Kila ninapojaribu kufuatilia mwenendo wa kampeni wa mgombea wa chama kilichokuwa kikitutawala nimekuwa nikitamani kusikia jambo moja kubwa. Kimsingi hali halisi ya maisha hapa Tanzania sio nzuri kwa waliowengi na hili sihitaji ubishi. Ila natakakujua ama kusikia kutoka kwa mgombea huyu aombaye urudi tena madarakani, Je, ni wapi ambapo serikali yake ina kiri mapungufu ya kifikra, kiutendaji na hata ki imani ambapo imepelekea watu kuzidi kuwa masikini? Natamani kujuwa udhaifu wenu na sio kujisifia kwa mafanikio pekee.