Nilizuia umwagaji wa damu Tanzania-Dr Slaa

KATIKA hili huwa sitafuni maneno! Dr. Slaa hakushinda urais mwaka 2010 na wale wanaoamini hivyo ni ama tu wanaamua kueneza propaganda au hawafanyi tafakuri za kina! Kwanini naamini hakushinda:

  1. Hadi General Election 2010 ( nap engine hadi sasa), nguvu ya CHADEMA nchini ilikuwa unevenly distributed. CHADEMA hawakuwa na ufuasi wa kutosha mikoa ya Lindi, Mtwara, Dodoma, Singida, Pwani, Morogoro, Tanga, Ruvuma, Rukwa, Tabora, Iringa Pamoja na Zanzibar. Hadi wanaingia kwenye uchaguzi (nna pengine hadi sasa), zaidi ya nusu ya nchi ilikuwa haijafikiwa na CHADEMA na wala hawakuwa na japo na ofisi huko!! Huwezi kushinda nafasi ya urais wakati zaidi ya nusu ya nchi hauna ufuasi wa kutosha!
  2. Hata ile mikoa ambayo ilikuwa na ufuasi wa kutosha, bado ufuasi huo ulikuwepo kwenye baadhi tu ya wilaya/majimbo na sio mikoa mizima! Hii ilikuwepo Kilimanjaro, Arusha, Kagera, Manyara na hata Mwanza.
  3. Mikoa ambayo CHADEMA ilikuwa na nguvu (Namba 2 bove), CCM pia ilikuwa na ufuasi wa kutosha....hivyo CCM ilitoa changamoto kubwa huko kuliko changamoto ya CHADEMA dhidi ya CCM kwenye mikoa ambako CCM ilikuwa na nguvu.
  4. Mikoa ambayo ilikuwa ni ngome ya CCM, CHADEMA ilikuwa ni mahututi kabisa lakini hii ni kinyume kwa sehemu ambako ilikuwa ni ngome ya CHADEMA….huko CCM haikuwa mahututi!
  5. Ilikuwa ukisikia sehemu Fulani CCM wana nguvu, basi ushindi wao huko unakuwa wa kishindo…..na hii ilitokea kwenye maeneo mbalimbali ya nchi! Kinyume chake, ilikuwa hata ukisikia sehemu fulani CHADEMA wana nguvu, basi ushindi wao ungekuwa wa kawaida (Less than 65%) kwavile CCM nako walikuwa na wafuasi wa kutosha kuzuia massive winning!
Huu ni ukweli ulio wazi ingawaje wafuasi na mashabiki wa CHADEMA wasioifahamu vizuri CHADEMA wanataka kuukataa na kuishia kulalamika eti kulikuwa na wizi wa kura!!!! Hata kama palikuwa na wizi wa kura, bado hata kama ingefanyika ON and OFF, still kura zisingetosha kuipa CHADEMA ushindi!!
Dr. Slaa na wenzake wanalifahamu hili, lakini katika kuendeleza propaganda za kisiasa ndipo wanawahadaa wafuasi wao kwamba waliibiwa kura!!! Na hakika CHADEMA haitakuja kushinda uchaguzi hadi watakapobaini na kukubali kwamba maeneo mengi ya nchi hawajafika huko!!! Kukubali peke yake haitoshi, ni hadi pale watakapofanya jitihada za makusudi kukieneza chama sehemu mbalimbali za nchi; hususani kwenye mikoa niliyoitaja in (1) above!!
CHADEMA hawatakuja kushinda uchaguzi (kwa nafasi ya urais) hadi watakapoondokana na dhana ya kwamba Watanzania watawachagua tu wasipowafikia! Tutake tusitake, hadi General Election inafanyika 2010, vijiji vingi walikuwa wanazikana, wanafanya sherehe, wanachanganyikana na makada wa CCM ambao wameenea from the grassroot!


Punguza jazba mkuu.Hata ukitumia hekima kidogo tu watu watakuelewa.
 
Anaweweseka baada ya kuona nyota ya zitto inang'aa zaidi yake anatafuta pa kutokea,mpuuzeni tu huyo mzee..anazeeka vibaya,eti kiongozi mkuu wa upinzani,ina maana yeye ni mkubwa kuliko mwenyekiti wake?

Wewe ni sawa na muhuni tu tena inawezekana wewe ni Lusinde.
 
Taarifa ya habari ya ITV imeonyesha umati wa watu uliokuwa ukimsikiliza dr. Slaa na kuhamia cdm.
Kweli magamba hawana chao mwaka huu!

Mkuu wangu acha mavuvuzela walioko hapa JF wazidi kujidanganya.Wanadhani kutoka mapovu hapa JF watazuia moto wa mabadiliko.Hawa ni sawa na wahuni na niwakuwapuuza tu kama tulivyompuuza Role model wao Lusinde.
 
Ni aje Mkuu Waberoya!!! Mbona vijembe vyako kwa Dr Slaa haviishi!? amekukosea nini hasa? kulikoni kati yako na Dr? Mbona Watanzania wengi tunasikia mengi toka kwake ya kufurahisha akili na kukipa CHADEMA mvuto mkubwa miongoni mwa Watanzania ukilinganisha na chama kingine chochote cha siasa na hadi sasa kuwa tishio kubwa la magamba?

Huoni magamba wanahaha huku na kule kuhofia kuja juu kwa kasi kwa CHADEMA na hivyo kuingiwa na wasiwasi kwamba watapokonywa tonge lao mdomoni ifikapo 2015!? Hebu acha hizo banaaa Dr Slaa amefanya mengi sana katika kutufungua macho Watanzania ili kujua udhalimu mkubwa unaofanywa ndani ya nchi yetu. Unakumbuka ile list ya mafisadi wa magamba ambayo walikuwemo pia Mkapa, Kikwete, Lowassa na wengineo ambao baadhi yao walitishia kwamba Dr Slaa afute kauli yake vinginevyo watambandisha kizimbani kwa kuwaharibia "reputation" zao? Hakuna hata mmoja aliyefungua mashtaka na ukweli ulipodhihiri ikabainika wote ni mafisadi. Unakumbuka Dr Slaa alipoanza kuzungumzia ufisadi mkuwa wa EPA!?

Nakumbuka Kikwete alikuwa Arusha kama sikosei kwenye sikukuu ya Wafanyakazi ambapo alitoa hotuba na kudai hakuna ufisadi wowote wa EPA kule BoT bali anachofanya Dr Slaa ni kutaka kusababisha umwagaji damu nchini, lakini ukweli leo hii Watanzania wengi tunaujua. Hebu acha hizo bana hata siku moja basi uandike mazuri mengi yaliyofanywa na Dr badala ya kumpiga vijembe kila kukicha.

Dr Slaa yuko juu sana fungua macho uyaone mengi aliyoyafanya hata kusababisha magamba waanze kuweweseka kwamba ile dhana yao kwamba, "CCM itatawala Tanzania milele" inaweza kabisa isiwe kweli. Pamoja na propaganda za hali ya juu kwamba CHADEMA ni chama cha Wachagga na Wakristu lakini bado wanapeta tu katika kila kona ya nchi na sasa magamba wanaweweseka. Kamwe Dr Slaa hawezi kufananishwa na msanii Kikwete.




Mkuu wangu ninachomshukuru Mungu wakati wanafiki wakiendeleza chuki na hila zao hapa JF huko mikoani mamia kwa maelfu wanazidi kujiunga na jeshi la ukombozi CDM.Wakati wanafiki hawa wakijiapiza CDM isingeshinda Arumeru kutaharuki Nassari alikuwa akiapishwa Dodoma.Naomba nimueleze Dr Slaa asitishwe wala kukatishwa tamaa na wala makombo.Tanzania yote imeshaamua yeye ndiye Rais ajaye!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Siamini kama hii nchi inao watu jasiri wakuingia barabarani zaidi ya watu wa AR,Tarime,Mwanza na Mbeya
Mabwege bado ni wengi sana nchi hii tunahitaji muda kutoka katika ukoloni wa Magamba
 
Mkuu wangu ninachomshukuru Mungu wakati wanafiki wakiendeleza chuki na hila zao hapa JF huko mikoani mamia kwa maelfu wanazidi kujiunga na jeshi la ukombozi CDM.Wakati wanafiki hawa wakijiapiza CDM isingeshinda Arumeru kutaharuki Nassari alikuwa akiapishwa Dodoma.Naomba nimueleze Dr Slaa asitishwe wala kukatishwa tamaa na wala makombo.Tanzania yote imeshaamua yeye ndiye Rais ajaye!


Naam Mkuu huo ni ushahidi tosha kwamba pamoja na kasoro zote zilizoandikwa hapa kuhusu Dr Slaa na CHADEMA lakini imejidhihirisha sasa kwamba CHADEMA inakubalika sana katika kona mbali mbali za nchi yetu hata ndani ya magamba na ushahidi wa hili ni wimbi la wale ambao walikuwa ndani ya magamba wanavyorudisha kwa kasi kadi zao za magamba ili kuwa wanachama rasmi wa CHADEMA. Nguvu ya umma kamwe haiwezi kushindwa. Saa ya ukombozi wa nchi yetu imewadia na hakuna kurudi nyuma.

:peace::peace::peace:


Alutta Continua.
 
Back
Top Bottom