ndetichia
JF-Expert Member
- Mar 18, 2011
- 27,772
- 6,555
Ilikuwa Nashera ya Morogoro, sasa Atriums ya Dar, sasa hotel gani yenye usalama? Hili ni doa kwa hiyo hotel.
ni elizabeth lorge pekee ndio safe..
Ilikuwa Nashera ya Morogoro, sasa Atriums ya Dar, sasa hotel gani yenye usalama? Hili ni doa kwa hiyo hotel.
shigongo huyu mwenye magazeti ya udaku..halafu jamaa kila anachoongea lazima amtaje mungu. hii ngumu kuamini.
Nilikuwa Dar Es Salaam kwa muda wa week moja, nilikaa Atriums Hotel na nikaibiwa night ya nne, niliibiwa chumbani usiku wa saa 3 wakati nikiwa restaurant nakula hapo hapo hotelini... Niliibiwa digital camera 2, na simu aina ya HTC, na pesa taslim usd 2300.., mbaya zaidi mmiliki wa hotel anaitwa Erik Shingongo alifika hapo hotelin baada ya kupigiwa sim na meneja wake ndugu Sunday nilieripoti wizi huo muda huo huo. Shigongo aliniambia kuwa anawajua wezi nimpe muda wa saa 3 atarudisha vitu vyangu, baada ya masaa 3 kupita alikuja tena akiwa na maaskari 3 toka kituo cha polis kijitonyama na wakanitaka kutoa maelezo., na wakati huo, ikiwa saa 7 usiku shigongo aliniambia kuwa tayari kesha washika wezi wanne ambao ni wafanyakazi wa hotelini hapo HIVYO nitulie nitapata mali zangu.Nimesubiri bila mafanikio, nikapewa maelekezo ya kumwona RCO wa osterbay, kamanda Wambura ambae alitoa maagizo ya kuwepo mkutano kati yangu na shigongo na meneja wake bwana sunday, mkutano ufanyike ofisin kwa rco ili tuweze kukubaliana namna ya kurudisha vitu nilivyoibiwa. Shigongo hakutokea, meneja wake alifika na akiwa amepewa na maagizo na Shigongo kuwa msimamo wa hotel ni kutolipa au kutoa fidia ya aina yeyote, kuwa wao kama hotel wanaona ilikuwa ni kosa langu kwenda hotelin ATRIUMS. na pia alisema hakuna wa kumfanya lolote Tanzania hii hata nikiripoti kwa RPC, RCO akaridhia na akaniambia hana la kufanya na sheria haimpi nafasi ya kumbana shigongo.
hiyo ndo ilikuwa final na kesi ikafungwa, Tanzania ya watanzania raia hana haki, hadi polis wanaubariki wizi na kuutetea, pale ATRIUMS ni kichaka cha kufuga wezi, mwizi namba moja akiwa Erik Shigongo. namba 2 meneja wake na namba 3 team yake ya wafanyakazi, Kuweni makini msiumie kama mimi.
Mkuu unayosema ni kweli kabisa, mtu hawezi kuibiwa hotelini kwako alafu useme hauko responsible na huo wizi. Tatizo ni kwamba nchi yetu hata mahakama imeshikwa na wenye pesa. Kama alithubutu kumwambia mteja nenda kwa RPC, hata akienda mahakamani, hao mahakimu wetu njaa hataweza kushinda kesi. Hii nchi ni yetu lakini Tanzania is more than you know it.Jamani ndugu zangu, hebu acheni kuwa watu wakusukumwa na kila mtu akiwemo huyu mkunga, kama uliibiwa nenda kaweke mwanasheria acha ubahili persue hiyo kesi hata miaka 100 people are getting away with murder, yaani unaweka na kupokea hela za wateja halafu unasema huwajibiki na wao kuibiwa hotelini kwako? hata mgeni anayetutembelea majumbani kwetu tunawajibika juu ya upotevu wa mali zao na usalama wao wakiwa ndani kwetu, kwa hiyo ukiwa hapo hotelini ukaingiliwa na kuumizwa ama kuuawa bado hutaki kuwa responsible?, hivi kweli kwa nini tuna simplify maisha yetu hivi? mnataka kuniambia kuna authority inayotoa kibali shigongo afungue hoteli lakini asiwe responsible for mali na maisha ya wateja wake? sasa hii ni hoteli ama machinjio? Nakataa kabisa hakuna mahali penye sheria kama hizi, ni sisi watanzania na upumbavu wetu kama tunaoufanya hapa tunaohalalisha ushenzi wa watu wenye vijisenti kama hivi, hebu weka wanasheria waulize, kwa hiyo hao askari hapo wanafanyanini? ama wanamlinda yeye mwenyewe na vitu vyake? tusijibweteke hela ulizoibiwa na mali ni kubwa sana weka nusu ya hizo mpeleke mahakamani hata kama anamamilioni ashughulikiwe hii haikubaliki
Nilikuwa Dar Es Salaam kwa muda wa week moja, nilikaa Atriums Hotel na nikaibiwa night ya nne, niliibiwa chumbani usiku wa saa 3 wakati nikiwa restaurant nakula hapo hapo hotelini... Niliibiwa digital camera 2, na simu aina ya HTC, na pesa taslim usd 2300.., mbaya zaidi mmiliki wa hotel anaitwa Erik Shingongo alifika hapo hotelin baada ya kupigiwa sim na meneja wake ndugu Sunday nilieripoti wizi huo muda huo huo. Shigongo aliniambia kuwa anawajua wezi nimpe muda wa saa 3 atarudisha vitu vyangu, baada ya masaa 3 kupita alikuja tena akiwa na maaskari 3 toka kituo cha polis kijitonyama na wakanitaka kutoa maelezo., na wakati huo, ikiwa saa 7 usiku shigongo aliniambia kuwa tayari kesha washika wezi wanne ambao ni wafanyakazi wa hotelini hapo HIVYO nitulie nitapata mali zangu.Nimesubiri bila mafanikio, nikapewa maelekezo ya kumwona RCO wa osterbay, kamanda Wambura ambae alitoa maagizo ya kuwepo mkutano kati yangu na shigongo na meneja wake bwana sunday, mkutano ufanyike ofisin kwa rco ili tuweze kukubaliana namna ya kurudisha vitu nilivyoibiwa. Shigongo hakutokea, meneja wake alifika na akiwa amepewa na maagizo na Shigongo kuwa msimamo wa hotel ni kutolipa au kutoa fidia ya aina yeyote, kuwa wao kama hotel wanaona ilikuwa ni kosa langu kwenda hotelin ATRIUMS. na pia alisema hakuna wa kumfanya lolote Tanzania hii hata nikiripoti kwa RPC, RCO akaridhia na akaniambia hana la kufanya na sheria haimpi nafasi ya kumbana shigongo.
hiyo ndo ilikuwa final na kesi ikafungwa, Tanzania ya watanzania raia hana haki, hadi polis wanaubariki wizi na kuutetea, pale ATRIUMS ni kichaka cha kufuga wezi, mwizi namba moja akiwa Erik Shigongo. namba 2 meneja wake na namba 3 team yake ya wafanyakazi, Kuweni makini msiumie kama mimi.
Kuna vitu huyu jamaa hasemi, naamini hoteli hiyo ni standard hotel, kuna maelekezo juu ya ku declare valuables na naamini vyumba vina safe deposits na kama havina, kuna tangazo reception kuhusu pesa ndio maana mmiliki kamtoleo nje na kama haya ni kweli, nenda popote, imekula kwako!. Pole zake kuibiwa!.Mkuu bila kutafuna maneno wewe ni mzembe! Sijapenda ulivyoibiwa ila inamaana wewe ni mara ya kwanza kulala hotel? Mbona sheria za hotel zipo wazi dunia nzima kwamba valuables tembea nazo or kabidhi reception! Wewe uliachaje chumbani ukaenda kula? Bt more so walijuaje wewe ni pedejee lazima ulionesha mazingira ya kujifanya uko njema wakakutime. Kwa hilo Shigongo humuwezi coz sheria zipo waziiii!
Kuna vitu huyu jamaa hasemi, naamini hoteli hiyo ni standard hotel, kuna maelekezo juu ya ku declare valuables na naamini vyumba vina safe deposits na kama havina, kuna tangazo reception kuhusu pesa ndio maana mmiliki kamtoleo nje na kama haya ni kweli, nenda popote, imekula kwako!. Pole zake kuibiwa!.
Hotel zote zinasema, ukiwa na vitu vya thamani, amma unaviacha reception kwa makabidhiano amma unaviweka kwenye safety box.
Jee, ulifanya hayo? hata kama kweli umeibiwa, ni uzembe wako na shigongo inamhusu nini? kataka kukusaidia mpaka saa saba za usiku kwa uzembe wako, leo yeye amekuwa mbaya?
Kwa hiyo shigongo kufanya kazi mpaka saa saba usiku ni tatizo we kinibu? Ni hoteli yake, ni kazi yake, on top of that alipromise kuifanyia kazi, what about hao wafanyakazi aliosema amewasweka ndani? Watanzania amkeni na kufanya critical analysis ya mambo, kwa hiyo mtu hata kama huna kosa ndo umtaje RPC Au IGP? kwa kosa gani? After all RPC anahusika vipi? Na ana bahati that shingo-ngoni.
shigongo huyu mwenye magazeti ya udaku..halafu jamaa kila anachoongea lazima amtaje mungu. hii ngumu kuamini.
Huyo mleta mada ni muongo.
Kwanini aweke fedha chumbani na yeye atoke? na juzi kasikia Adam Malima kaibiwa hoteli kubwa kuliko hiyo?
Asitake kutudanganya. Anajidai alikuwa na dollar, jee, alikuwa anangoja safari au karudi safari za nje?
Huyo ni mwongo na mjinga!