Nimechoka, Najisikia Uchungu sana!

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,927
22,083
Nimechoka, Najisikia Uchungu sana!

Hadi kupika napika! Hello Jane,

Sijajua kitu gani kimetokea katika ndoa yetu, tulizoea kuwa na tendo la ndoa mara 3 kwa wiki na sasa ni mara moja kwa miezi minne na hata tunapokuwa kwenye tendo la ndoa unajilaza kama gogo tu na unanipa sura ambayo inanipa nitafsiri kwamba unaniambia “Hujamaliza bado, ondoka mwilini mwangu unachofanya sijisikii chochote”
Je, ni kitu gani kimetokea kwani ulikuwa sexy, exciting na ulikuwa ni mwanamke niliyekuoa unayependa kufanya mapenzi na mimi.

Ndoa yetu ina miaka 10 sasa na ni miaka 3 tu ulifanya nijisikie nimeoa mke ambaye anatimiza ndoto zangu hata hivyo hii miaka 7 ambayo umekuwa huna hamu ya tendo la ndoa imesababisha nijikie nimechoka na nipo hatua ya mwisho hasa baada ya kuweka juhudi kubwa kukurejesha kwenye mstari na nimeendelea kuambulia kuendelea kukataliwa tendo la ndoa.

Nafahamu fika mke wangu unapenda vitu gani, ninafahamu unapenda affections, unajisikia raha kupendwa, unajisikia raha kupelekwa outing angalau mara mbili kwa wiki, unajisikia raha kupewa zawadi, unajisikia raha mimi kuwa na watoto na wewe ukapata muda wa ziada (free time), unapenda kupewa extra money kwa ajili ya shopping, pia unajisikia raha nikupe pesa kwa ajili ya kwenda vacation na dada yako, unajisikia raha ninapokusaidia kazi za nyumbani ili usiende kulala umechoka na nimekuwa najinyima, najipinda mgongo wangu kuhakikisha haya yote unayapata hii miaka 7 ambayo hata hivyo wewe umekuwa unaninyima tendo la ndoa na nikikuomba unaniamba “Nimepotoka na mpenda sex”

Nimekuwa najiuliza kwa nini nijinyime na kupinda mgongo wangu kujitoa kwa mambo yote haya kama wewe unashindwa kunitimizia hitaji moja tu la sex angalau mara mbili kwa wiki?
Kwa kweli nimechoka na nimeanza kujisikia hasira na nimepoteza interest kwani najisikia wewe huoni umuhimu wa kunitimizia mahitaji yangu.

Ninafahamu fika kwamba hamu ya kufanya mapenzi kati ya mwanaume na mwanamke ni tofauti na nimejitahidi mara zote kuhakikisha wewe unapata kile unahitaji ili ujisikie vizuri na uwe tayari kwa sex hata hivyo juhudi zangu zimekuwa hazina maana.

Sikukuoa ili unipe sex tu, na pia sikukuoa ili usinipe sex, sex ni moja ya sababu maelfu zilizonifanya nikuoe. Nilikuoa ili kuondoa upweke, ili uwe life partner, nishirikiane na wewe katika ndoto na malengo ya maisha pamoja, kulea watoto ambao Mungu ametupa na kupeana sex na mwanamke ambaye ninampenda na ambaye nimemchagua kufanya mambo haya yote.

Kumbuka naweza kupata vitu vyote kwa mtu yeyote ambaye naweza kuamua kuishi naye isipokuwa sex tu kwani ni wewe tu unaweza kunipa na ndiyo maana niliacha wazazi wangu ambao walinipa kila kitu nahitaji isipokuwa sex kwani hata kama ningetaka mtoto ningeweza kufanya adoption.
Sex inanifanya nijisikia nipo connected na wewe, sex inanifanya nijione na kukuona wewe ni mwanamke special.

Swali linakuja kwa nini mwanaume aweke commitment ya maisha kwa mwanamke ambaye hawezi kumpa sex?

Kama mke wangu ungeniambia tangu mapema kwamba hamu yako ya kufanya mapenzi itakuwa ni miaka 3 tu nina uhakika nisingepoteza muda wangu kukubaliana kuoana na wewe, nisingekubali kuingia katika shida kubwa namna hii ya kunyimwa sex na mke wako mwenyewe na unajua fika siwezi kupata hii huduma mahali popote isipokuwa kwako na kama nilivyokwambia siwezi kukuacha wala kushawishika kutembea na mwanamke mwingine kwani ninakupenda.

Kinachoniuma zaidi ni kitendo chako cha kuninyima na huku unafurahia na nikitaka tuongee unanijia juu eti mimi ni mpenda sex nisiyejali na ninayejua ndoa ni sex tu.
Nafahamu nimefanya the biggest mistake in my entire life, nimekwama kwa mtu ambaye nampenda na hawezi kutimiza hitaji langu, najiona nimenasa kwenye chambo ya kizamani na Inaumiza sana.
Najuta, najuta najuta mno!

Nimeamini inachukua efforts kidogo sana kumfanya mwanaume afurahi na ni ngumu sana kumfanya mwanamke afurahi.
Nipe sex mara 2 kwa wiki nitakuwa mwanaume mwenye furaha na nitakufanya uwe na furaha ziku zote.
Nini kigumu hapo mke wangu?

Ukinipa sex najisikia nipo connected na wewe kimwili, kinafsi na kiroho!

Najisikia uchungu sana!
 
Oooh dear, pamoja na stress zote za maisha haya bado kuna mtu ndani anakuzingu?

Vyuma viko vingi sana, za kununua, kuomba kupewa tu nk. Mwanamke akifikia hatua hii ni shetani achana nae.
 
Kumbe ndivyo mnavyoteseka mliooa huku sisi mabachela sex tunapewa hadi tunaikimbia wenyewe
 
Back
Top Bottom