HorsePower
JF-Expert Member
- Aug 22, 2008
- 3,612
- 2,566
Jamani mwenzenu ninafanya kazi kwenye ofisi moja hapa DSM. Kwa Bahati nzuri au mbaya, niko ofisi moja na my wife, lakini kwenye idara tofauti.
Nimezoeana na wadada kadhaa wa hapa ofisini husasan wa idara moja nami, utani na maneno ya hapa na pale mara nyingi huwatawala ofisi yetu! Asubuhi alikuja dada mmoja ambaye huwa tumezoea kutaniana tu Kamwe hatuna mahusiano yoyote aliniletea mafaili ya kufanyia kazi. Nilipomuangalia nikagundua kuwa kwa bahati mbaya alijichafua na vumbi kwenye kiti alichokalia huko ofisini kwake, na nilipogundua nikamfahamisha kuwa amechafuka. Alinirushia leso yake, akiomba nimfute, nami bila hiyana nikamfuta vumbi.
Wakati zoezi likiendelea wife akaingia na mafaili mengine kunipitishia, na kunikuta nikimalizia kumfuta dada huyu. Kwa kuona hivi, wife kaja juu kwa nini nimfute dada maeneo hayo kama kweli sina uhusiano wowote naye na limezuka zogo kubwa nyumbani kwangu.
Jamani, hivi ni kosa kumfuta mtu vumbi? Au ndo nimejiletea balaa mwenyewe?
Naomba ushauri, mahusiano ya ndoa yangu yameingia doa!
**** Kuna ndugu alituma malezo haya kuniomba ushauri, nami nimeamua kuwaletea kama ilivyo, kwa pamoja tumshauri ndugu yetu. *****
Wenu,
HP
Nimezoeana na wadada kadhaa wa hapa ofisini husasan wa idara moja nami, utani na maneno ya hapa na pale mara nyingi huwatawala ofisi yetu! Asubuhi alikuja dada mmoja ambaye huwa tumezoea kutaniana tu Kamwe hatuna mahusiano yoyote aliniletea mafaili ya kufanyia kazi. Nilipomuangalia nikagundua kuwa kwa bahati mbaya alijichafua na vumbi kwenye kiti alichokalia huko ofisini kwake, na nilipogundua nikamfahamisha kuwa amechafuka. Alinirushia leso yake, akiomba nimfute, nami bila hiyana nikamfuta vumbi.
Wakati zoezi likiendelea wife akaingia na mafaili mengine kunipitishia, na kunikuta nikimalizia kumfuta dada huyu. Kwa kuona hivi, wife kaja juu kwa nini nimfute dada maeneo hayo kama kweli sina uhusiano wowote naye na limezuka zogo kubwa nyumbani kwangu.
Jamani, hivi ni kosa kumfuta mtu vumbi? Au ndo nimejiletea balaa mwenyewe?
Naomba ushauri, mahusiano ya ndoa yangu yameingia doa!
**** Kuna ndugu alituma malezo haya kuniomba ushauri, nami nimeamua kuwaletea kama ilivyo, kwa pamoja tumshauri ndugu yetu. *****
Wenu,
HP