GAZETI
JF-Expert Member
- Feb 24, 2011
- 5,278
- 6,672
Habarini wana JF, Tar.17.05.2002 Nilifiwa na mchumba wangu kipenzi. Toka wakati huo mpaka kufikia 05/06/2011 Nimekuwa mwoga wa kwenda kucheki Afya. Mwaka jana nilikimbia majibu yangu pale kituo cha Afya tabata shule. Mchumba wangu alikufa kwa TB lakini sikuamini kabisa. Muda mfupi uliopita nilikwenda kupima katika hospitali moja binafsi. Ni uamuzi ambao sikuupanga kabla, yaani limenijia wazo ghafla, nikaamua liwalo na liwe. NIMEPIMA HIV sijawahi kufanya hivyo hapo kabla katika maisha yangu, Jamani leo nimekuwa mpya ni vizuri kwa wale wenzangu waliobaki nao wakichukua hatua hii. Yaani kwa matokeo yoyote yanavyokuja unajihisi kama umezaliwa upya........... Twendeni jamani.... twendeni tukapime tuondoke kwenye kifungo cha hofu na mashaka.