Nimeamua kuwajibika na kuachia ngazi!

kujiuzulu haitoshi, inabidi ushitakiwe kwa uzembe. Umesababisha vifo vya wakina mama wajawazito na watoto chini ya miaka mitano kwa ugonjwa wa malaria. haiwezekani muwe mnachezea akili zetu. utalipa garama.
 
Na ndio maana viongozi vijana tunatakiwa kuonesha mfano kama mimi!
Ww umeenda soma au kuzibua mitaro na kufagia?
V2 vingine mnajitakia wakati kuna makampuni yame-Tender kufanya usafi na yanalipwa kutokana na ada yako JKT tuliwaita viherehere wa kujitolea
Iko siku utaoa utakaposhindwa cha asubuhi utajiuzulu?
Msiige kila k2 hata kunya kwa tembo
 
Mwaka mmoja uliopita nilichaguliwa kuwa mwenyekiti wa kamati ya kutunza mazingira hapa chuoni kwetu na nilipitishwa kwa kura nyingi sana na wanachuo wenzangu na kupata ushindi wa kishindo.

Lakini jana katika mkutano wa mwaka wa kamati ya kutunza mazingira, taarifa yangu ya mafanikio yaliyofikiwa na kamati yangu yameonekana kuwa kinyume na matarajio ya wanachuo wenzangu, kwani kulikuwa na malalamiko mengi sana ya uchafu katika mazingira ya chuo, mitaro kuziba kutokana na uchafu, mazalia ya mbu kutothibitiwa na hivyo kusababisha wanafunzi kuugua malaria kwa kiwango cha kutisha.

Nilikubali udhaifu wa kamati yangu katika kutekeleza majukumu yake kama yalivyoainishwa katika muongozo wa kamati yetu, hivyo niliamua kujiuzulu ili kupisha mtu mwingine mwenye uwezo wa kuongoza.

Nawausia wana JF wenzangu na wananchi wote kwa ujumla, muige mfano wangu, pale inapoonekana mmeshindwa kutekeleza majukumu yenu mliopangiwa hata kama ni majumbani kwenu, basi mkubali kuwajibika na kuachia ngazi.

Nawasilisha!

Asante kijana na hongera Karibu CHADEMA
 
Ashakum si matusi bi Zinduna nimeupenda mkao wa Avatar yako; kujiuzulu pekee lilikuwa ndio suluhisho?

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Bi Zinduna mi nataka jua tu lini wamaliza skuli nilete posa? achana na hawa wabara na kiswahili chao kibovu.
 
hongera .. hapo mzizima high school upo kidato cha ngapi..??
 
Uchaguzi wa viongozi hufanyika kila baada ya miaka mitatu, mie nimeachia ngazi baada ya mwaka mmoja tu, si ujasiri huo?
Miaka 3? Hicho kitakuwa chuo gani ambacho ukifika tu unachaguliwa kiongozi- mwaka wa kwanza? Au ni Madrasa?
 
Swala ni kujua chuo gani au kujua kama nilishindwa majukumu na hivyo kuachia ngazi?
Kwani, wewe ulishindwa majukumu AU uliambiwa kuwa umeshindwa majukumu? Kwani hayo mazalio ya mbu yaliyaonekana siku ya mkutano tu ...!? YOU ARE NOT SERIOUS.
 
Ninavyokufahamu uliingia kichwakichwa ukijua kuna ulaji! Baada ya kuona hakuna ulaji unajishebedua, Mawaziri waliotolewa hakuna aliejiuzuru bali mkuu aliwatema kwa kutowajibika zingatia hilo linaweza kuwa swali ktk mtihani wako wa mwisho Zinduna uko chama gani? maana unalolinganisha halifanani na chama twawala hata kidogo.
 
Wakati unakubali majukumu ulikuwa na mpango gani wa utekelezaji? Je, ni nini kilichokukwamisha?

Kujiuzuru peke yake siyo ushujaa na wala siyo maamuzi magumu. Kumbuka kuwa umewapotezea wenzako mwaka mzima wa utekelezaji.

Kuna watu wanataka kuweka kwenye CV zao tu kuwa walikuwa viongozi na kuenjoy prevelages za ustaafu. Ninahitaji kujiridhisha kuwa wewe hauko kwenye kundi hilo, kwa sababu unaonekana kuamini kuwa kujiudhuru ni ushujaa. Ushajaa huanza na kuchukua jukumu unaloliweza, ikitokea likakushinda kama accident ndio unajiuzuru. Sio kuchukua jukumu, unalala mwaka mzima ili mwisho wa mwaka ujiuzuru na kuja JF kudai hongera!
 
Yaani wewe kiongozi wa mazingira unaangalia tu uchafu unajikusanya ili mwisho wa mwaka ujiuzuru halafu ujione shujaa?!!!
 
Wakati unakubali majukumu ulikuwa na mpango gani wa utekelezaji? Je, ni nini kilichokukwamisha?

Kujiuzuru peke yake siyo ushujaa na wala siyo maamuzi magumu. Kumbuka kuwa umewapotezea wenzako mwaka mzima wa utekelezaji.

Kuna watu wanataka kuweka kwenye CV zao tu kuwa walikuwa viongozi na kuenjoy prevelages za ustaafu. Ninahitaji kujiridhisha kuwa wewe hauko kwenye kundi hilo, kwa sababu unaonekana kuamini kuwa kujiudhuru ni ushujaa. Ushajaa huanza na kuchukua jukumu unaloliweza, ikitokea likakushinda kama accident ndio unajiuzuru. Sio kuchukua jukumu, unalala mwaka mzima ili mwisho wa mwaka ujiuzuru na kuja JF kudai hongera!

Swali hilo tuwaulize mawaziri waliotemwa hivi karibuni na mkuu wa nchi, kwa nini walisubiri mpaka wakatemwa, si bora mie niliona ni vyema niachie ngazi kuliko kuwa king'ang'anizi.
Kumbuka nimesema kwamba utendaji wangu haukukidhi matarajio ya wanachuo, sio kwamba nilishindwa, nilifanya kwa kiwango changu, lakini sikukidhi matarajio na ndio maana nikaona ni vyema nipishe mtu mwingine kwa amani kuliko kungoja kutimimuliwa. lilikuwa ni jambo la kidemokrasia kwa sababu niliambiwa nijipime kama naweza kukabiliana na changamoto zilizopo.
 
Miaka 3? Hicho kitakuwa chuo gani ambacho ukifika tu unachaguliwa kiongozi- mwaka wa kwanza? Au ni Madrasa?
Labda kwenu Bara, huku Visiwani hata njuka anaweza kuukwaa uwenyekiti wa kamati ndogo ndogo za chuo,(Kumbuka sijasema upresident wa chuo) kila mtu anajinadi kuonyesha uhodari wake katika kuongoza kamati ndogo ndogo za chuo na kila mwenyekiti wa kamati hutakiwa kuongoza kwa miaka mitatu,(Muda wa kukaa chuoni) lakini kila mwaka kunafanyika tathmini ya uongozi kama unafaa au la, ukifaulu unaweza kumaliza chuo ukiwa kiongozi na kukabidhi madaraka kwa mwingine.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom