Nimefowardiwa E-mail hii, nadhani ni utani tu.

Mvaa Tai

JF-Expert Member
Aug 11, 2009
6,159
4,443
Wapendwa Bwana Yesu asifiwe.

Wakati habari juu ya babu huko Loliondo zinapumzika kidogo, naomba niwape na haya niliyoyasikia kwa masikio yangu kutoka redio Imani. Hii ni redio ya Waislamu ambayo inatangaza kutokea mkoa wa Morogoro. Sijui kama husikika nchi nzima au la. Hapa kwetu Arusha kulikuwa na kongamano kubwa la Waislamu wa madhehebu yote, jana Jpili na lilianza tangu asubuhi hadi jioni. Walikuwepo watoa mada mbalimbali, lakini mimi nilifanikiwa kumsikia mmoja, pamoja na immamu wa mkoa aliyetoa maazimio ya kongamano.Bila shaka magazeti yataripoti vizuri.

Nimesukumwa kuandika tena kwa urefu kwani nilisikitika sana kusikia maneno ambayo sikuwahi kuyasikia tangu nizaliwe yakiongelewa hadharani ndani ya nchi yangu. Nakumbuka nilisoma maazimio ya Mwanza, lakini hii imenistua sana. Kama tunamwomba Mungu basi tuongeze nguvu, kama hatuombi basi tuanze. Kwa mtindo huu, ninawasiwasi na amani ya Tanzania ambayo tumejivunia miaka hamsini sasa. Mliopata neema ya kupata nafasi za juu serikalini, sijui serikali inayaonaje mambo haya. Hayajaanza leo, ila imeyaachia yaendelee. Makanisa yanazidi kuchomwa, hakuna msikiti uliwahi kuchomwa kama sijakosea. Wakristo wanavamiwa na kupigwa, hakuna mhadhara wa Waislamu uliwahi kuvamiwa. Redio Imani na magazeti ya Kiislamu (mfano Al-alnuur) yanazidi kumwaga sumu ya udini, na ubaguzi, na chuki, lakini sijawahi kusikia vyombo hivi vikikemewa. Huu, ukimya wa serikali na vyombo vyake, sijui maana yake ni nini? Sumu hii ikiishapandwa kuing’oa ni kazi. Jamaa hawa walifanya mambo yao sirini tangu enzi za Mwinyi, na sasa, wameamua kuyaweka wazi na kuhamasisha Watanzania waziwazi tuuane. Haiingii akilini mwangu. Je, viongozi wetu wa dini wanazo taaarifa za kutosha kuhusu mambo haya? Wanachukua hatua gani? Je, sisi tuchukue hatua gani?

Shehe Ilunga Hassan ndiye niliyeweza kumsikia. Ameongea mambo mengi, lakini yote ni ya kupandikiza chuki ndani ya Watanzania. Ameanza kwa kutoa pongezi kwa kile Waislamu walichokifanya huko Mto wa mbu (Arusha) kwa kuwapiga wachungaji, na kuwajeruhi, nk. Amesisitiza kuwa Tanzania inaongozwa na mfumo Kristo. Na sasa umefika wakati mfumo huo uondolewe na hiyo ndiyo itakuwa pona ya Waislamu. Serikali inaongozwa na maaskofu. Wao ndiyo wanaweza kumwambia rais tunataka hiki au la. Amesisitiza kuwa amani tunayoiona TZ ipo kwa gharama ya Waislamu. Umefika wakati Waislamu waseme basi kwa mfumo Kristo ili na Wakristo wabebe gharama ya amani hii.

Ametoa takwimu kuwa mwaka 1992 Serikali iliingia mkataba na Wakristo, na tangu hapo imekuwa ikitoa fedha za kuwaendeleza wao huko Waislamu wakibaki nyuma. Kwa mfano, mwaka 2009, serikali imetoa bilioni 45, mwaka 2010 bilioni 54, na mwaka huu kwa miezi miwili hii na siku imekwisha toa bilioni 611, zote hizi zikiwa ni kuwaendeleza Wakristo.

Wakati serikali ikifanya hayo yote, Waislamu wameachwa nyuma na watoto wao wamezidi kuwa wamachinga huku watoto wa Wakristo wakiendesha baiskeli za kizungu na kufurahia beach. Amesema ifike mahali Waislamu waamue kama walivyofanya Wahutu dhidi ya Watutsi. Ati Kikwete hawezi kuongoza nchi bila maaskofu, maana kila analotaka kufanya lazima awaone.

Amesema kuwa Chama cha kususa na maandamano kipo tu kwa ajili ya maslahi ya Wakristo. Waislamu wanadanganywa wakidhani hicho chama kipo kuwatetea WaTz kumbe kipo kwa ajili ya Wakristo. Makafiri wanasaidiana wao kwa wao hivyo waislamu waamke, waungane hili kuuondoa mfumo Kristo. Amesema mfumo huu ulianza zamani,kwani hata 1964, Nyerere aliwafunga kina Chief Fundikira na wenzake kwakuwa walikuwa Waislamu. Akaendelea kuwa hata Azimio la Arusha lilikuwa kiini macho kwani liliwalenga Waislamu hata mali zilizotaifishwa zilikuwa za Waislamu Wahindi kwani wakati huo wakristo wengi walikuwa makarani na hawakuwa na chochote. Kwa hiyo Azimio lililenga kuwakandamiza Waislamu. Wakristo na mfumo wao wamekanyaga nyoka mkia, au wanamkamata ng’e mkia.

Aliendelea kusema kuwa imefika sasa Waislamu kuongea lugha wanayoilewa makafiri kwani wao hawataelewa kama waislamu wataendelea kuongea kwa njia ya makongamano kama haya. Kuendelea kudai haki kwa njia hii ya mikutano na makaongamano ni kama mtu anayemwambia mbuzi lugha ya kibinadamu wakati hailewi. Mbuzi lugha yake ni kupigwa ndipo huelewa. Ndivyo walivyo makafiri. Ifike wakati waislamu waseme basi. Usilamu hauna historia ya kushindwa. Allah alikwisha wahaidi waisalamu ahela, hivyo wao wana kazi mbili tu, KUUA au KUUAWA, na ndipo watapata zawadi ya ahela. Hivyo ndivyo wanaweza kuuondoa mfumo Kristo.

Akasisitiza kuwa huko Rwanda ilifika ambapo ilipotakiwa kuubadili mfumo, Mtusi na Mhutu hakuna aliyelala ndani, sasa Waislamu waseme basi. Akasema kuwa hata kama kunasemwa mabadiliko ya katiba, nayo hayatakuwa na maana kama bado kuna mfumo Kristo. Akasema kwa mfano waislamu wanabaguliwa hata kama katiba inakataza ubaguzi, hivyo, shida si katiba bali ni mfumo Kristo.

Amesisitiza kuwa Waislamu hawana historia ya kushindwa hivyo hata sasa watashinda tu. Amekiponda sana chama cha kususa na maandamano akiwasihi Waislamu wasikiunge mkono.

Jamani yamesemwa mengi, laiti ningekuwa mwanahabari ningeadika mengi. Kwa ufupi yule bwana amehamasisha chuki, uuaji, kuchukia CHADEMA, nk. Muda wote wafuasi walikuwa wakishangilia kwa TAKBIR! TAKBIR! Yaani kama angesema sasa tunaaza kazi nakwambia kungekuwa na balaa hasa.

Ndugu zangu, inaonyesha hawa jamaa zetu waislamu wamefanya mikutano, Dar es Salaam, Kigoma, Tabora, Mwanza, Shinyanga, Morogoro, Singida, na sasa Arusha. Wanaendelea hadi nchi nzima wakihamasisha haya na Waislamu kuungana na kuondoa tofauti za madhehebu yao kwani mfumo huu, unawaathiri wote.

Baada ya hapo alikaribishwa Imamu wa mkoa wa Arusha naye akatoa maazimio ambayo yaligawanyika katika makundi mawili.

1. MAAZIMIO YA KITAIFA

i) Wanaunga mkono maazimio yote yaliyotangulia kutolewa katika mikoa mingine

ii) Wanaunga mkono tamko la Immam mkuu (Shehe Issa Bin Simba)- sasa dhuluma basi

iii) Wanaitaka serikali kuangalia uwiano wa kimadaraka katika ngazi zote za serikali

iv) Wanaiagiza Wizara ya Elimu ifuatilie na kuhakikisha waraka wa mavazi (hijabu,nk), na ibada kwa Waislamu wanafunzi inatekelezwa.

v) Wanamtaka waziri wa fedha kuthibitisha uhalali wa mkataba kati ya Wakristo na Serikali wa mwaka 1992.

vi) Wanasema suala la mahakama ya kadhi si ombi ila ni lazima litekelezwe na pia TZ ijiunge na OIC

vii) Wanaagiza ubalozi wa Vatican uondolewe nchini

2. MAAZIMIO YA KIMKOA

i) Halmashauri ya Arusha imepewa mwezi mmoja irudishe mali za Waislamu

ii) Waislamu wapewe kibali kujenga msikiti katika kiwanja cha NHC kilicho karibu na Mahali pa Kumbukumbu ya Azimio la Arusha.

iii) Mahali ilipo stendi ya daladala ni mali ya Waislamu, irudishwe mara moja

iv) Kwa kuwa serikali ya JK ni halali kwa mujibu wa sheria, wanaoleta chokochoko waache mara moja.

v) Waislamu wanamuunga mkono Meya wa jiji la Arusha kuwa alichaguliwa kihalali, na wanamtambua kwa nguvu zote. Aachwe afanye kazi. Wao hawatakuwa tayari kuona upuuzi huo wa kumpinga.

vi) Kama Chadema itaandamana kama ilivyotoa taarifa ya siku 21, basi nao watatoka ili wapambane nao ili kujihami kwani maandamano yaliyopita yaliwaathiri

vii) Wanamwagiza IGP amrudishe kazini yule askari aliyesimamishwa kazi kwa kuwakamata wachungaji huko mto wa mbu. Pia mkuu wa kituo aliyehusika kumsimamisha kazi achunguzwe na kushughulikiwa.

viii) Waislamu wanasema sasa dhuluma basi.

Ni hayo kwa ufupi jamani. Ninaagalia uwezekano wa kupata kanda zao kama zitakuwa zimerekodiwa. Kazi kwetu kanisa.

Tukumbuke: Hawa ndugu sio wa kudharauliwa, wako very systematic katika mambo yao. Walianza chinichini, wakaongeza mihadhara, wakadai OIC, wakadai mahakama ya kadhi, sasa wanatoka nje wazi wazi , sio mihadhara, bali makongamano tena ya madhehebu yao yote nchi nzima. Huko nyuma walikuwa wanabaguana, sasa wanahamasisha umoja ili wafanikiwe katika malengo yao. Na wanawatumia wasomi wao kupindisha mambo, kwa nia wanazozijua wao. Walihamasishana kuingia kwenye siasa, wakitaka kufanikisha mambo yao kwa njia hiyo, sasa wameona haitawezekana, maana chama walikojikita kinayumba sasa.

Mapendekezo yangu.

•Tusiwachukie, tuwapende na kuwasaidia kwa moyo wote. •Kanisa lizame katika maombi juu ya taifa hili •Kanisa lisijibizane na hawa jamaa zetu. •Kanisa litumie vyombo halali vya serikali tena wakati huu akiwepo mwenzao ili serikali itoe msimamo •Kanisa liharibu umoja huo (kama Mungu alivyochafua lugha ya Wajenzi wa mnara wa Babeli) •Kanisa lihakikishe kuwa linazo taarifa za kutosha kuhusu hawa ndugu zetu. Asante.

Wiston I M
 
Waislamu walafi sana na wanakubali kirahisi kutumiwa na kikwete na ccm
 
Mhhh...kama ni ya kweli haya basi iko hatari...na Mungu atuepushe na watu hawa ambao hawaitakii nchi yetu mema!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Watanzania tuendeleze utamaduni wa kuvumiliana na kuheshimiana ili tuweze dumisha AMAN tulio nayo,otherwise kitawaka!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
unapotunga uongo ...then what..? mm ni mkristo mbona sijawahi kupewa hela na serikali...! ila nalipa PAYE kubwa mnoo...!

GO AND TELL IT TO THE BIRDS...!
waTZ HATUDANGANYIKI..!
 
Kikwete anatakiwa awashtaki wote hao chini ya sheria ya usalama wa taifa!, uhuru wa kuabudu utaheshimiwa kama hauvunji sheria ya nchi!, uchochezi na kuhamasisha mauaji ni kosa!
 
Waislamu walafi sana na wanakubali kirahisi kutumiwa na kikwete na ccm
Hii si kauli ya kiungwana hata kidogo

Kwangu mimi nadhani tunachohitaji kusaidia ni kuchanganua misaada au pesa za serikali zilitumika kufanya nini... kama ni kujenga makanisa au kutibu na kusomesha watu au hata kusaidia kilimo na ufugaji.

Si vibaya pia kuona jinsi serikali yetu ilivyolala na kuacha intelligence inashindwa kuzuia potential disaster simply kwa kuwaachia watu wasio sahihi kutoa kauli kali na za kupotosha ukweli

Ninakereka zaidi kwamba hata waziri wa mambo ya ndani amekalia kimya matamko yasiyokwisha kutoka kwa waislamu na waktrisu... TUMECHOSHWA NA MATAMKO TUNATAKA MAENDELEO NA MAMBO YA IMANI NI YETU NA MUNGU WETU

sikitiko kubwa zaidi ni jinsi watu wanavyonyimwa vital information na kuishia kutunga habari
 
Hivi kweli serikali inatoa pesa kwa kanisa? Kama ni kweli iache mara moja?
Hivi kweli azimio la Arusha lilikuwa linawalenga waislamu tu? kama ni kweli serikali ifanye uchunguzi usio na upendeleo?
Hivi kweli serikali inaongozwa na maaskofu na sio katiba? Kama ni kweli hili sio jema?

Kama serikali ingekuwa inaongozwa na maaskofu kwa nini haijawakamata hawa jamaa na kuwaweka ndani? Inamaana maaskofu wanaunga mkono hawa jamaa wanaotaka kuleta fujo?. Haiwezekani! Haiwezekani serikali inayoongozwa na maaskofu wa kanisa iendekeze maneno ya kujenga chuki katika jamii.
 
Wana hangaika tu...sasa angalia baadhi wameanza kuwapinga wenzao!
Hila za kishetani mwisho wake ni motoni.....
 
Hivi kweli serikali inatoa pesa kwa kanisa? Kama ni kweli iache mara moja?
Hivi kweli azimio la Arusha lilikuwa linawalenga waislamu tu? kama ni kweli serikali ifanye uchunguzi usio na upendeleo?
Hivi kweli serikali inaongozwa na maaskofu na sio katiba? Kama ni kweli hili sio jema?

Kama serikali ingekuwa inaongozwa na maaskofu kwa nini haijawakamata hawa jamaa na kuwaweka ndani? Inamaana maaskofu wanaunga mkono hawa jamaa wanaotaka kuleta fujo?. Haiwezekani! Haiwezekani serikali inayoongozwa na maaskofu wa kanisa iendekeze maneno ya kujenga chuki katika jamii.

Hakuna Serikali ya hivi duniani!!!!!!!!!!!!
 
unapotunga uongo ...then what..? mm ni mkristo mbona sijawahi kupewa hela na serikali...! ila nalipa PAYE kubwa mnoo...!

GO AND TELL IT TO THE BIRDS...!
waTZ HATUDANGANYIKI..!

Nimesoma kwa shida sana, Sijawahi kupewa hela na RC wangu ila nawachangia kimango cha kutosha

Sasa nafantya kazi na Bado naichangia Nchi yangu pesa nyingi sana, Kama hivi ndivo wanavosema walete uthibitisho!, wanaleta ujinga
wao wamekaa kulalama sana,

I came from a poor family but baba yangu alipenda sana elimu and thats why leo hii nipo hapa!.

Wana lengo la kutuumiza kwa kuwa wameshindwa kukimbizana!,

Mbona kwenye soka,muziki, sanaa wanatamba sisi tupo kimya sio poa Mkiwa shuleni someni,

Mbona kuna waislamu kibao wameendelea na wanasaidia wakristu??

Sjaipenda na Morogoro polisi inatakiwa kuwa makini sana, Bigwa pale inatakiwa wawe makini sana.


MY TAKE: Waislamu wekezeni kwenye Elimu Someni sna Qran pia msisahau kusoma masomo ya Darasani,
 
Mimi namlaumu Kikwete na usalama wa taifa ambao wanajifanya hawalioni hili, kuna taarifa za uhakika sana kuwa vijana wengi wa kiislamu wanajifunza ngumi na uuaji na ukatili wa hali ya juu wakisema eti ni mazoezi ya kawaida, nenda kwene msikiti nyuma ya hosp ya mwananyamala utawakuta, nenda kwene misikiti Tanga, wapo but serikali iko Kimya!! kUMBUKENI KAULI YA MAKAMU WA RAIS KWENE MAULID ALISEMA.....KUHUSI MAHAKAMA YA KADHI, TUMEWASIKIA, TUPENI MUDA MTAONA MATUNDA YAKE" huyu ni kiongozi wetu sote!! haya
 
Back
Top Bottom