Nimefiwa na BABA Yangu Mzazi

Pole sana kaka! Mungu aiweke peponi roho ya Marehemu. Mungu akupeni subira.sote ni Mwenyezi Mungu na sote kwake yeye tutarejea.
 
Pole sana mkuu X-Paster.

RIP Baba yetu mpendwa. Tulikupenda lakini Mola amekupenda zaidi.

Inna Lillahi wa Inna Ilayhi Raji'un (Samahani kama ntakuwa nimekosea):amen::amen::amen:
 
Kamanda; pole sana kwa msiba.

Wote tuko njia moja.

Mungu awafariji sana. Tuko pamoja katika Maombi!
 
Mwenyezi Mungu akutie nguvu kipindi hii kigumu kwako na familia nzima.Mungu ailaze roho ya Marehemu mahala pema peponi. Amen
 
Inna lillahi wa inna ilayhi rajiuun. Mungu awape nguvu na uvumilivu wakati huu wa msiba mzito.
 
Taarifa ya Msiba.

Assalaamu 'Alaykum wa RahmatuLlaah wa Barakaatuh,

Ndugu wapenzi, marafiki na member wa JF, kwa majonzi makubwa sana nawataarifu msiba wa Baba yangu mzazi ulio tokea tarehe 31 Aug 2010, uko Dar ES salaam kitongoji cha Sinza viwanja vya Sigara. Insha'Allah Mazishi yatafanyika Tarehe 1 Sept 2010. Saa saba mchana, kwenye makaburi ya Kisutu. Kwa wale wakazi wa Dar ES salaam kama wataweza kufika msibani basi watawawakilisha Member wengine.

"Sisi ni wa Mwenyezi Mungu nasi kwake tutarejea, Ewe Mwenyezi Mungu nilipe kwa msiba wangu na unipe badili yake bora kuliko huo"

إِنّا للهِ وَإِنَا إِلَـيْهِ رَاجِِعُـونَ ، اللهُـمِّ اْجُـرْني فِي مُصِـيبَتي، وَاخْلُـفْ لِي خَيْـراً مِنْـها.

Pole, sijui anaitwa nani ili tukahudhurie msiba!
 
Taarifa ya Msiba.

Assalaamu 'Alaykum wa RahmatuLlaah wa Barakaatuh,

Ndugu wapenzi, marafiki na member wa JF, kwa majonzi makubwa sana nawataarifu msiba wa Baba yangu mzazi ulio tokea tarehe 31 Aug 2010, uko Dar ES salaam kitongoji cha Sinza viwanja vya Sigara. Insha'Allah Mazishi yatafanyika Tarehe 1 Sept 2010. Saa saba mchana, kwenye makaburi ya Kisutu. Kwa wale wakazi wa Dar ES salaam kama wataweza kufika msibani basi watawawakilisha Member wengine.

“Sisi ni wa Mwenyezi Mungu nasi kwake tutarejea, Ewe Mwenyezi Mungu nilipe kwa msiba wangu na unipe badili yake bora kuliko huo”

إِنّا للهِ وَإِنَا إِلَـيْهِ رَاجِِعُـونَ ، اللهُـمِّ اْجُـرْني فِي مُصِـيبَتي، وَاخْلُـفْ لِي خَيْـراً مِنْـها.
Pole sana mkubwa Mwenyezi Mungu akupe wepesi wakati huu wa majonzi!
 
Pole sana mkuu. Mungu akupe nguvu katika kipindi hiki kigumu
 
Pole ndugu yetu,rafiki yetu , mwana forum mwenzetu kwa msiba mzito. Inshallah Mwenyezi Mungu akujalie wepesi katika kipindi hiki kigumu
 
Inna lillahi wa inna ilayhi raji'un

Pole sana mkuu X-Paster tupo pamoja
 
Pole sana mkuu Mwanazuoni. Bwana ametwaa na jina lake libarikiwe. Hiyo ndiyo njia ya kila mmoja, hakuna atakayekwepa, kinachotofautiana ni siku na saa ambayo hakuna anayeifahamu.
 
R.I.P Dad, Mungu awape roho ya uvumilivu wakato huu mgumu.Amen.
 
Mkuu x-paster, pole sana mkuu, mungu akupe nguvu uweze kuvuka katika majonzi.
 
Pole sana X-Paster kwa msiba huu mzito. Nakuombea faraja ya Mnyezi Mungu wewe na familia yako katika kipindi hiki cha majonzi na machozi. Mnyezi Mungu airehemu roho ya marehemu, Amin.

Inna lillahi wa inna ilayhi raji'un
 
Mungu akupe nguvu na uvumilivu katika kipindi hi cha majonzi wewe na Familia yako
 
Pole sana ndugu yangu. I know how it feels kuondokewa na baba.
Am sure our loving God will give you and your family the required strength
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom