Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 301
MKE wa Rais Jakaya Kikwete, Mama Salma amesimulia namna wauguzi walivyomnyanyasa wakati akijifungua mtoto wa kwanza.
Salma hakuitaja hospitali hiyo lakini amesema,wauguzi walimlaza sakafuni wakati akisubiri huduma ya madaktari.
Amesema, kuwa alipofika hospitalini hapo,alilazwa chini na kwamba wahudumu walikuwa wakimjibu vibaya kama mtu asiye na thamani.
Kwa mujibu wa Salma,wakati huo alikuwa mke wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa lakini alikwenda katika hospitali hiyo kama mtu wa kawaida aliyekuwa akihitaji huduma. Amesimulia hayo leo wakati akizungumza na wakazi wa Lushoto, Tanga.
Mimi mwenyewe yamenikuta wakati najifungua mtoto wangu wa kwanza nililazwa chini. Nawaambia kabisa sitasahau kamwe hali ile niliyojisikia, nilijibiwa vibaya kama vile sina thamani, amesema Salma.
Alisema kilichomsaidia ni baada ya daktari kumtambua kuwa ni mke wa Waziri Jakaya Kikwete ndipo alipata huduma na lugha nzuri na kuondolewa chini hali ambayo hata hivyo ilimfadhaisha.
Aliwataka wauguzi kuacha tabia hiyo ili kusaidia kuongeza idadi ya wanawake kujifungulia hospitalini kwa kuwa watoa huduma za afya hasa wauguzi wanapokuwa na lugha chafu, huleta picha mbaya na kumkatisha tamaa mgonjwa.
Amewaasa wahudumu wa afya watumie lugha nzuri kwa wagonjwa hasa wajawazito.Salma amesema,uchungu alioupata hatausahau katika maisha yake.
Aliwataka watoa huduma hao wa sekta ya afya kutokutoa huduma bora kwa kuangalia sura, kipato au cheo na badala yake watoe huduma kwa usawa.
Huku kila mtu anatoka sehemu tofauti na kila mtu ndiye anayejua maisha ya wazazi wake sasa usione mwenzako amevaa viatu vizuri ukatamani wakati hujui alikovipata, alisema.
Baada ya kuzungumza na wakazi hao, alitoa msaada wa vifaa vya afya katika zahanati ya Mbuzii wilayani Lushoto mkoani Tanga ambako yupo katika ziara ya siku mbili.
Pia aliwataka wanafunzi kupigania kufikia malengo waliyojiwekea, waliowekewa na wazazi wao na Taifa kwa ujumla.
Mama Salma pia alitoa zaidi ya sh milioni nane kwa ajili ya kuwasaidia akinamama wajasiriamali, watoto wenye ulemavu na wanafunzi wenye mahitaji maalum.
Mama Salma Kikwete akisalimiana na baadhi ya wauguzi wa Kituo cha Afya Kaliua,mkoani Tabora muda mfupi baada ya kukabidhi vitanda viwili maalumu kwaajili ya wanawake wajawazito.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana (kushoto) akizungumza na wazazi waliojifungua katika Hospitali ya Mwananyamala, Dar es Salaam
Salma hakuitaja hospitali hiyo lakini amesema,wauguzi walimlaza sakafuni wakati akisubiri huduma ya madaktari.
Amesema, kuwa alipofika hospitalini hapo,alilazwa chini na kwamba wahudumu walikuwa wakimjibu vibaya kama mtu asiye na thamani.
Kwa mujibu wa Salma,wakati huo alikuwa mke wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa lakini alikwenda katika hospitali hiyo kama mtu wa kawaida aliyekuwa akihitaji huduma. Amesimulia hayo leo wakati akizungumza na wakazi wa Lushoto, Tanga.
Mimi mwenyewe yamenikuta wakati najifungua mtoto wangu wa kwanza nililazwa chini. Nawaambia kabisa sitasahau kamwe hali ile niliyojisikia, nilijibiwa vibaya kama vile sina thamani, amesema Salma.
Alisema kilichomsaidia ni baada ya daktari kumtambua kuwa ni mke wa Waziri Jakaya Kikwete ndipo alipata huduma na lugha nzuri na kuondolewa chini hali ambayo hata hivyo ilimfadhaisha.
Aliwataka wauguzi kuacha tabia hiyo ili kusaidia kuongeza idadi ya wanawake kujifungulia hospitalini kwa kuwa watoa huduma za afya hasa wauguzi wanapokuwa na lugha chafu, huleta picha mbaya na kumkatisha tamaa mgonjwa.
Amewaasa wahudumu wa afya watumie lugha nzuri kwa wagonjwa hasa wajawazito.Salma amesema,uchungu alioupata hatausahau katika maisha yake.
Aliwataka watoa huduma hao wa sekta ya afya kutokutoa huduma bora kwa kuangalia sura, kipato au cheo na badala yake watoe huduma kwa usawa.
Huku kila mtu anatoka sehemu tofauti na kila mtu ndiye anayejua maisha ya wazazi wake sasa usione mwenzako amevaa viatu vizuri ukatamani wakati hujui alikovipata, alisema.
Baada ya kuzungumza na wakazi hao, alitoa msaada wa vifaa vya afya katika zahanati ya Mbuzii wilayani Lushoto mkoani Tanga ambako yupo katika ziara ya siku mbili.
Pia aliwataka wanafunzi kupigania kufikia malengo waliyojiwekea, waliowekewa na wazazi wao na Taifa kwa ujumla.
Mama Salma pia alitoa zaidi ya sh milioni nane kwa ajili ya kuwasaidia akinamama wajasiriamali, watoto wenye ulemavu na wanafunzi wenye mahitaji maalum.
Mama Salma Kikwete akisalimiana na baadhi ya wauguzi wa Kituo cha Afya Kaliua,mkoani Tabora muda mfupi baada ya kukabidhi vitanda viwili maalumu kwaajili ya wanawake wajawazito.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Jordan Rugimbana (kushoto) akizungumza na wazazi waliojifungua katika Hospitali ya Mwananyamala, Dar es Salaam