Nimeacha kuishabikia Arsenal

Wakuu nimeamua kwa hiyari yangu na pasipo kulazimishwa na mtu yoyote kuitosa club ya Arsenal.Nina sababu nyingi za kuitosa The Gunners.

[1] Kukwepa magonjwa ya moyo.

[2] Imeshindwa kutwaa kikombe chochote kwa muda mrefu sana.

[3] Arsenal imekuwa gulio la kuuza wachezaji wake mahiri kwa Club nyingine

Baada ya kutafakari kwa kinaa na bila kushawishiwa au kulazimishwa na mtu au kikundi chochote nimeamua kujiunga na Club ya Manchester United yenye kutumia uwanja Old Trafold.Zipo sababu kibao lakini nitazitaja chache.

[1] Manchester United inaongozwa na manager mwenye mafanikio makubwa kuliko makocha wote wa UK.

[2] Manchester United imechukua ubingwa wa ligi kuu ya UK mara 19,timu inayoikaribia ni Liverpool pekee yake imechukua ubingwa mar 18 tu.

[3] Manchester United inakaribia kuweka rekodi mpya kwa kuchukua ubingwa mara 20, mpaka leo hii inaongoza ligi kwa tofauti ya point 12.

[4] Ukiishabikia Mancheter United uwezekano wa kupatwa na magonjwa ya moyo na kisukari ni mdogo sana.Kila wakati una kuwa ni mtu wa kucheka na kufurahia maisha duniani.

[5] Mwaka 1999 iliweka historia kwa kuchukua vikombe vitatu.Ubingwa wa ulaya.ubingwa wa Uk na Kombe la ligi.

[6] Mashabiki wa Manchester United ni wakarimu, wapole na wenye kujua kuchambua soka. Sifa hizo zinanihakikishia kwamba nitapokelewa vizuri.

Wapenzi wa Arsenal mtanisamehe sana kuhama club ni jambo la kawaida kwa mashabiki kama ilivyo kawaida kwa wachezaji. Siwezi kuendelea kusononeka hapa duniania kisa kupenda Club mbovu.

Nakala: Wacha1 Idimi Belo Steve Dii Mphamvu Dark City gfsonwin The Boss BAK Rejao Viper mfarisayo MwafrikaHalisi Kibunango Maxence Melo EMT Balantanda Mwita Maranya

bado hautengui kauli?
 
Arsenal 1 Bayern Munich 5

FC-Bayern-Muenchen-v-Arsenal-FC-UEFA-Champions-League
 
Manchester Unted 1 CSKA 0

Ni hayo tu ndugu zangu nimeona bora niwashirikishe kiduchu raha za dunia.

2E13AED100000578-0-image-a-29_1446678346589.jpg
 
Moja kati ya magoli bora kuwahi kushuhudiwa katika karne ya 21.

2E14594800000578-0-image-a-31_1446678354062.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom