Ndugu zangu habari zenu. Poleni na majukumu ya hapa na pale.
Leo ninaona niwafahamishe jambo lililonitokea.
Katika harakati za kutafuta mwenza wa maisha (mke) nilikutana na binti fulani ambae nilimpenda na nilitaka kumwoa nilifanya taratibu za kumweleza na alikubali tukaendelea ktk uchumba. Miezi sita baadae mawasiliano yakawa magumu nilikuwa nikipiga simu haipatikani na ikipatikana inaita bila kupokelewa kwa muda kama wa siku tatu. Baadae ya muda huo alinipigia simu kwa namba nyingine na kunijulisha kuwa ile namba aliyokuwa anaitumia hapo mwanzo haikuwa yake bali ni ya kaka yake (wa hiari) ambae anaishi nae, huyo kaka yake ameoa na anaishi na mkewe pia. So kuanzia hapo nikawa natumia namba simu mpya niliyopewa na huyo binti lakini baada ya miezi miwili hali ilijirudia tena, kila nikipiga simu inaita bila kupokelewa hata kwa siku nzima akipokea simu nikimuuliza anasema aliiacha nyumbani kwa vile kazini yuko bize. Nikimuuliza kuhusu mpango wetu wa kuoana anasema tutapanga muda tukutane na tukipanga appointment haji na simu inaita tu bila kupokelewa au haipatikani.
Nilipoona mwenzangu yuko bize nikaona isiwe tabu nikawa naenda hadi kazini ili tuongelee huko huko nikifika naambiwa kuna kazi. Nikaona isiwe tabu nikawa namwambia kuwa ni vizuri tukaweka mipango kwa ajili ya posa baadae kutoa mahari coz kwa kipindi hicho vijisent vya mahari nilikuwa nimevikusanya vipo tayari na nilikuwa naogopa kuvitumia. Kwa sababu tulishindwa kuonana physically nikamwambia tuongee kwenye simu akakataa na kusema hatuwezi kuongelea kwenye simu jambo hilo, yaani kila nililojaribu kulifanya ili tuongee nilishindwa... nakumbuka jumapili moja tulipanga tukutane ili tuongee yule binti alikuja na wadogo zake watatu akasema asingeweza kuwaacha nyumbani pekee yao kwa hiyo siku hiyo ikashindika
Baada ya juhudi kushindwa nilimwambia mama mmoja ambae ndio alituunganisha, nikamwambia hali halisi na nikamwomba akutane na binti ili aongee nae lakini yule binti alishindwa kuonana na huyo mama. walipanga appointment mara tatu bila mafanikio binti yuko bize sana. Nilikuwa nikiongea nae kwa njia simu lakini hataki kuongelea issue kwenye simu.
Kwa kweli uzlendo ulinishinda nikaamua kujivua gamba. siku ya valentines (2012) niliona niitumie kumwambia kuwa sitaweza kuendelea nae tena. nilimpigia simu tangu asubuhi hadi saa nne usiku bila kupokelewa ndipo nilipoamua kuandika ujumbe wa kuvunja uchumba wetu.
Jambo linalonishangaza ni kwamba binti amerudi kwa kasi sana. Anamsumbua yule mama kuwa mimi sikumpa yeye nafasi ya kujitetea ila niliamua kuvunja uchumba bila kumsikiliza yeye ana tatizo gani, nazidi kushangaa kwa sababu mimi hanipigii simu bali anampigia yule mama simu akimuuliza tumefikia wapi kuhusu suala hili... ni wiki mbili sasa anamsumbua huyu mama ili atukutanishe pamoja, sasa najiuliza kwa nini hanipigii wakati namba yangu anayo? mie nikimpigia kwa nini hapokei?
Duh kweli nimeshindwa kumwelewa kipindi kile nilichokuwa namtafuta alikuwa kweli yuko bize au alikuwa anatikisa kiberiti aone kama kuna njiti?
Naombeni maoni yenu katika hili
Leo ninaona niwafahamishe jambo lililonitokea.
Katika harakati za kutafuta mwenza wa maisha (mke) nilikutana na binti fulani ambae nilimpenda na nilitaka kumwoa nilifanya taratibu za kumweleza na alikubali tukaendelea ktk uchumba. Miezi sita baadae mawasiliano yakawa magumu nilikuwa nikipiga simu haipatikani na ikipatikana inaita bila kupokelewa kwa muda kama wa siku tatu. Baadae ya muda huo alinipigia simu kwa namba nyingine na kunijulisha kuwa ile namba aliyokuwa anaitumia hapo mwanzo haikuwa yake bali ni ya kaka yake (wa hiari) ambae anaishi nae, huyo kaka yake ameoa na anaishi na mkewe pia. So kuanzia hapo nikawa natumia namba simu mpya niliyopewa na huyo binti lakini baada ya miezi miwili hali ilijirudia tena, kila nikipiga simu inaita bila kupokelewa hata kwa siku nzima akipokea simu nikimuuliza anasema aliiacha nyumbani kwa vile kazini yuko bize. Nikimuuliza kuhusu mpango wetu wa kuoana anasema tutapanga muda tukutane na tukipanga appointment haji na simu inaita tu bila kupokelewa au haipatikani.
Nilipoona mwenzangu yuko bize nikaona isiwe tabu nikawa naenda hadi kazini ili tuongelee huko huko nikifika naambiwa kuna kazi. Nikaona isiwe tabu nikawa namwambia kuwa ni vizuri tukaweka mipango kwa ajili ya posa baadae kutoa mahari coz kwa kipindi hicho vijisent vya mahari nilikuwa nimevikusanya vipo tayari na nilikuwa naogopa kuvitumia. Kwa sababu tulishindwa kuonana physically nikamwambia tuongee kwenye simu akakataa na kusema hatuwezi kuongelea kwenye simu jambo hilo, yaani kila nililojaribu kulifanya ili tuongee nilishindwa... nakumbuka jumapili moja tulipanga tukutane ili tuongee yule binti alikuja na wadogo zake watatu akasema asingeweza kuwaacha nyumbani pekee yao kwa hiyo siku hiyo ikashindika
Baada ya juhudi kushindwa nilimwambia mama mmoja ambae ndio alituunganisha, nikamwambia hali halisi na nikamwomba akutane na binti ili aongee nae lakini yule binti alishindwa kuonana na huyo mama. walipanga appointment mara tatu bila mafanikio binti yuko bize sana. Nilikuwa nikiongea nae kwa njia simu lakini hataki kuongelea issue kwenye simu.
Kwa kweli uzlendo ulinishinda nikaamua kujivua gamba. siku ya valentines (2012) niliona niitumie kumwambia kuwa sitaweza kuendelea nae tena. nilimpigia simu tangu asubuhi hadi saa nne usiku bila kupokelewa ndipo nilipoamua kuandika ujumbe wa kuvunja uchumba wetu.
Jambo linalonishangaza ni kwamba binti amerudi kwa kasi sana. Anamsumbua yule mama kuwa mimi sikumpa yeye nafasi ya kujitetea ila niliamua kuvunja uchumba bila kumsikiliza yeye ana tatizo gani, nazidi kushangaa kwa sababu mimi hanipigii simu bali anampigia yule mama simu akimuuliza tumefikia wapi kuhusu suala hili... ni wiki mbili sasa anamsumbua huyu mama ili atukutanishe pamoja, sasa najiuliza kwa nini hanipigii wakati namba yangu anayo? mie nikimpigia kwa nini hapokei?
Duh kweli nimeshindwa kumwelewa kipindi kile nilichokuwa namtafuta alikuwa kweli yuko bize au alikuwa anatikisa kiberiti aone kama kuna njiti?
Naombeni maoni yenu katika hili