Nimeamua kujiunga na CCM

Huu ni unafiki tu, yaani uamuzi wako wa kujiunga na CCM nao ni mada ya kujadiliwa? Kama una mapenzi ya dhati na CCM ungejiunga nao kimya kimya. Unatutangazia ili tuamini kwamba CCM bado inaungwa mkono na Watanzania? Waacheni ambao hawakufanikiwa kuunda serikali waseme, mlio serikalini fanyeni kazi, vitendo vionekane, ndipo wananchi watawakubali. Kama unafanya kazi, wananchi wataona, huhitaji kuwatangazia wananchi kwamba unafanya kazi.
 
Na mimi napata hisia kumbe vijana kweli ni tatizo katika kuona mbele. Ndiyo hawa wanaoleta thread tasa humu na wale wanaogombana kule Bavicha. They are one and the same.

Ni vijana wa ccm. vijana wa CHADEMA bado hawajawa misukule kama hawa wa magamba.
 
Mimi nikutakie mema katika harakati za kutekeleza haki yako ya kikatiba.

Mimi nikubaliane na wewe katika pongezi zako kwa Rais Kikwete. Kwa kweli tumshukuru Mungu kwa jinsi huyu bwana alivyopewa moyo wa ustahimilivu na katika kulea na kuulinda uhuru wa watu kutoa maoni yao bila bughudha. Kwa kweli ni vigumu kuamini kwamba hawa leo wanaomtukana kila aina ya matusi wangekuwa wanashikilia dola wangetoa uwanja mpana wa kutoa maoni yao na wakati mwingine kukashfu kama ilivyo sasa.

Ni vigumu kujua thamani ya uhuru huu mpaka ama tuukose au kwa kuangalia wenzetu wanavyohangaika kutoa maoni yao na kuishia ama kuuawa au kuswekwa ndani. Mfano wa Besigye na Museveni kule Uganda unatosha kutukumbusha kwamba tuna tunu ambayo tunatakiwa kuiheshimu. Lakini ukiwa na fikra za karibu hoja hii itazaa majibu makali, hata hivyo ukweli ndivyo ulivyo. Unauma.


Wanasema ukimsifu baba yako mbio, msifie na yule aliyemkimbiza.

Rais kuruhusu uhuru wa maoni sio zawadi, ni wajibu-anatekeleza katiba aliyoapa kuilinda na kuitetea.

Uhuru wa kutoa maoni huko tuendako hauepukiki-mfano mtu anawezaje kuzuia uhuru wa kutoa maoni ktk social networks kama facebook? Lakini pia Rais wetu ni beneficially wa uhuru wa kutoa maoni.

Moja ya sababu ya kushinda kwa kishindo 2005 ni kuandikwa vizuri na vyombo vya habari wakati wagombea wenzake walikuwa wamebanwa kweli kweli. Hawezi kuuuma mkono unaomlisha. Sio dhambi kumkosoa Rais, maana amechaguliwa na wananchi ili awatumikie.
 
ukiamua kujiunga huna haja ya kutujulisha sisi ,upeo wako ndo umefikia hapo, pole
 
ondoa ujinga wako unasumbul4wa na elimu ndogo ya uraia hata hujui maana ya mfum6 wa vyama vingi nyie ndo mnapigwa mawe acha mawazo ya ukasuku na ulamba viatu be a man ie. Kuwa mwanaume

As if you yourself are a man enough! You wouldn't allow to be mentally enslaved by Slaa and his coterrie! You will at some stage require an emancipation in order to restore your manhood !
 
Rais kuruhusu uhuru wa maoni sio zawadi, ni wajibu-anatekeleza katiba aliyoapa kuilinda na kuitetea.

Uhuru wa kutoa maoni huko tuendako hauepukiki-mfano mtu anawezaje kuzuia uhuru wa kutoa maoni ktk social networks kama facebook? Lakini pia Rais wetu ni beneficially wa uhuru wa kutoa maoni.

Moja ya sababu ya kushinda kwa kishindo 2005 ni kuandikwa vizuri na vyombo vya habari wakati wagombea wenzake walikuwa wamebanwa kweli kweli. Hawezi kuuuma mkono unaomlisha. Sio dhambi kumkosoa Rais, maana amechaguliwa na wananchi ili awatumikie.
Hakuna asiyejua kwamba hiyo ni constitutional right. Lakini ni katiba ngapi zinatoa haki za msingi (bill of rights ) lakini viongozi walioko madarakani wanaamua kuzikalia hizo haki.

Ndo maana nimekupa mfano wa katiba ya Uganda ambayo iko more elaborate kuliko yetu, lakini muulize Kizza Besigye kama ameweza kuzi-enforce hizo haki zake. Kwa hiyo ni lazima uelewe kwamba kukubali kuzitekeleza hizo haki ni suala la utashi na uungwana wa mkuu wa dola.

Rais wetu ni democrat anayeruhusu watu kufikia hatua hata ya kuingilia staha yake na familia yake wakati hata huko CDM kuna watu wakimkosoa mwenyekiti tu tayari wako matatizoni. Muulize Kafulila!
 
Uamuzi wako ni kwenda CCM ni wako maana hatujui ulikuwa wapi. Nadhani unaenda kufua magamba! Hujui kabisa misingi ya Demokrasia. Demokrasia inasimama juu ya uwazi, uwajibikaji na kupinga ufisadi. CCM hakuna demokrasia hivyo nenda tu ukaendeleze unafiki wa ccm.
 
Kwakweli pamoja na mapungufu yote ambayo binadam wanayo na mfumo wowote unayo, CCM ni chama cha demokrasia ya kweli, kwa kukubali kukosolewa na kujirekebisha, mazingira yananionyesha CHADEMA kingekuwa madarakani kisengeruhusu kusemwa hv kama CCM inavyotoa uhuru wa kukosolewa na Rais Kikwete anatufundisha tuvumiliane mpaka tutakapozoea kusema na kusemwa.

Ushahidi ni jinsi tu mwenyekiti Mbowe anavyopingwa kwenye kikao na Zitto na kumtumia Lema kumshambulia Zitto, je siku wakiwa ikulu atakubali magazeti ya mpinge?

Hahahahaha, nina mashaka na maelezo yako. Kama wakishughulika kiyakinifu na hili moja la MAFISADI nitajua kweli wanakubali kukosolewa. Na hivyo wengi tutajiunga tena.
 
unajua waweza kumtambua mtu hata kwa maandishi tu.....hao wanaojiunga na chama cha magamba eti kwa sababu tu ****** mvumilivu......mmmmmh ninashaka na IQ ya hao watu !!!!!!!!! umaskini,ufisadi,rushwa na mambo yooote yanayoondelea bado kikwete anafaaa,,,,,hongereni sana nadhani kuna jambo siwezi kushangaa hata mchawi ana wapambe wake
 
Kwakweli pamoja na mapungufu yote ambayo binadam wanayo na mfumo wowote unayo, CCM ni chama cha demokrasia ya kweli, kwa kukubali kukosolewa na kujirekebisha, mazingira yananionyesha CHADEMA kingekuwa madarakani kisengeruhusu kusemwa hv kama CCM inavyotoa uhuru wa kukosolewa na Rais Kikwete anatufundisha tuvumiliane mpaka tutakapozoea kusema na kusemwa.

Ushahidi ni jinsi tu mwenyekiti Mbowe anavyopingwa kwenye kikao na Zitto na kumtumia Lema kumshambulia Zitto, je siku wakiwa ikulu atakubali magazeti ya mpinge?

Kwa akili zako hizo, mbona umechelewa sana kubaini kuwa ccm ndipo mahali pako muafaka!!
 
Hakuna asiyejua kwamba hiyo ni constitutional right. Lakini ni katiba ngapi zinatoa haki za msingi (bill of rights ) lakini viongozi walioko madarakani wanaamua kuzikalia hizo haki.

Ndo maana nimekupa mfano wa katiba ya Uganda ambayo iko more elaborate kuliko yetu, lakini muulize Kizza Besigye kama ameweza kuzi-enforce hizo haki zake. Kwa hiyo ni lazima uelewe kwamba kukubali kuzitekeleza hizo haki ni suala la utashi na uungwana wa mkuu wa dola.

Rais wetu ni democrat anayeruhusu watu kufikia hatua hata ya kuingilia staha yake na familia yake wakati hata huko CDM kuna watu wakimkosoa mwenyekiti tu tayari wako matatizoni. Muulize Kafulila!
Ni ukweli usiopingika kuwa pamoja na mapungufu makubwa ya JK kiuongozi, bado ni kiongozi aliyethubutu kuruhusu watu kujadili na kutoa maoni yao kwa uhuru zaidi, kuliko kipindi cha mkapa.

Lakini unapozungumzia chama kama ccm, binafsi nisiye na chama, ccm hakina mvuto tena na wananchi wengi wanaelewa hilo, CDM kinakubalika ni jambo lililowazi. CCM wamekubali kukosolewa kwa sababu CDM wanatoa hoja ambazo ccm hawawezi kuzipinga na kubwa zaidi wao wenyewe wamegawanyika na makundi yao.

Hivyo mtu kuhamia ccm ni uhuru wake kikatiba lakini LOGIC ya kuhamia kwa sasa siioni.
 
Uhuru wa umaskini wewe vipi ? Rais gani hajui alifanyalo? Angalia Burundi na Rwanda chumi zao zivyopaa kwa kasi pamoja na mataizo waliyapata, tatizo la wenye akili kama zako waoafikiri haki ya uhuru ni hisani ya mtu fulani hiyo hata mbiguni haipo, uhuru ni haki ya kila mtu kama ilivyo haki hupiganiwa ndivyo pia na uhuru.
Mimi nikutakie mema katika harakati za kutekeleza haki yako ya kikatiba.

Mimi nikubaliane na wewe katika pongezi zako kwa Rais Kikwete. Kwa kweli tumshukuru Mungu kwa jinsi huyu bwana alivyopewa moyo wa ustahimilivu na katika kulea na kuulinda uhuru wa watu kutoa maoni yao bila bughudha. Kwa kweli ni vigumu kuamini kwamba hawa leo wanaomtukana kila aina ya matusi wangekuwa wanashikilia dola wangetoa uwanja mpana wa kutoa maoni yao na wakati mwingine kukashfu kama ilivyo sasa.

Ni vigumu kujua thamani ya uhuru huu mpaka ama tuukose au kwa kuangalia wenzetu wanavyohangaika kutoa maoni yao na kuishia ama kuuawa au kuswekwa ndani. Mfano wa Besigye na Museveni kule Uganda unatosha kutukumbusha kwamba tuna tunu ambayo tunatakiwa kuiheshimu. Lakini ukiwa na fikra za karibu hoja hii itazaa majibu makali, hata hivyo ukweli ndivyo ulivyo. Unauma.


Wanasema ukimsifu baba yako mbio, msifie na yule aliyemkimbiza.
 
nimewahi soma mahali....."IF YOU CANT WIN THEM....JOIN THEM" and my teacher asked the group of boycotting students
"CAN YOU WAGE A WAR THAT YOU ARE GOING TO LOSE?" Nikumbukacho waliokuwa na masikio walisikia ...na waliokuwa "mashujaa" walisonga
 
nimewahi soma mahali....."IF YOU CANT WIN THEM....JOIN THEM" and my teacher asked the group of boycotting students
"CAN YOU WAGE A WAR THAT YOU ARE GOING TO LOSE?" Nikumbukacho waliokuwa na masikio walisikia ...na waliokuwa "mashujaa" walisonga

Hapo kweye RED ni vizuri maneno yako yangeendana na vitendo, kwa kuwa tumeshindwa vita ya kukomesha ushoga Tanzania, basi usichelewe ungana nao uanze kupakuliwa na wewe.
 
Kwakweli pamoja na mapungufu yote ambayo binadam wanayo na mfumo wowote unayo, CCM ni chama cha demokrasia ya kweli, kwa kukubali kukosolewa na kujirekebisha, mazingira yananionyesha CHADEMA kingekuwa madarakani kisengeruhusu kusemwa hv kama CCM inavyotoa uhuru wa kukosolewa na Rais Kikwete anatufundisha tuvumiliane mpaka tutakapozoea kusema na kusemwa.

Ushahidi ni jinsi tu mwenyekiti Mbowe anavyopingwa kwenye kikao na Zitto na kumtumia Lema kumshambulia Zitto, je siku wakiwa ikulu atakubali magazeti ya mpinge?

Usiku mwema
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom