Nimechoka kunyongwa usiku wa manane, tafadhali msaada wa haraka

Pole sana.. Ushauri wangu..weka maisha yako kwenye mikono ya Mwenyezi Mungu kupitia imani au dhehebu lako. Mwangukie Mungu kwa Moyo wako wote na hata ukisali hakikisha unasali toka moyoni na siyo kuimba sala kama shairi. Jenga imani hadi uone unamwomba Mwenyezi Mungu kuwa kama yeye anataka wewe uendelee unyongwe kila siku na iwe hivyo..lakini si kama wewe unavyotaka.

Kama unasali na unayo imani kwa Mungu basi haukuwa na haja ya kuhama ile nyumba ya kwanza. Pia kumbuka kama bado unaamini nyumba ya sasa bado ina mikosi basi hiyo ni dalili ya kuwa imani yako bado ni ndogo...

Endelea kusali kwa dhati na Amini Mungu atakusaidia..otherwise, utaendelea kupigika na kusaga meno..
 
Pole sana.. Ushauri wangu..weka maisha yako kwenye mikono ya Mwenyezi Mungu kupitia imani au dhehebu lako. Mwangukie Mungu kwa Moyo wako wote na hata ukisali hakikisha unasali toka moyoni na siyo kuimba sala kama shairi. Jenga imani hadi uone unamwomba Mwenyezi Mungu kuwa kama yeye anataka wewe uendelee unyongwe kila siku na iwe hivyo..lakini si kama wewe unavyotaka. Kama unasali na unayo imani kwa Mungu basi haukuwa na haja ya kuhama ile nyumba ya kwanza. Pia kumbuka kama bado unaamini nyumba ya sasa bado ina mikosi basi hiyo ni dalili ya kuwa imani yako bado ni ndogo... Endelea kusali kwa dhati na Amini Mungu atakusaidia..otherwise, utaendelea kupigika na kusaga meno..[/QU yaani mpaka nikitembea njian nikikumbuka usiku ninavyongwa mwili unasisimka isitoshe saa ambayo ninanyongwa huwa niko macho kabisa lakin nakosa nguvu ya kupiga kelele
 
Pole sana ndungu, kitu cha kwanza jikabidhi maisha yako na kazi zako mbele ya MUNGU wako kwa muda wote kulingana na imani yako. Pili, jitahidi kupunguza vyakula vizito wakati wa usiku au kula mapema masaa 3-4 kabla ya kulala. Tatu, jaribu kubadili staili ya ya ulalaji wako kwa kufanya majaribio tofauti.
 
Acha kulala umefunga madirisha na milango hadi hewa inaisha.

Hata kama unafungua kidogo, basi unajifunika gubigubi na mwisho unaishiwa hewa.

Pia angalia mto (Pillow) unayotumia maana inaweza kuwa ndogo na ukilala, unajibana kifua.

Ushauri wangu tu huu. Nenda kwa Dr. na usianze sana kuweka Mungu na Uchawi katika hili mara moja.

Mungu nisaidie na wewe unakimbia. Ila usiende kwa Sangoma bana.
 
Acha kulala umefunga madirisha na milango hadi hewa inaisha.

Hata kama unafungua kidogo, basi unajifunika gubigubi na mwisho unaishiwa hewa.

Pia angalia mto (Pillow) unayotumia maana inaweza kuwa ndogo na ukilala, unajibana kifua.

Ushauri wangu tu huu. Nenda kwa Dr. na usianze sana kuweka Mungu na Uchawi katika hili mara moja.

Mungu nisaidie na wewe unakimbia. Ila usiende kwa Sangoma bana.

MSAADA MKUBWA NI KUMUOMBA MUNGU KAMA WALIVYOSHAURI WENGINE,UKIENDA KWA DAKTARI HALI HIYO HAITIBIWI ZAIDI YA KUKUPA DAWA ZA WAGONJWA WA AKILI LAKINI PIA HUYU ALIYESEMA Mungu nisaidie na wewe unakimbia NILIPOWEKA ALAMA NYEKUNDU,MUNGU HAWEZI KUKUSAIDIA NA WW UNAKIMBIA NI MANENO POTOFU ,TENA MANENO YA UHUNI.KWANI HUWEZI UKAWANASEHEMU YA KUJISAIDIA NA SEHEMU NYINGINE MUNGU ANAKUSAIDIA.MUNGU HUFANYA JAMBO PEKEE HAHITAJI MSAADA.TOTAL HELP
 
pole sn, fanya uombewe na we mwenyewe sali na kusoma dua sn.
Lkn c vibaya pia if u see a doc.
Au angalia hilo tatizo limeanza lini na linarelate na tukio gani lililowahi kukupata.
Possible ni msongo wa mawazo, muone Dr
 
Apolinary inaelekea una tatizo la kitibabu, mwone daktari ili akushauri mambo ya metabolism.
Kwa kawaida mlo mzito unaleta usingizi na mwili kukosa nguvu maana damu yote inaenda sehemu ya matumbo ili kusaidia kuyeyusha na kuchukua virutubisho vinavyo tolewa kwenye chakula.
Inaelekea hii process ina matatizo ambayo yaneweza kurekebishwa ukimwona daktari.
Zaidi ya hapo rndelea kusali sana na Mungu atasikia kilio chako ili mwili ufanye kazi kama kawaida.
 
Ndugu pole sana kwa yanayokukumba, wapo wengi ambao wameteseka kwa namna hiyo ila walipochukua hatua ya kubadili life style ya maisha yao wamewekwa huru kabisa.
Piga moyo konde chukua hatua zifuatazo na kwa kumaanisha ndani ya moyo wako utawekwa huru kabisa.

1.Amini katika Jina la YESU, Yohana 1:12, tubu dhambi zako zote popote pale ulipomkosea Mungu yeye ni mwaminifu atakusamehe kabisa, Isaya 1:18, Isaya 43:25, Zab 103:3,11,12, Mkaribishe ROHO MTAKATIFU awe ndani yako na kuyaongoza maisha yako, Wagalatia 4: 6,

2. Kwa kumwamini Bwana YESU, kutubu dhambi zako zote, na kumwalika Roho Mtakatifu kuwa ndani yako, unayo mamlaka na nguvu za Mungu kushinda ulimwengu wote wa giza. Muda wowote utakapo jisikia hiyo hali tumia mamlaka ya JINA LA YESU kukemea hizo nguvu za giza wala hazitakuwa na uwezo juu yako. LUKA 10:19, MARKO 16:17-18,

3. Jiwekee utaratibu wa kusoma na kutafakari neno la MUNGU ndani ya Moyo wako popote pale utakapokuwepo. Kumbuka ibilisi atakuletea hofu ya kukunyonga kama kawaida yake, chukua hatua ya kukemea hiyo roho ya hofu, na mtafakari Mungu na uweza wake katika Jina la YESU badala ya kuwaza hizo hofu za ibilisi. Wakolosai 3: 1-2.

4. Ukifanya maombi usifanye maombi legelege, fanya maombi ya vita ya kujikomboa kutoka katika utawala wa shetani, tumia silaha zote za UFALME WA MUNGU kumpinga na kumpiga shetani ili asikufuatilie. Uhuru haupatikani kilegelege ni kwa vita ndugu. 2-Wakorintho10: 4-5

5. Acha dhambi yoyote ile inayokuzinga ambayo ibilisi anaweza kuitumia kama njia ya kuendelea kukushambulia. Kumbuka MUNGU ni Mtakatifu na anawatetea wale wote wanaoishi katika njia zake. Wagalatia 5:20-21.

6. Hakikisha unahudhuria vipindi vya maombi na kujifunza neno la Mungu katika kanisa linalohubiri Injili ya kweli na kuamini katika karama zote za ROHO MTAKATIFU na si ubabaishaji.

Ndugu, Bwana Yesu akusaidie na kukuweka huru kabisa.

 
Ndugu pole sana kwa yanayokukumba, wapo wengi ambao wameteseka kwa namna hiyo ila walipochukua hatua ya kubadili life style ya maisha yao wamewekwa huru kabisa.
Piga moyo konde chukua hatua zifuatazo na kwa kumaanisha ndani ya moyo wako utawekwa huru kabisa.

1.Amini katika Jina la YESU, Yohana 1:12, tubu dhambi zako zote popote pale ulipomkosea Mungu yeye ni mwaminifu atakusamehe kabisa, Isaya 1:18, Isaya 43:25, Zab 103:3,11,12, Mkaribishe ROHO MTAKATIFU awe ndani yako na kuyaongoza maisha yako, Wagalatia 4: 6,

2. Kwa kumwamini Bwana YESU, kutubu dhambi zako zote, na kumwalika Roho Mtakatifu kuwa ndani yako, unayo mamlaka na nguvu za Mungu kushinda ulimwengu wote wa giza. Muda wowote utakapo jisikia hiyo hali tumia mamlaka ya JINA LA YESU kukemea hizo nguvu za giza wala hazitakuwa na uwezo juu yako. LUKA 10:19, MARKO 16:17-18,

3. Jiwekee utaratibu wa kusoma na kutafakari neno la MUNGU ndani ya Moyo wako popote pale utakapokuwepo. Kumbuka ibilisi atakuletea hofu ya kukunyonga kama kawaida yake, chukua hatua ya kukemea hiyo roho ya hofu, na mtafakari Mungu na uweza wake katika Jina la YESU badala ya kuwaza hizo hofu za ibilisi. Wakolosai 3: 1-2.

4. Ukifanya maombi usifanye maombi legelege, fanya maombi ya vita ya kujikomboa kutoka katika utawala wa shetani, tumia silaha zote za UFALME WA MUNGU kumpinga na kumpiga shetani ili asikufuatilie. Uhuru haupatikani kilegelege ni kwa vita ndugu. 2-Wakorintho10: 4-5

5. Acha dhambi yoyote ile inayokuzinga ambayo ibilisi anaweza kuitumia kama njia ya kuendelea kukushambulia. Kumbuka MUNGU ni Mtakatifu na anawatetea wale wote wanaoishi katika njia zake. Wagalatia 5:20-21.

6. Hakikisha unahudhuria vipindi vya maombi na kujifunza neno la Mungu katika kanisa linalohubiri Injili ya kweli na kuamini katika karama zote za ROHO MTAKATIFU na si ubabaishaji.

Ndugu, Bwana Yesu akusaidie na kukuweka huru kabisa.

Well said mkuu!
 
Back
Top Bottom