Niko sahihi au?

Ninamaanisha SHOSTI member wa JF ndiye Salma Juma. Kajisahau akiwa kalog in kama SHOSTI akajibu post kama SALMA JUMA. Mineisoma wakati naiquote ili kumwambia nilimwambia hapo juu, akawa tayari kaifuta.
nimerudi ndugu,unalolisema halina ukweli hata kwa aslimia 0,ulomtaja hana mume mie nna mume mtu wa mbeya,ulomtaja anamtoto molato mie mtoto wangu mswahili kuanzia rangi mpaka nywele,ulomtaja mwanae ana miaka saba wangu anamiaka 14....ila yeye ndo mwanzo wa mimi kuuliza swali langu lakini nlichokipata mungu anajua.Mmenihukumu kwa nisiyoyatenda wala si tabia zangu..kama ntaendelea kuwamo humu utagundua nani ni nani mpendwa sina haja ya kuchezea akili za watu.
 
Ninamaanisha SHOSTI member wa JF ndiye Salma Juma. Kajisahau akiwa kalog in kama SHOSTI akajibu post kama SALMA JUMA. Mineisoma wakati naiquote ili kumwambia nilimwambia hapo juu, akawa tayari kaifuta.


Naona kama kuna kuchezeana akili sasa, Awe SHOSTI au Salma Juma, ukweli utabaki kuwa Ukweli, AMEZE au ATEME ni shauri yake. Mie kwa Upande Wangu naona kuna mengi yamejificha SHOSTI/SALMA hajayasema anataka baraka za watu kumtupia mumewe makosa hata kama yeye anaonekana hajatenda Vyema. Huwezi Kutamani Ndoa iliyo safi kama wewe u-play part yako kuitengeneza hiyo ndoa. Haiji kwa Miujiza bali mume na mke mnaitengeneza kwa Kumshirikisha Mungu. Miaka 4 hujaonana na mumeo ina maana una Bwana mwingine ndo anakupa kiburi mpaka kuamua kuhama Chumba. Kwa taarifa yako, kama unaye anakupa promise za motox2 kwa vile upo kwa mumeo. Ukisema uachane na mumeo (Namuona kama mpole vile asiye muongeaji) ukaambatani na huyo bazazi utakuja kumuona huyu wa sasa ni bora zaidi. Kaza mkanda dada, pigania ndoa yako. Sikushauri chochote zaidi ya kukwambia badilika na Mtegemee Mungu.
 
kwa kusoma majibu ya huyu anayejiita salma juma nimegundua tabia hizi toka kwake kwa huu muda mfupi tu niliofuatilia hii thread yake.

1-mkali
2-jeuri
3-hapendi kukosolewa bali anapenda kusifiwa tu
4-anajifanya yeye mtakatifu hamkosei mumewe/si mkosaji hata kidogo
5-ni mtu wa kujikweza si wa kujishusha
6-anachoamini yeye analazimisha na wengine waamini hivyohivyo pasipo kuhoji .
7-ni mtawala
8-anapenda kupokea misaada si mtoaji wa misaada
9-mkaidi
hizo tabia za huyu dada hauwezi kuzigundua haraka ila mpaka usome thread yake na maoni ya wanajf pamoja na majibu yake kwa wanajf.

mwanamke wa aina hii kujenga nyumba yake ni ngumu sana.
huyo mwanamme kuishi na mwanamke wa aina hii miaka yote hii anastahili pongezi.
mwanamke wa aina hii hastahili kuolewa bali kuwa single parent tu.

nadhani tungepata bahati ya kusikiliza upande wa mumewe angesema zaidi ya haya niliyoyasema.

pole sana salma nawe labda ndivyo ulivyoumbwa, ila fahamu hakuna binadamu mtakatifu wote waja wa mungu tuna mapungufu yetu, ndiyo maana tuna mungu,makanisa na misikiti ili tukaombe msamaha huko na kuomba baraka,hekima,utu,na busara ktk maisha yetu. Hiyo ndoa yako haina matatizo makubwa sana ila wewe umelazimisha yawe makubwa na magumu kwa hizo tabia zako chache nilizoorodhesha hapo juu,
pole sana ila kwa mungu yote yanawezekana.

 
sijaelewa inakuwaje mtoto mmoja awashinde muongeze wengine...

Bila kuacha kiburi hata huyo mmeo akikuacha hutapata mme tena,hadi ung'oe kiburi chote na majivuno!
Nahisi wakati ana kuchumbia ulikua mpole kweli duh,so bad jamaa hayumo JF angetwambia
 
Bila kuacha kiburi hata huyo mmeo akikuacha hutapata mme tena,hadi ung'oe kiburi chote na majivuno!
Nahisi wakati ana kuchumbia ulikua mpole kweli duh,so bad jamaa hayumo JF angetwambia
kiukweli unanihukumu kakangu,mungu atanisimamia kwa hili na lingine.....Amin.
 
kiukweli unanihukumu kakangu,mungu atanisimamia kwa hili na lingine.....Amin.

Samahani sana dadangu..
Ila inaniwia vigumu sana kukuamini,...nime jilazimisha sana nimeshindwa!
Naamini unafaa kuwa muigizaji kabisa sister,...
 
hapa tutachangia mpaka bahari ikauke, lkn tufanyacho ni sawa na kulima juu ya mwamba kwa sababu za tatizo hapa hazikutajwa, hili suala ki undani c hv lilivyo.
 
Samahani sana dadangu..
Ila inaniwia vigumu sana kukuamini,...nime jilazimisha sana nimeshindwa!
Naamini unafaa kuwa muigizaji kabisa sister,...

Watu wamekomaa kusema hili na lile, unabaki unashangaa mbona huyu hagutuki tu, kumbe kakubuhu mwenzetu. Anawachora mnavyohangaika mara this mara that. Bila shaka sio kwamba wanaishi vyumba mbali mbali na mumewe, inawezekana kabisa kwamba kamtoroka mumewe na wanaishi nchi mbali mbali.

Watu kama hawa ndio wanafanya wanawake wadharauliwe na wanaume, na kuwafanya wanaume wengine waogope kuoa.
 
Samahani sana dadangu..
Ila inaniwia vigumu sana kukuamini,...nime jilazimisha sana nimeshindwa!
Naamini unafaa kuwa muigizaji kabisa sister,...

Watu wamekomaa kusema hili na lile, unabaki unashangaa mbona huyu hagutuki tu, kumbe kakubuhu mwenzetu. Anawachora mnavyohangaika mara this mara that. Bila shaka sio kwamba wanaishi vyumba mbali mbali na mumewe, inawezekana kabisa kwamba kamtoroka mumewe na wanaishi nchi mbali mbali.

Watu kama hawa ndio wanafanya wanawake wadharauliwe na wanaume, na kuwafanya wanaume wengine waogope kuoa.

hapa tutachangia mpaka bahari ikauke, lkn tufanyacho ni sawa na kulima juu ya mwamba kwa sababu za tatizo hapa hazikutajwa, hili suala ki undani c hv lilivyo.

Umenena mpendwa.
 



Hapo kwenye Red Umejuwaje kama tatizo ni la mwanaume? Naona kama mtoa mada hajasema chcoche kilichomfanya mumewe asiwe karibu na familia.

Ameulizwa swali na mchangiaji hapo juu naona analikwepa, Ameulizwa ''Ulishamsaliti mumeo kwa kutoka nje'' hajajibu. Haiwezekani mwanaume aijali familia ya mkewe ila asimjali mkewe lazima mwanamke umechangia kwa njia moja au nyingine kumkimbiza mbali mumewe. Yawezekana na wewe dada unarefusha mabega kutaka uwe kichwa cha nyumba kitu ambacho mumeo hakikubali bali kukupuuza. Labda unaongea sana, mbele ya mtoto wenu unaongea vibaya kumkandya mumeo... hiyo nayo inaweza kufanya mumeo akupuuze maana anaona hujampa nafasi kama baba wa nyumba kila kitu unajifanya ni wewe.

Unasema mumeo anatowa matumizi yote ya familia ila ukaribu tu kwa familia ndo haupo... Haingii akilini kwa mtu wa kuhudumia familia asijali familia dada lazima na wewe kuna kitu ulikifanya kikamuumiza mumeo na hukuomba msamaha au ulifanya jeuri.

Unalalamika wachangiaji wengine wanatoa ushauri wa kukupinga, nadhani ni haki wa wachangiaji kupima maneno uliyotowa na wakatowa comments zao kwa kadili wanavyoelewa. Si lazima wote wakubaliane na wewe hata kama wanaona wewe ndo mwenye matatizo.

Kwa mwanaume kutokuwa karibu na mtoto wako tu kweli ndo kilicho kutowa chumbani na kuamia chumba kingine au kuna lingine hutaki kusema? Kwa mwanamke mcha Mungu usingezigi kuweka gap kiasi hicho na mumeo kwa kukimbia chumba. Kuhama chumba ni kuongeza tatizo zaidi ya kulipunguza. Umehama chumba umepata unafuu wowote hadi leo? Rudi chumbani kwa mumeo, na Ujishushe Uombe samahani kwake umwambie kama kuna kosa ulilifanya basi akusamehe.... hii yote kujionyesha kwake kuwa unampenda na bado unamuhitaji katika maisha yako. Acha jeuri/ukolofi kwa mumeo. Huyo ndo uliyempenda na kukubali awe mumeo,... mapungufu ni ya binadamu, jishushe kwa mumeo na zaidi mpe mumeo nafasi yake kama baba wa familia. Juwa wajibu wako kama mama na umwachie mumeo wajibu wake kwa familia na kwa mtoto.


Zaidi, Muombe Mungu akusamehe kwa mapungu uliyonayo, akailinde ndoa yako na familia yako. Akakuongoze katika kuongea kwako ili usimkwaze mumeo bali ukaongee yale yatakayoijenga ndoa yako.

bonge la ushauri hili Ngo!
 
nashukuru mpendwa kwa ushauri wako ntautekeleza japo mgumu kumeza,kiukweli mume wangu hachelewi kurudi nyumbani huwa anarudi wakati mwingine kabla yangu,laikini hata akirudi hwezi kumkuta mtoto akajaribu hata kuongea nae mawili matatu,nikirudi naanda msosi ukimuita anasema endeleeni nakuja mkibmaliza anachukua sahani yake anaanza kula...ungekuwa weye iungemwelewaje huyu mwanaume zaidi ya kuchukia tu...

Kuna kitu nimekiona hapa, naomba niulize mumeo ajawahi kulalamika kuhusu mtoto?

Tabia yake, au kutoamini kwamba ni wake?
 
kwa kusoma majibu ya huyu anayejiita salma juma nimegundua tabia hizi toka kwake kwa huu muda mfupi tu niliofuatilia hii thread yake.

1-mkali
2-jeuri
3-hapendi kukosolewa bali anapenda kusifiwa tu
4-anajifanya yeye mtakatifu hamkosei mumewe/si mkosaji hata kidogo
5-ni mtu wa kujikweza si wa kujishusha
6-anachoamini yeye analazimisha na wengine waamini hivyohivyo pasipo kuhoji .
7-ni mtawala
8-anapenda kupokea misaada si mtoaji wa misaada
9-mkaidi
10-Ana mpango wa kando,for 4years kanogewa anataka njia ya kumuacha mumewe
hizo tabia za huyu dada hauwezi kuzigundua haraka ila mpaka usome thread yake na maoni ya wanajf pamoja na majibu yake kwa wanajf.

mwanamke wa aina hii kujenga nyumba yake ni ngumu sana.
huyo mwanamme kuishi na mwanamke wa aina hii miaka yote hii anastahili pongezi.
mwanamke wa aina hii hastahili kuolewa bali kuwa single parent tu.

nadhani tungepata bahati ya kusikiliza upande wa mumewe angesema zaidi ya haya niliyoyasema.

pole sana salma nawe labda ndivyo ulivyoumbwa, ila fahamu hakuna binadamu mtakatifu wote waja wa mungu tuna mapungufu yetu, ndiyo maana tuna mungu,makanisa na misikiti ili tukaombe msamaha huko na kuomba baraka,hekima,utu,na busara ktk maisha yetu. Hiyo ndoa yako haina matatizo makubwa sana ila wewe umelazimisha yawe makubwa na magumu kwa hizo tabia zako chache nilizoorodhesha hapo juu,
pole sana ila kwa mungu yote yanawezekana.


Pamoja kiongozi na hiyo namba 10.
 
NALONGA,
ASANTE KWA KUONGEZEA HIYO # 10.........

japo naogopa hayo macho yako ...lol
 
hata mie nahisi huyu dada ana matatizo,sijaona tatizo kubwa kiviiile kny ndoa yake.....salma ushukuru kupata mume mpole kama huyo,ungepata mume mzinzi,mlevi asiyetoa hata senti kwa familia yake sijui ungefanyaje????eti kutoijali familia yake ndio kumekukimbiza chumbani??????its sooo hard for us to believe this????haimake sense kabisaa dada yangu!
 
hata mie nahisi huyu dada ana matatizo,sijaona tatizo kubwa kiviiile kny ndoa yake.....salma ushukuru kupata mume mpole kama huyo,ungepata mume mzinzi,mlevi asiyetoa hata senti kwa familia yake sijui ungefanyaje????eti kutoijali familia yake ndio kumekukimbiza chumbani??????its sooo hard for us to believe this????haimake sense kabisaa dada yangu!

Saaly mbona ume ni-grania ki uonevu bana why?
 
Pole sana dada, Hebu jaribu kufanya juhudi za kurudisha uhusiano, mmoja kati yenu lazima akubali kuwa mjinga ili kunusuru hili tatizo. kwasababu wewe umekuwa wa kwanza kuliona hili, anza kuchukua hatua. Lichukulie mzigo swala hili, funga na kuomba kwa siku tatu mpaka wiki moja mshirikishe Mungu wako katika hili, hakuna lisilo wezekana kwa Mungu.. Jitahidi kila jioni kuhudhuria ibada, kama kanisani kwenu hakuna ibada za kilasiku tembelea makanisa ya jirani. Usifanye ibada ya kawaida! ifanye iwe serious, unaweza washirikisha baadhi ya watu katika maombi yako na sio lazima uwaambie matatizo yanayo kukabili ila waambie unamatatizo ya kifamilia na wakukumbuke/shiriki katika maombi yako ikiwezekana wapige kambi ndogo (jioni) nyumbani kwako. Hilo ni pepo tu, Kwa Yesu hakuna lisilo wezekana
 
Mtu akiwa na shida na amechanganyikiwa si vizuri kutoa value judgements jamani.
I think she kept all these for four years afraiding of these kinds of blames.

Mimi dada ushauri wangu (regardless nani ni chanzo) jaribu kuongea na doctor wake maana nahisi mko nje ya nchi.

Nahisi mumeo amepata serious health problem na inawezekana hana huwezo wa sex tena. Sasa mmekutana wote ni loners ameshindwa kushare matatizo alonayo na wewe na wewe umeshindwa kushare matatizo yako na watu wengine (church, friends).

Anakeep distance ili usimwombe mambo kwani hana huwezo wa kukutimizia.

Chunguza kama afya yake iko sawa.


Hapo kuna jambo, dada anataka kuvunja ndoa, kafanya vituko aachwe hajaachwa. Sasa anatafuta sababu ya kuacha.

Huyu mama/dada anataka kubomoa na hapa anatafuta symphathy. Tatizo hapa ni yeye mwenyewe, asuke au anyoe at herr own risk.

JF tunatoa ushauri wa kujenga na si kubomoa; na ushauri huo unatolewa kuendana na tatizo lenyewe, tunasema ukweli unaostahiki. Ila kwako mleta mada tatizo ni wewe narudia tena, unachofanya si sahihi.
 
Tatizo ninaloliona hapo ni makuzi aliyokulia mumeo, ameshasema yeye hakuwahi kuona baba yake akila mezani na familia yake. Ni vigumu sana kumbadili mtu huyu ili awe kama unavyotaka. Mara nyingi malezi/makuzi yanaathiri sana maisha yetu ya kila siku tunayoishi. Kwa bahati wengine hubadilika na kuishi kutokana na mazingira au wenzi wao, na wengine ndio inabidi wewe ndio ubadilike ili uweze kuishi na mtu wa aina hiyo. Hivyo basi, kwa kuwa ameshakupa historia ya makuzi yake, huna haja ya kulazimisha abadilike utu uzimani. Mkubali alivyo na ujirudi uishi na mumeo kama zamani. Vinginevyo piga goti sali tena kwa bidii sana maana kwa Mungu hakuna linaloshindikana, itachukua muda ila anaweza kubadilika. Lazima pia na wewe ukubali hali yake katika kumsaidia kubadilika. Kila la kheri
 
Back
Top Bottom