Technician
JF-Expert Member
- Mar 30, 2010
- 841
- 222
Nikiwatimua kwa kuniambia dhaifu mtalalamika?
Mwandishi:Charles Misango
alhamis, 21 juni 2012
JUMANNE wiki hii, Watanzania waliokuwa wakifuatilia mkutano wa Bunge, walishuhudia Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA) akitimuliwa bungeni kwa amri ya Naibu Spika, Job Ndugai.
Kilichomponza Mnyika ni kukataa kwake kufuta kauli yake ya "kudai" kuwa Rais Jakaya Kikwete ni dhaifu.
Sitaki kujikomba kwa msomaji yeyote, kwa kuweka wazi kuwa binafsi, nakubaliana na maamuzi ya naibu spika kwa sababu mbili; mosi, ni kwamba alichofanya ni kutekeleza kanuni za Bunge.
Mnyika alikataa kufuta kauli hiyo na kanuni zinasema kwa tendo hilo apaswa kupewa adhabu ya kutolewa bungeni.
Pili, Ndugai pamoja na kushambuliwa kwa madai ya kutumia vibaya kiti chake, bado hakutoa adhabu ninayoamini ni nzito kabisa ya kumzuia Mnyika asihudhurie vikao vitatu vya Bunge, badala yake akatumia kifungu cha pili kinachomzuia mbunge aliyekataa kufuta kauli yake ya ‘kuudhi' kutoka nje ya ukumbi wa Bunge kwa muda wote wa kikao cha siku hiyo hadi kesho yake.
Pamoja na adhabu hiyo, Ndugai pia ameniudhi! Tena namtafutia nafasi naye nimpe adhabu yake. Ndugai anajua kuwa, ni mwiko kabisa kwa mtu hata kama ana hadhi kiasi gani kutudhalilisha sisi viongozi tuliopewa dhamana kubwa na mamilioni ya Watanzania wanaotupenda na kukipenda chama chake cha dole juu, hadharani na mchana kweupe.
Unashangaa nini na wewe msomaji? Ujasiri wa kutudhalilisha wenye nchi yetu nani kawapa? Hakuna heshima? Hamjui kuwa anayevaa khanga ya mama ndiye baba hata kama humpendi kwa sura iliyopondeka kama kitako cha sufuria?
Kama huyo huwezi kumtolea maneno ya kumuudhi, ukijua kwa kufanya hivyo, utamchefua mama, sembuse sisi viongozi wa nchi tuliyopewa ridhaa ya uongozi kwa ushindi wa kishindo?
Hivi nani kawaambia sisi tu wadhaifu? Katika lipi? Maana kuna watu wamediriki kuinua midomo yao na kutushambulia kuwa eti tumeshindwa kuwaletea maendeleo. Wanadai tumeruhusu wawekezaji waje kupora rasilimali zetu. Maudhi hayo!
Ngoja niwaleze tu namna gani tulivyojitahidi kuinua jina la Tanzania katika sekta ya madini, ingawa mnatuudhi kwa kutuambia kuwa tumeshindwa kuwadhibiti wachimbaji wa madini, ambao mnadai ni waporaji. Tena mshindwe na mlegee! Nani kawapa weredi wa kujali mambo haya mazito, wakati kwa hulka zenu watanzania ni watu msiojali? Mnaoshabikia mambo ya Simba na Yanga, na kubobea tu katika kuchangishana michango ya viharusi badala ya harusi, "siendi kwa hofu', na ‘twisheni pati" (potelea mbali hata kama nakosea majina yake).
Ngoja niwapake wote mnaotusakama; ninyi wavivu wa kufanya kazi na mabingwa wa maneno ya kuuudhi! Nani kawaleta wawekezaji bora katika sekta ya madini? Ninyi ama sisi viongozi wenu?
"Mnasema eti sekta ya madini imeshindwa kunufaisha nchi hii. Nani kasema? Hivi hamjui kuwa kutokana na uhodari wetu, tumeuwezesha mgodi wa Geita gold mine kuwa mkubwa kuliko yote hapa nchini, na wa tatu Afrika."
Hivi nani hajui kuwa tangu mwaka 1998, nchi yetu imekuwa mzalishaji mkubwa wa soko la dhahabu dunia na namba tatu kwa Afrika tukitanguliwa na Afrika Kusini na Ghana? Hamuoni kama tumelitangaza jina la Tanzania duniani na kujulikana? Hamjui kujulikana ni sifa? Halafu mnasema uongozi wetu ni dhaifu; Mnaudhi! Chama chetu oyeee!
Mnalalamika kuwa kampuni hizi zinamiliki ardhi kubwa ya machimbo ya madini, na zimekuwa zikitumia leseni za utafiti vibaya kwa kuchimba madini kwa miaka kadhaa na kisha kubadilisha majina, ama kuziuza kampuni hizi kwa makampuni mengine, hatua ambayo mnadai eti inatumika kukwepa kodi. Hayo nayo ni maneno ya kuudhi!
Kama mtu kashindwa biashara kwa nini asimuuzie mwingine? Na alipe kodi gani wakati kwa miaka mitano alikuwa anafanya utafiti?
Eti nimesikia watu wakitoa mfano wa jinsi Kampuni ya Ashanti Goldfields Company Ltd ilipoinunua Kampuni Samax Gold Inc mwaka 1998 hivyo na kupata faida katika mradi wa Golden Pride.
Eti Kampuni ya Barrick ndiyo inayoongoza kwa kupewa leseni nyingi za utafiti wa madini pamoja na uchimbaji hapa Tanzania.
Sasa ulitaka apewe mjomba wenu ambaye ni miongoni mwa waliofilisi mashirika ya umma miaka ileee? Si bora tumpe mzungu kuliko Mswahili wa kibaingwa? Acheni kudhihaki wenzenu. Mnacheza na wazungu ninyi!
Unadhani sisi viongozi ni wajinga kwa kuipa Barick leseni nyingi za utafiti na uchimbaji? Tunajua uwezo wake. Ona inaendesha moja kwa moja migodi ya madini ya Bulyanhulu ulioko Kakola wilayani Kahama, Mgodi wa North Mara wenye leseni mbili za SML 18/96 kwa eneo la Nyabirama na SML 17/96 eneo la Nyabigena wilayani Tarime mkoani Mara na ule wa Tulawaka SML 157/03 ulioko wilayani Bihalamuro mkoani Kagera.
Kwa hatua hizi pia mtatuita sisi dhaifu kisa tu, mnaona kwa akili zenu hawajatoa kodi kadri mnavyotaka? Tukiwapeni ninyi mtaweza kama hamtaishia kutambiana kwa mikogo ya wingi wa magari ya kifahari na kushindana kubadilisha ‘totozi' kila siku?
Mwandishi:Charles Misango
Mytake:
Mbona kama simwelewi huyu mwandishi vizuri,wewe umemuelewaje?
Mwandishi:Charles Misango
alhamis, 21 juni 2012
JUMANNE wiki hii, Watanzania waliokuwa wakifuatilia mkutano wa Bunge, walishuhudia Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA) akitimuliwa bungeni kwa amri ya Naibu Spika, Job Ndugai.
Kilichomponza Mnyika ni kukataa kwake kufuta kauli yake ya "kudai" kuwa Rais Jakaya Kikwete ni dhaifu.
Sitaki kujikomba kwa msomaji yeyote, kwa kuweka wazi kuwa binafsi, nakubaliana na maamuzi ya naibu spika kwa sababu mbili; mosi, ni kwamba alichofanya ni kutekeleza kanuni za Bunge.
Mnyika alikataa kufuta kauli hiyo na kanuni zinasema kwa tendo hilo apaswa kupewa adhabu ya kutolewa bungeni.
Pili, Ndugai pamoja na kushambuliwa kwa madai ya kutumia vibaya kiti chake, bado hakutoa adhabu ninayoamini ni nzito kabisa ya kumzuia Mnyika asihudhurie vikao vitatu vya Bunge, badala yake akatumia kifungu cha pili kinachomzuia mbunge aliyekataa kufuta kauli yake ya ‘kuudhi' kutoka nje ya ukumbi wa Bunge kwa muda wote wa kikao cha siku hiyo hadi kesho yake.
Pamoja na adhabu hiyo, Ndugai pia ameniudhi! Tena namtafutia nafasi naye nimpe adhabu yake. Ndugai anajua kuwa, ni mwiko kabisa kwa mtu hata kama ana hadhi kiasi gani kutudhalilisha sisi viongozi tuliopewa dhamana kubwa na mamilioni ya Watanzania wanaotupenda na kukipenda chama chake cha dole juu, hadharani na mchana kweupe.
Unashangaa nini na wewe msomaji? Ujasiri wa kutudhalilisha wenye nchi yetu nani kawapa? Hakuna heshima? Hamjui kuwa anayevaa khanga ya mama ndiye baba hata kama humpendi kwa sura iliyopondeka kama kitako cha sufuria?
Kama huyo huwezi kumtolea maneno ya kumuudhi, ukijua kwa kufanya hivyo, utamchefua mama, sembuse sisi viongozi wa nchi tuliyopewa ridhaa ya uongozi kwa ushindi wa kishindo?
Hivi nani kawaambia sisi tu wadhaifu? Katika lipi? Maana kuna watu wamediriki kuinua midomo yao na kutushambulia kuwa eti tumeshindwa kuwaletea maendeleo. Wanadai tumeruhusu wawekezaji waje kupora rasilimali zetu. Maudhi hayo!
Ngoja niwaleze tu namna gani tulivyojitahidi kuinua jina la Tanzania katika sekta ya madini, ingawa mnatuudhi kwa kutuambia kuwa tumeshindwa kuwadhibiti wachimbaji wa madini, ambao mnadai ni waporaji. Tena mshindwe na mlegee! Nani kawapa weredi wa kujali mambo haya mazito, wakati kwa hulka zenu watanzania ni watu msiojali? Mnaoshabikia mambo ya Simba na Yanga, na kubobea tu katika kuchangishana michango ya viharusi badala ya harusi, "siendi kwa hofu', na ‘twisheni pati" (potelea mbali hata kama nakosea majina yake).
Ngoja niwapake wote mnaotusakama; ninyi wavivu wa kufanya kazi na mabingwa wa maneno ya kuuudhi! Nani kawaleta wawekezaji bora katika sekta ya madini? Ninyi ama sisi viongozi wenu?
"Mnasema eti sekta ya madini imeshindwa kunufaisha nchi hii. Nani kasema? Hivi hamjui kuwa kutokana na uhodari wetu, tumeuwezesha mgodi wa Geita gold mine kuwa mkubwa kuliko yote hapa nchini, na wa tatu Afrika."
Hivi nani hajui kuwa tangu mwaka 1998, nchi yetu imekuwa mzalishaji mkubwa wa soko la dhahabu dunia na namba tatu kwa Afrika tukitanguliwa na Afrika Kusini na Ghana? Hamuoni kama tumelitangaza jina la Tanzania duniani na kujulikana? Hamjui kujulikana ni sifa? Halafu mnasema uongozi wetu ni dhaifu; Mnaudhi! Chama chetu oyeee!
Mnalalamika kuwa kampuni hizi zinamiliki ardhi kubwa ya machimbo ya madini, na zimekuwa zikitumia leseni za utafiti vibaya kwa kuchimba madini kwa miaka kadhaa na kisha kubadilisha majina, ama kuziuza kampuni hizi kwa makampuni mengine, hatua ambayo mnadai eti inatumika kukwepa kodi. Hayo nayo ni maneno ya kuudhi!
Kama mtu kashindwa biashara kwa nini asimuuzie mwingine? Na alipe kodi gani wakati kwa miaka mitano alikuwa anafanya utafiti?
Eti nimesikia watu wakitoa mfano wa jinsi Kampuni ya Ashanti Goldfields Company Ltd ilipoinunua Kampuni Samax Gold Inc mwaka 1998 hivyo na kupata faida katika mradi wa Golden Pride.
Eti Kampuni ya Barrick ndiyo inayoongoza kwa kupewa leseni nyingi za utafiti wa madini pamoja na uchimbaji hapa Tanzania.
Sasa ulitaka apewe mjomba wenu ambaye ni miongoni mwa waliofilisi mashirika ya umma miaka ileee? Si bora tumpe mzungu kuliko Mswahili wa kibaingwa? Acheni kudhihaki wenzenu. Mnacheza na wazungu ninyi!
Unadhani sisi viongozi ni wajinga kwa kuipa Barick leseni nyingi za utafiti na uchimbaji? Tunajua uwezo wake. Ona inaendesha moja kwa moja migodi ya madini ya Bulyanhulu ulioko Kakola wilayani Kahama, Mgodi wa North Mara wenye leseni mbili za SML 18/96 kwa eneo la Nyabirama na SML 17/96 eneo la Nyabigena wilayani Tarime mkoani Mara na ule wa Tulawaka SML 157/03 ulioko wilayani Bihalamuro mkoani Kagera.
Kwa hatua hizi pia mtatuita sisi dhaifu kisa tu, mnaona kwa akili zenu hawajatoa kodi kadri mnavyotaka? Tukiwapeni ninyi mtaweza kama hamtaishia kutambiana kwa mikogo ya wingi wa magari ya kifahari na kushindana kubadilisha ‘totozi' kila siku?
Mwandishi:Charles Misango
Mytake:
Mbona kama simwelewi huyu mwandishi vizuri,wewe umemuelewaje?