Nilipigwa na butwaa nilipomsikia kiongozi huyu mkubwa wa TUCTA taifa akibeza mgomo wa madaktari,akidai kuwa si halali,pamoja na mambo mengine.Pamoja na kuwa haya ni mawazo yake binafsi na anao uhuru wa mawazo,na pengine yuko sahihi,kauli aliyoitoa ni kauli isiyotegemewa kutoka kwa kiongozi anayeongoza taasisi yenye malengo ya kudai haki za wafanyakazi.Hajui kuwa iwapo madai ya madaktari yatafanyiwa kazi, hata wafanyakazi anaowaongoza wanaweza kufaidika.Kauli yake ni kielelezo cha uongozi wake,ambapo shirikisho hili limebakia likiwanufaisha viongozi tu,huku maslahi ya wafanyakazi yakipuuzwa licha ya gharama za maisha kupanda sana!Ni kauli ya kuvunja moyo,na no sawa na mtu anapovamiwa na wezi nyumbani na kupiga yowe ambapo jirani anajitokeza lkn badala ya kukusaidia wewe,anawasaidia wezi !Sielewi huyu jamaa huwa anachaguliwa na nani,ila mimi namwona kama kikwazo cha mustakabali na ustawi wa wafanyakazi