Naombeni ushauri maana kwakweli nashindwa kujishauri kama nisuke au ninyoe.
Miezi michache iliyopita(haifiki mitano) nilikutana na kaka mmoja sehemu yake ya kazi nikiwa napata huduma pale. Kutokana na kazi yake aligundua kwamba kuna kitu ningehitahi soon toka kwenye ofisi anazofanyia yeye, hivyo akaniambia nichukue namba yake ya simu ili siku nikiwa nahitaji hicho kitu nimtafute ili kurahisisha mambo kwa upande wangu. Sikuona ubaya maana najua nchi yetu hii inaendeshwa na connection kwahiyo nikaichukua. Siku kama tatu nne baadae nikamtafuta kumuuliza angewezaje kunisaidia kwa muda mfupi na nini atahitaji kutoka kwangu , mawasiliano yakaanzia hapo. Ni mcheshi kama mimi kwahiyo kulikua na utani mwingi, ila bada ya kunisaidia(alinifanikishia kazi yangu kwa muda mfupi sana tena bila kuchukua senti yangu) tukajikuta tunakuwa marafiki. Kujuliana hali, kutoka, kucheka na kufurahi mpaka kutembeleana.
Katika urafiki wetu aliwahi kuniambia kwamba alikua na mchumba hapo nyuma ila waliachana kutokana na familia yake kutokumpenda au kutokumkubali huyo binti. Hakunieleza zaidi kuhusu hilo kwa siku hiyo na mimi nikaliacha, ila aliishia kusema kuwa hakuwa na mtu kwa kipindi hicho nalo nikaliacha hivyo hivyo kwakua sikua nimemfikiria zaidi ya rafiki na mtu wakuflirt nae, haswa baadae ya kuanza kunirushia NAKUPENDA tunapoongea huku nikijua fika ni usanii tu.
Sasa mwezi uliopita kwenye «mikutano» yetu hii tukafanya mapenzi, bila majadiliano ya aina yoyote ile, yani ilitokea tu. Nilikua sina mtu na nilijua nae hana hivyo sikua na presha wala sikuwa na mawazo ya kuwa ndo tumeshaanza mahusiano japo yeye anauita ule.uhusiano. Siku ya pili nilikua nna safari ya mkoani kwahiyo nikasafiri na nikawepo mbali kwa zaidi ya wiki moja. Mawasiliano yakaendelea kama kawaida mpaka nikarudi. Niliporudi nikaanza kuhisi tofauti, nikaishia kuhisi nna mimba na nikamtafuta nikamwambia uso kwa uso. Alianza kwa kuuliza ikiwa haikua ya mtu mwingine sikuona tabu nikamjibu hapana. Mwisho akaishia kusema ya kua hakukua na ubaya.
Binafsi nilimhakikishia kwamba sijamwambia ili nimfunge kwa lolote(mahusiano au fedha) ila akadai kua anataka kuwa involved. Akafikia hata kuanza na habari za utakuja kukaa hapa, hili na lile, pia akagusia kabisa kwamba nikitoa atanichukia vibaya sana. Maisha yakaendelea.
Siku nilipopata uhakika nikamjulisha nadhani ilikua kwa msg. Siku mbili baadae akajitubia kua yeye ana mpenzi. Nikashangaa, kumuuliza kulikoni hakutoa taarifa mwanzo akasema eti sikumuuliza. Ikabidi nimpe live kwamba bila ya kuulizwa mapema kabisa alisema hana na huo utetezi wake ni wa kijinga maana hata mpenziwe akimuuliza hawezi kujitetea hivyo,utetezi wake ukaishia hapo.
Basi mi nikamjulisha kwamba hana haja ya kuwa na shaka, aendelee na maisha yake na mimi ntaanza yangu mapya bila ya kumhusisha yeye tena kwa lazima. Akaja na hoja ya kumwacha aliyenae ili awe na mimi. Akaniuliza kama ntaconsider kuwa nae(kuishi nae actually) kama ataachana na aliye nae. Nikamjibu kwamba hilo linahitaji muda mimi kufikiria, akasema sawa.
Mawasiliano yakaendelea kama kawaida, baadae nikaamua kumuuliza kuhusu mpenzi wake huyo aliyeko mbali. Niliyopata ni kwamba ANAMPENDA, HAWAJAWEKEANA MALENGO ila bado wazo la kumwacha kwaajili yangu bado lipo.
Sasa najiuliza, ni akili kweli kumwacha aachane na mtu anaempenda ili awe na mimi? Sindio mwanzo wa kunyanyaswa na kuchitiwa kila siku? Au hata kusimangwa kwamba sikupendwa mimi, alipendwa mwenzangu?Binafsi hisia zangu ni mchanganyiko, natamani kuwa nae (probability ni kwamba kama angeniambia tuwe kwenye mahusiano kabla ya hili sakata ningesema NDIO) ila nna wasiwasi sana. Sina imani nae, na kama sitokuwa na mahusiano nae nataka kila mtu ajali maisha yake ili kuavoid drama, kwenye hili naona sitokua namtendea haki. NIFANYEJE?
Miezi michache iliyopita(haifiki mitano) nilikutana na kaka mmoja sehemu yake ya kazi nikiwa napata huduma pale. Kutokana na kazi yake aligundua kwamba kuna kitu ningehitahi soon toka kwenye ofisi anazofanyia yeye, hivyo akaniambia nichukue namba yake ya simu ili siku nikiwa nahitaji hicho kitu nimtafute ili kurahisisha mambo kwa upande wangu. Sikuona ubaya maana najua nchi yetu hii inaendeshwa na connection kwahiyo nikaichukua. Siku kama tatu nne baadae nikamtafuta kumuuliza angewezaje kunisaidia kwa muda mfupi na nini atahitaji kutoka kwangu , mawasiliano yakaanzia hapo. Ni mcheshi kama mimi kwahiyo kulikua na utani mwingi, ila bada ya kunisaidia(alinifanikishia kazi yangu kwa muda mfupi sana tena bila kuchukua senti yangu) tukajikuta tunakuwa marafiki. Kujuliana hali, kutoka, kucheka na kufurahi mpaka kutembeleana.
Katika urafiki wetu aliwahi kuniambia kwamba alikua na mchumba hapo nyuma ila waliachana kutokana na familia yake kutokumpenda au kutokumkubali huyo binti. Hakunieleza zaidi kuhusu hilo kwa siku hiyo na mimi nikaliacha, ila aliishia kusema kuwa hakuwa na mtu kwa kipindi hicho nalo nikaliacha hivyo hivyo kwakua sikua nimemfikiria zaidi ya rafiki na mtu wakuflirt nae, haswa baadae ya kuanza kunirushia NAKUPENDA tunapoongea huku nikijua fika ni usanii tu.
Sasa mwezi uliopita kwenye «mikutano» yetu hii tukafanya mapenzi, bila majadiliano ya aina yoyote ile, yani ilitokea tu. Nilikua sina mtu na nilijua nae hana hivyo sikua na presha wala sikuwa na mawazo ya kuwa ndo tumeshaanza mahusiano japo yeye anauita ule.uhusiano. Siku ya pili nilikua nna safari ya mkoani kwahiyo nikasafiri na nikawepo mbali kwa zaidi ya wiki moja. Mawasiliano yakaendelea kama kawaida mpaka nikarudi. Niliporudi nikaanza kuhisi tofauti, nikaishia kuhisi nna mimba na nikamtafuta nikamwambia uso kwa uso. Alianza kwa kuuliza ikiwa haikua ya mtu mwingine sikuona tabu nikamjibu hapana. Mwisho akaishia kusema ya kua hakukua na ubaya.
Binafsi nilimhakikishia kwamba sijamwambia ili nimfunge kwa lolote(mahusiano au fedha) ila akadai kua anataka kuwa involved. Akafikia hata kuanza na habari za utakuja kukaa hapa, hili na lile, pia akagusia kabisa kwamba nikitoa atanichukia vibaya sana. Maisha yakaendelea.
Siku nilipopata uhakika nikamjulisha nadhani ilikua kwa msg. Siku mbili baadae akajitubia kua yeye ana mpenzi. Nikashangaa, kumuuliza kulikoni hakutoa taarifa mwanzo akasema eti sikumuuliza. Ikabidi nimpe live kwamba bila ya kuulizwa mapema kabisa alisema hana na huo utetezi wake ni wa kijinga maana hata mpenziwe akimuuliza hawezi kujitetea hivyo,utetezi wake ukaishia hapo.
Basi mi nikamjulisha kwamba hana haja ya kuwa na shaka, aendelee na maisha yake na mimi ntaanza yangu mapya bila ya kumhusisha yeye tena kwa lazima. Akaja na hoja ya kumwacha aliyenae ili awe na mimi. Akaniuliza kama ntaconsider kuwa nae(kuishi nae actually) kama ataachana na aliye nae. Nikamjibu kwamba hilo linahitaji muda mimi kufikiria, akasema sawa.
Mawasiliano yakaendelea kama kawaida, baadae nikaamua kumuuliza kuhusu mpenzi wake huyo aliyeko mbali. Niliyopata ni kwamba ANAMPENDA, HAWAJAWEKEANA MALENGO ila bado wazo la kumwacha kwaajili yangu bado lipo.
Sasa najiuliza, ni akili kweli kumwacha aachane na mtu anaempenda ili awe na mimi? Sindio mwanzo wa kunyanyaswa na kuchitiwa kila siku? Au hata kusimangwa kwamba sikupendwa mimi, alipendwa mwenzangu?Binafsi hisia zangu ni mchanganyiko, natamani kuwa nae (probability ni kwamba kama angeniambia tuwe kwenye mahusiano kabla ya hili sakata ningesema NDIO) ila nna wasiwasi sana. Sina imani nae, na kama sitokuwa na mahusiano nae nataka kila mtu ajali maisha yake ili kuavoid drama, kwenye hili naona sitokua namtendea haki. NIFANYEJE?