Mjomba wa taifa
JF-Expert Member
- Apr 20, 2012
- 231
- 161
Ikumbukwe hivi karibuni, Rais Kikwete alipangua baraza la Mawaziri kufuatia shinikizo la wabunge kutokana na ubadhilifu wa mali ya umma. Miongoni mwa Mawaziri/Naibu waliopoteza nafasi zao ni pamoja na Mustafa Mkulo, William Ngeleja, Omar Nundu, Ezekieli Maige, Cyril Chami, Haji Mponda na Lucy Nkya.
Mawaziri hawa hawakuondolewa madarakani kwa kushindwa kutekeleza majukumu yao bali Kutumia madaraka yao kuiba rasilimali za nchi. Ikiwemo kuuza Twiga (Wizara ya Maliasili), Kuuza viwanja vya umma (Wizara ya fedha) n.k.
Hivi ni kwanini mpaka leo watu hawa hawajafikishwa Mahakamani either wasafishwe kwa tuhuma hizo ama wapewe adhabu stahili. Licha ya kuwepo kwa mashaka ya kesi za viongozi wanapofikishwa mahakamani kuchukua muda mrefu kutolewa hukumu lakini bado wananchi wangerudisha imani iliyopotea kwa serikali hata kwa kuona viongozi wabadhilifu hawaishii tu kuondolewa madarakani bali kufikishwa mahakamani.
Mawaziri hawa hawakuondolewa madarakani kwa kushindwa kutekeleza majukumu yao bali Kutumia madaraka yao kuiba rasilimali za nchi. Ikiwemo kuuza Twiga (Wizara ya Maliasili), Kuuza viwanja vya umma (Wizara ya fedha) n.k.
Hivi ni kwanini mpaka leo watu hawa hawajafikishwa Mahakamani either wasafishwe kwa tuhuma hizo ama wapewe adhabu stahili. Licha ya kuwepo kwa mashaka ya kesi za viongozi wanapofikishwa mahakamani kuchukua muda mrefu kutolewa hukumu lakini bado wananchi wangerudisha imani iliyopotea kwa serikali hata kwa kuona viongozi wabadhilifu hawaishii tu kuondolewa madarakani bali kufikishwa mahakamani.