Mohammed Hamad
JF-Expert Member
- Jan 17, 2011
- 3,988
- 1,301
Nakupenda sana mpezni wangu Mungu atakupa shifaa tutaonana kwa furaha.
- Si kitu kunipuuza, kwako tamaa sikati
Kilio sitogeuza, roho yangu mahtuti
Nilani utavyoweza, lakini sikubanduki
- Usirudi japo mwaka, Mimi nitakungojea
Ukirudi nakutaka, wala sitoona haya
Moyo wangu meridhika, sichoki kuvumiliya
- Wajuwa ninakupenda, ndio maana waniringiya
. Unanifanyia inda, mapenzi kuyasusiya
Baada ya hichi kidonda, na moto unakitiya - Anayependa kikweli, hachoki kuvumiliya,
Habadilishi kauli, hata ukimchukiya.