Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,457
- 154,324
Ni tarehe ishirini na sita mwezi wa kumi na mbili mwaka jana, kwa kizungu boksing dei, anaingia msichana mrembo kutoka Sydney Australia. Alikuwa huko kwa ajili ya masomo, ni mwanasheria na amehitimu shahada yake ya pili na sasa amerejea nyumbani.
Siku hiyo mi nlikuwa kijijini kwetu Kamsamba wilayani Mbozi mkoani Mbeya, hivyo basi sikuweza kwenda kumpokea.
Tarehe 31 jioni na mimi nikawa naingia dar es salaam kwa basi la Okoa linalofanya safari zake kati ya Tunduma na Dar. Kituoni Ubungo nilimkuta mrembo wangu aliyekuwa Sydney amekuja kunipoa.
Ilikuwa ni siku ya furaha kubwa sana kwangu. tukaenda nyumbani kwangu mitaa ya Mwananyamala kwa Manjunju, tukakaa huko hadi saa nne usiku ambapo nikamrudisha kwao Mbezi Beach. huku tukipeana ahadi za mimi kwenda kumchukua kwao kesho yake saa nne asubuhi.
kesho yake mzee nikatimba hadi kwao, nikapaki kimkweche changu nje ya geti lao nami nikazama ndani.
Tukawa tumejinafasi tukifurahia mahaba yaliyojaa umaridadi na ujuzi wa kamsamba na ule wa sydney. Riha zikatuzidia, sikumbuki hata ni muda gani vivazi vikawa vimetuponyoka.
katikati ya mchezo, tukiwa hapo sebuleni, mara tukaona mlango umefunguliwa, huku mzee mrefu mwenye misuli mikubwa ya kimazoezi akiwa amesimama mbele yangu.
Niliinuka, nikatoka nduki sijui nilifikaje kwetu Mwananyamala.
Usiku ndipo nikakumbuka kuwa nimeacha gari langu Mbezi Beach.
kweli huu mwaka niliuanza kwa staili ya tofauti sana.
Siku hiyo mi nlikuwa kijijini kwetu Kamsamba wilayani Mbozi mkoani Mbeya, hivyo basi sikuweza kwenda kumpokea.
Tarehe 31 jioni na mimi nikawa naingia dar es salaam kwa basi la Okoa linalofanya safari zake kati ya Tunduma na Dar. Kituoni Ubungo nilimkuta mrembo wangu aliyekuwa Sydney amekuja kunipoa.
Ilikuwa ni siku ya furaha kubwa sana kwangu. tukaenda nyumbani kwangu mitaa ya Mwananyamala kwa Manjunju, tukakaa huko hadi saa nne usiku ambapo nikamrudisha kwao Mbezi Beach. huku tukipeana ahadi za mimi kwenda kumchukua kwao kesho yake saa nne asubuhi.
kesho yake mzee nikatimba hadi kwao, nikapaki kimkweche changu nje ya geti lao nami nikazama ndani.
Tukawa tumejinafasi tukifurahia mahaba yaliyojaa umaridadi na ujuzi wa kamsamba na ule wa sydney. Riha zikatuzidia, sikumbuki hata ni muda gani vivazi vikawa vimetuponyoka.
katikati ya mchezo, tukiwa hapo sebuleni, mara tukaona mlango umefunguliwa, huku mzee mrefu mwenye misuli mikubwa ya kimazoezi akiwa amesimama mbele yangu.
Niliinuka, nikatoka nduki sijui nilifikaje kwetu Mwananyamala.
Usiku ndipo nikakumbuka kuwa nimeacha gari langu Mbezi Beach.
kweli huu mwaka niliuanza kwa staili ya tofauti sana.