Aisay una speed kali sana, yani wewe unataka kuoa mwanamke hata humjui vizuri.
Aisay wewe umeshinda, congrats.
Ndugu zangu habari zenu. Poleni na majukumu ya hapa na pale.
Leo ninaona niwafahamishe jambo lililonitokea.
Katika harakati za kutafuta mwenza wa maisha (mke) nilikutana na binti fulani ambae nilimpenda na nilitaka kumwoa nilifanya taratibu za kumweleza na alikubali tukaendelea ktk uchumba. Miezi sita baadae mawasiliano yakawa magumu nilikuwa nikipiga simu haipatikani na ikipatikana inaita bila kupokelewa kwa muda kama wa siku tatu. Baadae ya muda huo alinipigia simu kwa namba nyingine na kunijulisha kuwa ile namba aliyokuwa anaitumia hapo mwanzo haikuwa yake bali ni ya kaka yake (wa hiari) ambae anaishi nae, huyo kaka yake ameoa na anaishi na mkewe pia. So kuanzia hapo nikawa natumia namba simu mpya niliyopewa na huyo binti lakini baada ya miezi miwili hali ilijirudia tena, kila nikipiga simu inaita bila kupokelewa hata kwa siku nzima akipokea simu nikimuuliza anasema aliiacha nyumbani kwa vile kazini yuko bize. Nikimuuliza kuhusu mpango wetu wa kuoana anasema tutapanga muda tukutane na tukipanga appointment haji na simu inaita tu bila kupokelewa au haipatikani.
Nilipoona mwenzangu yuko bize nikaona isiwe tabu nikawa naenda hadi kazini ili tuongelee huko huko nikifika naambiwa kuna kazi. Nikaona isiwe tabu nikawa namwambia kuwa ni vizuri tukaweka mipango kwa ajili ya posa baadae kutoa mahari coz kwa kipindi hicho vijisent vya mahari nilikuwa nimevikusanya vipo tayari na nilikuwa naogopa kuvitumia. Kwa sababu tulishindwa kuonana physically nikamwambia tuongee kwenye simu akakataa na kusema hatuwezi kuongelea kwenye simu jambo hilo, yaani kila nililojaribu kulifanya ili tuongee nilishindwa... nakumbuka jumapili moja tulipanga tukutane ili tuongee yule binti alikuja na wadogo zake watatu akasema asingeweza kuwaacha nyumbani pekee yao kwa hiyo siku hiyo ikashindika
Baada ya juhudi kushindwa nilimwambia mama mmoja ambae ndio alituunganisha, nikamwambia hali halisi na nikamwomba akutane na binti ili aongee nae lakini yule binti alishindwa kuonana na huyo mama. walipanga appointment mara tatu bila mafanikio binti yuko bize sana. Nilikuwa nikiongea nae kwa njia simu lakini hataki kuongelea issue kwenye simu.
Kwa kweli uzlendo ulinishinda nikaamua kujivua gamba. siku ya valentines (2012) niliona niitumie kumwambia kuwa sitaweza kuendelea nae tena. nilimpigia simu tangu asubuhi hadi saa nne usiku bila kupokelewa ndipo nilipoamua kuandika ujumbe wa kuvunja uchumba wetu.
Jambo linalonishangaza ni kwamba binti amerudi kwa kasi sana. Anamsumbua yule mama kuwa mimi sikumpa yeye nafasi ya kujitetea ila niliamua kuvunja uchumba bila kumsikiliza yeye ana tatizo gani, nazidi kushangaa kwa sababu mimi hanipigii simu bali anampigia yule mama simu akimuuliza tumefikia wapi kuhusu suala hili... ni wiki mbili sasa anamsumbua huyu mama ili atukutanishe pamoja, sasa najiuliza kwa nini hanipigii wakati namba yangu anayo? mie nikimpigia kwa nini hapokei?
Duh kweli nimeshindwa kumwelewa kipindi kile nilichokuwa namtafuta alikuwa kweli yuko bize au alikuwa anatikisa kiberiti aone kama kuna njiti?
Naombeni maoni yenu katika hili
ndo matatizo ya wapenzi wa 'kuunganishiwa'
ila inaelekea una haraka ya kuoa, je huyo binti unampenda kwa dhati? Unamjua kiundani? Unajua udhaifu wake na umeukubali? Anakujua vyema? Maana inaonekana kama hamjuani kivile.......
Take tame kwanza.......
Tuliza kichwa...
Jipe muda......
Kaka inaelekea uko desparate na ndoa sana. Haraka haraka hizi ndo huwa zinawaponza watu. Kaa utulie utafute mwanamke aliyetulia na mwenye moyo na wewe. Otherwise utajilaumu baada ya ndoa.
Kwa story nilivyoo-ielewa ni kwamba unaharaka sana na ndoa. Kaka hizo ni pingu za maisha. So tulia kwanza. Huyo mwanamke amewapanga kama nyie wengi. Ndo maana yuko busy hivyo
mambo ya mapenzi bana ......sasa hapo unataka ushauri wa nn au ili ukamwambie jf walinishauri nikuache?
tupa kureee huyo ,au oa ufe kwa stress.
Na mimi naungana na wengine achana nae huyo.
Mbona mabinti wako wengi tu tena wazuri wazuri na heshima zao, ya nini kushupalia hapo ambapo kwa hii leo panaonyesha hapana manufaa ya baadae?
Mfano, jaribu kupiga simu kwa ile namba ya zamani na ujitambulishe kama rafiki yake na unamtafuta. Halafu sikiliza mshindo utakuwaje? Unaweza ukakuta hiyo namba ni ya husband!
Aisay una speed kali sana, yani wewe unataka kuoa mwanamke hata humjui vizuri.
Aisay wewe umeshinda, congrats.
Kwanza umeniumiza kama kaka wa kuzaliwa, ulivyokua unamfuatilia msichana hivyo ingawa dalili zote kua hakutaki zlikua anakuaonyesha.
Kakaangu ndoa sio maigizo, na mapenzi yanatakiwa ya balance sio wewe upende tu halafu yeye hakupendi, ki ukweli huyo dada hutakiwi hata kumpa mda kwani sio wako, na ukimuoa utajuta sana baadae kwani hata kaa akuheshim na ukigombana nae tu kidogo atakua anakwambia kwanza mi sikukupenda ulinilazimishia kuolewa na wewe.
Na kitendo cha kuja na wadogo zake kwenye maongezi yenu ya muhim nitosha kabisa hakuhitaji, pia kua busy kila wakati ni picha kamili kua hakupendi uanamfwatafwata, najinsi waschana tulivyo ukute hata ofisini kwao ilikua ukienda anawambia lile lijinga limekuja tena kunisumbua yani silipendi, wanakuchungulia madilishani wanacheka.
Achana nae kabisa ndugu yangu la sivyo atakuja kukuumiza sana mbeleni, na wala usidhani alikua anatikisa kiberiti hapana, jibu ni kwamba hakupendi tena hakupendi kabisaaa, uamuzi niwako lakini.
hata mimi mmenisaidia coz namimi nipo katika harakati hizo najiona namimi nahusika kwenye hili....
Nafikri kwangu na huyo alieanzisha hii hoja tumenufaika vya kutosha yaani mie mmenifungua macho sana nawashukuru asanteni.
Ndugu yangu umeelewa hayo walioyasema wewe ulieleta hoja? chukua ushauri huo utakusaidia
Kwanza umeniumiza kama kaka wa kuzaliwa, ulivyokua unamfuatilia msichana hivyo ingawa dalili zote kua hakutaki zlikua anakuaonyesha.
Kakaangu ndoa sio maigizo, na mapenzi yanatakiwa ya balance sio wewe upende tu halafu yeye hakupendi, ki ukweli huyo dada hutakiwi hata kumpa mda kwani sio wako, na ukimuoa utajuta sana baadae kwani hata kaa akuheshim na ukigombana nae tu kidogo atakua anakwambia kwanza mi sikukupenda ulinilazimishia kuolewa na wewe.
Na kitendo cha kuja na wadogo zake kwenye maongezi yenu ya muhim nitosha kabisa hakuhitaji, pia kua busy kila wakati ni picha kamili kua hakupendi uanamfwatafwata, najinsi waschana tulivyo ukute hata ofisini kwao ilikua ukienda anawambia lile lijinga limekuja tena kunisumbua yani silipendi, wanakuchungulia madilishani wanacheka.
Achana nae kabisa ndugu yangu la sivyo atakuja kukuumiza sana mbeleni, na wala usidhani alikua anatikisa kiberiti hapana, jibu ni kwamba hakupendi tena hakupendi kabisaaa, uamuzi niwako lakini.
Nakushukuru dada yangu kwa ushauri huo