bila shida,nitaja kutoa moyo,
Nimekipata kigori,wenye wivu jinyongeni,

Mwisho naishilia,mwanzo wangu kumpenda,
Ishara naashilia,mapenzi chati kupanda,
Roho kaishikilia,sitaki tena kimada,
NIPE MAMA NIPE,TUFAIDI PENZI LETU.


Owa s'andame hadaa, moyo ukahadaiwa
Owa anaye kufaa, mke mwenye kusifiwa
Owa upate kuzaa, kama ulivyozaliwa
Owa ukijaaliwa, mupendane na mkeo

Owa aliye na kheri, muandamane kwa dini
Owa yai la johari, litiye nuru nyumbani
Owa mdomo mzuri, ukupambie lisani
Owa ungiye nyumbani, mupendane na mkeo


Owa moyo wa imani, usozumbua mafuja
Owa usiowe duni, anayeitwa kioja
Owa mtenda wa dini, ndiye mke mwenye haja
Owa utungiwe koja, mupendane na mkeo

Owa siowe tambara, linukiyalo vibaya
Owa mwanamke jura, mlekeze njema ndia
Owa usiowe sura, kutaka kuzangaliya
Owa mzuri tabiya, mupendane na mkeo

Owa kijana kitoto, mteshi wa kutekeya
Owa akwandike jito, mwenye kukuhurumiya
Owa usiowe zito, jabali likakwemeya
Owa aliye na haya, mupendane na mkeo

Owa s'andame uhuni, upate juwa kuzawa
Owa nami natamani, ela sijajaaliwa
Owa utiye chandani, pete uloiteuwa
Owa ujuwe kuowa, mupendane na mkeo

Owa uvishwe kilemba, na joho na mahazamu
Owa wapate kupamba, ukale twiba na tamu
Owa upambiwe chumba, upate tanganya damu
Owa usijidhulumu, mupendane na mkeo

Owa kinda la tausi, alo nadhifu mibele
Owa kiini cheusi, chendacho nyuma na mbele
Owa siowe tetesi, apaye watu uwele
Owa aliye lekele, mupendane na mkeo

Owa ualike watu, wahudhuriye arusi
Owa nawe uwe mtu, mkeo simnakisi
Owa muonyane utu, mukae mutaanasi
Owa mupane mepesi, mupendane na mkeo

Owa akukubaliye, akuizao siowe
Owa upendane naye, zamani sizo ujuwe
Owa akuridhiyae, mujikubali wenyewe
Owa mukae mutuwe, mupendane na mkeo

Owa chenye asimini, kikuba cha asiliya
Owa kilo na rihani, na waridi maridhiya
Owa kilicho na shani, na manukato kutiya
Owa ujuwe duniya, mupendane na mkeo

Owa utukuze cheo, na jina lipate kuwa
Owa apate mkeo, aambiwe meolewa
Owa kama waowao, moyo usiliye ngowa
Owa ujuwe kukuwa, mupendane na mkeo.

 
Sifa nampa muumba,aliemuumba kigori,
kamwe kwake sitoyumba,kama wana wa misri,
hata akina liyumba,kigori kwake makafri,
Mwaliko ukiupata,waambie na wengine,

sikutaka kuwaleti,chini wazazi wangu,
chini nao niliketi,kuhusu kigori changu,
mamangu alinileti,nijue maisha yangu,
Mwaliko ukiupata,waambie na wengine,

tabiaye sio kama,yule wa profu jei,
togwa taka boga mama,faidisha pedejei,
twanga pepeta mama,mwanamasanja jjei,
Ukiupata mwaliko,waambie na wengine,

Kwa kweli nime kukubali ..
nakuvulia kofia...
 
Hongera Magulumangu, heko ewe mla halwa
kufika hata uvungu, japo weye si kulwa,
wakiri heri za Mungu, kupata binti wamalwa,
Sasa muweke nyumbani, upate heri za Mungu

nilipokagua vina, mizani sikudharau,
kuona langu jina, Judi hukusahau,
yamoyo kufanya kina, katika yako nahau,
Sasa muweke nyumbani, upate heri za Mungu

Heko kupata kigori, uwajibike kwa huba,
japo waona cha pori, yadumu hayo mahaba
bila ogopa mahari, kibebe hadi kwa baba
Sasa muweke nyumbani, upate heri za Mungu

nimekubali mwaliko, harusiyo kujongea,
bila kusahau mwiko, wifi yetu mchongea,
siku afikapo kwako, apate kuyawezea
Sasa muweke nyumbani, upate heri za Mungu


duuuhh
asante mwaya
nafurahi kuona na we unawakilisha ...
 
Owa s'andame hadaa, moyo ukahadaiwa
Owa anaye kufaa, mke mwenye kusifiwa
Owa upate kuzaa, kama ulivyozaliwa
Owa ukijaaliwa, mupendane na mkeo

Owa aliye na kheri, muandamane kwa dini
Owa yai la johari, litiye nuru nyumbani
Owa mdomo mzuri, ukupambie lisani
Owa ungiye nyumbani, mupendane na mkeo


Owa moyo wa imani, usozumbua mafuja
Owa usiowe duni, anayeitwa kioja
Owa mtenda wa dini, ndiye mke mwenye haja
Owa utungiwe koja, mupendane na mkeo

Owa siowe tambara, linukiyalo vibaya
Owa mwanamke jura, mlekeze njema ndia
Owa usiowe sura, kutaka kuzangaliya
Owa mzuri tabiya, mupendane na mkeo

Owa kijana kitoto, mteshi wa kutekeya
Owa akwandike jito, mwenye kukuhurumiya
Owa usiowe zito, jabali likakwemeya
Owa aliye na haya, mupendane na mkeo

Owa s'andame uhuni, upate juwa kuzawa
Owa nami natamani, ela sijajaaliwa
Owa utiye chandani, pete uloiteuwa
Owa ujuwe kuowa, mupendane na mkeo

Owa uvishwe kilemba, na joho na mahazamu
Owa wapate kupamba, ukale twiba na tamu
Owa upambiwe chumba, upate tanganya damu
Owa usijidhulumu, mupendane na mkeo

Owa kinda la tausi, alo nadhifu mibele
Owa kiini cheusi, chendacho nyuma na mbele
Owa siowe tetesi, apaye watu uwele
Owa aliye lekele, mupendane na mkeo

Owa ualike watu, wahudhuriye arusi
Owa nawe uwe mtu, mkeo simnakisi
Owa muonyane utu, mukae mutaanasi
Owa mupane mepesi, mupendane na mkeo

Owa akukubaliye, akuizao siowe
Owa upendane naye, zamani sizo ujuwe
Owa akuridhiyae, mujikubali wenyewe
Owa mukae mutuwe, mupendane na mkeo

Owa chenye asimini, kikuba cha asiliya
Owa kilo na rihani, na waridi maridhiya
Owa kilicho na shani, na manukato kutiya
Owa ujuwe duniya, mupendane na mkeo

Owa utukuze cheo, na jina lipate kuwa
Owa apate mkeo, aambiwe meolewa
Owa kama waowao, moyo usiliye ngowa
Owa ujuwe kukuwa, mupendane na mkeo.



Daahhh
hii kali mkuu
kwa kweli nimeipenda
duuhh kipaji mnacho .. namzidi kuongezewa..
 
Magulumangu nakupongeza
Kigori wewe kumpata
Najua mimi ulikopita
Wivu mi ninao,kujinyonga sijinyongi!!

Kila la kheri nakutakia
Furaha katika ndoa
Watoto nao kupata
Wivu mi ninao kujinyonga sijinyongi

Changamoto kwenye ndoa
Ni sehemu ya maisha
Uvumulivu uwe nao pia
Wivu mi ninao kujinyonga sijinyongi
 
duuuhh
asante mwaya
nafurahi kuona na we unawakilisha ...

dada Afrodenzi, asante kwa kunisoma,
nashukuru kwa kunienzi, vilevile kunipima,
japo sitoshi konzi, hukuninyima alama
asante kwayo mapenzi, yadumu enzi na enzi

yule mtoa posa, alikuja na mizani,
akatujuza mkasa, aloufumba vinani,
akakifunga kitasa, cha shairi tusighani
asante kwayo mapenzi, yadumu enzi na enzi

Mwenyezi katukirimu, shairi kulithubutu,
japo sinayo elimu, nimeushinda ubutu,
pamoja naye hirimu, sijekuwa mtukutu
asante kwayo mapenzi, yadumu enzi na enzi

bwa harusi ndiye nguli, wa mashairi na vibonzo,
mie kama kibakuli, yeye kwangu kisonzo,
mengi yake maakuli, ya kale kama maganzo,
asante kwayo mapenzi, yadumu enzi na enzi
 
dada Afrodenzi, asante kwa kunisoma,
nashukuru kwa kunienzi, vilevile kunipima,
japo sitoshi konzi, hukuninyima alama
asante kwayo mapenzi, yadumu enzi na enzi

yule mtoa posa, alikuja na mizani,
akatujuza mkasa, aloufumba vinani,
akakifunga kitasa, cha shairi tusighani
asante kwayo mapenzi, yadumu enzi na enzi

Mwenyezi katukirimu, shairi kulithubutu,
japo sinayo elimu, nimeushinda ubutu,
pamoja naye hirimu, sijekuwa mtukutu
asante kwayo mapenzi, yadumu enzi na enzi

bwa harusi ndiye nguli, wa mashairi na vibonzo,
mie kama kibakuli, yeye kwangu kisonzo,
mengi yake maakuli, ya kale kama maganzo,
asante kwayo mapenzi, yadumu enzi na enzi


Hii nai print out..

kwa kweli nakupa heshma sana..
na uzidi kubarikiwa dear..
mtu smart anajulikana kwa asemayo..
i consider your one of them..
God Bless..
 
Hii nai print out..

kwa kweli nakupa heshma sana..
na uzidi kubarikiwa dear..
mtu smart anajulikana kwa asemayo..
i consider your one of them..
God Bless..

haha, nilikuwa najaribu tu mpenzi. asante kwa kunitia moyo. ubarikiwe sana mpenzi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom