Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,720
- 21,779
BIG UP MKUU KAMA ILITOKA MOYONI
Katibu wa Mambo ya Nje ya Sekretarieti ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Januari Makamba, amesema haogopi kufukuzwa kutoka katika chama hicho, ikiwa hatua hiyo inalenga kukidhi maslahi ya wanasiasa wasiokuwa wakweli.
Makamba ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli (CCM), anasema ukweli ni moja ya misingi iliyo nguzo ya kukikifanya chama hicho kukubalika kwa umma na kuendelea kushika hatamu za uongozi.
Hivi karibuni, Makamba alitajwa kuwa mmoja wa wabunge waliosulubiwa wakati wa kikao cha wabunge wa CCM cha hivi karibuni kutokana na kile kinachodaiwa kupingana na misimamo ya chama hicho.
Mbunge huyo amekuwa miongoni mwa 'makamanda' wanaopinga ongezeko la posho za vikao kutoka Sh. 70,000/- hadi 200,000/- kwa kila mbunge kwa siku, kwamba haliendani na hali ya uchumi wa nchi ama hali duni ya wananchi walio wengi.
Wabunge kadhaa wakiwemo wenye nyadhifa za uwaziri, wametajwa kuwa nyuma ya hoja hiyo, lakini Makamba anasema kila jambo analolifanya, linalenga kuinufaisha CCM na serikali.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mwishoni mwa wiki, Makamba alisema wabunge na mawaziri wanaoamini kuwa anastahili kufukuzwa uanachama wa CCM, wanapotoka na kwamba wameshindwa kupima matakwa ya jamii.
Wenye kutoa hoja hiyo wamepotoka, wanapaswa kuipima jamii tunayoingoza, ina matakwa gani, alisema.
Makamba ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, alisema CCM inakabiliwa na changamoto ya kutambua msukumo uliopo kwa wapiga kura na mtazamo wa wanasiasa wa kizazi cha sasa kinachohitaji suluhu ya matatizo badala ya maelezo.
Naye Mbunge wa Simanjro (CCM), Christopher Ole Sendeka alisema wana CCM wanaowaona wabunge wanaotoa maoni yanayotofautiana na maslahi yao kuwa ni wahalifu, hawajui misingi ya haki inayoanishwa kwenye Katiba ya nchi na ile ya chama hicho.
Alisema kuna baadhi ya watu ndani ya chama hicho wanaoshindwa kuutambua ukweli, badala yake kusimamia hoja inayolenga kuhujumiana miongoni mwao.
Kuhusu tabia ya wabunge wa CCM kupinga hoja za mawaziri, Ole Sendeka aliionya serikali ili ijiepushe na mazoea ya kukurupuka wakati wa kuwasilisha hoja na miswada bungeni.
Kwa upande wake, Mbunge wa Mvomero (CCM), Amos Makalla katika mazungumzo nami alisema katika masuala yenye maslahi kwa umma hususani ndani ya mipaka ya majimbo, hakuna sababu ya kuionea aibu serikali hasa pale inaposhindwa kutekeleza wajibu wake.
Anabainisha moja ya maeneo yasiyostahili chembe ya aibu dhidi ya serikali ni Muswada wa Sheria ya Marekebisho 17 ikiwamo Bodi ya Mikopo iliyobainika kuwa na ishara za ubaguzi hasa kwa raia walio masikini.
Mapema wiki hii, wabunge wengi wao wakiwa kupitia CCM, walishinikiza kuondolewa kwa hoja mbili za serikali zilizotolewa na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo na Mwanasheria Mkuu, Jaji Frederick Werema.
Hoja ya Mkulo ilihusu kuliomba Bunge liidhinishe punguzo la ushuru wa maji ya kunywa kutoka Shilingi 69 hadi Shilingi 12, wakati Werema aliwasilisha hoja ya mabadiliko ya sheria 17 ikiwemo ya Bodi ya Mikopo. Hoja hizi sasa zitaletwa tena kwenye mkutano ujao mwezi Aprili mwaka huu.
Katibu wa Mambo ya Nje ya Sekretarieti ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Januari Makamba, amesema haogopi kufukuzwa kutoka katika chama hicho, ikiwa hatua hiyo inalenga kukidhi maslahi ya wanasiasa wasiokuwa wakweli.
Makamba ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli (CCM), anasema ukweli ni moja ya misingi iliyo nguzo ya kukikifanya chama hicho kukubalika kwa umma na kuendelea kushika hatamu za uongozi.
Hivi karibuni, Makamba alitajwa kuwa mmoja wa wabunge waliosulubiwa wakati wa kikao cha wabunge wa CCM cha hivi karibuni kutokana na kile kinachodaiwa kupingana na misimamo ya chama hicho.
Mbunge huyo amekuwa miongoni mwa 'makamanda' wanaopinga ongezeko la posho za vikao kutoka Sh. 70,000/- hadi 200,000/- kwa kila mbunge kwa siku, kwamba haliendani na hali ya uchumi wa nchi ama hali duni ya wananchi walio wengi.
Wabunge kadhaa wakiwemo wenye nyadhifa za uwaziri, wametajwa kuwa nyuma ya hoja hiyo, lakini Makamba anasema kila jambo analolifanya, linalenga kuinufaisha CCM na serikali.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mwishoni mwa wiki, Makamba alisema wabunge na mawaziri wanaoamini kuwa anastahili kufukuzwa uanachama wa CCM, wanapotoka na kwamba wameshindwa kupima matakwa ya jamii.
Wenye kutoa hoja hiyo wamepotoka, wanapaswa kuipima jamii tunayoingoza, ina matakwa gani, alisema.
Makamba ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, alisema CCM inakabiliwa na changamoto ya kutambua msukumo uliopo kwa wapiga kura na mtazamo wa wanasiasa wa kizazi cha sasa kinachohitaji suluhu ya matatizo badala ya maelezo.
Naye Mbunge wa Simanjro (CCM), Christopher Ole Sendeka alisema wana CCM wanaowaona wabunge wanaotoa maoni yanayotofautiana na maslahi yao kuwa ni wahalifu, hawajui misingi ya haki inayoanishwa kwenye Katiba ya nchi na ile ya chama hicho.
Alisema kuna baadhi ya watu ndani ya chama hicho wanaoshindwa kuutambua ukweli, badala yake kusimamia hoja inayolenga kuhujumiana miongoni mwao.
Kuhusu tabia ya wabunge wa CCM kupinga hoja za mawaziri, Ole Sendeka aliionya serikali ili ijiepushe na mazoea ya kukurupuka wakati wa kuwasilisha hoja na miswada bungeni.
Kwa upande wake, Mbunge wa Mvomero (CCM), Amos Makalla katika mazungumzo nami alisema katika masuala yenye maslahi kwa umma hususani ndani ya mipaka ya majimbo, hakuna sababu ya kuionea aibu serikali hasa pale inaposhindwa kutekeleza wajibu wake.
Anabainisha moja ya maeneo yasiyostahili chembe ya aibu dhidi ya serikali ni Muswada wa Sheria ya Marekebisho 17 ikiwamo Bodi ya Mikopo iliyobainika kuwa na ishara za ubaguzi hasa kwa raia walio masikini.
Mapema wiki hii, wabunge wengi wao wakiwa kupitia CCM, walishinikiza kuondolewa kwa hoja mbili za serikali zilizotolewa na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo na Mwanasheria Mkuu, Jaji Frederick Werema.
Hoja ya Mkulo ilihusu kuliomba Bunge liidhinishe punguzo la ushuru wa maji ya kunywa kutoka Shilingi 69 hadi Shilingi 12, wakati Werema aliwasilisha hoja ya mabadiliko ya sheria 17 ikiwemo ya Bodi ya Mikopo. Hoja hizi sasa zitaletwa tena kwenye mkutano ujao mwezi Aprili mwaka huu.