Nikumbukwe kwa mambo nane nikiondoka ikulu 2015 -jk

ICHONDI

JF-Expert Member
Dec 3, 2008
600
134
brahim Bakari, Kaliua
MGOMBEA urais kwa tiketi ya CCM, Jakaya Kikwete amesema anataka Watanzania wamkumbuke kwa mambo nane wakati atakapoondoka Ikulu 2015.

Kikwete alisema hayo alipokuwa akizungumza na wananchi kwenye Jimbo la Urambo Magharibi alipokuwa akiomba ridhaa ya wananchi kumrejesha kuongoza serikali kwa kipindi kingine cha miaka mitano.


"Nimesema kuna mengi nayafanya, lakini nikimaliza kipindi changu nataka watu wanikumbuke kwa mambo nane... waseme Mungu amrehemu, yule bwana acha tu, amefanya kitu."

Huku akishangiliwa na mashabiki, wanachama na wapenzi wa CCM, Kikwete aliyataja mambo hayo kuwa ni; kuimarisha kilimo cha umwagiliaji kupitia mpango aliouasisi wa Kilimo Kwanza, matumizi bora ya mbolea, dawa za kilimo, kutoa wataalam na maofisa wengi wa kilimo.
Pia kusaidia upatikanaji wa masoko kwa mazao ya wakulima, kusimamia uwepo wa bei bora za mazao, kuimarisha barabara ili wakulima waweze kusafirisha mazao kutoka vijijini na kuachana na jembe la mkono na kutumia matrekta makubwa na madogo.


Kikwete aliyekiri kutofikiwa malengo kwa maeneo mbalimbali katika sekta ya maji na barabara, alisema katika kipindi cha miaka mitano ijayo serikali imejipanga kikamilifu kutekeleza ahadi zake.
Alisema kuna mengi yanahitaji misaada ya wahisani ikiwa ni pamoja na ujenzi wa barabara, ujenzi wa miundombinu ya kisasa ya maji hivyo ni lazima tuwatafute wahisani.

Akizungumzia safari zake za nje, Kikwete alisema: "Wapo wanaosema nasafiri sana, sasa ningekaa pale nyumbani kwangu nikamwangalia mke wangu Salma halafu nimwambie aisee ulivyopendeza, Watanzania wangekufa njaa na Wajapan wanaotaka kusaidia, leo hii wasingeijua Kaliua.

"Sasa kuyapata yote haya, lazima nisafiri. Nilikuwa Marekani, nikakutana na wahisani mbalimbali; wenyewe wananiuliza wanataka wanisaidie wapi, mimi nasema hapa na hapa na pale... kuna watu wanapesa nyingi tu."
Akizungumza katika mkutano huo, mbunge wa Urambo Magharibi, Prof. Juma Kapuya alisema CCM wameshafundishana kucheza mpira wa uchaguzi.

"Pasi ya kwanza anatoa diwani, diwani kwa mbunge na mbunge anatoa kwa rais anafunga goli... Kikwete ni (mshambuliaji wa Simba, Mussa Hassan) Mgosi wa CCM, ukimpa mpira anafunga," alisema Kapuya na kuamsha vicheko kwa wote waliofika kwenye mkutano huo.

Naye Kikwete aliyekuwa pembeni, baada ya Kapuya kumaliza, alisema: "Aah! Mimi bwana na Kapuya kuna mengi tunakubaliana, lakini katika soka, tuko timu tofauti, mimi siko huko," alisema Kikwete ambaye anajulikana kama shabiki mkubwa wa Yanga wakati Kapuya ni shabiki asiyejificha wa Simba. Hata hivyo alimaliza kwa kusema: "Timu bora inajengwa na ngome imara, kiungo imara na safu yenye mtazamo mmoja na ndiyo inayoshinda kuliko kuchanganya."

Naona JK sasa amechanganyikiwa moja kwa moja. Au la muandishi wa habari hakuandika mambo yote nane aliyosema JK. Kwa kuwa ameongelea sekta moja tu ya kilimo. Hata hicho kilimo kwanza ndio kwanza kinaanza, hatuna uhakika kuwa kitafanikiwa wakati wajanja wanakula fedha kila siku. Hata huo mradi wa kuagiza matrekta ulikuwa wa kifisadi sana!!!!
 
Huu ni upuuzi wa hali ya juu, kama mzee mzima ndio uchambuzi wake wa mambo ulivyo (kwamba hapo kuna mambo manane tayari), si ajabu hajui kwa nini tuko maskini. Inauma.
 
JK jana, anasema, ....."Nimesema kuna mengi nayafanya, lakini nikimaliza kipindi changu nataka watu wanikumbuke kwa mambo nane... waseme Mungu amrehemu, yule bwana acha tu, amefanya kitu (sourrce Mwananchi, 1/10/2010).

Swali langu kwa wana JF, huwa tunasema bwana amerehemu mtu akiwa hai au mfu. Kiswahili kimenipiga chenga.
 
Kiswahili hakijakupiga chenga Mkuu.
Kikwete ana maana hata atakapokuwa amekwishakufa watu wamuombee kwa Mungu wakikumbuka mema ambayo yuko supposed kuwa ameyafanya.
 
Nikumbukwe kwa mambo nane nikiondoka ikulu 2010.

Hatutakuwa na haja ya kukumbuka wewe jiondokee tu!!!!!!!
 

"
Nimesema kuna mengi nayafanya, lakini nikimaliza kipindi changu nataka watu wanikumbuke kwa mambo nane... waseme Mungu amrehemu, yule bwana acha tu, amefanya kitu."
Jamaa Kaahidi KIFO chake. Mungu mrehemu Marehemu sio mtu akiwa hai.
 
Tutamkumbuka kwa jinsi alivyotuingiza mkenge katika mikataba ya madini. Tutamkumbuka kwa jinsi alivyotuletea wawekezaji kuchukua ardhi yetu na wananchi kuhamishwa. Tutamkumbuka kwa jinsi alivyokumbatia mafisadi na kuacha ufisadi ushamiri chini ya uongozi wake. Tutamkumbuka kwa jinsi alivyosaidia kuua utawala wa kisheria nchini Tanzania. Tutamkumbuka kwa jinsi alivyoanza kutuletea utawala wa kifamilia.
 
Huyu jamaa nashangaza,baada awaache wananchi wamsifu anajisifu mwenyewe,hooooo nimeahidi nimetimiliza,hooooo nitanikumbuka kwa mengi,mi nakuomba uwaache wananchi wakuulize,au waulize maisha bora wamepata uliowaaidi,sio ujisifu mwenyewe,au ndio unatuaga?,mana dk wako sher hayaha kasema kuna mgombea atakufa kabla ya uchaguzi,twambie mzee mana toka umeanza kampeni haujaenda kubadilisha dam,yawezekana wadudu wamezidi.
 
Kiswahili hakijakupiga chenga Mkuu.
Kikwete ana maana hata atakapokuwa amekwishakufa watu wamuombee kwa Mungu wakikumbuka mema ambayo yuko supposed kuwa ameyafanya.


Mkuu pmwasyoke;1115501, asante sana kwa kunipamoyo kuwa kiswahili changu kiko fiti.

Ila tatizo linakuja pale JK anapotoa ahadi alafua anamalizia watu wasema MUNGU AMREHEMU. Huoni hapa kuna tatizo? Je ni ahadi kuwa baada ya kutoka ikulu 2015 moja kwa moja atakufa au? Mimi bado ninaomba msaada wa kueleweshwa!
 
No matter how hard I can try to remmember anything Mkwere huyu kafanya miaka 5 iliyopita honestly sipati japo dogo tu la kujifariji nalo! CCM wanalijua hilo wamekimbia midahalo yote! Ninacho kumbuka kila nikiwaza Kikwete, mshikaji narenare,kaanzisha vita dhidi ya ufisadi katishiwa kafyata mkia, (can you imagine a sitting president), ujenzi wa barabara ulimalizika pale ben alipoondoka imagine hata km 10 za mandela road zimekushinda, rushwa bandari ya dar wananchi wameihama, usimamaizi na ukusanyaji mbovu wa mapato ya serikali, mzee wa ahadi, tayari keshaahidi underground train, nadhani mradi wa mabasi yaendayo kasi keshaumaliza (jamaa anaahidi mpaka anasahau) naweza simulia siku nzima failures za mswahil huyu!
Kama lipo hata moja la kumkumbuka naomba mtu 1 atukumbushe!
 
Naona utabiri wa Shekhe unaanza kutimia taratibu du jamani niagieni du...
 
brahim Bakari, Kaliua
MGOMBEA urais kwa tiketi ya CCM, Jakaya Kikwete amesema anataka Watanzania wamkumbuke kwa mambo nane wakati atakapoondoka Ikulu 2015.

Kikwete alisema hayo alipokuwa akizungumza na wananchi kwenye Jimbo la Urambo Magharibi alipokuwa akiomba ridhaa ya wananchi kumrejesha kuongoza serikali kwa kipindi kingine cha miaka mitano.


"Nimesema kuna mengi nayafanya, lakini nikimaliza kipindi changu nataka watu wanikumbuke kwa mambo nane... waseme Mungu amrehemu, yule bwana acha tu, amefanya kitu."

Huku akishangiliwa na mashabiki, wanachama na wapenzi wa CCM, Kikwete aliyataja mambo hayo kuwa ni; kuimarisha kilimo cha umwagiliaji kupitia mpango aliouasisi wa Kilimo Kwanza, matumizi bora ya mbolea, dawa za kilimo, kutoa wataalam na maofisa wengi wa kilimo.
Pia kusaidia upatikanaji wa masoko kwa mazao ya wakulima, kusimamia uwepo wa bei bora za mazao, kuimarisha barabara ili wakulima waweze kusafirisha mazao kutoka vijijini na kuachana na jembe la mkono na kutumia matrekta makubwa na madogo.


Kikwete aliyekiri kutofikiwa malengo kwa maeneo mbalimbali katika sekta ya maji na barabara, alisema katika kipindi cha miaka mitano ijayo serikali imejipanga kikamilifu kutekeleza ahadi zake.
Alisema kuna mengi yanahitaji misaada ya wahisani ikiwa ni pamoja na ujenzi wa barabara, ujenzi wa miundombinu ya kisasa ya maji hivyo ni lazima tuwatafute wahisani.

Akizungumzia safari zake za nje, Kikwete alisema: "Wapo wanaosema nasafiri sana, sasa ningekaa pale nyumbani kwangu nikamwangalia mke wangu Salma halafu nimwambie aisee ulivyopendeza, Watanzania wangekufa njaa na Wajapan wanaotaka kusaidia, leo hii wasingeijua Kaliua.

"Sasa kuyapata yote haya, lazima nisafiri. Nilikuwa Marekani, nikakutana na wahisani mbalimbali; wenyewe wananiuliza wanataka wanisaidie wapi, mimi nasema hapa na hapa na pale... kuna watu wanapesa nyingi tu."
Akizungumza katika mkutano huo, mbunge wa Urambo Magharibi, Prof. Juma Kapuya alisema CCM wameshafundishana kucheza mpira wa uchaguzi.

"Pasi ya kwanza anatoa diwani, diwani kwa mbunge na mbunge anatoa kwa rais anafunga goli... Kikwete ni (mshambuliaji wa Simba, Mussa Hassan) Mgosi wa CCM, ukimpa mpira anafunga," alisema Kapuya na kuamsha vicheko kwa wote waliofika kwenye mkutano huo.

Naye Kikwete aliyekuwa pembeni, baada ya Kapuya kumaliza, alisema: "Aah! Mimi bwana na Kapuya kuna mengi tunakubaliana, lakini katika soka, tuko timu tofauti, mimi siko huko," alisema Kikwete ambaye anajulikana kama shabiki mkubwa wa Yanga wakati Kapuya ni shabiki asiyejificha wa Simba. Hata hivyo alimaliza kwa kusema: "Timu bora inajengwa na ngome imara, kiungo imara na safu yenye mtazamo mmoja na ndiyo inayoshinda kuliko kuchanganya."

Naona JK sasa amechanganyikiwa moja kwa moja. Au la muandishi wa habari hakuandika mambo yote nane aliyosema JK. Kwa kuwa ameongelea sekta moja tu ya kilimo. Hata hicho kilimo kwanza ndio kwanza kinaanza, hatuna uhakika kuwa kitafanikiwa wakati wajanja wanakula fedha kila siku. Hata huo mradi wa kuagiza matrekta ulikuwa wa kifisadi sana!!!!

nCHI MASIKINI ITAENDELEA KWA KUTEGEMEA MISAADA TOKA KWA WAHISADNI (jk)
NDO MAANA NAMPENDA SANA HUYU JAMAA NIMKWELI KABISAA!!
 
hiyo ahadi ya mwisho ndiyo itakayotekelezwa ndani ya miaka mitano. mungu amlaze mahali pema.aaaaaamin
 
akumbukwe kwa
ufisadi
kugawa vyeo kwa masela wake
kuanguka anguka
kucheka cheka
kujaza mabango
kuogopa midahalo
kutojua kwanini nchi ni maskini
kusafiri kama vasco da gama
:smow:
 
JK jana, anasema, ....."Nimesema kuna mengi nayafanya, lakini nikimaliza kipindi changu nataka watu wanikumbuke kwa mambo nane... waseme Mungu amrehemu, yule bwana acha tu, amefanya kitu (sourrce Mwananchi, 1/10/2010).

Swali langu kwa wana JF, huwa tunasema bwana amerehemu mtu akiwa hai au mfu. Kiswahili kimenipiga chenga.
Wahenga husema mtu akikaribia kufa huwa anaaga kwa aina yake, hata Baba wa Taifa alipokaribia siku zake alisema 'Najua watanzania mtalia lakini nitawaombea kwa Mungu'. Kama JK mwenyewe kasema hivyo basi nami nasema amrehemu marehemu mtarajiwa.
 
Back
Top Bottom