Nikapigwa ndoa ya mkeka Ununio…!

mmhhhhhh.......we mzee wewe kumbe ndo maana kuna siku TaiJike alikuja na uzi wa kukushinikiza umtajie baba na mama yake si ajabu ndo mbegu ulioicha huko Ununio mweeeehh.
 
Last edited by a moderator:
Outra história engraçada de Gustavo ( Mtambuzi )! Você é um superstar!
 
Last edited by a moderator:
alaaaah, kumbe ndio weweeee...
Kuna dada yetu tuliwahi simuliwa kuwa aliwahi fungishwa ndoa na mpiga mziki kipindi cha ngoma ya mtoto wa mwanakwetu alafu akakimbiwa mara baada ya ndoa na kuachiwa mimba ya mapacha watatu...
Tutafutane ndugu yangu japo tukapate moja moto, moja baridi!!!
Si vbaya ukaja na mkeo wa sasa na kama una binti pia ili tuweze fahamiana vizuri zaidi
 
Duh very ineresting like movie..... sasa mipango ya shule ndiyo ikawa imekufa nini...ulikuwa kidume kweli ila watu wa pwani nao noma Tanga mambo hayo khadi leo yamo.
 
wewe lazima utakua mwandishi wa habari au unaandikaga vitabu maana topic zako ndefu mno alafu kama huja copy n paste mahali inaonyesha ni jinsi gani una muda mwingi wa kukaa chini na kuandika gazeti lote hilo...lakini unajitahidi siwezagi kusoma posts zako coz ni ndefu sana bt am sure zina ujumbe mzuri

Jijengee tabia ya kupenda kusoma.
Wa TZ tunasemwa sana kuwa tu wavivu wa kusoma.
Hebu tuikomeshe hii tabia.lol!
 
Kwa kweli ni kiboko, thanks Mtambuzi keep it up,
Hii imenichekesha kweli!
But kuna ukweli mwingi sana katika hili kwa tabia za vijana wanaojipatia umaarufu kwa kuwa wajanja wajanja tu na wengi wao wamekatika na ukimwi kwa kujiona vistar uchwara na kulamaba vibinti bila mipaka...

Hii ya ndoa ya mkeka naona ilikuwa fundisho kwelikweli na ingekuwa mara nyingi linafanyika hivi nadhani lingepunguza kidogo udokoaji wa vibinti.
 
Hii imenikumbusha enzi namaliza o-level pale Ihungo Bukoba. Siku ya sherehe tukiliita bogy alikuja kupiga Bonge na vyomba vyake vya pamba musics sound.
Baada ya mziki kuna kademu nilikua nacheza nako kutoka rugie(rugambwa sec) ikabidi nikatoroshe.
tukala chochoro hadi kyaruyonga, tukashuka omumwani tukaibukia rwamishenye. deal ilikua ni kwenda guest ambayo ipo karibu na shule yao ili saa tisa usiku aingie room. tukapata chumba pale maeneo ya tanesco kibeta. tulilala kushituka saa nne asubuhi..P.T.O. mia
figganigga kumbe na wewe ulikuwa mkali aisee..........
 
Last edited by a moderator:
yaani nimecheka mpaka nimeishiwa point ya kuchangia.... Sipati picha ulivyotimua vumbi hadi barabara kubwa maana kuna mwendo pale, si bora sasa hivi kumerahisishwa kidogo kuna boda boda.
 
Asee nimecheka mpk machozi yamenitoka....ile sehemu jamaa alitimua mbio kawaachia vumbi tu
 
Mbimbinho mh, bora niuchune maana sijatafutwa na nadhani wameshanisahau.............
Isije ikawa kuna ndugu yake humu JF..................LOL
lolest kumbe ni weye ulikujaa ukaozwa na shehe jumaa pale kwa mzee Tilikele? uliozeshwa shemejiye omary Tilikele? aitwaye Mwana asha eeh! sasa siku hizi mwanaasha kesha olewa alikauwa anaishi Tandale jirani na mzee Chuche yule mmwera. Alisomeaga kozi ya recods keeping na kwasasa anafanya kazi wizara ya mali asili kama mtu wa records. Labda nikupe namba yake ya simu umpigie lakin anaish Kinyerezi. pOle sana Mtambuzi
 
Last edited by a moderator:
Mtambuzi naomba kujua kama hili tukio ni la kweli hahahah maana nimebakia mdomo wazi
Baba miaka ile ulikuwa hukamatiki ..naona vijana wa sasa wanafanya marudio tu..
Mwanangu FirstLady1, waswahili wanasema ya kale hayanuki, na yaliyopita si ndwele tugange yajayo...........
 
Last edited by a moderator:
Kwa kuwaachia watoto wa watu maumivu Mtambuzi ulikuwa mwenyewe.........tatizo ni kuwa mwosha naye za mwizi huwa ni arobaini mwishowe huwa anaoshwa huku machozi yakimtoka kwa kutoamini mpira umemgeukia mwenyewe.....................
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom