Ni Zanzibar ipi wanaitaka?

Katika hali isiyo ya kawaida huko Zanzibar watu wengi wamefurika na wamehudhuria mhadhara ya kupinga muungano uliofanyika viwanja vya Lumuba mjini Zanzibar na hivyo kupelekea mpaka Polisi nao kushiriki katika uchukuaji picha za video katika mhadhara huo.

Kwa kweli Wazenji wamevunja ukimya na kuiweka SMZ katk hali ngumu ya mchakato wa katiba mpya licha ya kuwa kuna polisi wengi waliopelekwa kutoka Tanganyika kwa hofu ya kutokea fujo.

Si wawape uhuru wao jama isitoshe hati ya muungano haipo na wasiwalazimeshe wasilolipenda walipende!
 
Dhambi ya ubaguzi itatutafuna tusipoangalia. Unakuwa hili swala la Utanganyika na Uzanzibari tusipoangalia utatumaliza bila ya sisi kujua. Baadhi ya wanasiasa wanatumia uelewa mdogo wa wananchi kuhusu muungano vibaya.
 
Leo Lumumba hali ilikuwa hivi jee Muungano mnautaka au hamuutaki? hilo ndio jibu la wa Zanzibari hapo wasioutaka wanyooshe mikono .
Nani sasa alikuwa anahesabu mikono ya wasioutaka? Halafu mbona wamenyoosha mikono miwili miwili, haiwezi ikawa dalili ya kuwa wasioutaka ni wachache?
 
a maana karume alikuwa hujui kusoma au ?

Ukisoma historia ya ukombozi bara la afrika kasi ya Nyerere na akina Kwame Mkuruma, na Yule rais aliyepinduliwa na Mabutu kule zaire na baadhi mtaongezea wenyewe wimbi la kuifanya Afrika shirikisho lilikuwa moto sana. Viongozi wachache waliokuwa vinara wa kuchora taswira ya shirikisho la Afrika kama Nyerere aliamua kuanza na nyumbani nchi ambayo ilikuwa bado changa kujenga mwanzo huo. Utakuwa jumuiya ya Afrika mashariki ilikuwa kama chachu ya kujenga shirikisho kutanuka lakini tofauti za kisera na ubinafsi ndizo zilizofanya azima hiyo kutotekelezeka. Mambo yalipomshinda Nyerere ndipo alipogeukia kuijenga nchi ya Kijamaa kushindana na washindani wake akina Kenyata.
 
naunga mkono kutengana na wazanzibari... wamechakachuliwa sana na CCM kwenye chaguzi tatu zilizopita, wakikaa kimya basi ni mabwege

kuna yule rais wa bara aliua wazanzibar wengi 2001 baada ya uchaguzi. isingekuwa bara ccm isingekuwa zanzibar. ccm ndo inaleta maafa zenji. waipinge ccm na muungano wao kuanzia wa nchi hadi vyama. mtaunganishaje vyama vyetu? Muungano ukifa hata ccm itakuwa umekufa.
 
nafikiri tatizo ni hawa wamiliki wa muungano kuogopa wazanzibar na watanganyika kujadili aina ya serikali waitakayo katika muungano,tatizo hili limezaa tatizo jipya kwa sasa wazinzabar wanahitaji kura ya maoni kwanza ili kujua kuwa muungano wanauhitaji ama la! Hivyo kama wanauhitaji ndo watakuja kujadili muundo wa muungano wenyewe.

MY TAKE;Tuache uoga swali hili linajadilika tulipe mdahalo wake ili tupate tunachokihitaji kwa pande zote mbili.
 
walau wao wanapinga hii kitu wazi wazi

sie tumekuwa waoga kama panya vile

CHADEMA toeni tamko kuhusu hili

swali la kizushi

hati za muungano kwa nini zinafichwa?

kwa niin sherehe za muungano hazifanywi zanzibar?

Zikifichuliwa itakua sooo, huenda ikagundulika Jmt imeidhulumu zanzibar na hivo kutakiwa kuwalipa hela zao kwa kuwadhulumu!
 
Bado wanaukubali Muungano. Wanajadili chini ya Picha ya Rais wa Jamhuri ya Muungano. Muungano wa Tanz Bara na Zanzibar ukishavunjika unaofuatia ni ule wa Pemba na Unguja kwa sababu Zanzibar ni muungano wa Pemba na Unguja na ndio maana kule kuna Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar(SMZ) na hakuna Serikali ya Pemba.

Dah kweli hujui kitu ndugu, hebu nambie, tarehe ya muungano wa kisiwa cha unguja na pemba? Sujawahu kuona wakisherekea iyo siku.... Hivi kuna muungano wa Arusha na Dar es salaam?
 
Wanaitaka nchi "yao" ya Zanzibar; Wanataka kurudia "utukufu wa Zanzibar" kwa kuwa hapa walipo sasa hawaoni manufaa "yoyote" kwa Zanzibar. Wanasema wanaitaka nchi yao waliyonyang'anywa na Wadanganyika (ati Watanganyika). Wanataka warudishiwe nchi yao waliyonyang'anywa na Nyerere na watu wa bara.

Ni Zanzibar ipi hiyo wanayoitaka?

  • Zanzibar ya historia ya kale (Zenj - nchi ya weusi?) ambayo ni zaidi ya visiwa vya Unguja na Pemba bali na mwambao wa Afrika ya Mashariki
  • Zanzibar ya Sultani(ambaye naye utawala wake ulizidi mipaka ya Unguja na Pemba)
  • Zanzibar ya Sultani chini ya Mwingereza
  • Zanzibar ya baada ya Uhuru na Sultani akiwa bado ni Mkuu wa Nchi na serikali ya Mseto
  • Zanzibar ya Mapinduzi kabla ya Muungano
  • Zanzibar "mpya" ambayo haijawahi kuwepo yaani ya baada ya muungano
Ni ipi hasa wanayoitaka? Ni ipi hasa Zanzibar "proper". Isije kuwa ni kama nchi ya ahadi ambayo iko katika fikra za watu tu lakini haijawahi kuwepo; yaani ile nchi imiminikayo maziwa na asali na kwamba watu wa bara na dunia nzima wanataka kuwanyang'anya Wazanzibari.

Na labda hapa itabidi tulijibu swali pia kuwa Mzanzibari ni nani hasa?

.....Ndugu yangu umeuliza swali zuri sana,lakini naomba kuuliza kwa wana JF,kwa hawa jamaa zetu wa znz waishio huku kwetu T.bara waanze kuomba Uraia wa bara kabla ya hao wanaodai zanzibar yao?maana wakishavunja muungano hawa ndugu zetu watakwenda wapi?Unguja au Pemba?
 
Wanaitaka nchi "yao" ya Zanzibar; Wanataka kurudia "utukufu wa Zanzibar" kwa kuwa hapa walipo sasa hawaoni manufaa "yoyote" kwa Zanzibar. Wanasema wanaitaka nchi yao waliyonyang'anywa na Wadanganyika (ati Watanganyika). Wanataka warudishiwe nchi yao waliyonyang'anywa na Nyerere na watu wa bara.

Ni Zanzibar ipi hiyo wanayoitaka?

  • Zanzibar ya historia ya kale (Zenj - nchi ya weusi?) ambayo ni zaidi ya visiwa vya Unguja na Pemba bali na mwambao wa Afrika ya Mashariki
  • Zanzibar ya Sultani(ambaye naye utawala wake ulizidi mipaka ya Unguja na Pemba)
  • Zanzibar ya Sultani chini ya Mwingereza
  • Zanzibar ya baada ya Uhuru na Sultani akiwa bado ni Mkuu wa Nchi na serikali ya Mseto
  • Zanzibar ya Mapinduzi kabla ya Muungano
  • Zanzibar "mpya" ambayo haijawahi kuwepo yaani ya baada ya muungano
Ni ipi hasa wanayoitaka? Ni ipi hasa Zanzibar "proper". Isije kuwa ni kama nchi ya ahadi ambayo iko katika fikra za watu tu lakini haijawahi kuwepo; yaani ile nchi imiminikayo maziwa na asali na kwamba watu wa bara na dunia nzima wanataka kuwanyang'anya Wazanzibari.

Na labda hapa itabidi tulijibu swali pia kuwa Mzanzibari ni nani hasa?
Tunataka Zanzibar ya Wazanzibari ambyao itajiamulia Mambo yake na Haitachaguliwa mamluki kutoka Dodoma
 
Back
Top Bottom