Nikijiuzulu hamtapata waziri kama mimi - Nchimbi

...Kama haya majibu yametoka kwa WAZIRI wa BARAZA LA MAWAZIRI LA TANZANIA kweli, Nasikitika sana.Kweli Wamelewa Madaraka.
 
majibu haya hata mtoto wangu wa darasa la kwanza hawezi kuyatoa kwani ni ya kiwango cha chini mno. bubu na mwanza ni kenya? mbona kulikuwa na mikutano?
 
Ni kweli akijiuzulu sidhani kama tutapata kiongozi asiyefaa/dhaifu kama huyu Nchimbi. Nchimbi jiuzulu tutapata faida wewe ni wa Janga La Kitaifa
 
Kura huwa zinaibwajwe? hili swali nimeisha liuliza mara kwa mara humu jamvini , ila hakuna mwenye majibu , may be ww ukawa mwarobaini wa swali hil

Mkuu, swali lako kamuulize kada wa ccm aliyejaribu kuiba kura mbele ya Kamanda Lema, uchaguzi wa Mbunge Arumeru atakupa jibu la mbinu za kuiba. Tahadhari usije ukaiba kura mbele ya Kamanda Lema utajuta kuwa gamba.
 
View attachment 63926 Bububu_2.jpg View attachment 63928View attachment 63929

Hapa ni Bububu, CCM wakifanya uzinduzi wa uchaguzi mdogo shughuli iliyoongozwa na makamu wa Rais Dk Bilal. Hii ilikuwa ni Tarehe 2 September, siku ambayo CDM walipotaka kufungua tawi na kufanya mkutano wao wa ndani pale Nyororo (Mfindi) na baadaye Polisi kuleta vurugu na kusababisha mauaji ya kinyama ya mwandishi wa habari Daudi Mwangosi.
 
Mbona majibu hafifu sana,
Kumbe huyu jamaa ni mbumbumbu sana,

Halafu anataka kugombea urais, na tusishangae mazezeta wa CCM wakaanza kumpigia debe awe mgombea urais wao.

Poor Poor CCM!!
 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Dkt. Emmanuel Nchimbi, alipoulizwa:

Kama yuko tayari kumsimamisha kazi Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa, Michael Kamuhanda ili kupisha uchunguzi huo alisema ndani ya tume hiyo kuna Naibu Kamishna wa Polisi; hivyo kamanda huyo ambaye cheo chake ni Kamishna Msaidizi hana ubavu wa kuharibu uchunguzi huo.

Kuhusu askari aliyempiga bomu Mwangosi kama anashikiliwa na Polisi au bado yuko nje, alisema atachukua hatua mara baada ya tume hiyo au ile ya Polisi, iliyoundwa na Mkuu wa Polisi, IGP Said Mwema kukamilisha uchunguzi wake.

Kuhusu kama atajiuzulu iwapo ripoti itabaini kuwa polisi ndio waliofanya mauaji hayo, alisema “Nikijiuzulu mtampata wapi Waziri kama mimi? (kicheko) Shauri yenu… lakini nawahakikishieni kuwa ukweli utaanikwa wazi.”

Kwamba Polisi wanatumiwa kukikandamiza Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na kwa manufaa ya CCM, alisema hataruhusu hali ya namna hiyo na akasisitiza kuwa Polisi wamekuwa wanatekeleza agizo la Msajili wa Vyama vya Siasa la kupiga marufuku mikutano ya kisiasa katika kipindi hiki cha Sensa ya Watu na Makazi. Alipotolewa mifano ya namna ambavyo wanachama wa CCM wamekuwa wakifanya mikutano yake bila kuingiliwa na Polisi, Dkt. Nchimbi alisema alipata taarifa hizo na akamjulisha Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama ambaye alimhakikishia kuwa hakuna mkutano wa hadhara unaofanywa na chama chake badala yake wanafanya vikao vya ndani, “Mikutano ya ndani haikupigwa marufuku, kilichokatazwa ni mikutano ya hadhara na ninaomba wenzetu wawe wastahimilivu kwani zimebaki siku nne tu za sensa.”

Source: http://www.wavuti.com

My Take: Hatuna Viongozi.


Maswali yote kwa Nchimbi ni kumwonea: CCM imefanya mikutano Z'Bar wakati sensa inaendelea, na hakuna jeshi wala sisimizi toka jeshi la polisi aliyejigusa kuuliza kama sensa imekiukwa...Nchimbi hajitambui na hatambui kuwa yeye ni waziri!
Tusijisahau kuwa huyu jamaa hivi majuzi tu alikuwa M/Kiti wa Vijana wa CCM, kwa hivyo tukikumbuka kuwa yeye ni kada na mmoja wa wale wanaotuma CDM izibitiwe, mtaona kuwa hata nafasi aliyopewa (Waziri-Mambo ya Ndani) ni strategic position kuzibiti siasa kwa manufaa ya CCM tunapokwenda Uchaguzi 2015.

Eti, akijiuzulu 'tutapata wapi mwingine kama yeye'....? Hii ni Kashfa kwa JAMII nzima, na matusi! Yaani, Nchimbi hamuoni yeyote kama yeye au wa kumzidi popote Tanzania nzima? (sijui anamaanisha ki-elimu au kwa mustache wake)...useless figure!! The Shigela types! Dear Great Thinkers, please vomit something equivocally on this 'useless structure'....!
 
msimlaumu huyu mtu kwa kusema hivyo. Pengine ana-uhakika kwa wabunge wa sasa Wa CCM ambao ndio wenye nafasi ya kuwa mawaziri, hakuna msafi/mzuri kama yeye. yaani yeye ni afadhali sana ya hao wengine.
 
Kuna waziri mmoja wa awamu ya tatu alitamka wazi kuwa ndege ya rahis ni lazima inunuliwe hata kama italazimu watanzania wale nyasi, sasa hivi yuko bench hata huko kwao ubunge hakupata.

Alipoenda kugombea ubunge aliwaambia wapiga kura wake kuwa hakuna mzazi aliyesomesha mtoto wake kama yeye ktk jimbo lake isipokuwa baba yake tu wanachi wakamwambia na kumwonyesha kuwa hata wao wamesomesha wakamweka kijan amwingine na sasa ni Mbunge kupitia CDM.

Emanuel, hicho kiburi kitakugharimu kwa sababu TZ ya leo sio ya jana na nakuambia japo mimi sio nabii, hautarudi tena kuwa waziri, hata ubunge siuoni kwako tena. I am very sorry to speak like that!! You will see!!
 
Alipokuwa anatangaza tume ya kuchunguza mauaji ya Marehemu D. Mwangosi, Nchimbi aliulizwa endapo yuko tayari kujiuzulu kama itabainika kwamba polisi ndio wanahusika na mauaji haya, akasema tena kwa kejeli 'nani ajiuzulu, nikijiuzulu mtapata wapi waziri kama mimi'.

My Take:
hizi ni dharau na kejeli kubwa sana kwa watanzania, sijui anaweza kutuambia lolote la maana alilofanya toka amewekwa kusimamia wizara hii, ninachokiona kwake ni kuratibu mauaji yanayoendeshwa na Polisi akishirikiana na Mwema. Nchimbi please swallow your pride and step down.


Mazingaombwe yanaendelea...
Hakuna kipya ktk nchi hii.
 
Huyu kenge kama wizara ya habari, utamaduni na michezo ilimshinda sasa ataiweza hii wizara nyeti?



Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Hii inaonyesha hali ya uozo iliyoko serikalini,kiukweli hii kauli aliyoitoa inadhihirisha wazi kuwa bila yeye muuaji waziri mwingine hakuna.
 
What i see in Tanzania is the begining of the end, no one can avoid it,its a process
"Mamlaka hutoka kwa M/Mungu ILA sio Mamlaka DHALIMU"
 
Mimi nimemwelewa Dr! :A S check_03: Nchimbi, amesema hatutapata Waziri Mwingine kama yeye kutokana na ukweli kuwa Rais dhaifu ameshabadilisha mawaziri mara nyingi sana na sasa CCM haina tena akiba ya Magamba yatakayoshika nafasi hiyo! Mbona rahisi sana kuelewa wana JF!
 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Dkt. Emmanuel Nchimbi, alipoulizwa:

Kama yuko tayari kumsimamisha kazi Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa, Michael Kamuhanda ili kupisha uchunguzi huo alisema ndani ya tume hiyo kuna Naibu Kamishna wa Polisi; hivyo kamanda huyo ambaye cheo chake ni Kamishna Msaidizi hana ubavu wa kuharibu uchunguzi huo.

Kuhusu askari aliyempiga bomu Mwangosi kama anashikiliwa na Polisi au bado yuko nje, alisema atachukua hatua mara baada ya tume hiyo au ile ya Polisi, iliyoundwa na Mkuu wa Polisi, IGP Said Mwema kukamilisha uchunguzi wake.

Kuhusu kama atajiuzulu iwapo ripoti itabaini kuwa polisi ndio waliofanya mauaji hayo, alisema "Nikijiuzulu mtampata wapi Waziri kama mimi? (kicheko) Shauri yenu… lakini nawahakikishieni kuwa ukweli utaanikwa wazi."

Kwamba Polisi wanatumiwa kukikandamiza Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na kwa manufaa ya CCM, alisema hataruhusu hali ya namna hiyo na akasisitiza kuwa Polisi wamekuwa wanatekeleza agizo la Msajili wa Vyama vya Siasa la kupiga marufuku mikutano ya kisiasa katika kipindi hiki cha Sensa ya Watu na Makazi. Alipotolewa mifano ya namna ambavyo wanachama wa CCM wamekuwa wakifanya mikutano yake bila kuingiliwa na Polisi, Dkt. Nchimbi alisema alipata taarifa hizo na akamjulisha Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama ambaye alimhakikishia kuwa hakuna mkutano wa hadhara unaofanywa na chama chake badala yake wanafanya vikao vya ndani, "Mikutano ya ndani haikupigwa marufuku, kilichokatazwa ni mikutano ya hadhara na ninaomba wenzetu wawe wastahimilivu kwani zimebaki siku nne tu za sensa."

---
Majibu yamenukuliwa kutoka kwenye gazeti la HabariLeo





Source: wavuti - wavuti
 
Back
Top Bottom