Nilichojifunza chadema vs ccm jangwani

JATELO1

JF-Expert Member
Oct 31, 2011
1,230
301
Wana-JF,
Baada ya kutazama mkutano wa Chadema uliofanyika Jangwani (26.05.2012) na wa CCM leo tarehe 09.05.2012,nimejifunza kwamba CCM imechokwa na wananchi walio wengi, hivyo CCM imebaki ikitumia mbinu nyingi sana ili kuwadhiirishia umma kwamba bado inapendwa na wananchi lkn si kweli. Nasema hivyo kwasababu zifuatazo,

1. Umati wa watu waliohudhuria leo Jangwani kwenye mkutano wa CCM bado haulingani na wa CHADEMA. Ukiangalia kwa makini utaelewa hiki ninachokisema, kwani leo watu wamekalia viti na kwa kawaida viti vinachukua nafasi kubwa tofauti na wa CHADEMA ambapo hakukuwa na viti na watu wengi walisimama. Katika hali ya kawaida, kiti kimoja kinaweza kuchukua nafasi ya watu 3-4 waliosimama.

2. CCM wametumia motives na incentives nyingi sana kuwahamasisha watu kuhudhuria kwenye mkutano wa leo. Motive walizotumia CCM ni kama usafiri, pesa na vitisho kwa walio wanachama wa CCM kimwili na si kiroho kuhudhuria mkutano wa leo. Nasema hivyo kwasababu pale Jangwani leo kuna watu ambao wamehudhuria tu kwasababu hizo nilizotaja hapo juu lkn si kwa hiari yao. Hili ni tofauti kabisa na CHADEMA ambao hakukuwa na motive yoyote ile tofauti na watu hao hao kutakiwa kuichangia CHADEMA kwa kile kidogo walichokuwa nacho. Ukiangalia hili utagundua kwamba ni kweli kwamba siyo wote walioko Jangwani leo wanaipenda CCM kutoka moyoni, HAPANA, nasema hapana tena kwa herufi kubwa kwasababu CCM wana Dola na CHADEMA hawana dola, hivyo CHADEMA haina nafasi ya kumtisha mtu yeyote tofauti na CCM yenye DOLA:

Hivyo, napenda kuhitimisha kwamba CCM wana kazi kubwa sana, kwani wengi walioko pale Jangwani leo wapo kimwili kwasababu ya PESA, USAFIRI, na VITISHO lkn KIROHO wako CHADEMA. Na kwa msingi huo naamini kwamba CCM wana kazi ya ziada ya kufanya ili kurejesha imani ya watanzania walio wengi. Nasema CCM wana kazi ya zaida ya kufanya tofauti na ilivyo sasa ambapo CCM imekuwa ikidandia KILA KITU TOKA CHADEMA. Hili liko wazi kama ifuatavyo,
1.CHADEMA walikuwa wa kwanza kuzindua M4C na sasa CCM nao wameiga.
2. CHADEMA walipofanya mkutano wao Jangwani mwezi jana, ghafla mapema mwezi huu CCM nao wanafanya mkutano Jangwani.
3.Chadema walipohamia kusini, Mawaziri wa CCM wamekimbia ofisi zao na kurejea kufukia mashimo huko mikoa ya kusini.
4. N.K

NB1: Swali la kujiuliza hapa ni JE CCM SASA WAMEFILISIKA KIASI KWAMBA WANASUBIRI KINACHOFANYWA NA CHADEMA ILI WAIGE? Je CCM AMBACHO KIKO MADARAKINI TOKA 1977 mpaka leo bado haina ubunifu wowote kiasi kwamba inakaa mlango wa nyuma ikisubiri CHADEMA wabuni kitu,ndipo CCM ijitokeze na kuiga? HII NI AIBU KUBWA SANA KWA CCM.

Je kwa UIGIZAJI huu unaofanywa na CCM, je kuna haja ya kuwalaumu hata mawaziri ambao hawana uwezo wala ubunifu wowote, kwani wao ni zao la CCM ambalo sasa kila siku inalala na kuomba CHADEMA wabuni kitu kingine ili wao nao waige.

NB2: Baada ya CCM kukosa ubunifu na kubaki kusubiri CHADEMA wabuni ili waige, sasa nimeelewa ni kwanini Viongozi wengi sana wa CCM wanajipa PHD ambazo hawajazisomea na hakuna anayewakemea. Ukiangalia CV zao hata qualifications za kuwawezesha kuitwa Dr., hawana lkn wanajiita Dr., refer Waziri wa Fedha wa sasa, Mwanjelwa yule wa Mbeya viti maalum, n.k, n.k. Huu pia ni uigizaji ambao umebuniwa na CCM lkn wenyewe wameuiga kutoka nje ya nchi bila kujua kwamba je ni kwa VIGEZO GANI mtu anastahili kuitwa Dr.?

Nawasilisha.
TELO.
 
Leo ulikuwa mkutano wa Ccm Na serikali yote ya nchi.. Watu ni kiduuchu sana.. INATISHA.. Wameongea porojo hakuna la msingi hata moja.. Shit!!
 
yaani upo right kabisa,nakupongeza mkuu coz umeangalia vtu kwa kina sana,ccm ni kirusi tunatakiwa tupambane nae bila woga wala aibu!
 
yaani upo right kabisa,nakupongeza mkuu coz umeangalia vtu kwa kina sana,ccm ni kirusi tunatakiwa tupambane nae bila woga wala aibu!

Pia kumbuka Kofia na Khanga walizogawa.Lkn bado hakuna cha maana kilichofanyika. Hakika CCM iko ICU.
 
kilichojili leo ni kuwanadi mawazir wenye sera mfu,pamoja na kusomba watu kwa malori,pamoja na kugawa pesa nyingi ambazo kwa upande wa pili ni kodi zetu
 
Kijiweni kwetu kuna jamaa kaja na T-shirt yake na kofia vya kupewa,matokeo yake kaishia kuzomewa ugomvi na kuchaniwa fulana lake.
 
Kama CCM nao wataanza kuiga na kuanzisha operation yao..itakuwa wanajitafutia matatizo maana hiyo pesa itakayotumika bora wangeitumia kutekelezea ilani..Tujaribu kupunguza siasa jamani tuwazie maendeleo ya nchi yetu. Coz nilichoona pale Jangwani ni siasa tupu.
 
Kuna haja gani kwa CCM kufanya mikutano mikoani kuelezea utakelezaji wa ilani kwani Rais Kikwate si anatoa hotuba ya kila mwezi ataweza kuelezea utakelezaji wake..pamoja na wakuu wa mikoa na wilaya..
 
Nilitegemea niwakute ccm site wakisimamia miradi ya ahadi walizotuahidi wametuita CDM square kutueleza utumbo ule mwenye akili timamu hawezi kwenda pale hata siku moja
 
Nape ni vema ukawaomba radhi waislam wa jumuiya ya Uamsho na mihadhara ya kisasa. Ukifuatilia hotuba ya Dr.Shein ni kwamba kundi hilo lilikuwa na ujumbe wa kisiasa kuhusu muungano ila liliwasilisha ujumbe wake kwa njia ya kidini. Napata shida kujua uwezo wa kufikiri wa Nape kabla ya kuzungumza.

Nape una nafasi ndani ya serikali ya CCM ya kufanya utafiti kuhusu chanzo cha vurugu na kutafuta namna ya kuzuia ili yasitokee tena. Pia Nape tunakubali vurugu zile ni mbaya lakini, kwa akili yako unaamini jumuiya ya UAMSHO ni wapumbavu? Unawaita majambazi na CCM tafsiri yake nini? We unadhani waislam wale ni wapuuzi tu na hawakuwa na madai ya msingi.

The means was not good but how about the claims! Ujinga huu hautakaa uvumiliwe kwani...kwenye vurugu mlizosababisha kwenye uchaguzi wa meya Arusha na kuua watu hamkujiita MAJAMBAZI. Kwa mantiki hii ni CHADEMA tu ndo huheshimu dini zote ila CCM inakipaka matope CHADEMA. NAPE jipangeee!
 
Kijiweni kwetu kuna jamaa kaja na T-shirt yake na kofia vya kupewa,matokeo yake kaishia kuzomewa ugomvi na kuchaniwa fulana lake.

Watu wamechoka na CCM na CCM wanalitambua hilo.
 
Kama CCM nao wataanza kuiga na kuanzisha operation yao..itakuwa wanajitafutia matatizo maana hiyo pesa itakayotumika bora wangeitumia kutekelezea ilani..Tujaribu kupunguza siasa jamani tuwazie maendeleo ya nchi yetu. Coz nilichoona pale Jangwani ni siasa tupu.

Hiyo ndiyo CCM na huo ndiyo ubunifu wao.
 
Hivi TANU nayo ilikuwa ikisomba watu kwa mabasi na kuwalipa ili wahudhurie mikutano ya hadhara?
Kweli ccm imepauka, kutoka kijani kibichi hadi white, yaani hamna kitu kabisa
 
Back
Top Bottom