Nilizuia umwagaji wa damu Tanzania-Dr Slaa

...Niliisikiliza ile kauli nikabaki nikijiuliza tu kama inawezekana kweli kufanya siasa bila kuwa muongo katika mazingira yetu, masikini mie...
 
Hakuna aliyebisha mkuu!

tatizo una kremu mno! una paper??
rudi hoja zangu ulichoandika hapa ni sawa kabisa

kumbuka nimesema udhaifu wa chama, udhaifu wa watanzania

sasa kuchukua sentensi moja kuonyesha ninamchukia unakuwa unakosea!!! nimeweka sababu kwanini mwongo!! hujakubali kuwa kasema uongo unasema mazuri yake!! kwani nani kabisha??

BAK vipi?

Nina paper ya Dr Slaa kupasi lazima uondoke na 90% vinginevyo umepigwa chini...Hata vyama vikongwe duniani kama Republicans na Democratics vina kasoro nyingi itakuwa CHADEMA ambayo haijafikisha hata miaka 30 tangu kuundwa!? Taratibu kasoro ambazo zitaweza kushughulikiwa haraka basi CHADEMA itazishughulikia na zile ambazo zinahitaji muda mrefu kushughulikiwa nazo zitasubiri lakini sidhani hata siku moja utaacha kuziona kasoro mbali mbali zilizomo ndani ya CHADEMA lakini nakuhakikishia pamoja na kasoro zote ulizozitaja bado CHADEMA ni tishio kubwa kwa magamba kuliko CUF, NCCR_Mageuzi, TPL na chama chochote kingine cha siasa nchini na kama kutakuwa na uchaguzi halali basi Watanzania wengi pamoja na kasoro ulizozitaja hapo juu wataridhia kuikabidhi nchi kwa CHADEMA.

 
KATIKA hili huwa sitafuni maneno! Dr. Slaa hakushinda urais mwaka 2010 na wale wanaoamini hivyo ni ama tu wanaamua kueneza propaganda au hawafanyi tafakuri za kina! Kwanini naamini hakushinda:

  1. Hadi General Election 2010 ( nap engine hadi sasa), nguvu ya CHADEMA nchini ilikuwa unevenly distributed. CHADEMA hawakuwa na ufuasi wa kutosha mikoa ya Lindi, Mtwara, Dodoma, Singida, Pwani, Morogoro, Tanga, Ruvuma, Rukwa, Tabora, Iringa Pamoja na Zanzibar. Hadi wanaingia kwenye uchaguzi (nna pengine hadi sasa), zaidi ya nusu ya nchi ilikuwa haijafikiwa na CHADEMA na wala hawakuwa na japo na ofisi huko!! Huwezi kushinda nafasi ya urais wakati zaidi ya nusu ya nchi hauna ufuasi wa kutosha!
  2. Hata ile mikoa ambayo ilikuwa na ufuasi wa kutosha, bado ufuasi huo ulikuwepo kwenye baadhi tu ya wilaya/majimbo na sio mikoa mizima! Hii ilikuwepo Kilimanjaro, Arusha, Kagera, Manyara na hata Mwanza.
  3. Mikoa ambayo CHADEMA ilikuwa na nguvu (Namba 2 bove), CCM pia ilikuwa na ufuasi wa kutosha....hivyo CCM ilitoa changamoto kubwa huko kuliko changamoto ya CHADEMA dhidi ya CCM kwenye mikoa ambako CCM ilikuwa na nguvu.
  4. Mikoa ambayo ilikuwa ni ngome ya CCM, CHADEMA ilikuwa ni mahututi kabisa lakini hii ni kinyume kwa sehemu ambako ilikuwa ni ngome ya CHADEMA….huko CCM haikuwa mahututi!
  5. Ilikuwa ukisikia sehemu Fulani CCM wana nguvu, basi ushindi wao huko unakuwa wa kishindo…..na hii ilitokea kwenye maeneo mbalimbali ya nchi! Kinyume chake, ilikuwa hata ukisikia sehemu fulani CHADEMA wana nguvu, basi ushindi wao ungekuwa wa kawaida (Less than 65%) kwavile CCM nako walikuwa na wafuasi wa kutosha kuzuia massive winning!
Huu ni ukweli ulio wazi ingawaje wafuasi na mashabiki wa CHADEMA wasioifahamu vizuri CHADEMA wanataka kuukataa na kuishia kulalamika eti kulikuwa na wizi wa kura!!!! Hata kama palikuwa na wizi wa kura, bado hata kama ingefanyika ON and OFF, still kura zisingetosha kuipa CHADEMA ushindi!!
Dr. Slaa na wenzake wanalifahamu hili, lakini katika kuendeleza propaganda za kisiasa ndipo wanawahadaa wafuasi wao kwamba waliibiwa kura!!! Na hakika CHADEMA haitakuja kushinda uchaguzi hadi watakapobaini na kukubali kwamba maeneo mengi ya nchi hawajafika huko!!! Kukubali peke yake haitoshi, ni hadi pale watakapofanya jitihada za makusudi kukieneza chama sehemu mbalimbali za nchi; hususani kwenye mikoa niliyoitaja in (1) above!!
CHADEMA hawatakuja kushinda uchaguzi (kwa nafasi ya urais) hadi watakapoondokana na dhana ya kwamba Watanzania watawachagua tu wasipowafikia! Tutake tusitake, hadi General Election inafanyika 2010, vijiji vingi walikuwa wanazikana, wanafanya sherehe, wanachanganyikana na makada wa CCM ambao wameenea from the grassroot!

 
Mtoa maada you have facts sana na naomba kama Dr. Slaa au Zitto n.k watapita hapa wa print na kusoma vema na kufanyia kaz umenena kwa hoja ambazo kama sisi Chadema tunakurupuka hatuwez kukuelewa.

Tunahitaji kujenga chama chetu ebu fikiria mpaka sasa viongoz wa chadema bado hawana mashina hasa kusini mfano Ruvuma, Rungwe, Mtwara n.k panahitajika hekima na lazima waje haraka ili kuandaa mawakala wa kila kona ya nchi for 2014-2015.
Ukweli 2010 Dr. aliibiwa kura nying sana na usalama wa taifa.
Mfano Kyela walitangaza matokeo ambayo ni uongo kuwa JK alimzid Slaa nakataa kabisa wanakyela tulimchagua Rais wa Chadema na Mbunge CCM na hata Slaa aliomba hivyo.
Mie nilikuwa msimamiz msaidiz kwan tulikuwa likizo dat time Vituo vyote vya Kyela Slaa alishinda kwa kishindo matokeo yetu tuliojumlisha yalikuwa yanaonesha kiwilaya Jk kamwagwa sana.
Ajabu matokeo yakaja tofauti toka TBC tulishangaa na hatukujua tufanyaje iliuma sana kwa wazee na vijana.
Slaa alishinda hata kama wabunge wa CDM wangepatikana wa 3 uraís JK hakushinda.
Nilikuwa wizara moja nyeti mwaka jana kwa field nilikuta mazungumzo watu wanajilaumu kuwa kwa nini tulimsaidia kuiba kura za Dr. Slaa huyu Jk n.k

I mean mpaka sasa CHADEMA IJIPANGE TUTASHIKA NCHI.
 
Kwa kweli hata mie uwa nawashangaa sana wale wanaosema Slaa alishinda urais kaibiwa kura..

Hakuna mwenye ushahidi sio Slaa, mwenyewe wala Pro-Chadema, mwenye takwimu kamili za matokeo, Slaa mpaka leo ukimwambia lete idadi za kura zilizoibiwa anakuletea matokeo ya jimbo la Ubungo kama reference.

Hivi hunaweza kushinda kiti cha urais halafu upate wabunge 23 tu.

Slaa, hakuibiwa kura kama kweli si alete idadi ya kura alizopata mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar.

Kuna diwani mmoja wa Chadema kule Mwanza maeneo ya Mkuyuni.

Alikuwa Shoe Shine hata siku mmoja hakuwai kufanya mkutano wa kampeni siku ya matokeo anaambiwa umeshinda udiwani alikuwa anakunywa bar anashangilia na huyu diwani ukimuuliza nae anakuambia Slaa, kaibiwa kura.
 
Hili mbona ni wazi wala halina shaka; nakumbuka jinsi watu walivyokuwa na shauku...

....Wengine wanaona ni kasoro kubwa ya Dr Slaa!!! eti angeachia tu kutokee umwagaji wa damu kwa sababu ukombozi hauji bila kumwaga damu!!!! Hongera sana Dr Slaa kwa maamuzi busara.
 
Mtoa mada usiwe mbishi kuwa Dr. Slaa hakuhusika kuzuia umwagikaji wa damu, unakumbuka hamasa waliyokuwanayo baada ya uchaguzi hasa pale ambapo matokeo yaliyotangazwa jimboni yalitofautiana na yaliyotangazwa na NEC? Unadhani Dr. angewahamasisha kuwa haki itapatikana kwa kuingia barabarani vijana wetu wasingepigwa risasi na polisi? Unakumbuka kilichotokea Zanzibar 1995 na 2000 baada ya cuf kudhulumiwa ushindi wao? Suala la wabunge wachache halimzuii Mgombea urais asipate kura za kushinda urais, unataka kutuambia wabunge wa Chadema ni 26% ya wabunge wote? Usituhadhae watanzania tunafahamu nini kilifanyika na mchango wa Dr. tunaujua.
 
Tanzania kwa watanzania tulivyo hakuna mapinduzi yatakayokuja kwa kumwaga damu, wala atakayefanya hilo. Nchi zinazofanikisha hilo mara nyingi huwa ni jamii fulani ambalo linakuwa linaonekana kukandamizwa. Kwa tanzania hakuna jamii inayokandamizwa ama hakuna jamii inayojineemesha ILA kuna Familia zinazojineemesha.

Tanzania umwagaji wake unaweza tokea tu kama kutatokea na ukandamizaji wa kidini, lakini kwa sababu rais kaibiwa kura aaa wapi.

Ningekuwa mie mkuu wa polisi maandamano wala nisingepeleka polisi ningewaacha wakandamana, nafahamu wana njaa kali hawataweza kuhimili maandamano siku 2, na wakiweza ina maana watakuwa wamevamia na kuiba mali ya wananchi in return wananchi watawaona kumbe hawa ni WAHUNI si wakombozi.

Baada ya wananchi kuibiwa vitu vyao na kulalamika, hapo ndo napeleka FFU na ninakuwa na full backup ya wananchi na in return wananchi wanakuaminia na kuona kumbe lile genge ni wahuni.
 
Slaa na Ndensamburo si ndio walisema watafanya nchi isitawalike tena na wakatoa amri kwa wafuasi wao wakavamie kituo cha polisi kwa maandamano sasa hapo na kazuia umwagaji wa damu polisi au Slaa.
 
Anaweweseka baada ya kuona nyota ya zitto inang'aa zaidi yake anatafuta pa kutokea,mpuuzeni tu huyo mzee..anazeeka vibaya,eti kiongozi mkuu wa upinzani,ina maana yeye ni mkubwa kuliko mwenyekiti wake?

Zitto hana ubavu wa kuitingisha ccm. Kabla ya dr slaa kuingia kwenye kampeni 2010 hapakuwepo na upinzani wa nguvu bongo. Zitto ni mpiga debe mzuri lakini gari lina dereva wake
 
2015 uvumilivu huo hautakuwepo tena!wala hakuna mtu atakayemuuliza slaa tuingie mtaani au la!! wakichakachua tutapambana nao juu kwa juu watatumia vifaru ndege lakini nguvu ya umma itashinda!!

Mimi nimeshaanza kutengeneza bomu la petroli litakalotumika 2015 kuangamiza magamba kama watachakachua kura za cdm
 
mimi 2015 niko tiyari kupingana na dr.slaa kuhusu hii amani,kwani nitaingia balabalani bila kuuliza mtu,kipindi hicha sitakua na cha kupoteza kama tutaibiwa.bora kufa tu pambafu!
 
Nani kampa Slaa ukiongozi mkuu wa upinzani?

Kuhusu kuzuia umwagaji wa damu huo ni uongo wa aina yake! nani asiyejua dhamira yake baada ya uchaguzi na kutangaza adhma ya nchi kutotawalika? tunajua ni nani alimzuia, muulizeni kabla ya kushabikia!

Msishabikie watu kibubusa, mfuatilie vyema siasa za Bongo sio kwenye magazeti

Kama siyo kwenye magazeti na TV tuambie ni source gani tutumie yenye habari za uhakika ambako wewe na familia yako mnazipata?
 
2015 watatupenda tu, hakuna tena kuibiwa kura tumeanza na arumeru na tulipata somo zur la namna ccm walikuwa wanaiba kura na tuliwadhbt, hakuna kulala mpaka kieleweke
 
Slaa na Ndensamburo si ndio walisema watafanya nchi isitawalike tena na wakatoa amri kwa wafuasi wao wakavamie kituo cha polisi kwa maandamano sasa hapo na kazuia umwagaji wa damu polisi au Slaa.

Mkuu ulikuwa likizo au ulikuwa semina?
 
Back
Top Bottom