Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,395
Kuna wanawake wengi sana ambao wanagombea kupendwa, au wanajipendekeza ili wapendwe. Hawa ni wanawake ambao wana kasoro kubwa kwenye mifumo yao ya kufikiri au ufahamu.
Unaweza kukuta mwanamke anadhalilishwa, anaoneshwa kwamba hatakiwi, amechokwa, ameshachezewa lakini amemngangania mwanaume huyo kama luba.
Unaweza kukuta anakwenda Baa na mwanaume, na mwanaume huyo anaanza kuwashika wanawake makalio mbele yake, anamtajia hawara zake, anamwonyesha wazi kwamba, hamthamini, bali anamtumia tu kama chombo cha starehe. Lakini manamke huyo amemngangania mwanaume huyo. Mwenyewe anaita kupenda.
Kwa kawida mwisho wa safari ya mapenzi kama haya ya kichaa ni mwanamke kuachwa, tena kuachwa kwa visa na mikasa mingi. Kumbuka unapojipendekeza badala ya kupenda, unamkera unayejipendekeza kwake. Lakini mbaya zaidi ni kwamba, kile tunachoita kupenda sana ni kuhemkwa na wala sio kupenda. Tunapopenda hatupotezi ufahamu wetu, bali tunakuwa na ufahamu zaidi.
Tunapohemkwa huwa hatutumii akili bali tunatumia hisia. Kwa hiyo tunakuwa watumwa wa hisia zetu. Katika hali kama hiyo, mwanamke anachanganya kupenda na kuhemkwa. Anafikia mahali anagundua kwamba, ameumia sana na hakupata alichokuwa anataka kutoka kwa mwanaume, ambaye alisema anampenda sana.
Lakini pia ili kumdhihirishia kwamba anampenda, atajaribu kujiua akikataliwa, atatafuta kila visa ili mwanaume ahisi kushtakiwa na dhamira, aone kuwa yeye ndiye mwenye makosa. Anataka kupendwa, anaomba kupendwa, anashurutisha kupendwa. Kwa nini?
Kama nilivyosema, hayo ni matatizo kwenye kwenye mfumo wa kufikiri. Mwanamke wa aina hiyo ni mgonjwa na ndio maana ana utegemezi.
Unaweza kukuta mwanamke anadhalilishwa, anaoneshwa kwamba hatakiwi, amechokwa, ameshachezewa lakini amemngangania mwanaume huyo kama luba.
Unaweza kukuta anakwenda Baa na mwanaume, na mwanaume huyo anaanza kuwashika wanawake makalio mbele yake, anamtajia hawara zake, anamwonyesha wazi kwamba, hamthamini, bali anamtumia tu kama chombo cha starehe. Lakini manamke huyo amemngangania mwanaume huyo. Mwenyewe anaita kupenda.
Kwa kawida mwisho wa safari ya mapenzi kama haya ya kichaa ni mwanamke kuachwa, tena kuachwa kwa visa na mikasa mingi. Kumbuka unapojipendekeza badala ya kupenda, unamkera unayejipendekeza kwake. Lakini mbaya zaidi ni kwamba, kile tunachoita kupenda sana ni kuhemkwa na wala sio kupenda. Tunapopenda hatupotezi ufahamu wetu, bali tunakuwa na ufahamu zaidi.
Tunapohemkwa huwa hatutumii akili bali tunatumia hisia. Kwa hiyo tunakuwa watumwa wa hisia zetu. Katika hali kama hiyo, mwanamke anachanganya kupenda na kuhemkwa. Anafikia mahali anagundua kwamba, ameumia sana na hakupata alichokuwa anataka kutoka kwa mwanaume, ambaye alisema anampenda sana.
Lakini pia ili kumdhihirishia kwamba anampenda, atajaribu kujiua akikataliwa, atatafuta kila visa ili mwanaume ahisi kushtakiwa na dhamira, aone kuwa yeye ndiye mwenye makosa. Anataka kupendwa, anaomba kupendwa, anashurutisha kupendwa. Kwa nini?
Kama nilivyosema, hayo ni matatizo kwenye kwenye mfumo wa kufikiri. Mwanamke wa aina hiyo ni mgonjwa na ndio maana ana utegemezi.