KATATANAMA
Member
- Feb 15, 2012
- 63
- 6
Pole sana ndugu. Ni vyema ukatafuta KANISA linalohubiri Wokovu na kuamini miujiza ya Yesu Kristo AU MCHUNGAJI hili akushauri na kukufanyia MAOMBI bila shaka utapata msaada.
Ndugu yangu sikiliza kwa makini usiende eti upate chanzo cha tatizo lako acha kupiga Ramli, kuagalia nyota kupiga ramli, faraki wote hao ni adui wa Mungu Baba!!! Watumishi wa Mungu aliye hai wapo wengi tuu hapo Dar, nenda makanisa ya kiroho uombewe upate uponyaji!!!! Usidharau makanisa ya Mungu aliye hai ya kiroho, nguvu ya Mungu kwa uwezo wa Bwana Yesu ipo tuu!!!! Majini na mapepo hayasimami kwa Yesu hiyo ni cha mtoto yapo mambo makubwa utajifunza utujua mengi na kuyafanyia kazi!!! Unapote za muda kutookoka ndugu yangu ili uufaidi uzuri wa Yesu, ubarikiwe!!!!
Huu ndio msaada wako haaasa""Mpokee YESU awe Bwana na Mwokozi wa maisha yako.utapata uhuruNdugu pole sana kwa yanayokukumba, wapo wengi ambao wameteseka kwa namna hiyo ila walipochukua hatua ya kubadili life style ya maisha yao wamewekwa huru kabisa.
Piga moyo konde chukua hatua zifuatazo na kwa kumaanisha ndani ya moyo wako utawekwa huru kabisa.
1.Amini katika Jina la YESU, Yohana 1:12, tubu dhambi zako zote popote pale ulipomkosea Mungu yeye ni mwaminifu atakusamehe kabisa, Isaya 1:18, Isaya 43:25, Zab 103:3,11,12, Mkaribishe ROHO MTAKATIFU awe ndani yako na kuyaongoza maisha yako, Wagalatia 4: 6,
2. Kwa kumwamini Bwana YESU, kutubu dhambi zako zote, na kumwalika Roho Mtakatifu kuwa ndani yako, unayo mamlaka na nguvu za Mungu kushinda ulimwengu wote wa giza. Muda wowote utakapo jisikia hiyo hali tumia mamlaka ya JINA LA YESU kukemea hizo nguvu za giza wala hazitakuwa na uwezo juu yako. LUKA 10:19, MARKO 16:17-18,
3. Jiwekee utaratibu wa kusoma na kutafakari neno la MUNGU ndani ya Moyo wako popote pale utakapokuwepo. Kumbuka ibilisi atakuletea hofu ya kukunyonga kama kawaida yake, chukua hatua ya kukemea hiyo roho ya hofu, na mtafakari Mungu na uweza wake katika Jina la YESU badala ya kuwaza hizo hofu za ibilisi. Wakolosai 3: 1-2.
4. Ukifanya maombi usifanye maombi legelege, fanya maombi ya vita ya kujikomboa kutoka katika utawala wa shetani, tumia silaha zote za UFALME WA MUNGU kumpinga na kumpiga shetani ili asikufuatilie. Uhuru haupatikani kilegelege ni kwa vita ndugu. 2-Wakorintho10: 4-5
5. Acha dhambi yoyote ile inayokuzinga ambayo ibilisi anaweza kuitumia kama njia ya kuendelea kukushambulia. Kumbuka MUNGU ni Mtakatifu na anawatetea wale wote wanaoishi katika njia zake. Wagalatia 5:20-21.
6. Hakikisha unahudhuria vipindi vya maombi na kujifunza neno la Mungu katika kanisa linalohubiri Injili ya kweli na kuamini katika karama zote za ROHO MTAKATIFU na si ubabaishaji.
Ndugu, Bwana Yesu akusaidie na kukuweka huru kabisa.
Kuomba sio ishu,ishu ni je waombaje? Isije kuwa unatoka baa ukiwa chakari ndio unaomba...ila nakushauri fanya mfungo wa dhati kwa mwezi mmoja,narudia tena kwa dhati na maombi ya nguvu..sidhani kama shetani atasimama kwa hapo.
Apolinary...sikia! Sala ni muhimu sana kwetu binadamu kwani ni chakula cha roho. Ila pia kuna kitu kinaitwa mizimu nayo ni hatari na lazima izingatiwe. Kama wazazi wako wamefariki uliza ndugu waliobaki ufanyeje ili utekeleze matakwa yao la sivyo utaishia kuhama hama kila kukicha! Kingine, je uliwahi kumdhulumu mtu mali yake? Nakuuliza hivi manake kuna yanki mtaani alijiua miaka ya nyuma baada kuteswa kijinsia kila siku. Sikutishi ila huyu yanki alikuwa anajivinjari na mke wa mtu then jamaa alipogundua akamuonya lakini yule marehemu alinogewa na vya bure. Kwa hiyo mwenye mali akafanya yake ya jadi na yule yanki akaanza kuweweseka usiku kila akienda kulala. Jamaa akawa anapata mateso ya kila aina mpaka mwishoni akawa anafilwa kabisa akiamka asubuhi ****** una muuma na anakuta kinyesi kitandani, jamaa akachoka na mateso akahamua atangulie mbele ya haki na kuacha barua kwa nini alichukua ile hatua. Kwa hiyo bwana kama umemlalia mtu tafadhali omba msamaha wakati muda bado upo!
Dah mi napita tu jamani, nimekumbuka enzi zile miaka ya 80 huko kijijini kwetu mdogo wangu alikuwa anachapwa viboko usiku kucha na mtu haonekani na purukushani nyiiingi usiku mwingi.
Aaaaah lakini kule ni jino kwa jino tu kuna wachawi na waganga pia, kama vipi njoo nikupeleke ukirudi utamuona live anaefanya mambo hayo na kumkamata, tayarisha nauli tu na labda zawadi ya shati la mtumba kule waganga c wasanii kama wa town, anakutibu kwanza ukipona ndo unajisachi mwenyewe umpe ngapi kama shukrani.
Mi naamini sana dini ila kuna sehemu tusidanganyane dini hua inachemka hasa kama huna imani ya kivileee !