Niliasisi CHADEMA si kwa lengo la kutafuta vyeo - Edwin Mtei

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
Mwasisi wa CHADEMA Edwin Mtei amesema anaamini chama chake kitaingia madarakani mwaka 2015 lakini hilo haliwezi kutokea kama viongozi wake wataanza malumbano na kuwagawa wanachama kwa lengo la kutafuta uungwaji mkono wa Urais.

Amebainisha kuwa CHADEMA kwa sasa hivi ndiyo mkombozi wa wananchi waliochoshwa na utawala wa CCM hivyo ni vema viongozi wake wakatumia muda mwingi kukijenga chama hapa nchini.

Mzee Mtei amesema CHADEMA kina utaratibu mzuri wa kumpata mgombea wa Urais lakini kama viongozi wake wataanza kutoa kauli za kuwania vyeo hivyo kuna kila dalili ya kuzaliwa makundi yatakayokimega chama.

Mzee Mtei amesema yeye aliasisi CHADEMA si kwa lengo la kutafuta vyeo bali alishirikiana na wenzake ili kiwe kimbilio la wanyonge na kiwasaidie kuboresha maisha yao.

Mzee Mtei kwa kauli yake amesema ''Nimemsihi Zitto kuwa kauli yake ya kutaka kuwania urais inabomoa timu yetu kuliko kuijenga na nimemtaka asubiri mpaka chama kitakapoanza mchakato wa wa kumsaka yule atakayepeperusha bendera ya chama katika uchaguzi mkuu ujao''

Mzee Mtei amesema kuwa Dk Slaa aliteuliwa na vikao vya chama kugombea urais 2010 na ndiyo maana umoja na mshikamano ndani ya chama ulikuwa mkubwa kiasi cha kukifanya Chadema kipate idadi kubwa ya wabunge katika uchaguzi mkuu uliopita.

Mzee Mtei amesema pia alishauriana na viongozi wakuu wa Chama hicho Freeman Mbowe na Dr Wilbroad Slaa kwamba wakati huu si wa kuwaza Urais bali wa kukifikisha Chadema vijijini na mijini ambako wananchi wanahitaji ukombozi.

Mzee Mtei alimalizia kwa kusema..''Unaweza kutangaza nia ya kuwania Urais lakini tujiulize kwanini sasa? Kwanini tusiutumie muda mwingi kujenga timu ya kuiunganisha Chadema badala ya kuisambaratisha?

Source: DIRA ya Mtanzania.
 
Well said Mzee Mtei. Hongera kwa kuliona hilo, kazi kubwa iliyopo mbele yetu kwa sasa ni kuwakomboa wananchi na sio kutangaza urais. Tumeona jinsi CCM walivomeguka kutokana na kauli zao. Mcahakato wa kugombea bado haujaanza. Kwanini Zitto et al wasisubiri mpaka tume itangaze muda wa kuanza harakati za uchaguzi ndio akaonyesha interest zake?

Zitto angekua na lengo zuri angekomaa sasa hivi kujenga jina kupitia MVC pamoja na kuwa mwiba bungeni ili umaarufu wake uwe maradufu. Zitto anajua kabisa kuwa popularity aliyo nayo pekee haitoshi kumvusha kupewa jukumu la kuongoza nchi. Uongozi unahitaji awareness kwa wananachi ya nini utafanya ukiwa pale magogoni kwaa jili ya kuwakomboa watu. Na hiyo wataiona kupitita harakati za kukijenga chama na kupambana na maovu.

Zitto hebu subiri kwanza kwa mustakabali wa chama chako na nchi yako pia
 
Thanx kwa maneno yenye busara hiz,ZITO K.Wamuite na amwambie maneno haya kwakuwa ni msom haitakua ngumu kuelewa!
 
Hongera Mzee Mtei kwa kuliona hilo,naomba uangalie chaguo la wananchi tusije tukawagawa wananchi,ukombozi umekribia hivyo mahali tulipofikia si kuchezea akili za wananchi,mwananchi wa leo si wa mwaka 1947,ukikosea kura ya wengi inaenda kwa EL
 
Tuangalie na upande wa pili wa shilingi...kwa nini kutangaza nia kwa Zitto kuchukuliwe kama njia ya kutaka 'kuisambaratisha' Chadema? Hivi kila kiongozi, mwanachama, shabiki/mpenzi wa Chadema angeichukulia kama kauli ya kawaida labda kumpongeza Zitto kwa kutangaza nia then tukasahau tukisubiri wakati muafaka mchakato utakapoanza..kungekuwa na malumbano yanayotishia 'kusambaratisha' Chadema?
Tatizo tunampa Zitto uzito mkubwa (overrate) hasiostahili...zikipigwa kura za maoni nani awe candidate wa uRais Chadema Zitto hatatokea kama favourite...hizi kura zinazoendelea hapa JF kati ya Dr Slaa na Zitto zinaonyesha jinsi Dr alivyomuacha kwa mbali. Kwa nini wanaChadema tuchachawe na kudhani Zitto anatishia kusambaratika kwa Chadema?
 
Mwasisi wa CHADEMA Edwin Mtei amesema anaamini chama chake kitaingia madarakani mwaka 2015 lakini hilo haliwezi kutokea kama viongozi wake wataanza malumbano na kuwagawa wanachama kwa lengo la kutafuta uungwaji mkono wa Urais.

Amebainisha kuwa CHADEMA kwa sasa hivi ndiyo mkombozi wa wananchi waliochoshwa na utawala wa CCM hivyo ni vema viongozi wake wakatumia muda mwingi kukijenga chama hapa nchini.

Mzee Mtei amesema CHADEMA kina utaratibu mzuri wa kumpata mgombea wa Urais lakini kama viongozi wake wataanza kutoa kauli za kuwania vyeo hivyo kuna kila dalili ya kuzaliwa makundi yatakayokimega chama.

Mzee Mtei amesema yeye aliasisi CHADEMA si kwa lengo la kutafuta vyeo bali alishirikiana na wenzake ili kiwe kimbilio la wanyonge na kiwasaidie kuboresha maisha yao.

Mzee Mtei kwa kauli yake amesema ''Nimemsihi Zitto kuwa kauli yake ya kutaka kuwania urais inabomoa timu yetu kuliko kuijenga na nimemtaka asubiri mpaka chama kitakapoanza mchakato wa wa kumsaka yule atakayepeperusha bendera ya chama katika uchaguzi mkuu ujao''

Mzee Mtei amesema kuwa Dk Slaa aliteuliwa na vikao vya chama kugombea urais 2010 na ndiyo maana umoja na mshikamano ndani ya chama ulikuwa mkubwa kiasi cha kukifanya Chadema kipate idadi kubwa ya wabunge katika uchaguzi mkuu uliopita.

Mzee Mtei amesema pia alishauriana na viongozi wakuu wa Chama hicho Freeman Mbowe na Dr Wilbroad Slaa kwamba wakati huu si wa kuwaza Urais bali wa kukifikisha Chadema vijijini na mijini ambako wananchi wanahitaji ukombozi.

Mzee Mtei alimalizia kwa kusema..''Unaweza kutangaza nia ya kuwania Urais lakini tujiulize kwanini sasa? Kwanini tusiutumie muda mwingi kujenga timu ya kuiunganisha Chadema badala ya kuisambaratisha?

Source: DIRA ya Mtanzania.

Hapo kwenye wekundu:

Kwani wanaotangaza kwamba watagombea urais kupitia CDM (Kama Zitto) wamesema kwamba watajiteua? Namsikia kila siku Zitto akisema "...kama nitapata ridhaa ya chama changu...." Hii inadhihirisha kwamba atatafuta ridhaa ya chama chake (CDM).
 
Hizi ni busara za hali ya juu.Mzee Mtei ni dhahabu ndani ya CDM.

Mkuu Molemo palilieni demokrasia ndani ya Chama. Watu wajitokeze mapema watangaze nia zao tuwajue kwa matendo yao.
 
Last edited by a moderator:
Kila mtu kama amekidhi vigezo vya kikatiba ana haki ya kuwania urais LAKINI nia ya awali ya kuwania urais inatakiwa ionyeshwe kwenye kipindi muafaka ndani ya kundi husika na tena inakuwa inapendeza zaidi kama utaona watu kwa nyakati mbalimbali wanakushawishi kufanya hivyo na sio kusukumwa na nia ya 'kuutaka' urais badala kupendekezwa na watu, halafu inabidi mtu ajue ni wakati gani wa kusema nia hiyo ili kuepusha dhana ya kuonekana una tamaa ya uongozi, hii mara nyingi huleta mitafaruku na kupunguza mshikamano ndani ya chama husika, tukiangalia mfano wa ccm- nia ya mapema ya baadhi ya watu kutaka urais inasababisha mitafaruku na malumbano ya hapa na pale yasiyo na tija na kwa chadema tunamuona zitto naye akitangaza nia ya kuwania urais kwa wakati na taratibu ambazo mimi nadhani si muafaka kwanini asingojee na kufuata taratibu mahsusi za kichama!!? yeye haoni kuwa jambo hili la kutangaza nia yake kwa wazi kiasi hiki ni kutikisa mshikamano wa chama? kwanini asitumie muda huu kukiimarisha chama na kuwaaminisha wananchi kuwa sera na utendaji wa chadema vitaleta tija na maendeleo kwa taifa? ili kwamba yoyote atakaeteuliwa kwa tiketi ya chadema kuwania nafasi hiyo watu wawe na matumaini nae kwa sababu ya sera anazoenda kutekeleza!! Hata akina lowasa,membe etc. licha ya kuwa watu wameshawawekea kauli mdomoni kuwa wanataka urais lakini wakiulizwa wanasema wakati mahsusi ukifika watasema kama ni ndio au la! hii ndio busara, yaani kusubiri wakati muafaka. Nawasihi wapiga kura wapime wenyewe kama wanampenda mtu basi waaangalie ni sera gani anaenda kutekeleza na kama wanapenda sera napo waaangalie ni nani ana uwezo wa kutekeleza sera hizo!
 
Mkuu Molemo palilieni demokrasia ndani ya Chama. Watu wajitokeze mapema watangaze nia zao tuwajue kwa matendo yao.

Kama kweli alilolisema Mzee mtei lina heri basi wamuunge mkono ZITTO apeperushe bendera ya CDM mwaka 2015 kwa vile tayari yeye ameonesha nia, na kama ni unafiki wa kutaka kumpalilia njia mkwe wake hakika patachimbika.
 
Hapo kwenye wekundu:

Kwani wanaotangaza kwamba watagombea urais kupitia CDM (Kama Zitto) wamesema kwamba watajiteua? Namsikia kila siku Zitto akisema "...kama nitapata ridhaa ya chama changu...." Hii inadhihirisha kwamba atatafuta ridhaa ya chama chake (CDM).

Huyo mzee Mtei amezeeka na hajui hata jinsi ya kupandikiza unafiki wake.
 
Hekima za Mzee Mtei ni lulu, pengine Mzee Mtei asingeongea hivi endapo John Shibuda angetangaza nia ya kugombea uraisi kupitia Chadema, bila shaka kuna masuala ambayo Mzee Mtei anayajua na sisi hatuyajui ndio maana anarudia hii kauli yake kwa mara ya pili, wakati mwingine waandishi wawaulize hawa wazee sababu zinazowasukuma kubomoa kabati zao za ushauri na kuongea falsafa za maana kama hivi.
 
Laiti CCM ingekuwa na wazee wenye hekima kama mzee Mtei basi taifa lingekuwa mbali sana kimaendeleo.
 
Hongera Mzee Mtei kwa kuliona hilo,naomba uangalie chaguo la wananchi tusije tukawagawa wananchi,ukombozi umekribia hivyo mahali tulipofikia si kuchezea akili za wananchi,mwananchi wa leo si wa mwaka 1947,ukikosea kura ya wengi inaenda kwa EL

Namuombea Mungu Mzee Mtei afikishe miaka 120 kwani ninaamini sasa hakuna mtu atakayeweza kusambaratisha chama mzee huyu akiwa hai
 
Hekima za Mzee Mtei ni lulu, pengine Mzee Mtei asingeongea hivi endapo John Shibuda angetangaza nia ya kugombea uraisi kupitia Chadema, bila shaka kuna masuala ambayo Mzee Mtei anayajua na sisi hatuyajui ndio maana anarudia hii kauli yake kwa mara ya pili, wakati mwingine waandishi wawaulize hawa wazee sababu zinazowasukuma kubomoa kabati zao za ushauri na kuongea falsafa za maana kama hivi.

Mzee Mtei ni aina ya wale wazee wasi wanafiki wanaaongea kweli daima bila kumuogopa mtu yeyote.Niliwahi kushauri kamati kuu iingilie hili swala na itoe mwongozo hakika nafurahi sana kuona mwasisi wa chama na mjumbe wa kamati kuu ametoa kauli hii.Nashauri wanachama sasa warudi vijijini kuimarisha chama na mijadala hii ya kijinga ya urais ifungwe.
 
Hapo kwenye wekundu:

Kwani wanaotangaza kwamba watagombea urais kupitia CDM (Kama Zitto) wamesema kwamba watajiteua? Namsikia kila siku Zitto akisema "...kama nitapata ridhaa ya chama changu...." Hii inadhihirisha kwamba atatafuta ridhaa ya chama chake (CDM).

Kila kauli ina athari zake,mfano zito katangaza na mwingine atafanya hivyo hapo ndo mwanzo wa makundi ktk chama.Kwa mazingira kama hayo unategemea nini kama si vurugu?Tujenge chama 1 muda ukifika hata wewe kama una vigezo utatangaza nia yako,huku M4C bado hatujajua imefanikiwa kipi wengine wanahangaika na kugombea maana yake nini kama si ubinafsi?
 
Namuombea Mungu Mzee Mtei afikishe miaka 120 kwani ninaamini sasa hakuna mtu atakayeweza kusambaratisha chama mzee huyu akiwa hai

Molemo, Chadema kinaitaji kuanza succession plan ya washauri wenye busara mapema mkuu, kwa sababu yaliyokikuta CCM yanaweza kukifikaCDM pia. Nyerere ametoweka na busara zimetoweka kabisa kwenye chama kile. Ni vema succession planning ikaanza mapema kuandaa mtu, au watu wataoendeleza busara hizi kukinusuru chama na ombwe la leadership baadaye.
 
Back
Top Bottom