Nimeibiwa ATRIUMS hotel Sinza.

Eric shigongo kawaweka polisi mfukoni,ndio maana juzi kulikua na thread nyingine ya kuwazalilisha watoto
 
Adam malima -part 2
mtajuta kuyaokota mnafikiri wamekuja na jembe kulima lami
 
pole sana, huwa tunaenda hotel za gharama kubwa tukiamini kuna usalama lakini mambo yake ni kama uswahilini. Nitakuwa nalala uswahilini kwa mtindo huu
 
mkuu opp kuna mombasa guest na mlangoni wameandika sukuma hapa sijui ulikimbilia nini....atriums
 
shigongo huyu mwenye magazeti ya udaku..halafu jamaa kila anachoongea lazima amtaje mungu. hii ngumu kuamini.

Amini nawaambieni,
Sio kila atakaeniita "Bwana" atauona ufalme wa Mbinguni!!
 
Eric Shigongo is a contraversial figure so are his bussiness. I think people should be aware of his dubious dealings. Am worried that he will not only be envolved in theft but it is possible for him to fix some cameras in rooms. Alert.. stay way from this scrupulous individiual with questionable moral values.
 
Nilikuwa Dar Es Salaam kwa muda wa week moja, nilikaa Atriums Hotel na nikaibiwa night ya nne, niliibiwa chumbani usiku wa saa 3 wakati nikiwa restaurant nakula hapo hapo hotelini... Niliibiwa digital camera 2, na simu aina ya HTC, na pesa taslim usd 2300.., mbaya zaidi mmiliki wa hotel anaitwa Erik Shingongo alifika hapo hotelin baada ya kupigiwa sim na meneja wake ndugu Sunday nilieripoti wizi huo muda huo huo. Shigongo aliniambia kuwa anawajua wezi nimpe muda wa saa 3 atarudisha vitu vyangu, baada ya masaa 3 kupita alikuja tena akiwa na maaskari 3 toka kituo cha polis kijitonyama na wakanitaka kutoa maelezo., na wakati huo, ikiwa saa 7 usiku shigongo aliniambia kuwa tayari kesha washika wezi wanne ambao ni wafanyakazi wa hotelini hapo HIVYO nitulie nitapata mali zangu.Nimesubiri bila mafanikio, nikapewa maelekezo ya kumwona RCO wa osterbay, kamanda Wambura ambae alitoa maagizo ya kuwepo mkutano kati yangu na shigongo na meneja wake bwana sunday, mkutano ufanyike ofisin kwa rco ili tuweze kukubaliana namna ya kurudisha vitu nilivyoibiwa. Shigongo hakutokea, meneja wake alifika na akiwa amepewa na maagizo na Shigongo kuwa msimamo wa hotel ni kutolipa au kutoa fidia ya aina yeyote, kuwa wao kama hotel wanaona ilikuwa ni kosa langu kwenda hotelin ATRIUMS. na pia alisema hakuna wa kumfanya lolote Tanzania hii hata nikiripoti kwa RPC, RCO akaridhia na akaniambia hana la kufanya na sheria haimpi nafasi ya kumbana shigongo.
hiyo ndo ilikuwa final na kesi ikafungwa, Tanzania ya watanzania raia hana haki, hadi polis wanaubariki wizi na kuutetea, pale ATRIUMS ni kichaka cha kufuga wezi, mwizi namba moja akiwa Erik Shigongo. namba 2 meneja wake na namba 3 team yake ya wafanyakazi, Kuweni makini msiumie kama mimi.

Pole sana mkuu nimeumia sana na najua ulikuwa na mipango yako.mungu alikuwezesha kuwa na mali hizo atafanya maarifa mengine na utapata zaidi ya hapo.
Kwako Shigongo mfanyabiashara mkubwa na mwanajf mwenzetu.tunaomba ufanye juu chini uweze kumsaidia mwenzetu apate mali zake na uonyeshe moyo wa huruma manake naye anaumia sana.

Usipofanya juhudi na kuja na report inayoeleweka wanajf wote tutagoma kuja Artumas.wee haya wee
 
Jamani ndugu zangu, hebu acheni kuwa watu wakusukumwa na kila mtu akiwemo huyu mkunga, kama uliibiwa nenda kaweke mwanasheria acha ubahili persue hiyo kesi hata miaka 100 people are getting away with murder, yaani unaweka na kupokea hela za wateja halafu unasema huwajibiki na wao kuibiwa hotelini kwako? hata mgeni anayetutembelea majumbani kwetu tunawajibika juu ya upotevu wa mali zao na usalama wao wakiwa ndani kwetu, kwa hiyo ukiwa hapo hotelini ukaingiliwa na kuumizwa ama kuuawa bado hutaki kuwa responsible?, hivi kweli kwa nini tuna simplify maisha yetu hivi? mnataka kuniambia kuna authority inayotoa kibali shigongo afungue hoteli lakini asiwe responsible for mali na maisha ya wateja wake? sasa hii ni hoteli ama machinjio? Nakataa kabisa hakuna mahali penye sheria kama hizi, ni sisi watanzania na upumbavu wetu kama tunaoufanya hapa tunaohalalisha ushenzi wa watu wenye vijisenti kama hivi, hebu weka wanasheria waulize, kwa hiyo hao askari hapo wanafanyanini? ama wanamlinda yeye mwenyewe na vitu vyake? tusijibweteke hela ulizoibiwa na mali ni kubwa sana weka nusu ya hizo mpeleke mahakamani hata kama anamamilioni ashughulikiwe hii haikubaliki
Mkuu unayosema ni kweli kabisa, mtu hawezi kuibiwa hotelini kwako alafu useme hauko responsible na huo wizi. Tatizo ni kwamba nchi yetu hata mahakama imeshikwa na wenye pesa. Kama alithubutu kumwambia mteja nenda kwa RPC, hata akienda mahakamani, hao mahakimu wetu njaa hataweza kushinda kesi. Hii nchi ni yetu lakini Tanzania is more than you know it.
 
Guys mmewahi kujua service za pale au mnamkashifu mleta mada? Mie napajua vizuri labda nianze na hili; mkiwa na meeting hata watu wawili na mkakaa meza mkionekana mpo kikazi mnalipishwa elfu hamsini. Na hawauzi bia pale, nawashangaa wanaoongea blah blah, ni sehemu ya kijinga sana na hakuna service ya maana ila shigongo na yule msela wake james lazima waende pale, wapuuzi sana, kama amesema hivyo na rco kasema hivyo we fungua kesi, wala usijali. Asikutishe yule mlokole feki, na wala usiogope mpuuzi sana, watu wataanzisha tabloid sababu ya upuuzi wake na uc- c? Em wake wa kujificha. Kuna mengi yamejificha wala asikupe pressure huyu she-gongo! Kumjua RPC AU IGP sio ishu! We mpe kubwa tu na watu wapo wanakusubiri uamue mwenyewe. Huyo ni tembe ya haradai.
 
Kwa hiyo yeye kuwa dinner na IGP au kukutana na RPC kwenye ocassion flani kumekuwa shida? Anakuwa mpu. Uzi sasa, huyu huyu mzee wa street university na yule bwanake james? Mfungulie kesi, nadhani kalewa vihela mbuzi, mpe kesi na tuone hao ma-RPC wake na ma-IGP! Even mawaziri, i did expect a lot from him but not this, ukiacha yaliyonikuta pale atriums!
 
inasikitisha sana! Ila kama japo unaamini uwepo wa Mungu basi amini pia utalipa kwa aibu na kudhalilika zaidi! Mkuu fungua kesi utashinda kirahisi tu!
 
Nilikuwa Dar Es Salaam kwa muda wa week moja, nilikaa Atriums Hotel na nikaibiwa night ya nne, niliibiwa chumbani usiku wa saa 3 wakati nikiwa restaurant nakula hapo hapo hotelini... Niliibiwa digital camera 2, na simu aina ya HTC, na pesa taslim usd 2300.., mbaya zaidi mmiliki wa hotel anaitwa Erik Shingongo alifika hapo hotelin baada ya kupigiwa sim na meneja wake ndugu Sunday nilieripoti wizi huo muda huo huo. Shigongo aliniambia kuwa anawajua wezi nimpe muda wa saa 3 atarudisha vitu vyangu, baada ya masaa 3 kupita alikuja tena akiwa na maaskari 3 toka kituo cha polis kijitonyama na wakanitaka kutoa maelezo., na wakati huo, ikiwa saa 7 usiku shigongo aliniambia kuwa tayari kesha washika wezi wanne ambao ni wafanyakazi wa hotelini hapo HIVYO nitulie nitapata mali zangu.Nimesubiri bila mafanikio, nikapewa maelekezo ya kumwona RCO wa osterbay, kamanda Wambura ambae alitoa maagizo ya kuwepo mkutano kati yangu na shigongo na meneja wake bwana sunday, mkutano ufanyike ofisin kwa rco ili tuweze kukubaliana namna ya kurudisha vitu nilivyoibiwa. Shigongo hakutokea, meneja wake alifika na akiwa amepewa na maagizo na Shigongo kuwa msimamo wa hotel ni kutolipa au kutoa fidia ya aina yeyote, kuwa wao kama hotel wanaona ilikuwa ni kosa langu kwenda hotelin ATRIUMS. na pia alisema hakuna wa kumfanya lolote Tanzania hii hata nikiripoti kwa RPC, RCO akaridhia na akaniambia hana la kufanya na sheria haimpi nafasi ya kumbana shigongo.
hiyo ndo ilikuwa final na kesi ikafungwa, Tanzania ya watanzania raia hana haki, hadi polis wanaubariki wizi na kuutetea, pale ATRIUMS ni kichaka cha kufuga wezi, mwizi namba moja akiwa Erik Shigongo. namba 2 meneja wake na namba 3 team yake ya wafanyakazi, Kuweni makini msiumie kama mimi.

Hotel zote zinasema, ukiwa na vitu vya thamani, amma unaviacha reception kwa makabidhiano amma unaviweka kwenye safety box.

Jee, ulifanya hayo? hata kama kweli umeibiwa, ni uzembe wako na shigongo inamhusu nini? kataka kukusaidia mpaka saa saba za usiku kwa uzembe wako, leo yeye amekuwa mbaya?
 
Mkuu bila kutafuna maneno wewe ni mzembe! Sijapenda ulivyoibiwa ila inamaana wewe ni mara ya kwanza kulala hotel? Mbona sheria za hotel zipo wazi dunia nzima kwamba valuables tembea nazo or kabidhi reception! Wewe uliachaje chumbani ukaenda kula? Bt more so walijuaje wewe ni pedejee lazima ulionesha mazingira ya kujifanya uko njema wakakutime. Kwa hilo Shigongo humuwezi coz sheria zipo waziiii!
Kuna vitu huyu jamaa hasemi, naamini hoteli hiyo ni standard hotel, kuna maelekezo juu ya ku declare valuables na naamini vyumba vina safe deposits na kama havina, kuna tangazo reception kuhusu pesa ndio maana mmiliki kamtoleo nje na kama haya ni kweli, nenda popote, imekula kwako!. Pole zake kuibiwa!.
 
Kuna vitu huyu jamaa hasemi, naamini hoteli hiyo ni standard hotel, kuna maelekezo juu ya ku declare valuables na naamini vyumba vina safe deposits na kama havina, kuna tangazo reception kuhusu pesa ndio maana mmiliki kamtoleo nje na kama haya ni kweli, nenda popote, imekula kwako!. Pole zake kuibiwa!.

Pasco, atriums kuna safebox? Please! Hebu try to be a professional lawyer not a journalist kama ulivyokuwa zamani, although you can make a better investigation reporter but please dont wear the shoes of the atriums hotel!
 
Hotel zote zinasema, ukiwa na vitu vya thamani, amma unaviacha reception kwa makabidhiano amma unaviweka kwenye safety box.

Jee, ulifanya hayo? hata kama kweli umeibiwa, ni uzembe wako na shigongo inamhusu nini? kataka kukusaidia mpaka saa saba za usiku kwa uzembe wako, leo yeye amekuwa mbaya?

Kwa hiyo shigongo kufanya kazi mpaka saa saba usiku ni tatizo we kinibu? Ni hoteli yake, ni kazi yake, on top of that alipromise kuifanyia kazi, what about hao wafanyakazi aliosema amewasweka ndani? Watanzania amkeni na kufanya critical analysis ya mambo, kwa hiyo mtu hata kama huna kosa ndo umtaje RPC Au IGP? kwa kosa gani? After all RPC anahusika vipi? Na ana bahati that shingo-ngoni.
 
Kwa hiyo shigongo kufanya kazi mpaka saa saba usiku ni tatizo we kinibu? Ni hoteli yake, ni kazi yake, on top of that alipromise kuifanyia kazi, what about hao wafanyakazi aliosema amewasweka ndani? Watanzania amkeni na kufanya critical analysis ya mambo, kwa hiyo mtu hata kama huna kosa ndo umtaje RPC Au IGP? kwa kosa gani? After all RPC anahusika vipi? Na ana bahati that shingo-ngoni.

Huyo mleta mada ni muongo.

Kwanini aweke fedha chumbani na yeye atoke? na juzi kasikia Adam Malima kaibiwa hoteli kubwa kuliko hiyo?

Asitake kutudanganya. Anajidai alikuwa na dollar, jee, alikuwa anangoja safari au karudi safari za nje?

Huyo ni mwongo na mjinga!
 
Pole sana Ndugu!! Hiyo itakuwa Bahati Mbaya!! Ushauri wangu ni Kuwa sio Busara sana Kutembea na Hard Cash Nyingi Kiasi Hicho Ndani ya mfuko wa Begi!! Najua Hata Ulaya Kutembea na Hard Cash ni Jambo ambalo sio Zuri!!
Pia sijajua wewe ni Mtu wa Aina Gani ila Nakuona Una Tabia Kama za Naibu waziri wetu ila magnitude Inatofautiana = Laptop 3 za Dell = Degital Kamera Mbili!! Dola 4,000 = Dola 2,300!! Inaweza Kuwa watu huwa wanashabiana kwa Tabia!!
 
Huyo mleta mada ni muongo.

Kwanini aweke fedha chumbani na yeye atoke? na juzi kasikia Adam Malima kaibiwa hoteli kubwa kuliko hiyo?

Asitake kutudanganya. Anajidai alikuwa na dollar, jee, alikuwa anangoja safari au karudi safari za nje?

Huyo ni mwongo na mjinga!

Mkuu unawakilisha kundi kubwa sana la watanzania. You just jump to conclusions without any critical analysis whatsoever.Tubadilike ndugu yangu.
 
Back
Top Bottom