Nimejichubua,je kuna dawa ya kurudisha ngozi ya zamani?

Boflo

JF-Expert Member
Jan 20, 2010
4,384
4,409
Wana JF Huyu Mdada an serious problem.....mnaweza kumsaidiaje?

Habari zenu

Mimi nina miaka 31, na mwaka 2000 baada ya kutoka tanzania na ngozi yangu asili (originol) ambayo ilikuwa ni nyeusi na ya kun'gaa, marafiki zangu hapa texas, walinishawishi niwe mweupe ili nami ning'ae. basi nikapata vidonge vya kungarisha mwili, yaani kuwa mweupe.

Na kusema kweli, nilibadilika ngozi, nikawa mweupe sana, na siyo rahisi mtu kujua kama kweli nimetumia madawa, isipokuwa walionifahamu tangu utotoni ndio wanaoshangaa uweupe huu nimeutoa wapi.

Sasa nilipataga mimba, ambayo ilikuja kutoka, ila sikujua tatizo ni nini. Hapa majuzi tena, nikashika mimba ya pili bahati mbaya mtoto kafa (yaani mimba imeharibika) nilienda kwa dakitari kutaka kujua tatito liko wapi, hapo ndo nikaambiwa kwamba kuna chemicals kwenye mwili wangu ambazo ndio chanzo cha watoto wangu kufa.

Nimeambiwa kwamba hayo madini ni mengi mno, na nisipoangalia nitakufa na cancer ambayo inaweza kuanza muda wowote. suluhisho linaweza kupatikana nikisafisha damu, na uwezo huo sina, au kama naweza kurudisha ngozi yangu ya zamani kwa sababu sasa hivi ngozi yangu haina kinga tena.

Sisikitikii weupe, kwa maana nikitu ambacho nilikitamani sana, kwa hiyo mzigo lazima niubebe, ombi langu ni ushauri wa kuweza kutoa hizi kemikali mwilini mwangu.kama ni kufa basi tena. cha ajabu ni kwamba mchumba wangu ametishia kuniacha kwani siwezi kuzaa tena. yaani sasa hivi analala nje full, naumia lakini sina jinsi..... naombeni ushauri wenu, niko njia panda

mdau, texas usa
 
Aroo.....hii kali sana, sasa kwa nini hukuomba ushauri kabla ya kujichubua???? tusubiri wada wakupe ushauri,
maji yameshamwagika, sijui kama yatazoleka!!!
 
Wana JF Huyu Mdada an serious problem.....mnaweza kumsaidiaje??????

Habari zenu

Mimi nina miaka 31, na mwaka 2000 baada ya kutoka tanzania na ngozi yangu asili (originol) ambayo ilikuwa ni nyeusi na ya kun'gaa, marafiki zangu hapa texas, walinishawishi niwe mweupe ili nami ning'ae. basi nikapata vidonge vya kungarisha mwili, yaani kuwa mweupe. Na kusema kweli, nilibadilika ngozi, nikawa mweupe sana, na siyo rahisi mtu kujua kama kweli nimetumia madawa, isipokuwa walionifahamu tangu utotoni ndio wanaoshangaa uweupe huu nimeutoa wapi. Sasa nilipataga mimba, ambayo ilikuja kutoka, ila sikujua tatizo ni nini. Hapa majuzi tena, nikashika mimba ya pili bahati mbaya mtoto kafa (yaani mimba imeharibika) nilienda kwa dakitari kutaka kujua tatito liko wapi, hapo ndo nikaambiwa kwamba kuna chemicals kwenye mwili wangu ambazo ndio chanzo cha watoto wangu kufa.
nimeambiwa kwamba hayo madini ni mengi mno, na nisipoangalia nitakufa na cancer ambayo inaweza kuanza muda wowote. suluhisho linaweza kupatikana nikisafisha damu, na uwezo huo sina, au kama naweza kurudisha ngozi yangu ya zamani kwa sababu sasa hivi ngozi yangu haina kinga tena. Sisikitikii weupe, kwa maana nikitu ambacho nilikitamani sana, kwa hiyo mzigo lazima niubebe, ombi langu ni ushauri wa kuweza kutoa hizi kemikali mwilini mwangu.kama ni kufa basi tena. cha ajabu ni kwamba mchumba wangu ametishia kuniacha kwani siwezi kuzaa tena. yaani sasa hivi analala nje full, naumia lakini sina jinsi..... naombeni ushauri wenu, niko njia panda

mdau, texas usa


POLE SAANA,japokuwa ni makosa umefanya kwa kujichubua.the only solution ni kusafisha hiyo damu as you hv mentioned.inaonekana huyo muenza wako hakupendi.couse hayuko kwenye shida na raha.nakushauri uonane naye huyo mwenzako na muongee ni jinsi mjipange ili muweze kusafisha damu.umueleze ukweli kuhusiana na tatizo lako.mnaweza mkajichangisha both wewe na mwenzako na mungu akawajaalia mkapata huo uwezo.mwaweza mkatafuta mdhamini.for example waweza kopa hela kazini kwako na wakukate kidogokidogo katika mshahara wako.


NAKUTAKIA KILA LA KHERI.MUNGU AKUJAALIE WEPESI KATIKA TATIZO LAKO UFANIKISHE TIBA YAKE.
Yote ni mitihani ya maisha
 
Wana JF Huyu Mdada an serious problem.....mnaweza kumsaidiaje??????

Habari zenu

Mimi nina miaka 31, na mwaka 2000 baada ya kutoka tanzania na ngozi yangu asili (originol) ambayo ilikuwa ni nyeusi na ya kun'gaa, marafiki zangu hapa texas, walinishawishi niwe mweupe ili nami ning'ae. basi nikapata vidonge vya kungarisha mwili, yaani kuwa mweupe. Na kusema kweli, nilibadilika ngozi, nikawa mweupe sana, na siyo rahisi mtu kujua kama kweli nimetumia madawa, isipokuwa walionifahamu tangu utotoni ndio wanaoshangaa uweupe huu nimeutoa wapi. Sasa nilipataga mimba, ambayo ilikuja kutoka, ila sikujua tatizo ni nini. Hapa majuzi tena, nikashika mimba ya pili bahati mbaya mtoto kafa (yaani mimba imeharibika) nilienda kwa dakitari kutaka kujua tatito liko wapi, hapo ndo nikaambiwa kwamba kuna chemicals kwenye mwili wangu ambazo ndio chanzo cha watoto wangu kufa.
nimeambiwa kwamba hayo madini ni mengi mno, na nisipoangalia nitakufa na cancer ambayo inaweza kuanza muda wowote. suluhisho linaweza kupatikana nikisafisha damu, na uwezo huo sina, au kama naweza kurudisha ngozi yangu ya zamani kwa sababu sasa hivi ngozi yangu haina kinga tena. Sisikitikii weupe, kwa maana nikitu ambacho nilikitamani sana, kwa hiyo mzigo lazima niubebe, ombi langu ni ushauri wa kuweza kutoa hizi kemikali mwilini mwangu.kama ni kufa basi tena. cha ajabu ni kwamba mchumba wangu ametishia kuniacha kwani siwezi kuzaa tena. yaani sasa hivi analala nje full, naumia lakini sina jinsi..... naombeni ushauri wenu, niko njia panda

mdau, texas usa

Mshahara wa dhambi ni mauti, pole mrudie Muumba wako maana yeye ndo aliyeumba mwili wako, yeye aliona rangi nyeusi ndo nzuri kwako, mwombe akurudishie, pole
 
hii habari hipo humu na imefika mbali mno, MODs ziunganisha hizi nyuzi
 
Duh!hapo mwana ndo mie Mdau huwa nachoka maana ni vyema ukitaka uzuri ujue na ubaya wake!But pole sana maana yaliyokukuta ni makubwa,bt wadau wanaojua mambo watakusaidia me nakupa pole mwana!
 
BOFLO, hayo umejitakia mwenyewe. Mungu alikuumba na kukupata rangi nyeusi nzuri lakini Lucifer akaingia akilini kwako na kukudanganya kwamba weupe ndio mali. Ona inakula kwako. Mchumba amesepa, cancer inanyemelea, mtoto huna na kaburi tayari umeshachimba bado kuweka tani saba za mchanga. Mwisho wako utakuwa kama wa Michael Jackson.
 
Ungekuwa huku ningekushauri ukajaribu kwenye makanisa kama ya akina Lwakatare, Mzee wa uponyaji, Fernandes nk - wako wengi tu.
 
Dah,sina ushauri ila nimepata "darasa" kubwa sana hapa,asante na pole sana
 
Mmh, nami nampa pole naona sina hata cha kumshauri, pengine angekuwa Dar ningemwambia akaonane na akina Dr. ndodi kwa ajili ya tiba mbadala.

Hakuna kitu naogopa katika dunia hii kama kujichubua, labda nitumie kitu kwa kutokujua lakini kama najua lotion sijui nini zina chemikal hatari sithubutu. Mungu atusaidie.
 
pole sana kwa kujichubua. na nasikitika kidogo kwani hukujua kuwa unafanya kosa kubwa kuliko!!!!!!!!!! cha msingi acha mara moja na utubu kwa Mungu kwa kufanya hayo marekebisho ambayo Mungu hakukuumba nayo na uridhike na ngozi yako
 
pole sana dada!
tatizo lako ni kubwa jitahidi ubadili damu kwa gharama yeyote ili uepuke hiyo cancer,kukosa mtoto unaweza kushukuru mungu ila hilo la kancer ni hatari!jaribu kwa wachina au wahindi unaweza kupata dawa mbadala za mitimiti.
 
Habari pole sana na asante kwa kutuambia naomba uniambie dawa gani hiyo ulinunua kwa sababu na mie pia nimenunua hiyo dawa ya glutathione ivory cost vidonge nataka nile kama vinazuru hv pia naomba mniambie nitaviuzq manake hata sijafungua bado na nimesearch net kote wnasema havina side effects je nyie ndugi zangu nisaidieni mtanzania mwenzenu
 
Habari pole sana na asante kwa kutuambia naomba uniambie dawa gani hiyo ulinunua kwa sababu na mie pia nimenunua hiyo dawa ya glutathione ivory cost vidonge nataka nile kama vinazuru hv pia naomba mniambie nitaviuzq manake hata sijafungua bado na nimesearch net kote wnasema havina side effects je nyie ndugi zangu nisaidieni mtanzania mwenzenu
Vitupe chooni usiuze! Ridhika ulivyo ndugu
 
Habari pole sana na asante kwa kutuambia naomba uniambie dawa gani hiyo ulinunua kwa sababu na mie pia nimenunua hiyo dawa ya glutathione ivory cost vidonge nataka nile kama vinazuru hv pia naomba mniambie nitaviuzq manake hata sijafungua bado na nimesearch net kote wnasema havina side effects je nyie ndugi zangu nisaidieni mtanzania mwenzenu

Mkuu Unlucky una kichwa kigumu sana thread yako kule michango yote inakukataza kutumia hizo dawa zako za kuwa mweupe,sasa unataka uthibitisho gani wakati huyu mwenzako yuko US na anasema mambo ni magumu anataka arudie weusi wake.

Dawa zako tupa chooni maana utayemuuzia utamletea shida za jamaa wa US Texas. Mbona dada zetu mnatuangusha na weupe wa Shop jamani?

Nilitegema Mkuu Unlucky baada ya kusoma vzr hii thread ungebatirisha uamuzi wako lakini ajabu unauliza ikiwa havina madhara huku huyu aliyeko US mimba mbili zimetoka lakini pia inabidi damu ibadilishwe.

Usiufanye moyo wako mgumu utaumia Mkuu,sauti ya wengi ni ya Mungu.
 
Back
Top Bottom