Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,936
- 22,095
NIC vituko vitupu
MASIKINI Mary Mtengeti. Uteuzi wake kuwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) umefutwa kabla hajamaliza hata saa 24 kwenye kiti.
Badala yake serikali imemteua J.P Mwandu, ambaye amekuwa Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Idara ya Usimamizi wa Bima wa NIC kushika nafasi hiyo.
Mtengeti ambaye amekuwa mwanasheria wa NIC kwa miaka tisa, aliteuliwa na Bodi ya Wakurugenzi kushika wadhifa huo Alhamisi iliyopita kuziba nafasi ya Margret Ikongo, Mkurugenzi Mtendaji aliyehamishiwa makao makuu ya wizara ya fedha.
Hakuna taarifa yoyote iliyotolewa na serikali kuhusu kuenguliwa kwa Mtengeti ambaye uteuzi wake ulifanywa chini ya mwenyekiti wa Bodi ya NIC, Dk. Hamis Kibola.
Margret Ikongo alitema ukuu wa shirika hilo wiki iliyopita baada ya madai ya muda mrefu, kutoka kwa wafayakazi na wadau wengine wa NIC, kuwa utawala wake umekosa dira, usimamizi na umesababisha shirika kuporomoka kibishara.
Kubanduliwa kwa Mtengeti kitini kunahusishwa na taarifa ofisa mmoja wa shirika alivujisha maswali ya usaili kwa Mtengeti, jambo ambalo wachunguzi wanasema lilifanya Mtengeti aporomoshe majibu kama aliyekariri.
Mmoja wa watu waliotuhumiwa kuvujisha maswali kwa Mtengeti ni Harun Mgude ambaye hata hivyo, MwanaHALISI lilipomuuliza kuhusiana na hatua hiyo, alikana katakata kujua lolote juu ya vitendo hivyo.
Alipoambiwa kuwa ni yeye aliyekuwa kaimu katibu wa bodi iliyoteua Mtengeti, alikana na kusema Sihusiki. Sijui na kisha kukata simu yake ya mkononi.
Ingawa serikali haijatoa taarifa juu ya hatua yake ya kumkataa Mtengeti, imefahamika kuwa mwanasheria huyo wa NIC amekuwa karibu sana na Mkurugenzi Mtedaji (Ikongo) aliyengolewa na kwamba mmoja asingekuwa mchafu na mwingine kubaki safi.
Katika taarifa yake ya ukurasa mmoja aliyoitoa kwa wafanyakazi, Ikongo alitaka wafanyakazi waliobakia NIC kutoa ushirikiano kwa Mtengeti huku akiahidi kuwa balozi wa shirika huko aendako.
Naomba ushirikiano mlionipa mimi, pia mumpe Bibi Mary Mtengeti aliyeteuliwa kuwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji. Nami nitaendelea kuwa balozi wa NIC, alisema.
Toleo la wiki iliyopita la MwanaHALISI liliripoti kuwa tayari serikali imemwagiza Ikongo kukabidhi ofisi za NIC kwa mwenyekiti wa Bodi, Dk. Hamis Kibola na yeye (Ikongo) kuripoti wizara ya fedha kitengo cha usimamizi wa shughuli za bima (ISD).
MASIKINI Mary Mtengeti. Uteuzi wake kuwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) umefutwa kabla hajamaliza hata saa 24 kwenye kiti.
Badala yake serikali imemteua J.P Mwandu, ambaye amekuwa Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Idara ya Usimamizi wa Bima wa NIC kushika nafasi hiyo.
Mtengeti ambaye amekuwa mwanasheria wa NIC kwa miaka tisa, aliteuliwa na Bodi ya Wakurugenzi kushika wadhifa huo Alhamisi iliyopita kuziba nafasi ya Margret Ikongo, Mkurugenzi Mtendaji aliyehamishiwa makao makuu ya wizara ya fedha.
Hakuna taarifa yoyote iliyotolewa na serikali kuhusu kuenguliwa kwa Mtengeti ambaye uteuzi wake ulifanywa chini ya mwenyekiti wa Bodi ya NIC, Dk. Hamis Kibola.
Margret Ikongo alitema ukuu wa shirika hilo wiki iliyopita baada ya madai ya muda mrefu, kutoka kwa wafayakazi na wadau wengine wa NIC, kuwa utawala wake umekosa dira, usimamizi na umesababisha shirika kuporomoka kibishara.
Kubanduliwa kwa Mtengeti kitini kunahusishwa na taarifa ofisa mmoja wa shirika alivujisha maswali ya usaili kwa Mtengeti, jambo ambalo wachunguzi wanasema lilifanya Mtengeti aporomoshe majibu kama aliyekariri.
Mmoja wa watu waliotuhumiwa kuvujisha maswali kwa Mtengeti ni Harun Mgude ambaye hata hivyo, MwanaHALISI lilipomuuliza kuhusiana na hatua hiyo, alikana katakata kujua lolote juu ya vitendo hivyo.
Alipoambiwa kuwa ni yeye aliyekuwa kaimu katibu wa bodi iliyoteua Mtengeti, alikana na kusema Sihusiki. Sijui na kisha kukata simu yake ya mkononi.
Ingawa serikali haijatoa taarifa juu ya hatua yake ya kumkataa Mtengeti, imefahamika kuwa mwanasheria huyo wa NIC amekuwa karibu sana na Mkurugenzi Mtedaji (Ikongo) aliyengolewa na kwamba mmoja asingekuwa mchafu na mwingine kubaki safi.
Katika taarifa yake ya ukurasa mmoja aliyoitoa kwa wafanyakazi, Ikongo alitaka wafanyakazi waliobakia NIC kutoa ushirikiano kwa Mtengeti huku akiahidi kuwa balozi wa shirika huko aendako.
Naomba ushirikiano mlionipa mimi, pia mumpe Bibi Mary Mtengeti aliyeteuliwa kuwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji. Nami nitaendelea kuwa balozi wa NIC, alisema.
Toleo la wiki iliyopita la MwanaHALISI liliripoti kuwa tayari serikali imemwagiza Ikongo kukabidhi ofisi za NIC kwa mwenyekiti wa Bodi, Dk. Hamis Kibola na yeye (Ikongo) kuripoti wizara ya fedha kitengo cha usimamizi wa shughuli za bima (ISD).