Nimechoka kusubiri ajira za walimu

UFAFANUZI.
1/Kama wewe ni mwalimu ujue una bahati kubwa sana ya kuja kuajiriwa na serikali. Wahitimu wa fani nyingine hawana hiyo bahati.

2/Ni jambo la kweli na uhakika kuwa serikali itaajiri walimu, Tatizo ni Lini wataajiri, wangapi wataajiriwa, wapi utapangiwa na utalipwa nini?

3/Upo uwezekano wa baadhi ya walimu wanaweza wasiajiriwe na serikali kama sio mwaka huu basi miaka michache ijayo. Kwanini? Serikali kwa sasa inaona watumishi wa umma ni wengi, ufanisi ni mdogo sana, gharama za kuwalipa ni kubwa sana. Kifupi kabisa serikali inaona wingi wa watumishi wa umma ni MZIGO na JIPU.

4/Mpaka sasa Serikali imeshasema kuwa haitawaajiri wahitimu wote wa Udaktari wa Binadamu. Kati ya madaktari zaidi ya 1000 waliohitimu Mafunzo ya Vitendo hivi karibuni, ni 400 tu ndio watakao bahatika kuajiriwa na serikali mwaka huu. Kwanini? Serikali haina pesa za kuwalipa wote.
Sasa jiulize suala la kuajiri walimu Elfu 40 kwa mkupuo mmoja kama linawezekana kirahisi rahisi mwaka huu?

5/Serikali imekuwa na vipaumbele vingi sana, na inataka vyote vitimizwe kwa wakati mmoja na hapo hapo mtizamo wa Rais kwa sasa ni kupunguza matumizi ya serikali na hapo hapo kukusanya mapato zaidi ili kujenga miundombinu na kununulia vifaa, na sio kuzifanyia matumizi ya kuwalipa watu Posho, mishahara mikubwa nk.
Katika hali hiyo, tegemea kabisa suala la kuajiri walimu litakuwa sio kipaumbele chake.

NI VYEMA UKIJIANDAA PIA KUISOMA NAMBA!!
 
Tatzo muwapo vyuon mnajisahau hamkumbuk kwamb kuna maisha baada ya boom sasa matokeo ndo hayo by the way mm nipo chuo na nasoma education lkn nkimaliza hata nicpopata ajira life litasonga2 bcz i have plan b already
Hembu share na sisi hiyo plan b mimi tangu nimemaliza mwaka jana mwezi wa sita education mpaka sasa nimefanya kazi sehemu tatu na sasa niko gvep international na education yangu niambie umejipangaje naweza share nawe uzoefu
 
Walimu km nyie lazima mnyanyaswe sana na serkal. maana huna plan B

Mimi baada ya kumaliza advance niliomba ajira shule Moja ya private kwa mwez nikawa nachukua laki Tatu na nusu, jion nikawa nafundisha tuition kila ijumaa nikawa nachukua alfu 45
Kidogo nihairishe mambo ya chuo maana maisha yalikuwa mzuri tu, ila pesa nilizochuma ndo zinanisaidia kwenye matumiz yangu huku chuon

Wewe ni graduate bado unalia na serkal!!!!!!
 
Walimu km nyie lazima mnyanyaswe sana na serkal. maana huna plan B

Mimi baada ya kumaliza advance niliomba ajira shule Moja ya private kwa mwez nikawa nachukua laki Tatu na nusu, jion nikawa nafundisha tuition kila ijumaa nikawa nachukua alfu 45
Kidogo nihairishe mambo ya chuo maana maisha yalikuwa mzuri tu, ila pesa nilizochuma ndo zinanisaidia kwenye matumiz yangu huku chuon

Wewe ni graduate bado unalia na serkal!!!!!!
sasa kuajiriwa ndo plan b....acha kujifalagua....kama mtu hajabahatika kupata shule ya private na wala hakupata kituo cha tuition je
 
Wakati mwinginee watuu tunashindwa kuelewa kuwaa maishaa unayoishi wewe ni tofauti na mwenzio daimaa hatuwezi kulinganaaa......oooh mtoa madaa hakuwaa na plan B ooooh mlitumiaa vibaya boom mlipokuwa chuoo ooo sijuiii niniii!...

Malawamaaa meeengiii!...

Mfano mie since nimeenda shule karibu NNE za private......ja kilaa mmoja anakwambiaa tukupee mkatabaa tenaa sio chinii ya mwakaaa maana ukifanya kazii miezii miwilii utaharibuu mipangoo yaoo maana wanafunzii kucop na mwalimu mpyaa inahitaji mudaaa!......

Na hataaa ukisemaa ufanyee biasharaaa!...
BIASHARA MTAJI REMEMBER!.....

Na kwa u-delicate wa ualimu ni vizuri mwalimuu aingie kazin fresh from school akiwa na harii yoooteee!....

Ni kwelii mamlakaa husikaa hawakututendeaa hakii kabisaaa ilaa namshaurii mwalimu tarajali mwenzangu......
Tulichaguaaa huu #witoo tunahitajikaa kuwa wavumilivuu na naamin hakunaaa wa kutuzuiaa kufanyaaa kilee tunachostahilii hataaa wakitoaa this month kamaaa wasemavo akina Jafo na Simbachawene au hata wa sabaa kama alivosemaa P.M na hataa wakitaka next year!....,

Tuvumiliee tuu na wakati huo tutengeneze mawazo (proposal) zitakazotusaidiaa kufikia malengo kimaishaaaa..

NAAMINI WALIMU TUNA UPEO MKUBWA WA KUFIKIRI NA IT'S GONA BE ALRIGHT.
...wewe mwalimu unaandika kama unaimba...halafu unaenda shule ya kata kufundisha...ghafla tunasikia mchina flani somewhere kapata B ya kiswahili!,halafu tunaanza kushangaa mbona wa kwetu hawajapata?!
 
Shule binafsi zishajichukuliaa walimu wao mapemaa wakiwemo wa masomo ya sayansi ambao ndo restricted commodity leo hii... Nipo wilaya ya bunda kuna shule inaitwa Dr. NCHIMBI SEC toka january form 1 hawajasoma physics na hesabu ata definition tuu... Na shule ipo mjini eb serikal ktk mgawanyo wa walimu iangaliee sanaa
Brother huko humu.
 
Tatzo muwapo vyuon mnajisahau hamkumbuk kwamb kuna maisha baada ya boom sasa matokeo ndo hayo by the way mm nipo chuo na nasoma education lkn nkimaliza hata nicpopata ajira life litasonga2 bcz i have plan b already
Usipende kuongea bila kutafakari,, kama we ni mwanachuo na wenzio walikua kama wewe kwa kulopoka mipango ya maaana akiwa chuoni
Bora ukae kimya tuu usome mawazo ya watu
 
...wewe mwalimu unaandika kama unaimba...halafu unaenda shule ya kata kufundisha...ghafla tunasikia mchina flani somewhere kapata B ya kiswahili!,halafu tunaanza kushangaa mbona wa kwetu hawajapata?!
Sijakusomaa Mkuu!....

Sasa uandishi wangu unaingiliana vipii na kufeli kwa wanafunzi!?...
Au unataka kuniambia kuwa kwa namna nilinanyoandika naonekana kama mwalimu asiye na maarifaa amaa!?........

Maana bado sijaona kosa nililofanya katika hoja yangu ambayo inaonesha kuwa sina uwezo wa kuwafanya wanafunzi kufauluu!.......

Sometimes tunahitaji jicho la TATU kabla ya kuchangia madaa!......

Sent from my TECNO-Y4 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom