NIKO LIVE toka Diamondo Jubilee

................JK anaharibu kuanza kushambulia watu ambao walisimama kidete kuamsha umma wa watanzania na wabunge juu ya Richmond...angekaa kimya ingetosha pia kuwa kampeni ya CCM, kuanza kutangaza huku wengi tunaingiwa na mashaka juu ya maamuzi yake..................

hapo umenena ndg yangu Chuma................haswaaa, hakukuwa na haja ya yeye JK kushambulia akina Dk. Slaa.....................kwani statement kama hizo hazina impact/mvuto wowote kwa wananchi na hasa baada ya wananchi kusikia/kuwekewa wazi issue nzima ya Richmond na kamati teule iliyoongozwa na Dr. Mwakyembe
 
eti embu nisaidieni hili.eti ni kweli issue ya richmond hawakuanza wapinzani?au JK anatupiga changa la jicho?nisaidieni wadau.
 
Now JK akiri kwamba alitaka kufanya mabadiliko ya baraza . Long LIVE JF tulisema mapema akawa ana buy muda kwamba hadi Bush aondoke .Lakini siku zote alisema ni uvumi leo amekiri LIVE.Hongera JF kwa nyeti .
MI NILISTUKA NILIPOWASHA TV NIKAKUTA WAZEE WA SISIEM NDIO WAMEJAA DIAMOND NIKAWEKA STAR TV NAKO KUKAWA KAMA TVT.HIV HAWA WANATUTAFUTA NINI JAMANI.tATAKIRUDIA SAA TANO USIKU STAR TV TUONE WALISEMA NINI WALIOTANGULIA.Tena hii ta kuongea na wazee ilikuwa iwe saa tisa ghafla wakachange nwa walijua kabisa akina zito ndio wataanza kuongea jamni umechoka kuburuzwa mengi tusaide rusha na wewe live hili bunge
 
Hii habari ya Richie bado mbichi kwa kuwa bado wananchi tunailipa Richmond kila kukicha lazima tulilie vichwa vya akina karamagi, Aziz na Lowassa unajua tunafanya kazi na kuwalipa pesa zetu kupitia Umeme kwa hiyo tunawekeza kwenye mali zao.

Baada ya muda tutagawana walicho nacho na kuwafungulia mashitaka. Majambazi lazima wafungwe tu haiwezekani wakaendelea kutanua mijini kwa pesa za watanzania.

Lazima vijwa vyao ni halali yetu tu, ninachoona polisi wawachukue haraka wasiendelee kukaa bungeni kabisa. Hawawezi kukaa bungeni na wanamwakilisha nani wakati ni wezi wa watanzania?
 
Hapa naona bunge limechangamka na haswa baada ya wajumbe wa kamati kuanza kuzungumza na hapa anazungumza Mnyaa na anasema kuwa kwenye uchunguzi wao mitambo tuliyokodi ya Richmond inapatikana pamoja na kuisafirisha kwa dola 56 milioni, wakati sisi tumekodisha mitambo hiyo kwa dola 86 milioni huku tukiendelea kudaiwa capacity charge kila siku na kila kukicha .

Ukiangalia kwa umakini hapo utaona jinsi amabavyo mafisadi hawa walivyoweza kutulalia na kutufanya mandondocha wa kutisha .
 
Kesho mjadala utafungwa na mwenyekiti wa kamati majira ya saa sita na nusu mchana .


Nitakuwepo ndani ya nyumba ili kuweza kufanya kazi hii na kuwajulisha kama wabunge wamekubaliana na mapendekezo ya kamati ama wameamua kufanya kitu gani juu ya hoja hii kama ni kuwafunga ama kuwashitaki na kuwafilisi.
 
Spika anahitimisha bunge kwa kuwatangazia wabunge kuwa leo ni siku ya wapendanao na anawatakia kila la kheri.

Pia anatangaza kuwa leo ukumbi wa royal village Beatrice Shelukindo amendaa party ya wapendanao ukumbi wa royal village na wote wawe wamevaa nguo nyekundu.

Spika anasema kuwa yeye hatakuwepo kwani kwa utamaduni wa nyumba yake huwa siku hiyo wanaisheherekea wakiwa wawili tuu vyumbani wabunge wanacheka.
 
Lunyungu,

..nimesha-conclude kwamba Kikwete is the man behind Richmond. Haiyumkiniki Waziri Mkuu akiuke maagizo ya cabinet na kuwa-pressurize mawaziri bila "baraka" za Raisi.

..Kikwete alijaribu kulizima suala hili kwa kuwahamisha wizara Msabaha na Masha. Hata ktk mahojiano na tume Msabaha amesema yeye atatolewa kafara. Inaelekea Msabaha hakuafikiana na mkataba wa richmond.

..Waziri ni mteule wa Raisi kama alivyo Waziri Mkuu. Ikitokea waziri akatofautiana na waziri mkuu, basi waziri ana nafasi ya kushtaki kwa Raisi. Je, Msabaha alifanya hivyo? Je, Msabaha aliripoti ukiukwaji wa maadili wa Waziri Mkuu kwa Raisi?

..Ndiyo maana nasisitiza ni bora tuone viambatanisho vyenye mahojiano ya Msabaha na Tume ya Mwakyembe. Specifically nataka kuona kama Msabaha alimripoti Lowassa kwa Raisi.
 
hapo umenena ndg yangu Chuma................haswaaa, hakukuwa na haja ya yeye JK kushambulia akina Dk. Slaa.....................kwani statement kama hizo hazina impact/mvuto wowote kwa wananchi na hasa baada ya wananchi kusikia/kuwekewa wazi issue nzima ya Richmond na kamati teule iliyoongozwa na Dr. Mwakyembe
Ni kwamba muungana hajui kama watu huwa tunapoteza muda kufuatilia bunge kwa masaa kibao na kuacha shughuli nyingine.sisi tunakumbuka hoja hii ilitolewa na wapinzani na kilangu alipotaka kujua zaidi akafungwa mdomo.hii inanifurahisha kuona mkuu wetu anajichanganya kwa kiasi hiki,inataka kufanana na bot mana wamejifaya walianza uchunguzi mapema so hoja ni yao.sisi hatujali iwe yao iwe ya slaa tunataka watu wawajibishwe kwa kulisababishia taifa hasara
 
JK aingia ushabiki atangaza kwamba CCM ndiyo wenye issue ya Richmond na kwamba ni CCM ndiyo wanafanya kazi .Amponda Dr.Slaa na kusema anataka sifa binafsi na si mkweli kabisa .Kawataja wana CCM kwenye kamati na kuonyesha kwamba ni Shelukindo kaanza issue .

hapa mkuu ulipindisha kwa makusudi hukutupa vile ambavyo JK alisema, uligtulisha kasa.


JK ameeleza kuwa suala lile ni suala la wabunge wote isipokuwa watani wao wamelifanya lao peke yao, na akaeleza na huenda wabunge wa CCM walikuwa wakali zaidi kuliko wao.

pia akasisitza kuwa kuna mmoja huyo analitumia kiteto ktk kampeni ati yeye ndio ameiangusha serikali ya kikwete dodoma.

mkuu jitahidi kuleta habari kama zilivyosemwa usitulishe kasa hadhi yako itashuka na authentication yako itakuwa chini mzee ni ushauri tu
 
Kuna siri kubwa kati ya hawa wakuu yaani RA, EL na JK .Kaeni macho watanzania .

Maji yanazidi kuwa tope zaidi. Lakini uhakika upo, wajuzi wa kuyachuja yote haya ili pabakie na maji safi wapo.
Hatimae, wananchi wataupata ukweli wote.

Matumaini yangu ni kwamba matukio kama haya yanafanyiwa kazi ipasavyo na wapinzani; ili wayapange vizuri na kuwaelimisha wananchi wote. Hii ndio kazi hasa ya 'wataalam' wa mambo ya kisiasa walioko huko.
 
Now JK akiri kwamba alitaka kufanya mabadiliko ya baraza . Long LIVE JF tulisema mapema akawa ana buy muda kwamba hadi Bush aondoke .Lakini siku zote alisema ni uvumi leo amekiri LIVE.Hongera JF kwa nyeti .

mbona mkuu wa kaya ana tabia ya kuwa kigeugeu,au amesehau kwamba alishawahi kusema ni uvumi,au LOWASSA Alimkataza,kuna haja ya kumuuliza maswali magumu kama haya..lazima mkuu wa nchi uwe na msimamo,bush??
 
JK asema Lowasa ni safi sana .Ni mzalendo na mtu ambaye anaipenda Tanzania na kaisukuma mbele sana Ilani ya CCM. JK anasema kwamba Lowasa kaondoka lakini kaacha alama kubwa .

Mungu wangu weeee!.. hivi huyu JK vipi lakini?.. Yaani Tanzania nzima wamepigwa na bumbuazi n hili sakata la Richmond n BoT, leo aja na utetezi ambao hauna hata kichwa?....tena baada ya kupokea report toka ktk kamati aliyoichagua yeye mwenyewe?..
Hivi JK anafahamu ni asilimia ngapi ya wananchi wake wamechoka na kubebana kwa CCM hasa ktk maswala ya Kitaifa?..
Haogopwi mtu wa la hapendwi mtu hapa!...
Mimi naona ipo haja ya impeachment!...
Wanasheria, kuna process gani haswa inayotakiwa kuunda somekind of a legislative body tumwondoe yeye ama serikali yake madarakani...
 
Ki-Protocol Rais anastahili kupewa vyombo kuliko Bunge. Hii kwa katiba ya sasa. may be tukibadilisha . Isije kuwa ile issue ya Adam Malima Vs Mengi ktk vyombo vyake vya Habari...nafikiri hii kesi yafahamika.

JK anaharibu kuanza kushambulia watu ambao walisimama kidete kuamsha umma wa watanzania na wabunge juu ya Richmond...angekaa kimya ingetosha pia kuwa kampeni ya CCM, kuanza kutangaza huku wengi tunaingiwa na mashaka juu ya maamuzi yake.

Kwanza Baraza lenyewe BOMU...may be kikao cha bungeni kiwe kidedea kuutokomeza ufisadi...

Yaleyale ya kuleta Taifa Stars bungeni wakati wapinzani wanasoma Bajeti mbadala, ili kuhamisha attention ya Wadanganyika. Huu ni usanii wa JK kunyima haki watanzania kusikia yanayojiri Bungeni kwa kisingizio cha protocal. Kwa ameshindwa kuongea na Wazee wa Dar siku au muda ambao haungiliani na matangazo ya mojamoja kutoka Bungeni? Shame on you TVT , JK and sisiem for thinking they have come up with a well craved technique and yet it is the poorest technique. Ni suala la muda tu mambo yote yatafunuliwa kwani Watanzania wa leo si wa mwaka juzi.
 
Kwa mshangao mkubwa na mtisiko TVT sasa wameacha kutupa habari za Dodoma ambazo zina mambo ya kugusa Taifa .Mjadala wa Richmond sina hakika kama Watanzania wanaweza kuusikia labda iwe recorded.Sasa JK anaongea na wazee wa Mkoa wa Dar Es Salaam .CCM again kwa mara nyingine inakuwa ya kwanza na issue za Taifa zinakuwa za mwisho .

I am confused lakini niko LIVE hapa Dar

JK hakuwa na sifa za uongozi (tuliingizwa mjini tu), hawezi kuongea na wazee wa Dar wakati kuna kikao cha bunge, na lazima afahamu tabia ya kuongea na wazee wa Dar ilikuwa ni kuongea na taifa in some way lakiniyeye anavurunda tu.


Zitto anasisitiza kuwa mikataba sio siri kwani wao kama wajumbe wa kamati ya madini wamepewa mikataba bila hata ya kiapo kwa nini wabunge wasipewe mikataba hiyo?

Anasisitiza kuwa kuna haja ya mikataba kudaiwa na wabunge na kama serikali ikikataa wabunge wa kila kamati waanzishe kamati kama ya mwakyembe ili kudai mikataba husika .

CCM kwa kweli wamekwama hivi sasa ule ujanja ujanja wao unaelekea ukingoni. Waswahili walisema za mwizi ni arobaini.

Mbunge wa CCM anasisitiza kuwa Daniel Yona na Rostam Azizi waletwe na waseme kwa nini wamekaidi amri ya bunge ya kwenda kuhojiwa na kamati ya bunge na kwanini wanalidharau bunge .

Anasisitiza pia kuwa lazima viongozi wote waliohusika kwenye richmond basi wawekwe rumande ili kuruhusu uchunguzi wa haki na wafunguliwe mashtaka mara moja.

Wabunge waendelee kukaza sharubu kama rais hataki basi alivunje bunge twende kwenye uchaguzi. Pongezi kwa wabunge wote wanaofanya kazi waliyotumwa na wananchi.

JK asema Lowasa ni safi sana .Ni mzalendo na mtu ambaye anaipenda Tanzania na kaisukuma mbele sana Ilani ya CCM. JK anasema kwamba Lowasa kaondoka lakini kaacha alama kubwa .

Hataki ashitakiwe kama rafiki yake DITO. time will come watakutana Keko.

Kwa mara nyingine tena JK anazima mjadala wa bunge kumhusu Lowassa. Mapema leo mbunge wa Sikonge alikuja juu na kudai chama kiwashughulikie. Sasa wabunge hawa wakijua baadaye kuwa JK amemtetea Lowassa kesho mjadala utaanza kubadilika na watetezi wake wataanza kujitokeza. Wabunge wa CCM ambao wataendelea kulilia 'kichwa cha Lowassa' kwenye sahani wataonekana wanaenda kinyume na Rais.

Huu mjadala hawawezi kuuzima kama wabunge wataendelea na kudai haki yao kikatiba.

Nimekuwa na wasiwasi mkubwa sana na mkuu wa kaya yetu, inaelekea anamuogopa sana sana EL na RA kwani anadiriki kujitetea kuwa haukuwa uamuzi wake ila ni uamuzi wa kamati ya wabunge wa CCM kuwaajibisha wote waliotajwa kuhusika na sakata la Richmond. Pili anasema kama mambo fulani yangefanyika tusingefika hapa, yaani kujiuzuru PM, mbaya zaidi anasema ni mchapa kazi ameisukuma mbele ilani ya CCM. Ina maana haoni hali za waTZ zinavyozidi kuwa duni? Hakuona jinsi mafisadi walivyolitia hasara taifa hili? Hajaongea na Salva akamwelezea jinsi alivyofanya kazi na Richmond? Alivyoongea Viongozi wa CCM wanamwangusha siku ile ya miaka 31 ya CCM kule Pemba alimaanisha nini? Mbona Muungwana simuelewi? Je ni kweli ana nia ya dhati kabisa ya kutufikisha tunakopataka. Nafikiri tunahitaji Mtu wa kuthubutu, mwanamapinduzi, Jasiri kama Nyerere, Sokoine na Mwakyembe. Nilizima redio kabisa. sikufurahia. Ufisadi unapakwa mafuta!!!!! Haiwezekani. Rais umekosea,Usiwaogope hawa wana mtandao, tupo nyuma yako waTZ wote. Tupo tayari kupambana na hao wana Mtandao, najua EL ananguvu na ushawishi mkubwa ndani ya chama, lakini kwa hili hatukubali na tunakuomba uchukue msimamo thabiti ussitetereke na kuanza kutoa speech nyepesi.

Akiendelea na tabia hii bora wabunge wapige kura kutokuwa na imani nae.

Mtu wa Pwani.
Umesahau huyu huwa anaruka kwa ungo?

Huo ungo utampeleka Bagamoyo tu.
 
Toka Dodoma muda huu , Selelii amaliza kusema Bungeni .Ameliambia Bunge kwamba wanatishiwa maisha na yeye kesha pokea sms kibao za matisho .Kasea wametoa majina ambayo hayajatajwa na yeye ama wao wakifa Spika ajue walio waua ni akina nani na hatu kali zichukuliwe .Kweli I felt him huy Mbunge .

Sasa anaongea Marmo .
 
Wajumbe wa kamati kwa kweli wanaonyesha kabisa kuwa wanatishwa na wana hofu juu ya maisha yao.

Makamu mwenyekiti wa kamati anasema kuwa amajitolea uhai wake kwa ajili ya watanzania wote na yupo kufa kwa kujali wananchi masikini.

Pia huyu mama anapingana na mwenyekiti wake wa chama JK kwani anasema hilo ni suala la kitaifa na sio suala la viongozi wa vyama kuwaambia wananchi kuwa hii ni hoja ya chama chao ama laa hapa sms sent to JK ajue kuwa mwisho wa maigizo na usanii umefikia ukomo .
 
Sasa Stella Manyanya anaongea .Naona naye anaongea kwa Mbwembwe sana .Wacha tuone anataka kusema nini .

Amethibitisha kwamba RDC is never existed.Amewalaumu sasa wataalamu wa mikataba anasema they are too weak.
 
Mwakyembe hewani sasa .Aanza kwa kuomba Lwakatare amuombee maana sauti yake imepata mkwaruzo .Anawapongeza walio jiuzuru kuanzia Lowasa na wote .Sasa anaanza kuzamia ripoti yenyewe
 
Back
Top Bottom