Nimeamua kumuacha mke wangu……………..!

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,810
15,398
Ni takriban miezi miwili sasa mgogoro huu umekuwa ukifukuta chini kwa chini na sasa imefikia mahali humu ndani hapakaliki wala hapaliki, ilimradi tafrani kila kitu vululu vululu. Nimelinyamazia jambo hili lakini sasa nimeamua kumuacha mke wangu mama Ngina ili roho yangu ipate kutulia.

Ni miaka mitatu sasa imepita mke wangu hajaenda kuwaona wazazi wake huko kijijini, na hiyo ilitokana na majukumu ya kibiashara anayoiendesha, nakumbuka mwanzoni mwa mwezi wa sita tulikubaliana itakapofika mwezi wa kumi mwaka jana aende kuwaona wazazi wake lakini ilibidi tuiahirishe safari hiyo kutokana na mimi kupata ajali na kulazwa hospitalini. Lakini tangu nipone na kurejea kazini mwenzangu kanibadilikia anataka kwenda kuwaona wazazi wake kwa sababu amewa-miss sana.

Nilikuwa nimepanga aende mwishoni mwa mwaka huu kwa sababu alilazimika kufunga biashara kwa takriban miezi miwili akiniuguza, na tangu afungue hajakaa hata miezi miwili na sasa anataka kufunga tena asafiri. Swala hilo limekuwa likizua manung’uniko na sasa imekuwa nongwa kila nikirudi nyumbani jioni hakuna maelewano na anachotaka ni kusafiri ili akawaone wazazi wake.

Sasa nimeona bora yeshe, nimruhusu aende kuwaona wazazi wake akae huko kwa mwezi mmoja mpaka hamu yake iishe ndipo arejee, lakini kakataa anataka akakae wiki moja tu ndipo arudi kwani hayupo tayari kuniacha peke yangu kwa muda wote huo ikizingatiwa bado sijapona vizuri na ninahitaji ukaribu wake. Nimeona isiwe tabu tumeafikiana na sasa anajiandaa kwa safari wiki ijayo Mwenye enzi Mungu akipenda atasafiri, na mimi nitabaki nyumbani na wanangu Ngina, Ngano na Ngadu. Muombeeni mama yenu, wifi yenu au shemeji yenu safari njema……………………….LOL
 
Mtambuzi nimeipenda sana heading, lakini muda huu nafuatilia kuagwa kwa mpendwa wetu, nitacomment jioni!
 
Kichwa cha habari kama gazeti la udaku vile. . . Lolz

Nwy mtakie safari njema, awarudie na zawadi toka kijijini.
 
Ni takriban miezi miwili sasa mgogoro huu umekuwa ukifukuta chini kwa chini na sasa imefikia mahali humu ndani hapakaliki wala hapaliki, ilimradi tafrani kila kitu vululu vululu. Nimelinyamazia jambo hili lakini sasa nimeamua kumuacha mke wangu mama Ngina ili roho yangu ipate kutulia.

Ni miaka mitatu sasa imepita mke wangu hajaenda kuwaona wazazi wake huko kijijini, na hiyo ilitokana na majukumu ya kibiashara anayoiendesha, nakumbuka mwanzoni mwa mwezi wa sita tulikubaliana itakapofika mwezi wa kumi mwaka jana aende kuwaona wazazi wake lakini ilibidi tuiahirishe safari hiyo kutokana na mimi kupata ajali na kulazwa hospitalini. Lakini tangu nipone na kurejea kazini mwenzangu kanibadilikia anataka kwenda kuwaona wazazi wake kwa sababu amewa-miss sana.

Nilikuwa nimepanga aende mwishoni mwa mwaka huu kwa sababu alilazimika kufunga biashara kwa takriban miezi miwili akiniuguza, na tangu afungue hajakaa hata miezi miwili na sasa anataka kufunga tena asafiri. Swala hilo limekuwa likizua manung'uniko na sasa imekuwa nongwa kila nikirudi nyumbani jioni hakuna maelewano na anachotaka ni kusafiri ili akawaone wazazi wake.

Sasa nimeona bora yeshe, nimruhusu aende kuwaona wazazi wake akae huko kwa mwezi mmoja mpaka hamu yake iishe ndipo arejee, lakini kakataa anataka akakae wiki moja tu ndipo arudi kwani hayupo tayari kuniacha peke yangu kwa muda wote huo ikizingatiwa bado sijapona vizuri na ninahitaji ukaribu wake. Nimeona isiwe tabu tumeafikiana na sasa anajiandaa kwa safari wiki ijayo Mwenye enzi Mungu akipenda atasafiri, na mimi nitabaki nyumbani na wanangu Ngina, Ngano na Ngadu. Muombeeni mama yenu, wifi yenu au shemeji yenu safari njema……………………….LOL

Ni vizuri ulivyoamua kumuacha mke wako aende kuwaona wazazi na kurudi baada ya wiki moja hakuna sijaona sababu ya msingi hapo ya kumzuia kwenda kuwaona wazazi, hizo biashara zipo tu na zitaendelea kuwepo kutafuta pesa hakuna mwisho. Labda kama unalako jambo zaidi ya ulioandika. NAMTAKIA SAFARI NJEMA, AENDE NA KURUDI SALAMA BAADA YA WIKI MOJA.
 
lol..................yan io headin mtambuz duh! nilikuwa nawasubiri kina canta na king waje wakushambulie hapa mmh.
nami namtakia mama ngina safari njema.
 
Heshima yako baba,
Dah hiyo heading imenistua nikampigia mama kabla sijasoma akawa hapokei na uzi ukawa umeshafunguka lol!
Sijui ingekuwaje kwa nilichokuwa nimepanga kumuuliza,
Poa tunamtakia mama safari njema,na mungu ampeleke salama na amrudishe salama.
 
imeaandikwa mwanamume atawaacha wazazi wake naye ataambatana na mkewe watakuwa mwili mmoja.....
sasa hapa kuna vitu vya kuvikubali kwanza (hii kwa uelewa wangu) inamaana mwanamke yeye haachi wazazi wake hivyo lazima aende maandiko hayajamfunga lakini la pili ni kwamba sielewe vizuri mkiwaacha wazazi ukiambatana na mkeo inamaana unaenda kwao hivyo nenda naye ka vipi kwa sababu maandiko hayakutoa mnaaenda wapi
lakin katka hali ya kawaida ni vizuri akaenda likizo ni siku nyingi akirudi atakuwa na akili mpya na mawazo mapya kuliko ukin'gangania akae hapo (japo kwa shida na raha) vumilia m2 wangu
 
Duuu isipokuwa makini huwezi kuelewa kinachoongelewa hapa maana kichwa cha hbr ni kizito ...okay twamtakia safari njema.
 
lol..................yan io headin mtambuz duh! nilikuwa nawasubiri kina canta na king waje wakushambulie hapa mmh.
nami namtakia mama ngina safari njema.
Huyu mdingi wetu sometimes mtata sana1
Mie mwenyewe niliposoma heading nikajua labda yule dada glady aliyemchungulia siku zile kesha muweka dingi yetu mtu kati lol!
 
Kichwa cha habari kiliniudhi sana kabla sijaisoma hii habari. Maana sipendi mtu anayezungumzia kuacha mke. Lakini baada ya kuisoma habari nimekuelewa. Mungu ampe shemeji ulinzi wake wakati woote wa safari. Ameni
 
Mtambuzi nimeipenda sana heading, lakini muda huu nafuatilia kuagwa kwa mpendwa wetu, nitacomment jioni!

Unajua hiyo safari sikuipenda kwa sababu sipendi mke wangu akae mbali na mimi hata kwa siku moja, na ndio sababu sikutafakari hata kichwa cha habari kiweje................ hata hivyo nimeona umeelewa
 
Anko umefanya la mana sana kumuachia aende kuwaona wazee,siunajua sie wanawake lazima ukamuone Baa na Maa ndio roho itulie....
ulimpa mwezi ulikua ume nuna au?
 
Anko umefanya la mana sana kumuachia aende kuwaona wazee,siunajua sie wanawake lazima ukamuone Baa na Maa ndio roho itulie....
ulimpa mwezi ulikua ume nuna au?

Nilikuwa natishia Nyau, akikaa mwezi si nitazimia..............He! mwezi bila naniliu!
 
Back
Top Bottom