Nimechanganyikiwa, sikujua kama mwisho utakuwa hivi

labda nikuambie tu...32yrs bado unalipa saaanaa tu!

I second you on that Nyamayao,plus mdada ana kazi yake nzuri na ndio baba wa familia,achilia mbali the abuses-physically,mentally and emotionally....ah ah jamani, thats too much. There is a limit to what a woman can take in the name of marriage.
 
samahani dada lakini nashindwa kuelewa iweje wapenzi wanakorofishana kiasi cha kuachana. hapana naomba kuwa na hekima tofauti kidogo. nendeni kwa councellors mtapata mwongozo.
 
samahani dada lakini nashindwa kuelewa iweje wapenzi wanakorofishana kiasi cha kuachana. hapana naomba kuwa na hekima tofauti kidogo. nendeni kwa councellors mtapata mwongozo.

wewe....wewe...nadhani bado hujakua vzr!
 
I second you on that Nyamayao,plus mdada ana kazi yake nzuri na ndio baba wa familia,achilia mbali the abuses-physically,mentally and emotionally....ah ah jamani, thats too much. There is a limit to what a woman can take in the name of marriage.

my daughter...thats y ckutaka kuongea mengi bali kumuonyesha tu kwamba yeye bado wamooo sanaaa!
 
Sijui nianzie wapi?? naandika kwa masikitiko makubwa, miaka 7 iliyopita niliolewa na mwenzangu ambaye nilimpenda baada ya urafiki wa miaka kama 5 japo baadhi ya ndugu zangu hawakupenda niolewe nae coz hana kazi na wala hakusoma aliishia std7 na mimi ni graduate, hakuwa mtu wa kujishughulisha na biashara wala kuajiriwa bali mishen town tu, ila mimi nilimsaidia kamtaji sababu nilimpenda sikusikia wala kuona.
Mwenzangu huyu kiukweli kuna watu walikuwa wanasema hajatulia ila binafsi kwa upofu wa mapenzi sikulijali hili, lakini tatizo la shughuli kutokuwa na shughuli maalumu nililiona lakini mwenzangu alisisitiza kuwa hawezi kusoma labda biashara japo hakuonyesha juhudi niliamini angebadilika maisha yakaendelea. mie ni muajiriwa nakipato cha kuweza kuitimizia familia hata peke yangu. Niliingia kwenye ndoa nikiamini akiwa mume na baba angebadilika

Tumeingia kwenye ndoa ndio naanza kuona matatizo mengi hap tuna watoto wawili, si muaminifu kwa pesa za watu wala zangu akiazima basi inabidi nilipe kufunika aibu, ni muongo mara nyingi ni uongo usio na sababu sijui ninini?? yote tisa kumi kesi za wanawake ni kibao na ameshaattempt kuoa mara mbili yeye nikazikamata kwenye mtandao, anakaogonjwa na wanawake wazuri na weupe (hata mimi ni mweupe na mzuri lol) so kila nikimkamata ni ugomvi tu na mwisho anaomba mara msamaha lakini anarudia tena. Biashara nilimuanzishia japo biashara yenyewe alikuja kushindwa akafanya eneo la biashara ndio kituo cha kukutana na wanawake wake mpaka nikawa naogopa kupita hiyo mitaa.

Mbali na yote haya jamaa ni abuser, physically, verbally, and emotionally,, huwa napigwa mie nikijaribu kuargue kuhusu tabia yake au mambo ya ndani, pia ananihisi hisi na anapenda kunicontrol kama mtoto. kuna events nyingi sana nikiandika nitawachosha

Sasa wandugu imefikia kipindi mimi mapenzi yameisha na tunawatoto 2, tumejenga (90% ni mchango wangu), gari (90% mchango wangu) na kulisha familia 90% ni mimi, mapenzi yameisha kabisa sio mchezo sidhani kama yatarudi na ninataka kuachana naye, ndoa tulifunga kanisani, nimejaribu kumwambia nataka tutengane kwa muda analia anaomba nafasi ya mwisho anadia ananipenda na anawapenda watoto wake hawezi kuishi mbali nao ila mimi nahisi anaogopa ukali wa maisha na sio mapenzi kwangu, japo wanae kweli anawapenda sana. Natamani nisiondoke lakini ninavyomjua huwa anaomba msamaha zikipita wiki mbili mwezi vituko vinarudi pale pale so naogopa na umri unakimbia natakiwa niwe na misimamo mapema kwani naona hata kwa malezi ya watoto si vizuri kuwa na baba mwenye sifa ya uongo na utapeli mtaani au watu wanakuja hapo kudai watoto wataadapt hizo tabia. naomba nikiri udhaifu wangu katika kupenda naomba msinirushie sana mawe kwa hilo kwa nimeshajua wapi niliteleza.

Naombeni ushauri utakaonisaidia mimi na watoto wangu, based on your experiences maana naogopa hata kuwaambia ndugu zangu kwani watanichua haraka, wameshajitolea hadi nyumba ya mimi kuishi na wanangu, na vikao vimeshakaliwa vingi na kila siku wananiambia niachane nae lakini mimi nilikuwa kichwa hakijakaa vizuri bado, yani siamini kama nitaishi hivi maisha yangu bila mume coz sipendi wala sifurahishwi na maisha ya kuwa single parent at my age of 32, na hili ndio linanifanya nifikirie sana kuhusu maamuzi yangu.
Pole sana dada yangu, sina uhakika kama nakushauri vema, lakini unaweza kujaribu yafuatayo....!
  1. Mkaribishe Munge katika maisha yako, muombe sana, na ikiwezekana huyo mumeo ajue unafanya hivyo....!
  2. Mkalishe chini, umuelezee kwa kina madhara yanayoweza kutokea kutokana na tabia yake....! Katika maisha yenu, na hata watoto wenu pia....!
  3. Jaribu kumrubuni akili kwa kumuaminisha kuwa hata jamii inayowazunguka wanamchora tu..., na wala sio sifa ya kuigwa...! Mfanye aamini kuwa kwa sasa kila mzazi anawashauri watoto wake wasiwe kama yeye...!
  4. Kuwa na msimamo, na ajue hilo, na alione katika maisha yenu ya kila siku.....! Kuwa hutampatia tena chakula chake hadi mmepima na kujua afya zenu kwa kila mmoja wenu...!
  5. Hakikisha nyaraka zote za mali kama vile nyumba, gari, nk ni nyako au watoto wenu...!
  6. Kamwe usifikirie kulipiza kisasi kwa kumtafuta mwanaume nje....!, na yeye ajue uamuzi huo vema....! Ondoa utata wowote kama upo, juu ya uaminifu wako kwenye ndoa....!
  7. Aamini kuwa unaweza kuamua kuachana naye na ukaishi bila yeye...!
  8. Kamwe usiinitiate divorce, lakini muweke katika mazingira ya yeye kuinitiate kama amepania...! Then, have peace of mind....!
  9. Kuwa strong hasa juu ya jinsi anavyokuendesha kama mtoto...! Always get organized on your issues, na mkipishana usiwe talkative, bali usichokipenda na ajue wazi kwamba hukipendi....!
  10. Kama vipi jaribu kuwashirikisha wazazi wake, wasimamizi wenu, na wazee waliowafungisha ndoa...!
Just to say a little....!
 
Pole sana Ndeo.. kuna vitu inabidi ufikiri haraka sana..
  • Kama wewe ndiyo unatafuta mkate wa kila siku wa familia yenye watoto 2, Je kama msongo wa mawazo "stress" ikizidi hadi kukuweka chini, watoto wataishi vipi?
  • Baada ya kuwa na watoto wawili. Je bado unajihesabia una maisha yako au sasa umeshajitoa muhanga kwa maisha ya watoto?
  • Kama umeshajitoa kwa maisha ya watoto.. Maisha unayoishi ndiyo sahihi?
  • Ili watoto wawe na maisha ya uhakika angalau kupata chakula Je, ni lazima wewe ubebe msalaba wa ndoa ambayo inaweza ku-kuua?
  • Je ni lazima ubebe msalaba wa ndoa ili kumwonea huruma yule ambaye anaomba msamaha bila ya kuwa na nia thabiti? na anarudia kukosa..
  • Je dalili gani unataka zitokee ili uone kuwa unachofanya kung'ang'ania ndoa siyo sahihi?
  • Ni wazazi wangapi wameweza kulea familia kama single parent na zikafanikiwa (Ingawa kumbuka hakuna anayependa hilo lakini huwezi kuepuka reality).
Ok. Jiulize mara mbili hayo maswali ..halafu fanya uamuzi.. Unatakiwa kufanya uamuzi wewe mwenyewe bila kushawishiwa..kwani hata kama utakuwa mchungu au mtamu..radha yake utaijua wewe mwenyewe..

Kumbuka kufanya kile unachoona wewe kinafaa mbele ya Mungu hata kama kitapingana na mafundisho..kwani Imani iko ndani ya moyo wako na siyo mahubiri na porojo zetu..
 
uhhh Nimesoma kwa masikitiko habari yako na the way walivyokushauri. Sivutiki na kukushauri muachane ila kwa kuwa wewe ndio baba na mama wa familia you have to do something extra. Huyo baba hajali hata watoto wanaishi vipi hajui wanakula nini au wanaishije wala hana habari nao. Jilinde kwanza wewe na watoto wako.

Wajengee watoto wako msingi wa maisha yao ya baadae ikiwa ni pamoja na property ulizo nazo uhakikishe ziko salama kwa ajili ya watoto wako. Linda afya yako kwanza maana ndio ya muhimu kwa namna alivyo na tabia za ajabu hakikisha kuwa hujiingizi kwenye kitu kitakachohjaribu maisha yako au kukuondoa duniani mapema yaani unprotected sex maana kama bado anaona wanawake wa nje ni wazuri kupita wewe huko huko atakuleleta magonjwa so jilinde sana dhidi ya hilo.

Usije ukafanya jambo lolote ambalo litaonekana kama wewe ndio unamtafuta ili muachane au kuvunja ndoa yako ni yeye ajue au aivunje yeye kwa vituko vyake usije ukamwonyesha kuwa umemchoka.

Wanasema silaha nzuri ya kumshinda mtu ambaye ni muongeaji ni kukaa kimya japo kwa wengine ni dharau ila jariubu as much as u can kutojibishana nae wakati akianza kelele zake.

Sishabikii kuachana ila jali kwanza watoto wako kabla ya kufikiria kuachana wala usimfikirie yeye.
 
Mambo haya magumu....(Kanambia Babu Yangu, KESI za watu, wajifinika Blanket mmoja kuamua vigumu!!!, sasa hivi wawa mbaya wakirudiana!!!)
 
Pole sana ndeonasi, hayo ni maisha yatapita tu, madam ni mumeo na mmefunga ndoa kanisani hukulazimishwa na mtu huna budi kuvumilia, usione wamama wamekaa kwenye ndoa zao ukaona wanafanya kazi ndogo, wanapitia mapito makubwa zaidi ya hayo,usichoke kumkumbusha mlipotoka nina imani bado mapema anaweza badilika,kama ukiona huwezi kabisa nenda kwa mchungaji aliyewafungisha ndoa mweleze akupe ushauri
Bronty, Ah no Muda wa kuwavumilia hawa watu umekwisha
Its the end of mfumo dume!
 
me sikushauri uachane naye since mna watoto na wanamhitaji baba yao. bali unahitaji umwonyeshe kwamba u can survive bila yeye. yaani anza kumfungia pazia. ignore kila anachofanya, ishi hapo ndani kama vile yeye hayupo but at the same time mpe respect. usihoji kuingia wala kutoka kwake. piga pamba kali, kula vizuri always tabasamu. akileta biashara za kujaribu kukupiga mpeleke kwenye vyombo vya dola.
Mh! Na ule ugonjwa wetu wa kisasa umeutafakari hapa!
 
pole mdada...
break up inakuhusu...
bora single parent, kuliko kumvumilia m2 ambaye mwisho wa siku atakuletea maradhi...
kuna vya kuvumilia, sio hili la uzinzi...mtauana kwa magonjwa muache watoto wanateseka, mpige chini fasta uendelee na maisha yako...
Yes 100% No coment!
 
Asanteni kwa michango yenu, tatizo kubwa mapenzi yameisha kabisa na ikumbukwe mapenzi ndio pekee yaliyotuunganisha, mimi simfuatilii tena na hata yeye anajua mapenzi yameisha,, na nataka kuondoka kweli ndani kabisa ya moyo wangu natamani kuondoka ila nikiwaangalia watoto roho inasita! sio yeye ninayemuhurumia bali ni watoto yani simtamani hata kumuona natamani aondoke asafiri aende mbali huko.
Acha kufikiria watoto wewe ndio mwenye watoto katika hali kama hiyo,
Mbona kuna wanawake wengi kwa sasa wao ndio baba wao ndio mama
Piga chini huyo walee wanao! We unafikiri watakuwa wanafaidika nini kama
mambo yenyewe ndiyo hayo? Mama anapigwa wao wanashuhudia acha acha
kabisa.......... Sasa tutaishi kimikataba na si mapenzi tena!
 
kwakweli Ndeonasiae, nimesikitika sana kwa kusoma hii stori yako!
kiukweli inaonyesha inatoka hasa moyoni kwako, akili inanituma kudhani hivo.........
Wazee walipokuwa wanatuasa kuwa maisha ya ndoa ni safari ndefu yenye kuvuka mito na mabonde,
basi nadhani hii kauli sasa unaweza kuithibitisha kwa uzuri kabisa....

Nimesikitika sana binafsi, kweli wanaume wengine tunaingia kwenye ndoa pasipo kujua hata chembe ndogo tu,
ya majukumu yatakayotukabili kwa familia tutakazozijenga hapo baadae....................
Nakiri wazi kabisa anachokufanyia mumeo sio kitendo cha kiungwana kabisa, kwa binadamu na hata mbele ya mwenyezi mungu..........

Ok,ameshakuwa wa hivo sasa ufanye nini ili uendelee na maisha yako kama kawaida, huku watoto hao wawili wanakutizama,
huo nao ni mtinahi mkubwa, lakini ukijipanga vizuri tu sioni shida hapo................

Kwanza lazima ukiri kabisa na ukubali kutoka moyoni kuwa huyo ni mumeo, pamoja na mapungufu yake /visa/vitimbi vyake n.k.
Basi ukilitambua hilo, lazima ujue kuwa jukumu lako ni kujaribu kumweka sawa, aukwa kumshauri, au kwa kutafuta maazo mbalimbali ya kutatua tatizo hili kutoka kwa ndugu zake hata jamaa wa karibu.

Usichukue maamuzi ya haraka, ndoa hizi tunazoendelea nazo zina vioja vya kila aina,
unaweza ukaona la kwako ni zito sana na halibebeki, lakini kumbe kwa jirani ndo kunawaka moto usiombe................
Jikaze mtoto wa kike, weye ni msomi, mungu kakujalia una kakibarua kanakokuingizia kipato kidogo cha kuendesha familia yako,
basi elekeza nguvu zako huko kwa sasa........................

kumbuka una watoto pia...................huyu mumeo naamini kabisa kadri muda unavyokwenda atabadilika tu na kurudi katika njia iliyo sahihi...
wakati mwingine kwenye maisha huwa tunapatwa na maswahibu ya ajabu kiasi kwamba ni kama tunaongozwa na giza fulani hivi..........
hao wanawake wake anaoranda nao nje, itakuja kuonekana baadae kama alikuwa anajiaibisha tu mwenyewe.........kumbuka hapo anahitaji sana ushauri wako.......mshike mkono, mwongoze!ukikata tamaa, basi ni sawa na kuzidi kuchochea moto...............

NGOJA NINYWE KAHAWA KIDOGO,
NITARUDI BAADAE....................
HABARI HII IMEAMSHA HISIA ZANGU NYINGI KWELI MPENDWA..................
 
halafu huwa simuelewi mwanamke ambaye anajimudu kwa kila kitu...kuvumilia upuuzi,tutakanyagwa mpaka lini jamani..umefika wakati tuwakanyage!

Ndoa inahitaji kushikamana,
ndoa ndoana......................
kuna ups and down......................!!!!!!!!!!!!!!!!!
sio kila tatizo linahitaji kukimbiwa ili ufumbuzi upatikane!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
poooooola sana dada'angu! kwangu mim 32 si umri wa kutisha sana coz nina ushahidi wa watu walioolewa zaidi ya umri huo..Ni kweli hupend kuwa single parent,yet u know huyo mtu ni mnafiki,then Y UNG'ANG'ANIE kubaki nae!? Km vip wewe sepa tu, u can meng tu kwa kipato chako japo ckijui na maisha yatasonga tu.....Kumbuka MAOMBI lakini...
 
Back
Top Bottom