Nile maharage kwani mi muha

mfianchi

Platinum Member
Jul 1, 2009
11,855
8,251
''Nile maharage kwani mi Muha''hii ni kauli ambayo ilipendwa sana kutumiwa miaka ya nyuma na wakazi wa Kunduchi wakati huo njia ya kwenda Bagamoyo ilipita Kawe hadi nyumba za polisi Kunduchi,kauli hiyo ilitokana na wakazi wengi wa Kunduchi wakati huo wakiwa Wazaramo kupendelea kula samaki ambao walikuwepo kwa wingi,hao Waha wanaosemwa walikuwa wanfanya kazi kwenye shamba la mkonge la giriki liliokuwepo kuanzia Tangibovu hadi pale Mbuyuni , vibarua wengi wa hilo shamba walikuwa watu wa kuja kutoka Kigoma ambao ndio walikuwa wengi,na pia ndio walikuwa vibarua kwenye machimbo ya kokoto Kunduchi menu yao kubwa ilikuwa harage na dona.Kwa vijana wa CCM ya Jakaya naona mtashangaa kuwa kuanzia Tangibovu hadi Mbuyuni palikuwa shamba la mkonge,hivi sasa familia ya huyo giriki imebakiwa na kipande cha ardhi kuanzia kona ya Africana hadi Mbuyuni.Hawa Waha ambao walikuwa wanataniwa enzi hizo kwa kula maharage sasa ndio matajiri wa vitongoji vya Tengeta na Kunduchi na wale ambao walikuwa wanajifanya hawali maharage sasa maharage kwao ndio menu kubwa na ndio malofa,ama kweli dunia imebadilika .
 
Ye braza wee, naona hao jamaa hakuwahi kula maharage ya luwese ndio maana walisema hivyo. Ugali kwa maharage ya luwese, hapana bwana, nyama nyuma!
 
''Nile maharage kwani mi Muha''hii ni kauli ambayo ilipendwa sana kutumiwa miaka ya nyuma na wakazi wa Kunduchi wakati huo njia ya kwenda Bagamoyo ilipita Kawe hadi nyumba za polisi Kunduchi,kauli hiyo ilitokana na wakazi wengi wa Kunduchi wakati huo wakiwa Wazaramo kupendelea kula samaki ambao walikuwepo kwa wingi,hao Waha wanaosemwa walikuwa wanfanya kazi kwenye shamba la mkonge la giriki liliokuwepo kuanzia Tangibovu hadi pale Mbuyuni , vibarua wengi wa hilo shamba walikuwa watu wa kuja kutoka Kigoma ambao ndio walikuwa wengi,na pia ndio walikuwa vibarua kwenye machimbo ya kokoto Kunduchi menu yao kubwa ilikuwa harage na dona.Kwa vijana wa CCM ya Jakaya naona mtashangaa kuwa kuanzia Tangibovu hadi Mbuyuni palikuwa shamba la mkonge,hivi sasa familia ya huyo
giriki imebakiwa na kipande cha ardhi kuanzia kona ya Africana hadi Mbuyuni.Hawa Waha ambao walikuwa wanataniwa enzi hizo kwa kula maharage sasa ndio matajiri wa vitongoji vya Tengeta na Kunduchi na wale ambao walikuwa wanajifanya hawali maharage sasa maharage kwao ndio menu kubwa na ndio malofa,ama kweli dunia imebadilika .
Thx alot kwa huu uzi, umenifanya nijue kwa nini tegeta kuna waha wengi sana, kuanzia pale skaska mpaka kibaoni ni wamejaa waha tu na wengi wao wanamiliki maduka
 
Back
Top Bottom